Russia yavurugana na Wagner Group, waanza kutuhumiana kwa Uasi

Russia yavurugana na Wagner Group, waanza kutuhumiana kwa Uasi

Sempede zedesiso matulebe ngabo
Screenshot_20230624-100147_Chrome.jpg
 
1687591660412.png


Rais #VladimirPutin amemtuhumu Mmiliki wa Jeshi Binafsi la Wagner, Yevgeny Prigozhin, juu ya jaribio la mapinduzi dhidi ya Majeshi ya #Russia baada ya Wagner kudai Serikali inahusika na mauaji ya Wapiganaji wa Wagner

Kwa mujibu wa #ABCNews, Rais Putin amejulishwa rasmi kuwa Vikosi vya Wagner vimetangaza kuuteka Mji wa Rostov-on-Don pamoja na kushikilia kambi zote za Majeshi ya Urusi zilizopo eneo hilo

Kupitia taarifa ya Video, Prigozhin amekaririwa akiitaka Ikulu ya Urusi (Kremlin) kumkabidhi kwake Mkuu wa Vikosi vya Kijeshi vya Urusi vinginevyo wataingia Jijini #Moscow na kufanya mashambulizi kwa yeyote anayewaingilia

Ikumbukwe Russia na #WagnerGroup walikuwa na makubaliano ya ushirika katika Vita dhidi ya #Ukraine ambapo Wagner walikuwa msaada mkubwa kwa Serikali ya Rais Putin tangu kuanza kwa Vita hiyo.

=========

The owner of the Wagner private military contractor made his most direct challenge to the Kremlin yet, calling for an armed rebellion aimed at ousting Russia’s defense minister. The security services reacted immediately by calling for the arrest of Yevgeny Prigozhin.

In a sign of how seriously the Kremlin was taking the threat, security was heightened in Moscow and in Rostov-on-Don, which is home to the Russian military headquarters for the southern region and also oversees the fighting in Ukraine.

While the outcome of the confrontation was still unclear, it appeared likely to further hinder Moscow’s war effort as Kyiv’s forces were probing Russian defenses in the initial stages of a counteroffensive. The dispute, especially if Prigozhin were to succeed, also could have repercussions for President Vladimir Putin and his ability to maintain a united front.

Prigozhin claimed early Saturday that his forces had crossed into Russia from Ukraine and had reached Rostov, saying they faced no resistance from young conscripts at checkpoints and that his forces “aren’t fighting against children.”

The head of Russia's Wagner mercenary group appears to be threatening an armed rebellion against Russia's military leadership, after accusing it of deliberately shelling his forces on Friday.

Wagner's founder Yevgeny Prigozhin in an audio message on Friday claimed his forces would now punish Russia's defense minister and chief of general staff, telling other units to stand down and not offer resistance.

"There are 25,000 of us and we are coming to sort things out. ... Those who want to join us, it's time to finish with this mess," Prigozhin said.

Prigozhin published a shaky video on Friday that showed a shattered group of trees and a burning trench, claiming it was a Wagner camp shelled by Russian troops and alleging many Wagner troops were killed.

Russia's defense ministry has already denounced the video, calling it an "information provocation."

A Kremlin spokesperson said Russian President Vladimir Putin is aware of the video.

"President Putin has been informed of all the events around Prigozhin. Necessary measures are being taken," the spokesperson said.

Russia's FSB has issued a statement accusing Prigohzin of calling for "the start of an armed civil conflict" in Russia.

The FSB called on Wagner fighters not to follow Prigozhin's orders and to assist in his arrest.

Prigozhin has denied this is a "military coup" calling it a "march for justice."
 
Hili swala la Wagner sijui likoje, ila watu wanajifunza zaidi huwezi tumia vikundi na ukawapa silaha ukategemea hawatakugeuka
Taarifa zinasema wanazidi kusonga mbele katika miji mingine ya Krasnodar na Volgograd bila resistance kubwa !
 
Katika muendelezo wa kinachoonekana ni uasi kwa serikali ya Urusi Wagner group wanaripotiwa kutekea na kutwaa makao makuu ya jeshi katika mji wa Rostov. Misururu ya wapiganaji wa Wagner katika maeneo mbalimbali inazidi kuoenkea ndani ya Urusi, kwa sasa wapo Voronezh na kuna taarifa wanataka kuelekea Moscow.

Katika upande mwingine, vyombo vya Usalama vya Urusi vimevamia makao makuu ya Wagner huko St. Petersburg.

