Rupia: Hazina ya Mjerumani

Rupia: Hazina ya Mjerumani

Nikubali marekebisho kwenye vita pengine ni kweli....hayo mengine umekosea sizungumzii watu waliozikwa na vitu. Wala makaburi nazungumzia mali zilizofichwa ikiwemo pesa za rupia ...hebu rudia kusoma tena kwa makini nilichoandika
Katika kuficha ilifanyika kafara ya kufukia Watu wakiwa hai ili kuweka ulinzi.
Kitu kilichofichwa kwa mbinu hiyo kukipata ni kwa kutoa kafara ya kuizidi ile iliyowekwa kama ni watu wawili unaweka watatu au kuwapata wahusika wenyewe.

Mifano ni Mingi hasa sehemu walizoweka Makanisa na Mashule unaweza chimba mita nne chini unakutana na zege ya kutosha ila GTZ wakiona mnachimba wanakuja mbio kuwabadilisha mawazo kwa kuwapa msaada mbadala
 
Mshana katika hili naamini hujalifanyia uchunguzi wa kutosha au leo umemuachia mtu akuandikie wewe upo Kanisani.

Kwanza Vita ya Pili Wajerumani walikuwa hawapo washaondoka vitu vilizikwa kabla ya Vita ya kwanza

Pili utaratibu wa kuficha vitu kwa kuzika pamoja na watu hai umekuwepo Ulaya Siku zote na ndicho walichofanya na zege nyingi tunazovunja sehemu hizo unakuta kabisa mafuvu ya watu waliokufa kwa kulazimishwa ( kawekewa zege miguu tuu au kichwa tu)
Em tiririka kwa mtindo wako ili tujifunze kitu, mi nilikua mwanza mwaka fulani nikawa naona zile alama km chokaa kwenye mawe katika kuuliza nikaambiwa zile ni ramani, kuchimba zaidi nikaelekezwa junsi zinavyotafsiriwa nikafatilia hadi sehwmu fulani nilichokiona nilisita kuendelea BUT nlijisemea nitaenda nikijipanga..

So em tupe kiundani zaidi haya mambo yalivyo.
 
Mkuu umenivunja nguvu kabisa yaan,nipo mkoani mtwara wilaya masasi kuna milima mingi(rock mountans) ila kuna huu mlima mkubwa mmoja upo sehemu kuna itwa mailisita watu wengi hupanda juu kwa ajili ya matambiko ila kuna wanaoamini kwamba juu ya mlima huu kuna dhahabu nyingi ndipo na mimi nikaunda timu yangu ya watu watatu twende juu uko sijawah fika ila wenyeji wangu wamefka na wanasema kuna pango kubwa limezibwa na zege,dah sasa kuna uwezokano hawa jamaa washachukua vyao kwa sababu chini ya mlima kuna nyumba za masista.Sasa bora nlurudishe majeshi tu .
 
Kuna maeneo mengi watu waliamka asubuhi na kukuta mashimo tu yaliyofukuliwa usiku...ukweli ni upi!? Walipata?walikosa? Haijulikani
Eneo moja pale Mbwewe tulikuta mizoga miwili ya kondoo hirizi tunguli kaniki na zana za kuchimbia
Sijui nini kiliwatokea hao watu lakini inaelekea walitimua mbio. .
Mashimo kama haya yapo sehemu nyingi[emoji116] [emoji116] [emoji116] View attachment 526144
Kuna lipo maeneo ya kule kwetu Kwakoa maeneo flani wanaita Nyata ila wanadai kuna vitu vyaajabu sana mimi binafsi sijachunguza
 
Aliingia ktk hayo mashimo alipofika kulikuta hilo sanduku lenye fedha akamtokea mdada mrembo akamsalimia ...anko akashindwa kujibu basi yule mdada alikaa kwa dkk kadhaa akatoweka anko alivotoka kule ktk shimo tu hakuchukua muda akafa
Sasa hapa napingana na mshana anavyosema hakuna ulinzi wowote kule bali shimo likiwa halina watu hua wadudu hukaa, sasa nataka kujua huyo mdada naye anafanyaje huko kama sio kweli kwamba hawa wajerumani wamelinda mali zao kichawi?

