Rupia: Hazina ya Mjerumani

Rupia: Hazina ya Mjerumani

Mwenye zile hela za matobo kuanzia mwaka 1916 kurudi nyuma tafadhali tuwasiliane
 
Gramu 1 ya original red mercury ambayo imehifadhiwa vyema ni zaidi ya Bil 12. Hata kama imepungua nguvu kwa maana ya mionzi yake bado inauzika na utapata bei safi tu. Pm me kwa details
Mkuu inauzwa wapi hiyo?
 
Mkuu achana na hzo mambo aisee.. Waambie ndugu zako watafute pesa kwa njia nyingine sio rupia.

Nina uzoefu aisee, tumepoteza nyumba na maisha mazuri kisa tu baba etu alijiingiza kwa hyo biashara..

Sasa tunalipa madeni yasiyotuhusu[emoji26] [emoji24] [emoji24] [emoji24] [emoji29]
Embu tupe somo mkuu
 
i was once involved with wht i kol "rupia and mercury corn artists.

....... kwnz rupia yenyewe niliifata hko Lushoto Milimani mwaka 2009 na huyo babu alikua anataka 15m in exchange ya hyo rupia......

tatzo ilikua sio pesa koz aliejiita mteja alitoa dau la 400m, ila hayo masharti tuliopewa ndio kiboko halaf hayaishi.

mara uchinje ng'ombe wa matambiko, mara ukachome mishumaa 52 baharini, mara usisafiri jumanne ..........etc

inshort am dealin with gems for a livin lakini we don't have any rituals........ nw y rupia?

i stand strong to tell all jf members nt to engage in dis staff........ unaeza geuka mganga at the end of the day
chif umenikumbusha mbali sana
 
Step ya kwanza: nenda kahakikishe kweli kuna pango lenye zege? kisha mlikague jinsi lilivyo, mlango ulipo, mandhari ikoje.

Step ya pili: Ukishajiridhisha rudini na team yako, anzeni kuchambua madhara ya sehemu hiyo kutokana na mazingira yake..... hii itawasaidia kujua namna mtakavoingia kwa kujilinda.

Step ya tatu: Mkishajua namna na kujipanga, hapa mnapanga kwenda kuchunguza ndani.... step hii mjiandae kisaikolojia zaidi mkiwa na vitu vya kujikinga na madhara, pia muwe tayari kurudi na chochote, hivyo jiandaeni na vibebeo kabisa(kumbuka step hii ni ukaguzi wandani)

Step ya nne: Mmeshajua ndani kuna nn(yawezekana hakuna kitu, vimeshabebwa) lakni kama vipo muwe mnajua kilichopo ni nini, hivyo mmejipanga kubeba, taa za chemli zinazowaka bila mafuta, pasi za dhahabu ambazo haziwekwi mkaa, vikombe vya dhahabu.... sarafu, manwe kukuta buti(sema hapa zitakuwa zimeshaharibika na kuwa km bigijii)au bunduki na masanduku ya unga wa baruti, hizi acganeni zazo kwa kuwa ni rahisi kukamatwa nazo..... lkn km una mtu unaeza muuzia, chukua.

Kwa step hizo, mko tayar kuwa matajiri.... pangeni safari fasta.

ANGALIZO: kuna mitego mingi sana, ukiachilia ya kichawi, kuna.mitego ya gesi chafu(wataalamu wanazijua kwa majina) hizi ni pale umekuta kikombe maridadi cha dhahabu( hasa mwanzoni mwanzoni mnapoingia) halafu ww unakibeba kwa pupa kumbe limetegeshwa na unapokitoa unategua kitu kinachoatoa hiyo gesi.... hivyo MNAKUFA MNAJIONA kabla ya kusonga mbele, inaweza kuwa sehem yamepangwa mawe, mkaondoa moja tu, lkn hilo ndo limebeba uzito wa mengine yaliyopangwa kiustadi yatakayopelekea kuporomosha mengine yatakayoziba njia mliyoingilia(MNAKUFA MNAJIONA)

Kwa hiyo mnapaswa kuwa makini sana kugusa vitu msvyovijua kwa kuwa mpo kwenye hatua ya uchunguzi, pia hakikisheni mna kamera yenye flash, taa zenye mwanga mweupe, na diary ili kunote kila mnachokiona.
Mkuu hapo kwenye mitego ni hatari
 
