Watanzania elimu yenu imewaathiri sana mpaka mnakaa kama mazombi fulani hivi, kujadili na nyie mada yoyote inabidi mtu awe mvumilivu sana, you're very thick with low IQ.
Wewe hapa unaleta vipimo vya joto ambavyo kila nchi inavyo, hivi havisaidii chochote maana mtu aliyesheheni Corona ambayo haijakolea hagunduliki na hivi vipimo kwenye viwanja vya ndege, ndio maana mataifa mengi yameingia kwenye "lockdown", hakuna kuingia au kutoka.
Mfano Marekani amefunga haruhusu raia wa bara Uropa au hata Uingereza kuingia kwake, maana vipimo vya uwanja wa ndege sio vya kutegemewa.
Kinachozungumzwa kuhusu humu ni uwezo wa kumpima mshukiwa na kubaini kama kweli anayo Corona. Kumbuka vipimo hivi vya uwanja wa ndege vinapima joto, na kuna aina nyingi ya maradhi yanayoweza kusababisha kiwango cha joto kupanda.
Wewe jiulize Marekani pamoja na jeuri yake ya teknolojia alizo nazo kaamua kufunga, nyie na njaa zenu hapo mnaona mumejilinda sana kwa kupima joto, mnasahau kuna mtu akiambukizwa Corona, inapita wiki kabla joto kumpanda au kuhisi chochote, atapita hivyo vipimo vyenu na kutinga uswahilini na kuendeleza maambukizi.