Sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010

amejizungusha na timu mbovu alioitengeneza mwenyewe kwa nia aijuayo yeye; imejaa wezi; wazembe na watu wasio jua wajibu wao wala kuwa uzalendo wa taifa.
 

Najua Pretty anaposema Kikwete atashinda tu iwe isiwe si kwamba anataka Kikwete ashinde ila ni watu gani watakaompa ushindi ndio wanaomkatisha tamaa amekata tamaa hadi anasema hatapiga kura.

Ila sijui kama watu wa vijijini anaowasema Pretty ndio wasiopiga kura, nikiangalia wabunge wengi wa upinzani wanatokea vijijini na kura nyingi za upinzani zinatoka vijijini kama tutasema Miji ni Dar , Mwanza, Mbeya, Arusha, Dodoma, miji hii haina mbunge hata mmoja wa upinzani ukiacha mji wa Moshi.

Kweli rais wetu wa sasa ameonyesha mapungufu nafikiri hata yeye analijua hilo halina ubishi, tukubali Kikwete ana machinery kubwa itakayomsaidia wala si uwezo wake, naungana na Pretty kuwa atashinda ingawa si kwa kura nyingi, lakini napingana na Pretty kutokwenda kupiga kura, mimi nitakuwa wa kwanza kupiga kura ingawa niseme ukweli najua kura yangu itaibiwa lakini sikati tamaa wakiiba yangu mpinzani mwingine atajaza. Pretty asipopiga kura atatufanya tushindwe kwa kishindo nenda kapige kura.

Pretty angalia mfano wa wamarekani walikuwa hawaamini watakuja kuongozwa na Mweusi tena kijana tu asiyejulikana, kabla ya 2000 Obama alikuwa si Obama wa leo nothing is impossible under the sun, vote for change, it is possible.
 

Hapana mzee, the stakes are too high. Our democracy is still very young, progress we have made is still very fragile so we can't afford to take chances. Opposition may get in power and do so much damage worse than Kikwete and CCM. Time for opposition to assume power in Tanzania will come but it is not now. Rome was not built in one day. Opposition is not ready yet. Kikwete and CCM must come back.
 

I can bet your sentiments represent those of the majority of the people. They don't want change because they don't know what change will bring. What if change is inevitable?
 
Atakufa ghafla bin vu baada tu ya kupiga kura na kuchovya dole gumba kwenye wino hapo Novemba 2010! mimi nasema hivyo kama Geza Ulole mtabiri nguli hapa Africa! I say it!
 
I smell truth in this!
Truth, and nothing but truth!
 
I can bet your sentiments represent those of the majority of the people. They don't want change because they don't know what change will bring. What if change is inevitable?

Not this year but in due time. You can't force change nor rush it. It will come naturally once opposition has matured. Right now we must bring back Kikwete and CCM.
 
Inajulikana kwamba ni mgonjwa kwahiyo hawezi kutimiza majukumu yake kikamilifu kama kiapo cha rais kinavyomtaka afanye; kwa kuendelea kuwa rais akijua kuwa ni mgonjwa ni ukiukwaji wa kiapo cha ofisi hiyo!
 
Nimeguswa na hizo sababu 51,tatizo la watanzania wengi hawana elimu ya URAIA,Ndio maana tunazidi kudanyika.
 
Inajulikana kwamba ni mgonjwa kwahiyo hawezi kutimiza majukumu yake kikamilifu kama kiapo cha rais kinavyomtaka afanye; kwa kuendelea kuwa rais akijua kuwa ni mgonjwa ni ukiukwaji wa kiapo cha ofisi hiyo!

Kwa kweli, CCM kama CCM bado ina nguvu ya kushinda 2010, Kwasababu mpaka sasa hivi wapinzani bado hawajaonyesha kama wanaweza kushikamana, Wasipotumiwa na CCM wanaweza kubadili sura ya bunge , Urais bado uko CCM Tena huyu huyu KIKWETE, Tatizo kubwa linaloonekana hapa ni uwezo wa kitendaji, Afya Pia. Afya imekuwa tatizo ninahisi hawasemi ukweli juu ya Nini anasumbuliwa kiasi cha kuwa anaishiwa nguvu ghafla.Hata akichaguliwa miaka mitano ijayo itaisha? au ndo ataishiwa nguvu kabisa?????????
 

