Sababu ni ipi jiji la Mbeya kukosa show za wasanii?

Sababu ni ipi jiji la Mbeya kukosa show za wasanii?

Okay sasa umekuja vizuri. Umekuja kimjadala zaidi.
Ni hivi si kweli kwamba mzunguko wa Pesa Mbeya ni mdogo, kama utakumbuka vizuri Mbeya ni kati ya wanaochangia sana pato la taifa ila serikali imekuwa haiwarudishii wana Mbeya kile wanachostahiki kupitia maendeleo. Uendelezwaji wa mkoa wa Mbeya na jinsi uuonavyo ni matokeo ya nguvu za individuals wa mkoa huo.
Aina ya uwekezaji ambao tulitarajia seikali kuufanya mkoani humo ili ku influence maendeleo ni kama vile uwanja wa ndege (ambao hivi sasa tunao), na miundo mbinu mingine kama barabara majengo ya ofisi na kuviinua vivutio vingine vilivyomo mkoani humo. Siasa zimechangia sana kuua mkoa wa Mbeya.

Kuhusu kukosekana kwa Clubs.
Tatizo kubwa lililopelekea mkoa wa Mbeya kuwa nyuma upande wa clubs and the likes ni suala zima la usalama. Kama utakumbuka kumekuwa na matukio ya ujambazi na upigwaji nondo watu ulishamiri sana hapo mkoani na mida watu kupigwa nondo ilikuwa ni baada ya giza kuingia, mbaya zaidi swala hilo lilihusishwa na imani za kishirikina hivyo unaweza ukaona namna vile jamii inapokuwa na hofu katika kuitikia mabadiliko yanayokuwa yanaletwa ndani ya jamii husika.
Watu watapata wapi ujasili wa kutoka nyumbani usiku kwa ajili kwenda kula bata!? Sasa hivi Mbeya ina recover kutoka kwenye majeraha hayo ya kisiasa, ujambazi na kishirikina.
Pia, to underline that and conclude, Mbeya si wapenzi wa Bongo fleva
Uchangiaji wa Mbeya katika pato la taifa haupo relevant na mzunguko wa pesa kwenye jiji la mbeya, Tunduma walikua wanasaisia mno katika hii ishu na kwa sasa wana mkoa wao wa songwe bila kusahau shughuli za uchimbaji madini chunya na chai huko tukuyu, Ukija kwa hapa Mbeya mjini mzunguko wa pesa ni wa kawaida mno

Wilaya kama zenye mzunguko mkubwa wa pesa wasanii wanaendaga na kuna kipindi Diamond alienda kufanya show kwa kiingilio cha elf 50 na tiketi ziliuzika kama njugu, Mbeya mzunguko wa pesa ni mdogo na ushahidi unaanzia kwenye bidhaa zinazonunuliwa sana, kwa mfano kwenye maduka ya simu mengi ni tecno na itel ndio zinatoka sana hasa pale kwa mtawa ilomba na maduka ya kabwe, Wachache sana wanaomudu bei za samsung ndio huwa wanaenda dubao phones pale town.

Kwenye usalama hapo hio ni hoja isio na uzito, kuna watu wengi tu wanakwenda majumbani kwao wakitokea city pub na bar nyingi za kila kona ya hili jiji, pia kuna wanaokwenda majumbani kwao usiku wakitokea kwenye biashara zao,

Narudia tena, Huenda wewe ni wakuja au unajifungia sana ndani ukiwa hapa Mbeya, hizi nondohuwa zinakuja kwa haraka na kuisha kwa haraka, zikianza mara nyingi zinadumu kwa wiki 2 tu mara moja kwa mwaka na mara chache mara 2 kwa mwaka, Hizi nondo kwa hapa Mbeya hazitakuja kuzuia watu wachelewe kurudi makwao kutoka city pub, kwenye mikesha ya kanisani au sherehe.
 
Kama kweli ungekua umekaa Mbeya muda mrefu wala hakukua na haja ya kuanzisha uzi ili kujua sababu ya kwanini hakuna clubs au shows nyingi. Kunaweza kuwa na sababu nyingi sana lakini zote zitakua narrowed down to "watu wa Mbeya sio watu wa starehe".

Asilimia kubwa ya population ya Mbeya ni watu wa nyanda za juu kusini hasa Mbeya yenyewe na Njombe. Hawa sio watu wa starehe, ni watu ambao hawawezi kutoa elfu 10 ili waingie club kuvuja jasho. Halafu sio lazima miji yote ifanane, kila sehemu ina sifa yake ya pekee. Let them be
 
