Rwanda katuzidi wapi kwenye kutangaza utalii?

Rwanda katuzidi wapi kwenye kutangaza utalii?

IMG_6349.jpg
 
Warwanda wametuzidi akili mazingira yao ni mabovu ndio maana akili zinachaji ili wapate pesa sisi tupo busy kufikiri mpesa itajenga bara bara wakati tuna vyanzo vingi vya kupata pesa kupitia wageni huyo Spika hajui chanzo anaamini katika ongezeko la makato kwa Wananchi ndio wao watapata magari wanakera kweli hawa watu..
 
Huyu ni Lionel Messi wakati akiwa anawasili kwenye viunga vya Paris Saint Germain (PSG).

Hii video imepostiwa kwenye official page ya PSG yenye mamillion ya followers, video hii hii imetazamwa na wapenzi wa kandanda wengi sana duniani na media kubwa duniani za football kama skysport,bt, supersport n.k wame repost hii video.

Kilichonivutia ni hilo neno hapo nyuma kwenye jezi ya MESSI.

Hakuna jina lake wala maandishi mengine zaidi ya VISIT RWANDA.

Nimewaza sana hivi RWANDA kuna kivutio gani kikubwa cha kushawishi hadi waende kuitangaza kwenye jezi ya club kubwa namna hii kwenye mgongo wa mtu maarufu hivi ulimwenguni.Wanavitu gani ambavyo Tanzania hatuna hadi waende kufanya promo kubwa kama hii?

Hapo nikakumbuka ile kauli ya Yericko Nyerere kuwa wenzetu wamewekeza kwenye ujajusi wa KIUCHUMI sisi tumewekeza kwenye ujajusi wa kumkamata mbowe na wafuasi wa Chadema.

Peter Msigwa aliwahi kusema kuliko kuwachukua kundi kuuubwaa la kina pierre liquid,babalevo,manara,steve nyerere nk watu ambao ni maarufu ndani ya Tanzania tu eti unaenda kufanya nao promo ya kuutangaza mlima Kilimanjaro kwa kupanda ule mlima,ni bora kuleta watu maarufu wachache duniani waje kuupanda bure au kwa bei nafuu zaidi, wetu wenye ushawishi kubwa kwenye soka,music au tasnia nyingine pendwa sana duniani.

Watu kama kina Messi, CR7, Tiger Woods, Maria Sharapova, Drake n.k watu ambao wakija Tanzania dunia itaangalia wamekuja kufanya nini na ulimwenguni utakuwa na attention kwa kiasi fulani.

Wanyarwanda wametuzidi wapi aisee? Ile nchi na mkoa wa kagea ni kama sawa tu, ila wapo intelligent sana kuliko sisi.Wapi tunafeli au intelligence yetu ndio ina shauri kuweka Tozo ili kupata hela na sio kutangaza utalii kama Rwanda?

#Nawaza Tu.

Didas TumainiView attachment 1888379
Apa Tanzania sidhani kama Kuna kiongozi mwenye hakili ya kufikiria mambo ya muhimu zaidi ya kupiga makofi na vigelegele kwenye maswala ya kipuuzi kusema kweli!! Labda itokee Rais ndo kaamua kufanya ivo ndo watapaiga makofi na kusapot itokee ila viongozi wengine ni wapuuzi tu.
 
Warwanda wametuzidi akili mazingira yao ni mabovu ndio maana akili zinachaji ili wapate pesa sisi tupo busy kufikiri mpesa itajenga bara bara wakati tuna vyanzo vingi vya kupata pesa kupitia wageni huyo Spika hajui chanzo anaamini katika ongezeko la makato kwa Wananchi ndio wao watapata magari wanakera kweli hawa watu..
Apa Tanzania sidhani kama Kuna kiongozi mwenye hakili ya kufikiria mambo ya muhimu zaidi ya kupiga makofi na vigelegele kwenye maswala ya kipuuzi kusema kweli!! Labda itokee Rais ndo kaamua kufanya ivo ndo watapaiga makofi na kusapot itokee ila viongozi wengine ni wapuuzi tu.
Viongozi wetu wanachaguliwa sio kwa kuangalia uwezo bali ukada wa chama! Leo hii una kiongozi kama sabaya au msukuma au makonda unatarajia nini?
 
Viongozi wetu wanachaguliwa sio kwa kuangalia uwezo bali ukada wa chama! Leo hii una kiongozi kama sabaya au msukuma au makonda unatarajia nini?
Bungeni kwenyewe wamejaa CCM kazi yao ni kuwaza posho tu na kupiga makofi ilo wazo la kutangaza utaliii wanatoa wapi Sana Sana akitokea wa kutoa hiyo hoja Lazima watamfata after break kwajili ya kumuuliza ujasiri huo kautoa wapi!!!
 
Viongozi wetu wanachaguliwa sio kwa kuangalia uwezo bali ukada wa chama! Leo hii una kiongozi kama sabaya au msukuma au makonda unatarajia nini?
Nchi yao tu hii imewashinda Kuna shule moja uko Bush flani walimu wawili wanafundisha darasa moja kwa kuwa Kuna uhaba wa madarasa Leo hii waje kueka pesa kwenye kutangaza utaliii aiseh bongo bado Sana!!!
 
Nchi yao tu hii imewashinda Kuna shule moja uko Bush flani walimu wawili wanafundisha darasa moja kwa kuwa Kuna uhaba wa madarasa Leo hii waje kueka pesa kwenye kutangaza utaliii aiseh bongo bado Sana!!!
Lkn hela za kununua ma viete wanazo mkuu.
 
Kuweka matangazo ya visitings pasipo cha kwenda kuona ni utapeli.
kwa watalii.

Akienda, na atakachokikuta ni vitu viwili contrary kabisa na hatarudi.

Ukitangaza mlima k'njaro upo kenya huku ukijua sikweli, na mtalii kaja na asiukute ni kutafuta kuharibikiwa.

sasa subr tuone kwanza outcome ya mess kuvaa kit yenye maneno ''visit Rwanda''

Nachojua hata serikali ingegharimika kuwaleta macelebrity wa nje bado gharama zingelalamikiwa tu na baadh yetu.

Wangesema serikali imewaleta beyonce, jayz na bekham (mfano) wakati watoto hawana vyumba vya madarasa.

Mkataba wa Rwanda na Arsenal juu ya kuitangaza Rwanda kiutalii, uliigharimu Rwanda paundi milion 60
na hapo ni matangazo ya kwenye soksi na kwny pindo tu.

mnakumbuka jinsi vyombo vya habari vya uingereza vilivyopga kelele kushangaa uamuzi wa serikali ya rwanda kutumia mabilion kuipa arsenal wakt nchi yao ingali maskn
Sisi tuna Tv channel yetu ya Tanzania Safari Channel inayotangaza vivutio vyetu vya Utalii dunia nzima.
 
Back
Top Bottom