19:Anataka kutuletea utawala wa Kisultani kwa kufanya yafuatayo.
--Mtoto wake ameshinda uchaguz wa madogo CCM ki magumashi.
--Amemtuma mtoto wa Makamba (January mwenyewe kawaambia wananchi wa bumbuli though wamemtolea nje) kuwa katumwa na Rais kutwaa Jimbo.
 
Ni rais aliyeonyesha udhaifu mkubwa katka mahusiano ya kimataifa baada ya mteule wake mwenye hadhi ya kujengewa makazi nyumbani ya Tsh.1.4billion kufa na kuzikwa uchochoroni katika nchi ya ughaibuni bila yeye(rais) kuhususishwa.
 

51: Alisema kuwa akichaguliwa tena ataleta vijana na kuwa watu wa rika "lake" waanze kuachia ngazi. Well, kwa vile yuko rika moja nao basi na yeye aungane nao! -HALAFU NANI ATEKELEZE HILI SASA?

50: Hajui kwanini Tanzania ni maskini licha ya kuwa kwenye utumishi wa serikali kwa karibu miaka 30 sasa! Kiongozi asiyejua chanzo cha tatizo ataweza vipi kuliondoa isipokuwa kuziba tu dalili zake. UMEJUAJE KUWA HAJUI. ULIMUULIZA AKASEMA HAJUI. HAPA NI MANDONDOCHA TU YENYE CHUKI BINAFSI NDO YATADANGANYIKA.

49: Aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania. Ahadi hii haionekani kutekelezeka. Inaonekana ametimiza ahadi ya maisha bora kwa kila muwekezaji wa kigeni! YAANI ITOKEE KWA GHAFLA WE UKO REAL KWELI?

48:Alitangaza kuwa wizi umefanyika Benki Kuu kwa kukombwa mabilioni; badala ya kuacha uchunguzi wa jinai akaunda Kamati kuchunguza jinai. Matokeo yake ni kucheleweshwa kwa upatikanaji wa haki. YAANI ASITUMIE SHERIA BALI UDIKTETA?

47: Serikali yake imeshindwa kutekeleza maazimio yote ya wananchi wa Tanzania kama yalivyoanishwa na wawakilishi wao Bungeni katika maazimio kufuatia Kamati Teule ya Kuchunguza Richmond. Matokeo yake ni kuchochea mgawanyiko mkubwa kabisa wa kimaslahi katika historia ya taifa letu. IMESHINDWA KWELI? HAKUNA WALIOJIUZULU HATA KABLA YA VIKAO VYA BUNGE KUISHA. ANGEKUWA RAIS MWINGINE UNAFIKIRI SPIKA ANGERUDISHWA KUTOKA ZIARA YA NJE?? SI BADALA YAKE UNGEPITISHWA MSWADA WA NISHATI?

46: Aliahidi kupitia mikataba yote mikubwa ya madini ili kutengeneza hali ya "win win win". Hadi hivi sasa hakuna mkataba hata mmoja uliopitiwa na kusahihishwa na badala yake serikali yake imetangaza kuwa mabadiliko ya sheria ya madini yataendelea kuwanufaisha wawekezaji wa sekta hiyo. UNA UHAKIKA?

45: Akiwa ni Mwenyekiti wa Chama Tawala ameshindwa kuleta nidhamu ndani ya chama na matokeo yake wanachama wake mashuhuru wanatukanana na kuitana majina hadharani. Kile kilichoitofautisha CCM miaka ya nyuma sasa hakipo tena. KWANI ALIIKUTA NIDHAMU HUMO. ALICHOONDOA NI WOGA NA SIYO NIDHAMU. HAKUKUWA NA NIDHAMU HUKO HATA KIDOGO. AU KUSEMA NYERERE ANAZEEKA VIBAYA ENZI ZILE ALIPOKUWA HAI NDIYO NIDHAMU?

