Chukwu emeka
JF-Expert Member
- Jan 12, 2018
- 24,314
- 38,919
Rwanda imeingia mkataba wa poundi takribani milioni 150 ili ipokee wakimbizi haramu watakaodakwa nchini UK.
Mpango aina hii muasisi ni Macron wa France. Yéyé aliingia mkataba na Libya. Pamoja na kuhamishiwa wakimbizi haramu Toka France Kwenda Libya mkataba wao pia unaitaka mamlaka ya Libya kuzuia wanapenda Libya ili waende France.
Mkataba huu umesababisha haya:
1. Kuongezeka kwa wahuni wanaosafirisha binadamu (human traffickers). Libya inalipwa kulingana na wingi wa wahamiaji haramu wanaorejeshwa Libya. Sasa kinachofanyika ni kuhakikisha wahamiaji haramu wengi wanaenda France Ili wakamatwe ili malipo yawe endelevu. Ni akili ya Biashara. Kama utalipwa kwa idadi ya mbuzi wanaokamatwa wakila mazao si utahakikisha mbuzi wengi zaidi wanakula mazao? Hutataka mbuzi waache kula mazao! Kuna Kila dalili Inasemekana mamlaka za Libya zinashiriki biashara hii. Zimefungua makambi ya kuhifadhi wakimbizi wapya na wanaodakwa France. Yaani biashara ya binadamu imefanywa halali na wanaodai wanajali haki za binadamu.
2. Libya kuna mamlaka zaidi ya 2. Japo Moja ndioo inatambuliwa na EU zote zimeona hii ni njia mojawapo ya kujipatia kipato cha kuendesha harakati.
3. Makambi yalioanzishwa kwa gharama za France yamegeuka mateso haswaa kwa watu weusi. Awali haikuruhusiwa kujenga makambi ya kuhifadhi binadamu. Sasa yanajengwa kwa héla ya France. Wati wanateswa! Hâta mtu alitaka mkazi wa ndani au kibarua anapenda "kumnunua" hapo!
4. Makambi haya yanaendeleza ubaguzi. Yapo ya wa gredi A (wahindi, waarabu, wazungu, walatino) na yapo ya gredi B (watu weusi). Yote huduma mbovu lakini ya waafrika weusi ndioo balaa haswaa. Kubakwa, kulawitiwa, kupigwa, kunyipwa chakula'). Dunia unaona lakini Iko kimya. Umoja wa Afrika unajua lakini nao haujafanya lolote la maana zaidi ya kukemea. Hakuna tena kina Nyerere, Kaunda, Mandela!
Sasa jirani na mwanachama mwenzetu wa EAC na AU kachukua héla naye apokee wakimbizi haramu Toka UK! Na huenda hatahojiwa! Hii kusema ukweli ni Biashara haramu na bidhaa ni binadamu!
Halafu mkataba huu una kipengele cha ajabu. Hâta ombi la kupewa ukimbizi UK likikubaliwa bado utapelekwa Rwanda na utahesabika uko UK!
Je sisi kama majirani wa Rwanda hatutaathirika? Fikiria mhindi wa Bangladesh aliyezamia UK aletwe Kigali? Hatatamani aende Dar au Nairobi kwenye wahindi?
Tumuulizeni Kagame kwa nini héla imemtoa utu kiasi hiki?
Hebu Fikiria kijana kutokea Pemba azamie London halafu adakwe apelekwe Rwanda? Si kichekesho? Saa ingine wazungu wanavaa suti lakini akili kolo!
Miaka 4 iliyopita Uholanzi ilianzisha mpango ukiitwa "a taxi for a returnee"! Ulianza kwa kuwalenga wazamiaji toka Ghana. Yaani Ukiwa Uholanzi ukikubali kupewa "taxi" urudishwe Ghana kuanzia biashara ya taxi ili usitamani Kwenda Uholanzi. Tukawaambia "mnajaza gunia upepo" wakadharau. Matokeo: waghana wakaambizana "twendeni uholanzi tukachukue taxi za bure". MTU anarudi Accra anaenda ubalozi wa Uholanzi anapewa taxi mpyaaa. Anampa ndugu yéyé anarudi Uholanzi au anawezesha NDUGU waende uholanzi. Waholanzi wakastuka! Wakimbizi ndioo wanamiminika tena wengine ni ambao walirudi n'a kupewa taxi. Wameanza "upyaaaaaaa" kama bwege!
Rwanda itashangaa imepokea wakenya, waganda, wazambia, warundi, wakongo, wanaija, wahindi, waarabu, n.k. Itaweza au itatusababishia matatizo EAC?