Prigozhin alikutana na manaibu wa waziri wa Ulinzi na GRU akiwasilisha madai yake ya kukabidhiwa Waziri wa Ulinzi, Shoigu na mkuu wa majeshi, Gerasimov ili Wagner wasitishe operation yao ndani ya Urusi.

Helicopter kadha zimeshambuliwa na kuangushwa maeneo mbalimbali ndani ya Urusi ila hazijajulikana ni za upande gani. Kuna video nyingi pia zilizogaa zikidaiwa na Wagner ni jeshi la Urusi linashambulia kambi za Wagner ndani ya Ukraine na misafara yake ya wapiganaji ndani ya Urusi.

Putin anatarajiwa kutoa kauli muda mfupi ujao kuhusu hali inavyoendelea ndani ya Urusi. Utawala wa Biden umetoa taarifa unafuatilia kwa karibu yanayoendelea ndani ya Urusi.
---
Rais Vladimir Putin amemtuhumu Mmiliki wa Jeshi Binafsi la Wagner, Yevgeny Prigozhin, juu ya jaribio la mapinduzi dhidi ya Majeshi ya Urusi baada ya Wagner kudai Serikali inahusika na mauaji ya Wapiganaji wa Wagner

Kwa mujibu wa ABCNews, Rais Putin amejulishwa rasmi kuwa Vikosi vya Wagner vimetangaza kuuteka Mji wa Rostov-on-Don pamoja na kushikilia kambi zote za Majeshi ya Urusi zilizopo eneo hilo

Kupitia taarifa ya Video, Prigozhin amekaririwa akiitaka Ikulu ya Urusi (Kremlin) kumkabidhi kwake Mkuu wa Vikosi vya Kijeshi vya Urusi vinginevyo wataingia Jijini #Moscow na kufanya mashambulizi kwa yeyote anayewaingilia

Ikumbukwe Russia na Wagner Group walikuwa na makubaliano ya ushirika katika Vita dhidi ya Ukraine ambapo Wagner walikuwa msaada mkubwa kwa Serikali ya Rais Putin tangu kuanza kwa Vita hiyo.
Ndiyo maana wajomba walikua wanalalamika kunyimwa silaha.. kumbe walikua na lengo lao huenda walikua wanapewa silaha wanapeleka geto
 
Mrusi wa Block E, Kigamboni Yericko Nyerere anasema

Mvutano wa muda mrefu kati ya Waziri wa Ulinzi wa Urusi na Mkuu wa Wagner PMC ulichukua sura nyingine 23/6/2023 pale kiongozi wa Wagner Yevgen Prigozhin alipotangaza kutotii amri ya Wizara ya Ulinzi akisisitiza ni wakati sasa wakubadili safu za uongozi wa jeshi. Tangazo hilo lilifuata baada ya muda mrefu tangu Wagner PMC imalize Oparesheni kule Bakhmut ambapo imekuwa ikinyimwa tenda huku Wizara ya Ulinzi ikiwapatia Akhmat kikosi cha Chechinia kilicho chini ya Ramzan Kadryov. Wagner wanalalamika kuwa Waziri wa Ulinzi wa Urusi Jenerali Shoigu hawapendi anaona wanafaidika sana wakifanikiwa misheni wanazopewa, na kwamba kule Bakhmut aliwahujumu sana kwakuchelewesha kuwapatia silaha hali iliyofanya mji ule kukombolewa kwa gharama kubwa ya damu ya mamluki wengi.

Tangu Wagner wamalize kazi kule Bakhmut, Kiongozi wao Yevgen amekuwa akifuatilia mkataba mwingine bila mafanikio, na hivi karibuni tarehe 18/6/2023 alipewa mkataba ambao atatakiwa kuanza kazi mwezi wa 8, 2023 hali iliyomkwaza akitoa sababu kwamba jeshi lake la watu zaidi ya 30,000 walio katika ajira rasmi na vibarua zaidi ya 50,000 wako tu wanasubiri kazi, huku akishuhudia Ukraine ikianzisha mashambulizi katika milki ya Urusi. Hilo anaona kama ni dharau kubwa kwake. Alianza ukosozi wa kijeshi, ambapo Mkuu huyo wa Wagner tarehe 20/6/2023 alisema Jeshi na waziri wa Ulizi wa urusi wanamdanganya Rais juu ya maendeleo ya Oparesheni ya Urusi,

Tangazo hili la Yevgen Prigozhin lilikuwa kama uasi dhidi ya Jeshi, ambapo Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilifungua kesi ya jinai dhidi ya mkuu wa Wagner PMC, Yevgeny Prigozhin, Kamati ya Kitaifa ya Kupambana na Ugaidi (NAC) iliripoti. Kwamjibu wa sheria ya Jinai ya Urusi kuna kifungu cha 279 "Uasi wa Silaha", inasema: "Kupanga uasi wa kutumia silaha au kushiriki kikamilifu ndani yake kwa madhumuni ya kupindua au kubadilisha kwa nguvu utaratibu wa kikatiba wa Shirikisho la Urusi au kukiuka uadilifu wa eneo la Shirikisho la Urusi, mtu/watu hao wataadhibiwa kwa kifungo jela cha miaka 12 hadi 20 na kizuizi cha uhuru kwa muda wa hadi miaka miwili."

