Rwanda imeweza kutangaza Utalii kwenye klabu kubwa za Ulaya (Arsenal na Bayern). Tanzania inakwama wapi?

Rwanda imeweza kutangaza Utalii kwenye klabu kubwa za Ulaya (Arsenal na Bayern). Tanzania inakwama wapi?

kinachohitajika sasahivi hapa ni njia nafuu ya kuitangaza nchi tu. viwanja vipo. kuna DSM, hii inahudumia pia na zanzibar, kuna Kilimanjaro ambako madege makubwa yeyote yanatua na hii ni kwa ajili ya utalii wa mlima kilimanjaro, mbuga zilizoko arusha na Manyara hadi serengeti. mbeya uwanja tayari upo kwa ajili ya kuhudumia Ruaha national park kwa kuingilia mlango wa mbarari. mwanza hakuna utalii wowote wa kuhangaisha pesa yetu, labda kama tukiwekeza miundombinu/recreation ziwani, michezo ya ziwani, mashindano ya boat na mitumbwi n.k ila kuna wasukuma walishakula wanyama wooote. hata wale walioko kisiwa cha Lubondo wapo hatarini kuliwa na wasukuma.
Asee nimecheka kama sio mimi 😀 wasukuma wamekuwaje tena
 
Asee nimecheka kama sio mimi 😀 wasukuma wamekuwaje tena
Unajua jamaa anautani sana! Ila mi nijuavyo kuna watu wengi sana hawapendi kuona maendeleo ya mikoa ya wasukuma! Ila ukienda unawashuhudia jamaa wanaendelea tu na hawana neno na mtu!
 
Na kwenye conference kwa sasa Kigali inaipiga bao Arusha kwa sasa nuchi ya Rwanda inaupromote sana mji wao wa kigali!
Saizi Fly Emirates wanabase yao Kigali!
Ndo maana mwaka jana uliona Ifantino wa FIFA alifanyia mkutano hapo!
Kagame ni big brain na innovation anayo ya kutosha Sie tunafanya mambo locally sana!
Sana yan viongozi wetu wana akili ya miaka 10 ya nyuma ndo inawaongoza
 
Tanzania pia ili upate watalii wengi lazima iwe na viwanja vya ndege vya kimataifa kama Mbeya na Mwanza kwa kuwa utalii pia huchochewa na biashara! Miji hiyo niliyotaja ikiwekewa mazingira hayo lazima impact itaongezeka sana!
NAKAZIA
 
NAKAZIAUlishawahi kujiuliza migodi
Ulishawahi kujiuliza wafanyakazi wa migodi na wafanya biashara wa madini na watu wa kawaida wakipata uwanja wa Ndege Mwanza itakuwaje? Diaspora anatoka Ulaya anakuja Mwanza au Kagera hashuki tena Dar anakuja direct Mwanza! Mzunguko wa biashara utakuwa mkubwa sana na Flight za Mwanza Dubai zitakuwepo maana wafanya biashara wa miji ya Mwanza,Katoro,Kahama ,Musoma ,kigoma na Bukoba hawataenda tena kupanda ndeg Dar!
 
kinachohitajika sasahivi hapa ni njia nafuu ya kuitangaza nchi tu. viwanja vipo. kuna DSM, hii inahudumia pia na zanzibar, kuna Kilimanjaro ambako madege makubwa yeyote yanatua na hii ni kwa ajili ya utalii wa mlima kilimanjaro, mbuga zilizoko arusha na Manyara hadi serengeti. mbeya uwanja tayari upo kwa ajili ya kuhudumia Ruaha national park kwa kuingilia mlango wa mbarari. mwanza hakuna utalii wowote wa kuhangaisha pesa yetu, labda kama tukiwekeza miundombinu/recreation ziwani, michezo ya ziwani, mashindano ya boat na mitumbwi n.k ila kuna wasukuma walishakula wanyama wooote. hata wale walioko kisiwa cha Lubondo wapo hatarini kuliwa na wasukuma.
Mwanza utalii upo mkuu kwano Kutoka Mwanza kwenda Serengeti National Park in kilometa 100 tu wakati kutoka KIA kwenda Serengeti ni zaidi ya kilometa 300 issue hapo utalii wa Serengeti, Ngorongoro, Manyara na Tarangire upo centralized Arusha na tumekaririshwa hivyo mpaka unakuta mtu yupo Shinyanga kama anataka kwenda Serengeti kama hafahamu vizuri anajikuta anaenda Arusha kumbe alitakiwa kupasua hapo Bariadi to Lamadi ndani ya masaa 2 yupo Geti la Ndabaka)

