Rwanda yaondoa Majeshi yake DRC baada ya tishio la SA

Hiyo barua ni ya kuondoa majeshi ya Rwanda yaliyopo ndani ya Rwanda sehemu za mipakani yarudi mjini.

Ulichoandika kwamba majeshi yarudi jutoka Congo hakipo katika hiyo barua.

Kagame kwanza wala hajakubali kwamba Rwanda ina majeshi Congo.
Hiyo ni lugha ya kutokubali kuwa majeshi yapo Congo ila mipakani so ukweli wanaujua wa Rwanda.
 
Hiyo ni lugha ya kutokubali kuwa majeshi yapo Congo ila mipakani so ukweli wanaujua wa Rwanda.
Nilijua tu mtasema hivi.

Lakini hapa tunajadili kilichoandikwa kwenye barua, si kuagua kitu ambacho hakijaandikwa kwenye barua ambacho kinaweza kuwa kimemaanishwa na barua.

Mtoa mada alivyoandika ni kama vile barua imeandika wanajeshi wa Rwanda walio Congo warudi Rwanda.

Barua haijaandika hivyo.
 
Hiyo barua ni ya kuondoa majeshi ya Rwanda yaliyopo ndani ya Rwanda sehemu za mipakani yarudi mjini.

Ulichoandika kwamba majeshi yarudi jutoka Congo hakipo katika hiyo barua.

Kagame kwanza wala hajakubali kwamba Rwanda ina majeshi Congo.
Mwizi tuko lini akakiri kosa lake, hata Marehemu JK , kuna vitu vya kisiasa au kijeshi vinawekwa kama Kagame alivyoweka
 
Hakuna nchi ambayo inaandika kukiri makosa yake .
 
Mwizi tuko lini akakiri kosa lake, hata Marehemu JK , kuna vitu vya kisiasa au kijeshi vinawekwa kama Kagame alivyoweka
Sawa mwizi labda hakiri kosa lake lakini usiseme amekiri wakati hajakiri.

Umeelewa hoja?
 
Mkuu watu wanapenda upotoshaji ndio maana barua imeandikwa vingine na wachangiaji wanajadili mengine.
 
Navy seals ni nani na wangepitia wapi kufika Rwanda.
Hata hivyo uamuzi wa Kagame ni wa busara kwani nchi yake iko mbioni kuvurugwa kwa uzembe wake kama ilivyotokea kule Ukraine.
 
Sawa mwizi labda hakiri kosa lake lakini usiseme amekiri wakati hajakiri.

Umeelewa hoja?
Shillingi ina pande mbili mwenge au mkia na kichwa, katika utoaji wa habari unatoa picha Zote mbili, ni juu yako kuchukua upande, kutokana na hiyo taarifa.
 
Sawa.

Lakini usiseme imeandika kukiri makosa yake wakati haijakiri.
Haijakiri, bali imeamua kuondoa majeshi yake kutokana na Hali walioitengeneza au tuseme Hali ya hofu ya kushambuliwa
 
Navy seals ni nani na wangepitia wapi kufika Rwanda.
Hata hivyo uamuzi wa Kagame ni wa busara kwani nchi yake iko mbioni kuvurugwa kwa uzembe wake kama ilivyotokea kule Ukraine.
Kuna lile ziwa
 
propaganda za kivita na ukiangalia kwa jicho lingine ni kama ni kweli hawa wasouth Africa na mataifa mengine ni kama wanaiba madini kutoka DRC mbona wanataka kutumia nguvu nyingi kukabiliana na Rwanda .
Nguvu gani?
 
Sasa analinda mji mkuu, nani atalinda mipaka?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…