RUNGU: TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha matangazo kwa Miezi Sita (6) kuanzia leo kwa kurusha Maudhui ya utupu

RUNGU: TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha matangazo kwa Miezi Sita (6) kuanzia leo kwa kurusha Maudhui ya utupu

Hivi hawa tisiaraei hawaonagi vifurushi vya mitandao kila siku wao na tv tu..😅
Tiivii yao haina mvuto. Wamefunga zote za ndani tusizione kupitia DStv zikabakia clouds 2 wasafi na tve. Ssas wameondoa wasafi.
Msimamo wetu Ni ule ule Bora kuangalia katuni DStv kuliko ...............
 
Kwa picha niliyoiona Mimi ya gigy money nikilinganisha na sehemu aliyokuwepo na kitu alichokuwa akikifanya pia nikiangalia hadhira ilikuwa ni watu wa aina gani walikuwa pale kufanya nini na kupata nini hakika sioni kabisa mahari ambapo gigy amekosea.

Lile vazi na nyimbo yake ya nampa papa vinaendana kabisa ukizingatia hakuwa mtupu wala hakuvaa chupi ila ni vazi LA kubana na huo urembo uliopo hapo kwenye nyeti.

Kitendo cha mamlaka kumfungia sijui walichoona wao ni nini. Natamani niijue hiyo sheria ya 1980s ambayo ukiachana na sanaa pamoja teknolojia kukuwa bado wanaishi kuifuata na kuitumikia na wakiichukulia kama ni Holly grail.

Napenda kujua kosa walilolifanya WCB ikiwa kama baada ya tukio kutendeka waliomba radhi kwa watanzania. Siji sana lakin huwa naona pia media zngine kama TBC etc wanaporusha kipindi live na maudhui kama hayo yanapotokea huomba radhi kwa watanzania alafu mambo mengine yanaendelea.

naomba kufahamishwa
 
Nmeota hili la Wasafi kuna mtu atalitumia kama platform ya kisiasa, atakuja na kukanusha hilo Rungu walioshushiwa wasafi, alafu tutaanza kumsifia mtetea haki za wanyonge... mark this[emoji23][emoji23]Uzi Tayari
IMG_20210105_210425.jpg
 
TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha kurusha matangazo kwa miezi sita kuanzia leo kutokana kwa kukiuka kanuni za utangazaji kwa kurusha maudhui ya utupu....
Awapeleke karantini watangazaji wake
 
TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha kurusha matangazo kwa miezi sita kuanzia leo kutokana kwa kukiuka kanuni za utangazaji kwa kurusha maudhui ya utupu.....
Hawa adhabu waliopewa ndogo sana ...wangefungiwa angalau kuanzia miaka miwili wapate muda wa kwenda kusoma kwenye vyuo vya habari
 
Wewe ndugu siujui umri wako ila tambua hakuna gharama kubwa kama kulinda maadili ya kizazi hasa wakati huu tuliopo ambao baba kuangalia Tv na watoto ni jambo la kawaida kabisa na watoto wenyewe siku hizi wanachagua kabisa station za kuangalia sasa tu-assume ndo wewe baba upo na wanao aged 11/13 sitting room mnaangalia Tv kisha mara anapita jiji mane anakatiza uchi kwenye kioo wewe kama baba utajificha wapi?maana siyo unatetea tu jua na hasara zake!!!
Maadili Wanayajua!? Acha tupambane tu. Wale wengine waliletewa kioo wakauza nchi... Wa sasa hivi wameletwa kioo wamesahau who they are... Wanatetea vitu vya ajabu kabisa
 
Kufungiwa inaweza isiwe issue ila kufungiwa miezi 6 kwa ajili ya Giggy Money ni upuuzi wa hali ya juu..
This is the best move...

Sasa hivi TV stations na Watu wengine wote waandaaji wa matamasha na vipindi vya redio watakuwa makini kuchagua ni Watu(wasanii na presenters) wa namna gani wajihusishe nao..

Ushauri wangu: kwenye bodaboda mmiliki wa chombo aende jela kwa ajali ya uzembe inayohusishwa na chombo chake.. itakuwa safi sana.. vet people you associate with..

Wa magari ukisababisha ajili uwe charged na attempted murder. 🙂

This is beautiful.. and it's working.. tazama in the next six months utulivu utakaokuwepo na mizaha ya kipuuzi itakavyokisha
 
Dili ya rushwa imetengenezwa hapo.. ukitaka mtu atoe hela mpe mkwara mkubwa
 
Back
Top Bottom