Huu msemo ni kweli kabisa. Hizo fedha za kijerumani zipo sehemu mbali mbali Chini ya ardhi au milima. Miaka ya 90 wazungu walifika kijijini kwetu na kununua eneo kubwa kwa ajili ya ufugaji, wakaajiri wafanyakazi kama 50. Katika shamba Lao hawakufikisha hata ng'ombe 100. Walikaa kama miaka saba hivi, sasa inasemekana walikuwa wanatafuta mali ambazo zilifukiwa na babu zao, na walifanikiwa kupata sanduku mbali za shaba, ila haikujulika mlikuwa na nini. , walipofanikiwa tu walikabidhi shamba Lao kwa serikali wakaondoka zao, mifugo, magari ng'ombe na mbuzi hawakuwa na shida nao tena. Watu wengine hubahatika kuoteshwa wapi zilipo pesa hizo ila masharti yake magumu, uwe na roho ya jiwe, unaweka mwanao hapo unaichimba, kila ukiikaribia mwanao anazidi kudhoofika,.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji115]
 
Maeneo ya mvomero kwenye safu za milima ya Unguu kuna Mzee wangu aliungana na wasaka rupia walipanda kuelekea kileleni kwa muda wa siku 4 walishangaa kumkuta mjeruman kapiga suti na yupo bize kwenye kaofisi kazuri ka vioo huko karibu na kilele!, kuna mganga walikuwa nae akapiga manyanga bila mafanikio wakaamua kupiga jiwe mlangoni walishtukia yule mjerumani yupo miongon mwao! Walitimua mbio walikutana nyumban yule mganga aliuacha mkoba wake hakuufata tena. Kuna wengine walikuta pango lenye mlango finyu wakaona masanduku lakini kwa juu kuna bunduki ikielekea mlangoni halafu kuna nyaya zimeingia kwenye trigger lakini chanzo cha zile nyaya hakionekani na kuna mjeda ndugu yangu aliefika hapo aliàmua kurusha jiwe mlangon anasema bunduki ilitema risasi hadi jiwe lililokuwa kwa mbele liliçhakaa na akagundua kuna mkanda wa risasi usioisha kibaya zaidi ile bunduki inacheza pande zote za mlango! Alikwenda karibu Mara 7 bunduki bado active.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1], si mchezo aiseee
Hear say ni kuwa wakati wanazifukia wale wapagazi walioingiza masanduku walipigwa risasi na kufa wakiwa wameinama na walifukiwa hivyo. Hiyo ndiyo mizimu inayozilinda.
 
Money+Mashetani=Rupia
Power+Mashetani=Rupia

Rupia Zipo but zilihifadhiwa kishetani na zinatafutwa kishetani na kazi kubwa ya kishetani
ipo 1/2 rupia na 1 rupia
hiyo 1/2 haina issue but 1 rupia ndio mzigo

even jama ipo mahali huchimbwa usiku, maana kafara hufanyika ili zichukuliwe,

ukikuta mtu anayo yenyewe afu eti anaiuza ujue michezo ya kitapeli
japo wapo wenye bahati huzipata pasipo ushetani wowote tena itakuwa ni moja.

but hufanya kazi nyingi sana za kishetani kutokana na nguvu iliyoko ndani yake.

all in all rupia ilihifadhiwa kishetani ili mtu yeyote asiione
so kama wewe kuipata hauna tofauti na mtu anaye tafuta mali kwa njia ya mganga vile

namfahamu mzee mmoja kwetu alitoa kafara ili wapate hizo rupia, then hakuzipata waziuze wanafanyia kazi zao za kishirikina tu.

mie naujua upande huo kidogo tu hapo
 
Morogoro maeneo ya Mvuha kijiji cha Lukulunge kuna bwawa hivi flani, nakumbuka miaka ya 2000 kuna mGerman flani hivi alikuja akawa anajenga shule pale mvuha na lukulunge.
Yule mzungu alijenga porini kabisa pembezoni mwa bwawa kabisa, basi yle mzungu alijitolea kwa kila kitu yale maeneo. Baada ya miaka kadhaa yule mzungu akaenda zake na kutelekeza vitu vyote, na wale watu wake wa jirani waliambulia kupata ajar na kufariki
 
Naskia hata mbozi_songwe karibu na MTO mbimba zilikuwepo hizo TREASURES wazungu wa Chavda walizibeba
 
Kunajamaa aliniambia morogoro zipo mlimani lakini hamuwezi kuzipata hadi mtumie mambo ya kienyeji kwasababu zile hela ukifikilia kwenda kuzichukua huwa zinapotea.
 
Back
Top Bottom