Rushwa katika uchaguzi ni mbegu mbaya inayopandwa na CCM

Rushwa katika uchaguzi ni mbegu mbaya inayopandwa na CCM

Patriot

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2008
Posts
5,705
Reaction score
4,703
Nimeanza kuona watu wakitetea tatizo hili la rushwa kwa kusema lete ushahidi. Ukweli ni kwamba nafasi ya wajumbe wa CCM kuamua nani awe mgombea, inatumika vibaya sana!

Hawa ni watu ambao hawalipwi mshahara. Wakati wa uchaguzi hutegemea kipato toka kwa wgombea huu ni mtindo ambao umejionesha wazi kwamba, uchaguzi ndani ya chama hauleti mtu bora, bali ni sehemu ya kuchochea rushwa. Bahati mbaya sana baada ya wabunge, sasa tena madiwani wanapatikana kwa mtindo huo.

Viongoziwa kitaifa wanaweza kujifanya kutoona kwa kuwa tu tayari wanaowagombea ambao watatumika kuunda serikali, lakini hali ya Bungeni itakuweje? Ni salama kuamini siasa ni sehemu ya kupeana rushwa?

Kifuatacho, sisi ambao siyo wajumbe, nasi tutaomba kupewa chochote na bila hivyo, lazimisheni matokeo maana haiwezekani tupoteza muda kupitisha viongozi wenye uwezo mdogo kiasi hiki.
 
Utaratibu ni uleule, kama wametoa rushwa kupitishwa na wajumbe ndani ya chama chao,
Na sisi wananchi tunawasubiri watupatie kiwango kilekile cha fedha walichoyoa kwa wajumbe na wananchi watupatie hichohicho kwa kila kura moja!
 
Mimi nimeshajiandaa kupata chochote kwa wagombea. Hawataki, tusionane na wategemee kura za hasira!
 
Kina shefa kanunua wajumbe kila mjumbe laki nne na.jamaa katoboa.
 
Pale Ukerewe wahusika waligawa pesa hadi ndani ya ukumbi wa mkutano.

Pale Sengerema ikawa ni kufukuzana na mtoa rushwa.

Pale Bunda ikawa ni kushindana na msela Msiba kwa vurugu ya pesa

Pale Kibaha ikawa ni kusumbuana kwa kuwaficha wajumbe.

Pale Ilala ikawa ni matembezi ya usiku wa manane, pesa mlango kwa mlango

Kwa nchi nzima ni kama PCCB walishikwa na ganzi ya CCM.
 
Jimbo la Rorya ndiyo ilikuwa hatari wakati wauchaguzi wa watia nia wa CCM.
 
Jimbo la Namtumbo Rushwa ilitamalaki na kugawiwa bila uoga wowote. Karibu top five (5) yote inahusishwa na ugawaji wa Rushwa. Viongozi wa Chama wa Wilaya waliwekwa mifukoni mwa baadhi ya wagombea na hivyo kutumika vibaya na baadhi ya wagombea. Kama Vikao vya juu havitaingilia Kati. Ni dhahiri kuwa mgombea asiyefwata maadili ya chama na asiyekubalika na wananchi, atapita.
 
Dawa kama ingewezekana kamati kuu iteue majina kuanzia namba mbili kushuka chini, 2,3,4,5 ndiyo wapewe ushindi bila kuogopa cheo cha mgombea serikalini
 
Hiki chama kimekuwa kikihadaa wananchi kuwa chini ya Magufuli kimedhibiti. Tumekuwa tukisema rushwa haujadhibitiwa, bali mahasimu wa rais walikuwa wanakomolewa.


