Nyie mnaotumia chuki zenu dhidi ya Tutsi hamjui mnachoongea. Kwa taarifa yenu adui wakubwa wa Kagame ni Tutsi wenzake. Hutu sio tatizo sana ila fellow Tutsi ndio hasa Kagame anawahofia. Hili suala la vijana 18 wa Kirundi kudai kupewa mafunzo ya kijeshi halina mantiki. Nchi haipinduliwi kirahisi namna hiyo. Vile vile huwezi iamini BBC kwa kuwa ni chombo kilichobobea kwa kupiga tarumbeta kueneza propaganda hasi dhidi ya kiongozi au uongozi wowote usiowapendeza. BBC na serikali ya uingereza hawampendi Kagame kama walivyomchukia na kujaribu kumchafua Mugabe. Tujaribu kutenganisha pumba na mchele. Suala la Rwanda si u-Tutsi au u-Hutu bali ni kushika dola. Chuki za kikabila zipo za chini chini ila adui ni wa karibu kwa Kagame zaidi.