Kumbe unaweza piga kotekote yaani MTU anashuka KIA ataingia Tarangire, Manyara, Ngorongoro akifika Serengeti anaweza akatokezea Mwanza akarudi Dar au akaendelea na destination zingine za utalii hence anakuwa ameokoa muda na nguvu vivyo hivyo akishuka Mwanza akiingia Serengeti akifika Ngorongoro anaingia Karatu, Manyara, Tarangire na kuondokeq Arusha Airport au KIA (Ni issue ya Bodi ya Utalii na wadau wake kuweka sawa kwenye routes na namna ya ku-promote yaani kama Kenya wanavyofanya mtalii anaingia kwao alafu anapewa routes ya Kilimanjaro akifika mpakani ndo anagundua anaingia nchi nyingine lakini wao wameshamwambia ukifika Kenya utaona Mlima Kilimanjaro)
 
Rwanda cha kutalii kule labda yale mafuvu na mifupa kwa wazungu washamba a.k.a walugaluga wa ulaya.
 
Ulishawahi kujiuliza wafanyakazi wa migodi na wafanya biashara wa madini na watu wa kawaida wakipata uwanja wa Ndege Mwanza itakuwaje? Diaspora anatoka Ulaya anakuja Mwanza au Kagera hashuki tena Dar anakuja direct Mwanza! Mzunguko wa biashara utakuwa mkubwa sana na Flight za Mwanza Dubai zitakuwepo maana wafanya biashara wa miji ya Mwanza,Katoro,Kahama ,Musoma ,kigoma na Bukoba hawataenda tena kupanda ndeg Dar!
nje ya mada kdg Hiv serikali huwa wanapitiaga kwenye mitandao kuangalia wananchi wake wanasemaje
 
wewe hata hueleweki hata unachoongea. social media kwa dunia ya ulimwengu wa kwanza ndio inafikia mamilioni wengi kwa uhakika kuliko television. pia kama hauelewi ndio option yenye bei nafuu zaidi. hata hiyo mipira wanatangazia mwisho wa siku clips zinasambazwa kwenye mitandao na watu wanaionea huko na kwenye mitandao clip inakaa muda mrefu zaidi, mtu anaweza kuidownload na kuwa nayo kuiona mara kadhaa. peng'a kamasi hizo mkuu zimesambaa hadi kwenye ubongo wako.
Kagame angeishia YouTube tu na si arsenal na Bayern..watalii Kuna sehemu wanapatikana siyo kila sehemu,kuja kutalii kunahitaji hela siyo bando la youtube
 
kwahiyo tuseme kweli Rwanda kuna watalii wameenda kutokana na matangazo hayo? kwenda kuona nini? wanawake?
Kuona sokwe wa milimani na makumbusho ya kilichotokea mwaka 1994
 
Hii haijakaa sawa au ndio tuseme Rwanda inatuzid nini. Hivi Rwanda kuna nini cha kuangalia. Embu tuambieni au ndio hao sokwe? Haya matangazo sielewi elew.
 
Hii haijakaa sawa au ndio tuseme rwanda inatuzid nn. Hivi rwanda kuna nini chakuangalia. Embu tuambieni au ndio hao sokwe?? Haya matangazo sielewi elew
Tembelea upagawe na mizimu ya watu waliouliwa kikatili na mauaji ya kimbali! Ukitembelea unasaidia kuipunguza maana ukiondoka unaondoka nayo ukapambane nayo makwenu!
 
Tanzania hatujazoea, vikifanyika tunaenda kuhoji gharama bila kujali kutangaza kimataifa ni gharama tofauti na tulizozoea hapa nchini. Kuna kipindi tulitangaza CNN, lile jambo lilifika bungeni..
 
Back
Top Bottom