44: Aligawa fedha za walipa kodi wa Tanzania kwa kile kilichojulikana kama "mabilioni ya Kikwete" Hadi hivi sasa haijaoneshwa ni kiasi fedha hizo zimeweza kubadilisha maisha ya waliozipata na kurudisha faida. ALIGAWA KWA NANI? KWA MANUFAA YA NANI? NI WANANCHI MASKINI. ULITAKA AKUPE WEWE?

43: Aliahidi kuunda Baraza dogo la Mawaziri lakini matokeo yake Baraza lake limekuwa kubwa na lenye ufanisi mdogo. BARAZA LIWE NA MAWAZIRI WAWILI?

42: Alidai hadharani kuwa anawajua vigogo wa kuuza madawa ya kulevya na kuwa amewapa muda wajirekebishe. Miaka minne baadaye hajatuambia kama watu wale wamejirekebisha au la. HATUJAAMBIWA AU HUJAAMBIWA?

41: Aliahidi kuwa hakuna mwanafunzi wa Kitanzania anayehitaji elimu ya juu ambaye atashindwa kuipata. Lakini serikali yake iliwarudisha vijana wa Kitanzania waliokuwa wanasomea shahada mbalimbali ikiwemo Uhandisi na Udaktari kutoka Ukraine kwa kudai kuwa serikali haina fedha. Vijana wale 30 ingewagharimu shilingi milioni 400 tu kwa muda wa miaka minne. Kiasi hicho ni sawa na kiasi kilichochangwa na serikali kuipongeza Taifa Stars kwa kuifunga Togo! KWA MUDA UPI?

40: Amewaruhusu watendaji wake wakubwa kutumia vyeti vya kielemu ambavyo havitambuliki na vyenye utata. Miongoni mwao ni Waziri wa Fedha Bw. Mustafa Mkullo na Naibu Waziri wa Ulinzi na JKT Bw. Emmanuel Nchimbi. AMERUHUSU KWELI?

39: Licha ya kuahidi kutatua tatizo la nishati chini ya uongozi wake Tanzania imezidi kukabiliwa na upungufu wa nishati ya umeme kuliko wakati mwingine wowote huku nchi yetu ikiwa na vyanzo vya kutosha kabisa nishati hiyo ambayo serikali yake imeshindwa kuviendeleza. KUTATUA KWA SEKUNDE MOJA?

38: Amekuwa akiendeleza safari za nje yeye na viongozi wa ngazi za juu ambazo zimegharimu zaidi mabilioni ya shilingi kwa safari, posho, matumizi ambayo hataki kuyaweka hadharani. UNAJUA SAFARI HIZO ZIMEINGIZA NA ZINATARAJIA KUINGIZA FAIDA KIASI GANI KWA TAIFA?

37: Ameendeleza fikra za uduni wa Mtanzania kwa kutukuza wageni na hivyo kuendeleza kuhukumu taifa letu kwenye utegemezi wa kudumu kwa kupokea misaada ya kiudhalilishaji ya mambo ambayo yamo ndani ya uwezo wa kuzaliwa wa Watanzania. WEWE UNALIPA KODI KIASI GANI? UNAKWEPA KIASI GANI?

36: Serikali yake imeendelea kuwaficha wananchi wa Tanzania mambo muhimu yanayohusu serikali yao na hivyo kuwanyang'anya wananchi usimamizi wa serikali yao kwa kuficha mambo ya Meremeta, Deep Green Finance, Mwananchi Gold, na Tangold. MTOTO WAKO ANAFUA NGUO YAKO YA NDANI?

35: Akionesha kutokujali sifa za watendaji wake amewateua watu mbalimbali wenye utata wa maadili, na elimu na kuwapa nafasi za kuongoza wizara, na idara nyeti. Miongoni mwao:

- Mustaffa Mkullo - Waziri wa Fedha- ELIMU YAKE HAITOSHI?
- Emmanuel Nchimbi - Naibu Waziri wa Ulinzi na JKT -AMEISHIA LA SABA?
- Andrew Chenge - Alikuwa Waziri wa Miundombinu-YUKO MADARAKANI?
- Peter Noni - aliyesimamia akaunti ya EPA ikichotwa na sasa kapewa Benki ya Raslimali -ALIMTEUA YEYE? MKAPA NI KIKWETE?
- n.k

34: Serikali chini yake imevumilia vitendo vya uharibifu mkubwa wa mazingira na hata kutishia maisha kama yale yaliyotokea huko mgodi wa Mara ambapo watu wamerudhika kutokana na sumu inayotoka mgodini. UNA UHAKIKA NA HILI LA MARA? UTAKUJA UMBUKA BAADAYE.