Nawasilisha
 
Mkuu umenivunja nguvu kabisa yaan,nipo mkoani mtwara wilaya masasi kuna milima mingi(rock mountans) ila kuna huu mlima mkubwa mmoja upo sehemu kuna itwa mailisita watu wengi hupanda juu kwa ajili ya matambiko ila kuna wanaoamini kwamba juu ya mlima huu kuna dhahabu nyingi ndipo na mimi nikaunda timu yangu ya watu watatu twende juu uko sijawah fika ila wenyeji wangu wamefka na wanasema kuna pango kubwa limezibwa na zege,dah sasa kuna uwezokano hawa jamaa washachukua vyao kwa sababu chini ya mlima kuna nyumba za masista.Sasa bora nlurudishe majeshi tu .
Step ya kwanza: nenda kahakikishe kweli kuna pango lenye zege? kisha mlikague jinsi lilivyo, mlango ulipo, mandhari ikoje.

Step ya pili: Ukishajiridhisha rudini na team yako, anzeni kuchambua madhara ya sehemu hiyo kutokana na mazingira yake..... hii itawasaidia kujua namna mtakavoingia kwa kujilinda.

Step ya tatu: Mkishajua namna na kujipanga, hapa mnapanga kwenda kuchunguza ndani.... step hii mjiandae kisaikolojia zaidi mkiwa na vitu vya kujikinga na madhara, pia muwe tayari kurudi na chochote, hivyo jiandaeni na vibebeo kabisa(kumbuka step hii ni ukaguzi wandani)

Step ya nne: Mmeshajua ndani kuna nn(yawezekana hakuna kitu, vimeshabebwa) lakni kama vipo muwe mnajua kilichopo ni nini, hivyo mmejipanga kubeba, taa za chemli zinazowaka bila mafuta, pasi za dhahabu ambazo haziwekwi mkaa, vikombe vya dhahabu.... sarafu, manwe kukuta buti(sema hapa zitakuwa zimeshaharibika na kuwa km bigijii)au bunduki na masanduku ya unga wa baruti, hizi acganeni zazo kwa kuwa ni rahisi kukamatwa nazo..... lkn km una mtu unaeza muuzia, chukua.

Kwa step hizo, mko tayar kuwa matajiri.... pangeni safari fasta.

ANGALIZO: kuna mitego mingi sana, ukiachilia ya kichawi, kuna.mitego ya gesi chafu(wataalamu wanazijua kwa majina) hizi ni pale umekuta kikombe maridadi cha dhahabu( hasa mwanzoni mwanzoni mnapoingia) halafu ww unakibeba kwa pupa kumbe limetegeshwa na unapokitoa unategua kitu kinachoatoa hiyo gesi.... hivyo MNAKUFA MNAJIONA kabla ya kusonga mbele, inaweza kuwa sehem yamepangwa mawe, mkaondoa moja tu, lkn hilo ndo limebeba uzito wa mengine yaliyopangwa kiustadi yatakayopelekea kuporomosha mengine yatakayoziba njia mliyoingilia(MNAKUFA MNAJIONA)

Kwa hiyo mnapaswa kuwa makini sana kugusa vitu msvyovijua kwa kuwa mpo kwenye hatua ya uchunguzi, pia hakikisheni mna kamera yenye flash, taa zenye mwanga mweupe, na diary ili kunote kila mnachokiona.
 
Sasa hapa napingana na mshana anavyosema hakuna ulinzi wowote kule bali shimo likiwa halina watu hua wadudu hukaa, sasa nataka kujua huyo mdada naye anafanyaje huko kama sio kweli kwamba hawa wajerumani wamelinda mali zao kichawi?

Nawasilisha
Unapingana nami kwa ushuhuda huu mmoja tu niliposema kuna mauzauza mengi hukunielewa kwani?
 
