Saa 11 jioni siyo muda sahihi wa kuanza mechi ya mpira

Saa 11 jioni siyo muda sahihi wa kuanza mechi ya mpira

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Nimefuatilia kuhusu mechi ya kesho ya Simba na Yanga, nimesikia mechi inatakiwa kuanza saa 11:00 jioni. Najua hata huko nyuma, kuna mechi kadhaa zilianza muda huo ila naona hili ni kosa la kiufundi.

Mechi ikianza muda huo inamaanisha nusu ya mechi itakuwa wakati wa mwanga wa jua na nusu itakuwa kwenye mwanga wa taa (kama kipindi cha pili kinaanza saa 12:00 kitategemea zaidi taa kuliko jua). Nashangaa hata Azam hawajawahi kulilalamikia hili maana hata katika upigaji picha kutakuwa na usumbufu mdogo wa kubadili 'settings' za camera katikati ya mchezo.

Tuamue, mechi iwe jioni au usiku lakini siyo nusu nusu. Hauwezi kukuta hili linafanyika popote kwingine duniani.
 
Hiyo ratiba inajulikana na Azam. Labda tu useme mtaalam wa timu yenu atashindwa kuset mitambo kwenye jua na taa[emoji1787][emoji16][emoji3516][emoji106][emoji2222][emoji1][emoji2223]

Kwani Timu Yenu Haijawahi Kufungwa Na Yanga Na Mechi Ikiwa Imeanza Kwenye Muda Huo?, Af Kwanini Nyie Mnaamini Sana Mnarogwa Na Yanga Kwani Yanga Haina Quality Ya Wachezaji Wa Kuwafunga Nyie?
 
Mechi ikianza muda huo inamaanisha nusu ya mechi itakuwa wakati wa mwanga wa jua na nusu itakuwa kwenye mwanga wa taa (kama kipindi cha pili kinaanza saa 12:00 kitategemea zaidi taa kuliko jua). Nashangaa hata Azam hawajawahi kulilalamikia hili maana hata katika upigaji picha kutakuwa na usumbufu mdogo wa kubadili 'settings' za camera katikati ya mchezo.

Kamera za kisasa zinafanya auto tuning, na hata kama ni manual basi huwa ni kuclick button mara moja tu...
 
Hiyo ratiba inajulikana na Azam. Labda tu useme mtaalam wa timu yenu atashindwa kuset mitambo kwenye jua na taa[emoji1787][emoji16][emoji3516][emoji106][emoji2222][emoji1][emoji2223]
Jibu ndo hii sasa[emoji115],shida ni fundi mitambo mzee Mpili.
 
Kwani Timu Yenu Haijawahi Kufungwa Na Yanga Na Mechi Ikiwa Imeanza Kwenye Muda Huo?, Af Kwanini Nyie Mnaamini Sana Mnarogwa Na Yanga Kwani Yanga Haina Quality Ya Wachezaji Wa Kuwafunga Nyie?
Kipimo sahihi cha ubora wa timu ni mechi za kimataifa.
Zaidi ya hapo hakuna unavyoweza kusema
 
Azam ndie mmiliki wa hati xa matanbazo ya televisheni hivyo ni yeye huashirikishwa na kushriiki katika upangaji wa ratiba ili mechi zote zionyeshwe..hivyo usumbufu huo unaousema wao ndio kazi yao ili watu walipwe
 
Hiyo ratiba inajulikana na Azam. Labda tu useme mtaalam wa timu yenu atashindwa kuset mitambo kwenye jua na taa[emoji1787][emoji16][emoji3516][emoji106][emoji2222][emoji1][emoji2223]
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]eti mtaalamu wao kwan hyu n timu gan
 
Back
Top Bottom