Rwanda yakana mpango wake wa siri wa kuigawa Congo DRC kwa kunyakua eneo la Mashariki

Rwanda yakana mpango wake wa siri wa kuigawa Congo DRC kwa kunyakua eneo la Mashariki

Freed Freed

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2017
Posts
6,547
Reaction score
7,167
Habari JF.

Waziri mkuu wa zamani wa Congo Matata Mponyo na kiongozi moja wa kanisa, wamedai kwa nyakati tofauti kuwa Rais Kagame anataka kuipanua Rwanda. Mpango huo wa Kagame ni kushinikiza utawala wa majimbo nchini Congo na baadae kuliingilia jimbo moja kwa kuliomba kupiga kura ya kujitenga na kujiunga na Rwanda.

Jimbo hilo ni maeneo ya Mashariki yakijumuisha Kivu kusini na kaskazini. Eneo hili lina Watusi wengi ambao ni kabila la Kagame na pia kuna raslimali nyingi kama madini, misitu, uvuvi, udongo wenye rutuba, wanyama pori nk.

Viongozi hao wawili pia wamedai vita vya Mashariki ya Congo vinachangiwa na Kagame kufanikisha mpango wake Ovu. Pia wanadai Kagame ametumia vikundi vya uasi ambavyo vimetafuta muafaka kwa kuandikishwa jeshini na vina mpango wa kuasi baadae kwa kudai taifa lao huru la KIVU.

Waziri wa nchi za nje wa Rwanda Leo ameitisha mkutano wa dharura na wanahabari wa kimataifa na wa ndani na kuwashutumu viongozi hao wa Congo kwa uchonganishi. Amesema Rwanda inataka kuona maelewano mazuri baina ya jirani zake wote ikiwepo Congo. Anedai pia maridhiano na Uganda yanaendelea na yamefika pazuri. Amesema Congo ni rafiki mzuri wa Rwanda na angependa uhusiano huo mzuri udumu na usivurugwe kwa kauli hizi tata.

NB: Jamhuri hiyo itaitwa RWAKI kwa maana ya Rwanda na Kivu.
 
Hivi Kagame kajitolea maisha yake kwa Rwanda inawezekana akawa bonge la mzalendo kama alivyo yule mzee aliyejenga international airport chato
 
Huo mpango (kama bado upo) kwa dunia ya sasa inawezekana kutekelezwa?

Je raia wa Drc wanaoishi huko Kivu wako tayari kuwa sehemu ya Rwanda?

Je makundi ya waasi huko Kivu ikiwemo Maimai, FDLR (waasi kutoka Rwanda) wako tayari kwa hilo?
 
Fdlr hili ni kundi la wabakaji
Maimai hawana dira

Asilimia kubwa ya wakazi wa kivu ni watusi(wengi wapo hapo kimkakati)
Huo mpango (kama bado upo) kwa dunia ya sasa inawezekana kutekelezwa?

Je raia wa Drc wanaoishi huko Kivu wako tayari kuwa sehemu ya Rwanda?

Je makundi ya waasi huko Kivu ikiwemo Maimai, FDLR (waasi kutoka Rwanda) wako tayari kwa hilo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huo mpango (kama bado upo) kwa dunia ya sasa inawezekana kutekelezwa?

Je raia wa Drc wanaoishi huko Kivu wako tayari kuwa sehemu ya Rwanda?

Je makundi ya waasi huko Kivu ikiwemo Maimai, FDLR (waasi kutoka Rwanda) wako tayari kwa hilo?
Raia wengi wa kivu kaskazin na kusini ni wahutu na watutsi
 
Kagame anapiga congo muda wowote akitaka,congo na burundi hawanajeshi imara.
Kagame kama angekua mbabe kweli angejaribu kujibu mapigo wakati mzee wa msoga.

Sent using Jamii Forums mobile app
jeshi la burundi si ndyo hilo lilifukuza waasi mkoani cibitoke waliokua wameandaliwa na kagame waliozima zoezi la mapinduzi 2015 ,kifupi kagame hawezi ingia vitani na burundi atakua amefungua mlango wa chumbani anako lala ,afanye hayo DRC kichwa cha mwendawazimu
 
Jirani gan mwenye uwezo wa kumzuia PK kijeshi ndani ya congo asilima kubwa ya askari wa congo ni watiifu kwa PK

Sent using Jamii Forums mobile app
ili afanikishe azma hyo paka itamlazimu awaue wa congo wote awamalize maana hata mtoto wa congo ambaye yuko tumboni hajazaliwa anajua kagame ndye mtesi wao ,rejea maneno ya msaani koffi olomide majuzi kuhusu rwanda
 
Back
Top Bottom