33: Alitangaza kwa wananchi kuwa msukosuko wa kiuchumi uliokumba dunia usingeleta matatizo ya kiuchumi kwa Tanzania; miezi michache baadaye serikali yake ikaidhinisha zaidi ya shilingi trilioni moja kwa ajili ya "kusisimua" uchumi bila kuweka utaratibu wowote wa kupima mpango huo na kuonesha kitaalamu haja ya mpango huo zaidi ya kuongeza matumizi yasiyo ya lazima ya serikali. HII NI POROJO SASA NI SAWA NA KUSEMA MVUA HAIJANYESHA LAKINI KUNA MAFURIKO.

32: Ameshindwa kuliongoza Taifa kwa misingi ya Ujamaa ambayo imeanishwa katika Katiba ya Jamhuri na Katiba ya Chama chake na hivyo kuendelea kufanya kazi na kuendesha serikali kinyume na Katiba aliyoapa kuilinda na kuihifadhi. ALIUKUTA HUO UJAMAA? NANI KAUACHA MKAPA?

31: Licha ya kupigiwa kelele dhidi ya uwekezaji wa kampuni ya India ya Rites Consortium kwenye shirika letu la Reli, aliendelea na kuhakikisha wanawapa mkataba huo. Matokeo yake ni yale yale tuliyoyaona wakati wa Mkapa; mwekezaji kashindwa na anaondoka tajiri! YALE NI MAMBO YA KISHERIA SIYO YA KUKURUPUKA TU. YEYE NI RAIS MAKINI. UMAKINI WAKE NDIO UNAMSULUBU HAPA.


30: Licha ya kubuni na kuhubiri juu ya umuhimu wa Kilimo, ameshindwa kuiongoza CCM kama chama na jumuiya zake kuwekeza katika kilimo kikubwa cha mfano kama chanzo cha mapato endelevu. YEYE AU WALIOMTANGULIA. KWANI AMEANZA KUHUBIRI LINI. NA UMEMPA MUDA GANI KUMPIMA. YAANI MTOTO WAKO WA DARASA LA SITA AMEFELI MTIHANI WA DARASA LA SABA AMBAO HAJAUFANYA?

29:Kama ilivyokuwa kwenye sakata la Richmond, serikali yake imeingia mkataba na kufanya kazi na kampuni ya kitapeli ya Dowans ambayo iliingia nchini kinyemela na kuhalalishwa kwa kutumia maelezo ya uongo. Hadi hivi sasa hajakubali kuanzisha uchunguzi dhidi ya kampuni hiyo. KWANI HUJUI YALIYOTOKEA. MBONA HUKO KIJIJINI ULIKO UMEWEKEWA UMEME NA NYUMBA YAKO YA UDONGO INA SATELITE DISH. MZEE MWANAKIJIJI ACHA LAWAMA ZA POROJO. AU NA WEWE UNAZEEKA VIBAYA?
 
- Aliahidi kutembelea na kufuatilia wizara zote mara kwa mara sikumbuki mara ya mwisho alizitembelea lini, na pia sijaona wala kusikia akitoa taarifa / ripoti maalumu kuhusu ziara yake kwenye wizara alizotembela zote.

- Standard ya Ikulu imeanza tena kushuka, siyo kama wakati wa Mkapa. Raisi aliyeondoka aliiacha Ikulu kwenye standard nzuri sana, wakati wa raisi Mwinyi Ikulu iliharibika sana, thamani ya Ikulu ilishuka sana na uswahili swahili ulienea sana. Hali hiyo imerudi tena kipindi hiki cha JK, tukumbuke raisi Mkapa alitumia pesa nyingi sana za walipa kodi kuitengeneza Ikulu na kuiweka kwenye kiwango kinachotakiwa, mende na mapanya hayakuonekana hakuna mfanyakazi aliruhusiwa kulia chakula ofisini, wote walikwenda kula staff canteen, sasa hivi ni mende na mapanya kama kazi, Ikulu ni mali ya watanzania, inatunzwa kwa pesa za walipa kodi.