Haya mambo nilsikia kwa rafiki wangu wa karibu niko nae hapa anatokea Mbeya,
Kuna mzungu alikuwa anaenda sana maeneo fulani Mbeya wakamfatilia wakajenga urafiki na jamaa fulani ambaye alikuwa close na huyu mzungu
wakafanikiwa kumshawish jamaa ili siku amzunguke yule mzungu ili washkaji( rafiki yangu na bri ake) wapate kupekua mabegi ya mzungu
walifanikiwa na wakakuta kuna ramani ya hii story ya RUPIA wakafanikiwa mpaka kutoa nakala zoezi lilifanyika bila mzungu kujua.
Wakatafuta mpaka kifaa cha ku detect madini( Sort of EM Ground Penetrating instruments).
Wakaenda kweny location one wakakuta kuna nyumba imejengwa wakaongea na mwenye nyumba ili wafanye vipimo na kifaa chao, ni kweli waligundua kuna sanduku, lenye bunduki na mercury though hawakuchimba..
Maeneo mengine kweny ile ramani wanadai yapo sehem za hatari sana hata kufikika,..
Kuhusu Zege Inakumbuka alinambia eneo moja kuna mtu tajiri Mbeya alitumia hadi greda akashindwa kuvunja.
[HASHTAG]#Hashtag[/HASHTAG] Kusaka Rupee.....
Haya ndio niliyowahi kusikia ndugu zangu,
Alexander
 
storyteller ungetupa kidogo uzoefu wako
Kiukweli mm bado sina uhakika kama yapo kwasababu BINAFSI sijafuatilia kiundani na sikutilia maanani kwa kuwa kuna mengine kama hayakuniingia akilini(niliona ni mepesi sana), ILA ninachofahamu hadi sasa kuna eneo nilienda kulingana na maelezo niliyopewa nikakuta kuna dalili za hiyo kitu.

ILIKUWAJE:
Nilivoulizia zile alama ktk mawe kule mwanza(mawe mengi yana alama za michoro km chokaa, mfano alama ya jiwe ambalo maji yalikua yakitiririka kupitia hapo kisha yakakauka)..... Maelezo nlopewa yaliendana na hicho mshana jr alichosema, ila jamaa alikua na ushahidi zaidi, kwa kuwa alinifundisha maana ya alama zote kuanzia hiyo michoro ya chokaa, aina ya miti, mchanga.... na alinipitisha ktk maeneo yote yaliyo karibu ili kuona mifano halisi.

Kwa ufukunyunyu wangu siku moja nikaenda mbali sana huko nyegezi af unapanda huko ndani ndani. Nikachagua moja ya alama na kuanza kufatilia kadri alivyonieleza..... nikakuta kuna mahali kuna jiwe(ama zege hivi) kama limeegeshwa...... nilipologonga.... ulitoka mlio mithili kuna uwazi kwa chini....sikufatilia zaidi ya hapo kwa kuwa nilijawa hofu........ ila ipo siku nitakwenda na team tukafanye mambo.

Maeneo yenye hizi mambo mengine unakuta ni kambi za jeshi, na kwa maelezo ya jamaa waliofanikiwa kupata hazina hii ni wajeda wakubwa tu(haiwekwi wazi) ingawa wao walitumia njia rahisi ya kununua maji(au mafuta) toka kwa familia za kijerumani zinazojua maswala haya(hii ni kwa mujibu wa maelezo ya jamaa).

Masharti ya kuingia maeneo haya.

1. Usisex wala kujielekeza sana na mawazo ya sex kwa muda usiopungua miezi6(maana yake uwe masafi(pure), kuna uwezekano ukiwa bikra unafanikiwa zaidi) pia usiwe na mawazo ya chuki, hasira.
2. Ukiwa eneo hili hamtakiwi kula kula(kama ni kula mkalie mbali huko)
3. Usiende kwa mganga kwa nia ya kudhuru(wapo waganga wanaoelewa hilo na wanajua namna ya kuwashauri)
4. Mnapoenda, msiwe na mawazo ya kidhuluma(yani km ni mgawo, uwe sawa sawa kama mlivokubaliana)
5. Uwe jasiri, vile vitu unapokutana navyo ni vitisho tu, havidhuru, mtu anadhurika kwa woga wake na panic, na pia utakapoogopa na kupiga kelele ndo mauza uza yanapozidi.
6.Msiwe waropokaji, hapa jamaa alisema utakaposema sema habar hizo kwa wasiohusika(kwamba mna mzigo) utakua unapotea potea....
7. Haitakiwi kelele, msiongee ongee, mnatakiwa kuweka akili yote katika jambo mnalofanya(ikiwezekana mjifunze kuwasiliana kwa ishara kabla hamjaingia)

Kikubwa hapa ni kuwa waangalifu kwa mazingira yanayokuzunguka, kuchunga hali ya hatari ili usidhurike na vitu halisi mfano nyoka, wanyama, wadudu na mawe kuporomoka.
 
Back
Top Bottom