Au na Tanzania tuingie mkataba kama huu na Belgium, Canada, US na Finland ? Waletwe😄😂
CC Yahya Msangi
Mpango aina hii muasisi ni Macron wa France. Yéyé aliingia mkataba na Libya. Pamoja na kuhamishiwa wakimbizi haramu Toka France Kwenda Libya mkataba wao pia unaitaka mamlaka ya Libya kuzuia wanapenda Libya ili waende France.
Mkataba huu umesababisha haya:
1. Kuongezeka kwa wahuni wanaosafirisha binadamu (human traffickers). Libya inalipwa kulingana na wingi wa wahamiaji haramu wanaorejeshwa Libya. Sasa kinachofanyika ni kuhakikisha wahamiaji haramu wengi wanaenda France Ili wakamatwe ili malipo yawe endelevu. Ni akili ya Biashara. Kama utalipwa kwa idadi ya mbuzi wanaokamatwa wakila mazao si utahakikisha mbuzi wengi zaidi wanakula mazao? Hutataka mbuzi waache kula mazao! Kuna Kila dalili Inasemekana mamlaka za Libya zinashiriki biashara hii. Zimefungua makambi ya kuhifadhi wakimbizi wapya na wanaodakwa France. Yaani biashara ya binadamu imefanywa halali na wanaodai wanajali haki za binadamu.
2. Libya kuna mamlaka zaidi ya 2. Japo Moja ndioo inatambuliwa na EU zote zimeona hii ni njia mojawapo ya kujipatia kipato cha kuendesha harakati.
3. Makambi yalioanzishwa kwa gharama za France yamegeuka mateso haswaa kwa watu weusi. Awali haikuruhusiwa kujenga makambi ya kuhifadhi binadamu. Sasa yanajengwa kwa héla ya France. Wati wanateswa! Hâta mtu alitaka mkazi wa ndani au kibarua anapenda "kumnunua" hapo!
4. Makambi haya yanaendeleza ubaguzi. Yapo ya wa gredi A (wahindi, waarabu, wazungu, walatino) na yapo ya gredi B (watu weusi). Yote huduma mbovu lakini ya waafrika weusi ndioo balaa haswaa. Kubakwa, kulawitiwa, kupigwa, kunyipwa chakula'). Dunia unaona lakini Iko kimya. Umoja wa Afrika unajua lakini nao haujafanya lolote la maana zaidi ya kukemea. Hakuna tena kina Nyerere, Kaunda, Mandela!
Sasa jirani na mwanachama mwenzetu wa EAC na AU kachukua héla naye apokee wakimbizi haramu Toka UK! Na huenda hatahojiwa! Hii kusema ukweli ni Biashara haramu na bidhaa ni binadamu!
Halafu mkataba huu una kipengele cha ajabu. Hâta ombi la kupewa ukimbizi UK likikubaliwa bado utapelekwa Rwanda na utahesabika uko UK!
Je sisi kama majirani wa Rwanda hatutaathirika? Fikiria mhindi wa Bangladesh aliyezamia UK aletwe Kigali? Hatatamani aende Dar au Nairobi kwenye wahindi?
Tumuulizeni Kagame kwa nini héla imemtoa utu kiasi hiki?
Hebu Fikiria kijana kutokea Pemba azamie London halafu adakwe apelekwe Rwanda? Si kichekesho? Saa ingine wazungu wanavaa suti lakini akili kolo!
Miaka 4 iliyopita Uholanzi ilianzisha mpango ukiitwa "a taxi for a returnee"! Ulianza kwa kuwalenga wazamiaji toka Ghana. Yaani Ukiwa Uholanzi ukikubali kupewa "taxi" urudishwe Ghana kuanzia biashara ya taxi ili usitamani Kwenda Uholanzi. Tukawaambia "mnajaza gunia upepo" wakadharau. Matokeo: waghana wakaambizana "twendeni uholanzi tukachukue taxi za bure". MTU anarudi Accra anaenda ubalozi wa Uholanzi anapewa taxi mpyaaa. Anampa ndugu yéyé anarudi Uholanzi au anawezesha NDUGU waende uholanzi. Waholanzi wakastuka! Wakimbizi ndioo wanamiminika tena wengine ni ambao walirudi n'a kupewa taxi. Wameanza "upyaaaaaaa" kama bwege!
Rwanda itashangaa imepokea wakenya, waganda, wazambia, warundi, wakongo, wanaija, wahindi, waarabu, n.k. Itaweza au itatusababishia matatizo EAC?
Au na Tanzania tuingie mkataba kama huu na Belgium, Canada, US na Finland ? Waletwe😄😂
CC Yahya Msangi