-Hajashughulikia wezi / mafisadi kama alivyoahidi.

- Nilitegemea angetatua tatizo la KUUZIANA / KUPEANA BURE NYUMBA ZA SERIKALI, kwanza yeye mwenyewe arudishe ile nyumba yake serikalini halafu na wenzake wotee wazirudishe. Na kama wanataka kuzinunuwa basi hizo nyumba zilipiwe bei ya soko ambayo ni thamani ya kweli na siyo uongo, ili serikali ipate pesa, na wanaodaiwa walipe ndani ya mwaka mmoja tu. Kuna viongozi wametumia milioni 50 kukarabati nyumba za serikali, halafu baada ya ukarabati wakajiuzia kwa shilingi milioni 10 imagine.

-Sijaona viwanda vipya vikijengwa.

- Wamachinga bado wanazagaa mitaani kibao, na wizi / vibaka wamezidi, pia omba omba.
 

Very sad jamani...
 
Wakuu zangu,
Ni jambo moja kuandika mapungufu ya Kikwete lakini ni jingine unapojaribu kumlinganisha na MKAPA...Na haswa sababu kubwa inayojitokeza kiuandishi ikiwa na vundo la Udini...(rejea maandishi ya jamaa hapo juu)..
Je, Nini hadhi gani ya Ikulu ktk mtazamo wake na huo mtazamo unahusiana vipi na Uongozi bora..Ikulu imeharibika toka Mkapa aliyeuza wanyama wote na kuacha tausi wakizagaa ktk mabarabara ya mjini..
Na ifikie wakati Watanzania wenzangu tuandike mapungufu ya Kiktwete kwa kuwaelemisha wananchi ama wahusika kitu ambacho kinaweza kujenga ama kuleta tofauti ktk Uongozi ujao..
majuzi nilikuwa na kundi la watu wanaomchukia sana marehemu mwl. Nyerere na kusema yeye ndio sababu ya maafa yote yanayoikumba Tanzania, imekuwa kama Nyerere alipigwa laana..Lakini cha ajabu wakamsifia Mwinyi na Mkapa ambao pia ni matokeo ya laana ile ile ya Nyerere...sasa imekuwaje kuwepo na sifa nzuri kwa Mwinyi na Mkapa ili hali, Nyerere ndiye chanzo cha matokeo haya?..

Kikwete anayo mapungufu yake, yaweza kuwa mengi sana lakini sidhani kama yanazidi ya wale anaowaongoza..Toka nimefika hapa Tanzania ni maajabu tu ya Firaun maanake nayokutana nayo sijawahi kuyaona mahala popote duniani maanake watu wamekuwa kama ndama...hakuna program yoyote inayoweza kufanywa kwa ufasaha na huyo Kikwete mkuu wa nchi hawezi kusimamia kila kitu kuhakikisha ufanisi wake. Kikwete anashindwa kufanikisha lolote sii kwa sababu hawezi yeye ila sisi wenyewe ndio kwanza kila mmoja wetu kaondoa Uzalendo..
Nitarudia kusema hivi leo hii wewe mpe Madaraka Mtanzania yeyote kusimamia mali yako nyumbani kisha utakuja nambia baada ya mwezi mmoja..Kila mtu hapa ni striker wakuu zangu hakuna kuamini mtu na hiyo imekwenda hadi ktk vitengo vyote vya serikali na mashirika. Watu wamegeuka kuwa wanyama wala nyama..Na ni imani yangu kwamba hawezi kuja kiongozi yeyote atakayeweza kuibadilisha hali hii kwa mtazamo wa kawaida pasipo sisi wenyewe kuadhibiwa..
Pengine Kikwete anahitaji kuwa Dikteta kuweza kuimudu hii nchi yetu lakini kwa kutumia hiyo demokrasia yenu sijui..na pengine haiwezekani kabisa.. hapa ndio Dar es Salaam njoo uliwe ukiwa hai!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…