Kipindi chote cha miaka mitano wanaccm wamekuwa wakihadaa umma, tena kwa shuruti kuwa serikali yao imedhibiti rushwa. Sisi wakosoaji tukasema hakuna vita yoyote ya maana ya rushwa, bali kuna wala rushwa kadhaa, wanakomolewa kwa kisingizio cha kupambana na rushwa. Tukasema kabisa, hakuna mtu au serikali yoyote inayoweza kupambana na rushwa huku ikilidhoofisha bunge na mahakama, kuwa adui wa vyombo vya habari, na wakati huo huo ukazuia vyama vya upinzani kukosoa.

Ukiona mtu au serikali yoyote inadhibiti hizo checks and balances za kupambana na rushwa, basi ujue haipambani na rushwa, bali inapambana na matumizi ya neno rushwa. Kwa bahati nzuri Mungu hamfichi mnafiki, hatimaye wale Makada waliokuwa wanapiga propaganda kuwa chama chao kinapambana na rushwa, ndio sasa hivi wanagawa rushwa kama njugu hadharani! Kibaya kuliko vyote, hata hiyo taasisi ya kupambana na rushwa, imegeuka kuwa sehemu ya hiyo rushwa.

Hatari itakayojitokeza, kwakuwa sasa hivi box la kura limekuwa ni sehemu ya kupitisha wanaccm bila ridhaa ya wananchi, tutakuwa na bunge linalotokana na wala rushwa. Hivyo tutegemee bunge linalolinda rushwa, na litakalopitisha sheria mbovu. Na sana sana hilo bunge litatumika kubadilisha katiba kwa ajili ya kujilinda, na kulinda wizi wao, ikiwemo kumuongezea rais muda wa kukaa madarakani zaidi ya miaka 10.
 
Utaratibu ni uleule, kama wametoa rushwa kupitishwa na wajumbe ndani ya chama chao,
Na sisi wananchi tunawasubiri watupatie kiwango kilekile cha fedha walichoyoa kwa wajumbe na wananchi watupatie hichohicho kwa kila kura moja!

Utapewa na nani boss, kumbuka wakishatoka huko kwenye vikao vya ccm, kwenye uchaguzi mkuu hawashindani bali tume ya uchaguzi imepewa maagizo vya kuwatangaza washindi. Husikii wanasema watashinda kwa asilimia 90%. Wanajua fika kwa uchaguzi huru na wa haki watashinda kwa shida.
 
Maskini hawezi kupata uongozi ndani ya CCM, ni hatari sana

Paskali Mayalla ndio aliingizwa mkenge na propaganda mfu eti kuwa sasa hivi rushwa imedhibitiwa ccm, na kila mtu anaweza kugombea bila kujali utajiri wake. Akajichanganya akaliwa kahela kake akaishia kupata kura moja. Alidhani zile mada zake anazoanzishi huku kwenye mitandao ya kijamii zitambeba kwakuwa huwa anajiita mzalendo. Kumbe hajajua hilo neno uzalendo linatumika kama gia ya kuhadaa mabwege. Matokeo yake walioshinda na watakaopitishwa, wengi ni hao hao watoa rushwa.
 
Pale Ukerewe wahusika waligawa pesa hadi ndani ya ukumbi wa mkutano.

Pale Sengerema ikawa ni kufukuzana na mtoa rushwa.

Pale Bunda ikawa ni kushindana na msela Msiba kwa vurugu ya pesa

Pale Kibaha ikawa ni kusumbuana kwa kuwaficha wajumbe.

Pale Ilala ikawa ni matembezi ya usiku wa manane, pesa mlango kwa mlango

Kwa nchi nzima ni kama PCCB walishikwa na ganzi ya CCM.

Hao pccb wenyewe ndio kiungo muhimu cha rushwa. Kama kwenye jengo lao lenyewe wamepiga, ndio itakuwa kwenye hizo hela za kuokota za ccm?
 
Mimi nimeshajiandaa kupata chochote kwa wagombea. Hawataki, tusionane na wategemee kura za hasira!

Utapewa na nani, ww kujiita mzalendo kunakutosha. Nyie wazalendo huwa hamli rushwa.
 
Back
Top Bottom