mara ya mwisho nilikanyaga Mbeya 2012.....asilimia 80 ya vijana wa kiume kule wanavaa suruali za vitambaa aina ya mabwanga na mchomekeo wa mashati ya kuteleza yaliyotuna kama puto nyuma....chini wanavaa viatu aina ya skuna za wanichoma kumoyo...kila mtaa kuna kanisa....kwenye baa wanapiga nyimbo za bahati bukuku, boniphace Mwaitege au Martha Mwaipaja...wasichana wa Mbeya wamekomaa sana mikono na vigimbi vya miguu..nafikir ni kwa sababu kilimo cha viazi na mbaazi...wadada wengi wanajichubua ngozi ..ngozi ya juu ni mirinda chini ni pepsi..matozi wa Mbeya karibia wote ni wauza mitumba...kule ujanja ni kumiliki kibanda cha kuuza mitumba maeneo ya Kabwe dox na kufungua kiosk Tunduma...katikati ya mji kumechangamka kidogo vigorofa viwili vitatu vya floor moja huwezi kosa, shukran kwa shirika la nyumba NHC..ila nje kidogo ya mji vijumba vingi kama vibiskut..vitofali vya matope...kuanzia maeneo ya simike mpaka mbalizi huko na kuendelea ni vibiskuti vitupu..hotel nyingi za kufikia wageni kama wasanii wa muziki kwa ajili ya shows zina hadhi ya lodge au guest house...vijana wa mbeya wana asili ya fujo fujo..kale ka vibe ka uhuni uhuni na fujo ndo kanafanya angalau wakumbukwe kwenye show za muziki...nje ya hapo hakuna mvuto wa shows huko..
 
Uchangiaji wa Mbeya katika pato la taifa haupo relevant na mzunguko wa pesa kwenye jiji la mbeya, Tunduma walikua wanasaisia mno katika hii ishu na kwa sasa wana mkoa wao wa songwe bila kusahau shughuli za uchimbaji madini chunya na chai huko tukuyu, Ukija kwa hapa Mbeya mjini mzunguko wa pesa ni wa kawaida mno

Wilaya kama zenye mzunguko mkubwa wa pesa wasanii wanaendaga na kuna kipindi Diamond alienda kufanya show kwa kiingilio cha elf 50 na tiketi ziliuzika kama njugu, Mbeya mzunguko wa pesa ni mdogo na ushahidi unaanzia kwenye bidhaa zinazonunuliwa sana, kwa mfano kwenye maduka ya simu mengi ni tecno na itel ndio zinatoka sana hasa pale kwa mtawa ilomba na maduka ya kabwe, Wachache sana wanaomudu bei za samsung ndio huwa wanaenda dubao phones pale town.

Kwenye usalama hapo hio ni hoja isio na uzito, kuna watu wengi tu wanakwenda majumbani kwao wakitokea city pub na bar nyingi za kila kona ya hili jiji, pia kuna wanaokwenda majumbani kwao usiku wakitokea kwenye biashara zao,

Narudia tena, Huenda wewe ni wakuja au unajifungia sana ndani ukiwa hapa Mbeya, hizi nondohuwa zinakuja kwa haraka na kuisha kwa haraka, zikianza mara nyingi zinadumu kwa wiki 2 tu mara moja kwa mwaka na mara chache mara 2 kwa mwaka, Hizi nondo kwa hapa Mbeya hazitakuja kuzuia watu wachelewe kurudi makwao kutoka city pub, kwenye mikesha ya kanisani au sherehe.

Unafahamu implications za uharifu unaodumu kwa wiki mbili na kupptea lakini ukajirudia mara tatu au zaidi. Hija yako ya kwamba eti ni wakuja ni dhaifu sana, na bahati mbaya sitajishughulisha na kukuthibitishia eneo hilo maana mimi si type ya uliowazoea wewe wa kujitapa kuwa unajua mimi ni blah blah blah.
Kingine hata ningekuwa ni wakuja kama utakavyo unachotakiwa kujishughulisha nacho ni hoja.
Nimeongelea kuhusu uchangiaji wa mkoa katika pato la taifa naona wewe unaamua kuutenganisha mkoa na Wilaya zake wakati hoja yako iliilenga Mbeya lakini ukakosa umakini wa kueleza kama umelenga Mbeya kama mkoa au Wilaya.
 
Kwa kukusaidia kama unataka starehe za aina uzitakazo acha kulialia, vuka border nenda Zambia au nenda Iringa au Moro fanya starehe zako, halafu urudi Mbeya kufanya kilichokupeleka.
Wapenda starehe siyo watu wa kulialia huzifuata popote zilipo. Unadhani hao wanaoishi Mbeya wangetaka starehe za hicyo wangeshindwa kuwekeza!?
 
Kwa kukusaidia kama unataka starehe za aina uzitakazo acha kulialia, vuka border nenda Zambia au nenda Iringa au Moro fanya starehe zako, halafu urudi Mbeya kufanya kilichokupeleka.
Wapenda starehe siyo watu wa kulialia huzifuata popote zilipo. Unadhani hao wanaoishi Mbeya wangetaka starehe za hicyo wangeshindwa kuwekeza!?
Ulichosema hakuna utofauti na kwenda kwa jiranj yako Mara kwa Mara kuangalia mechi za mpira kwasababu kwako huna TV wala dstv. Ni vyema kutatua hili tatizo kuliko kulizika kutegemea cha jirani.

Yani mtu atoke Mbeya hadi iringa safari ya masaa manner hii ale bata na arudi tena mbeya kwa masaa manne 😳 😳 atafika kachoka na pia huu ni usumbufu tu,
 
Back
Top Bottom