Idara hiyo ilisisitiza kuwa madai yote yaliyoenezwa kwa niaba ya mwanzilishi huyo wa Wagner hayana msingi. wowote. Wizara ya Ulinzi iliripoti kwamba habari iliyochapishwa na Yevgeny Prigozhin kuhusu "mgomo" kwenye kambi za nyuma za kikundi cha Wagner sio kweli. Wizara ilizitaja tuhuma hizo kuwa ni uchochezi. Pia walibaini kuwa wanajeshi wa Urusi wanaendelea kutekeleza misheni ya mapigano kwenye mstari wa ulinzi katika eneo la operesheni maalum. Msemaji wa Ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov alisema kuwa, Rais Putin anafahamu kwa karibu hali inayoendelea ya Mkuu wa Wagner Yevgen Prigozhin na Waziri wa Ulinzi Shoigu, hatua zote muhimu zinachukuliwa. Asubuhi ya 24/6/2023 kundi la Wagner lilirusha Video iliyonyesha Mkuu wa Wagner Yevgeny Prigozhin akikutana na Kanali Jenerali Yunus-Bek, Naibu Waziri wa Ulinzi wa Wilaya ya Kijeshi ya Kusini ya jeshi la Urusi huko Rostov wakizungumza. Prigozhin aliripotiwa kufanya mazungumzo na Yunus-Bek. Hili halikuthibitishwa na Wuzara ya Ulinzi ya Urusi.

Rais Putin wa Urusi alizungumza na vyombo vya habari asubihi ya tarehe 24/6/2023 kuelezea na kufafanua kilichojiri 23/6/2023. Putin alianza kwakusema kwamba usiku alizungumza na makamanda wa pande zote: askari wanapigana kishujaa. Putin aliendelea kusema, "Ninatoa wito kwa Warusi, jeshi na vyombo vya kutekeleza sheria na kwa wale ambao walisukumwa kwenye njia ya uasi wa kutumia silaha kwa udanganyifu na vitisho kuzingatia umoja, uimarishaji na uwajibikaji".

Akaendelea kusema, "Migogoro yoyote inapaswa kutupiliwa mbali wakati wa operesheni maalumu, hatima ya watu wetu sasa inaamuliwa", Putin aliita vitendo vya kugawanya umoja ni ukengeufu. Akasema, "Tunachokabiliana nacho ni usaliti, Viongozi hawataruhusu mgawanyiko nchini Urusi ujirudie, tutalinda watu, Kila mtu ambaye alianza kwa makusudi njia ya usaliti atapata adhabu isiyoepukika, Vikosi vya jeshi vitapokea maagizo yanayofaa, Hatua zitachukuliwa ili kuleta utulivu huko Rostov-on-Don, wanajeshi walipokea amri ya kudhibiti viongozi wa uasi.

Kwa upande mwingine, Oparesheni ya ulinzi wa maeneo yaliyotwaliwa na Urusi iliendelea chini ya vikosi vya Akhmat, Vikosi vya Urusi vimekikomboa kijiji cha Sinkovka katika Mkoa wa Kharkov na sasa vinapigana huko Petropavlovka. Wapiganaji wa Urusi wanasonga mbele kwenye viunga vya jiji la Kupyansk, na kutengeneza daraja la shambulio dhidi ya jiji hilo. Hii inaweza kuwa hasara kubwa kwa Ukraine katika mkesha wa mkutano wa kilele wa NATO, ndiyo maana jeshi la Ukraine lilianza haraka kuhamisha akiba kuelekea Kupyansk kutumia katika kile kinachoitwa 'kukabiliana na mashambulizi'. Na Vikosi vya Anga vya Urusi viliendelea na mashambulizi ndani ya Jiji la Kyiv na mikoa mingine likilenga kambi za kijeshi na miundombinu ya kijeshi, maghala ya silaha za kimagharibi nk.

Kwa undani zaidi utapata katika kitabu kipya cha MOSCOW: Oparesheni Ukraine kinachokujia hivi karibuni.

Na Yericko Nyerere
 
Back
Top Bottom