Sababu ya simba kuwa vile vile misimu yote ni, "comfort zone" inawaponza viongozi na mashabiki

Sababu ya simba kuwa vile vile misimu yote ni, "comfort zone" inawaponza viongozi na mashabiki

Mda utaongea kwa sauti nzuri zaidi kuliko sisi
Ila yanga tuna mtihani mkubwa sana wa kupata 4th trophy Kisha baada ya hapo ndio turudi kwenye mstari wa kukimbilia
 
Simba na viongozi wake mpaka mashabiki wao huwa hawaangalii wala kujali sanaa matokeo bali wao huangalia kama timu imecheza vizuri tu basi inatosha na ndio furaha yao wao hawajali sana kuhusu matokeo.

Simba ilivyotolewa na wydad kwa mikwaju ya penati kule morocco enzi zile wydad ya moto viongozi na mashabiki walikuwa na furaha kuliko wydad wenyewe kisa tu walicheza vizuri mashabiki wakadai timu yao imekufa kiume huku viongozi wakidai hawana cha kumdai kocha na wachezaji wamecheza vizuri kuliko wydad na kwamba wametolewa kwa figisu na bahati haikuwa yao.

Hapa unaona kabisa hawana dira sio viongozi sio mashabiki. Ndio maana warabu wanatuzidi kila mwaka, wao huwa hawaangalii timu imechezaje bali wao huangalia matokeo ndio jambo kubwa kwao.

Simba ikifungwa na Al ahly viongozi na mashabiki watakuambia walikuwa wanacheza na bingwa mtetezi tumecheza vizuri kibu ni moto.

Ukiwauliza mmejifunza nini wao hilo sio jambo kubwa kikubwa wamecheza vizuri licha ya kuondolewa kwenye mashindano.

Mnakumbuka Yanga aliifunga USMA siku ya fainali ila kikanuni USMA walikuwa washindi kwa goli la ugenini wao walishangilia uwanja mzima kwa sababu kombe ni lao bila kuonyesha aibu yoyote.

Yanga hairidhiki na mafanikio iliyoyapata hata azam nao wameamka, yanga imewaamsha azam. Yanga inaimarika kila msimu imefikia hatua sasa inawaza kuwa bingwa wa CAFCL.

Waulize simba wao wana malengo gani ? Sio viongozi sio mashabiki akili zao ni sawa. Mfano jana wqmefungwa wamepoteza taji la ngao ya jamii walilo kuwa wanalitetea hata haiwaumi wao ndio kwanza wanafuraha kuliko yanga wanakwambia jana tumecheza vizuri kocha Fadlu ni kocha mzuri.

Hii simba ni timu ya burudani au ni timu ya makombe? Mimi naona haina dira. Au ni timu maalumu kwaajili ya kutangaza matangazo ya biashara ?

Sio ajabu mkaishia makundi shirikisho, na mashabiki wakamsifia kocha na kumlaumu mangungu wakisahau kuwa mgunda aliwatumia wachezaji wale wale tena wengine hatukuwa tukiwafahamu mfano akina Balua.

Anayejua dira ya simba na malengo yake atuwekee hapa. Maana naiona simba ya miaka kadhaa mbele ikiwa kama kaizer chiefs huku azam ikigeuka mamelod.
Mtu wa Kwanza kuadhibu pale Simba ni Msemaji Ahmed Ally. Huyu ndo anawajaza ujinga mashabiki Mbumbumbu na kuwaaminisha Makubwa wakati timu inafanya madogo. Aliwaaminisha mashabiki Mukwala ni Striker mrefu na Bora Sana, akasema mpira ukija *waaa goli", juzi kaonyeshwa Udhaifu wake Leo timu inaongelea kutafuta Striker mwingine kabla ya August 15. Timu imekosa ubingwa wa Ngao ya Jamii anawaambia mashabiki "wala hatuumii maana hatukuwa na haja na Ngao yenyewe" maana ni ubao.
Wa pili wanaoharibu timu ni mashabiki wanaotumika na viongozi kupumbaza wenzao wakiwemo Wachambuzi wanaolipwa kupamba timu Kwa ubora bandia kama Comical Alli wa Iraq wakiongozwa na Goef Lea. Siku viongozi wakiambiwa ukweli mafanikio ya Simba yataanza kuonekana, lakini mkiendelea kuvishana vilemba vya ukoka, ubingwa mtausikia radioni.
 
Kingine, hakuna kitu kinaweza wapa stress wachezaji kama kelele za mashabiki... Kelele zikiwa nyingi mchezaji lazima aingiwe na maradhi ya wasiwasi... Viongozi wa Yanga wamejua kucheza na mashabiki wao, kuwafanya mashabiki wao kuwa mashabiki wa mpira na sio mashabiki wa matokeo... Na ndio maana mashabiki wa Yanga ni wepesi kuridhika

Ukiona kuweka bango, mara supu, mara mchakamchaka ni mambo ya kitoto basi endelea kufikiri hivyo, huku watu wakitengeneza timu yenye base kubwa ya mashabiki wenye furaha na waliokomaa kisoka...
Wao sasa hivi wanakuambia kapombe na mzamiru ni magarasa, msimu uliopita ilikuwa ni boko saido na baleke.

Unaona kabisa hawa wanashida
 
Uko sahihi mkuu [emoji23].....hawa makolo ni Mbu Mbu mbu
 
Bado azam hajageuka mamelodi? Yanga wanawaza ubingwa wa cafcl? Kumbe unaweza kuchukua ubingwa wa cafcl bila kucheza robo wala nusu fainaili wala fainali? Basi hata maniema anaweza kuchukua ubingwa wa cafcl si na yeye anashiriki.
 
Bado azam hajageuka mamelodi? Yanga wanawaza ubingwa wa cafcl? Kumbe unaweza kuchukua ubingwa wa cafcl bila kucheza robo wala nusu fainaili wala fainali? Basi hata maniema anaweza kuchukua ubingwa wa cafcl si na yeye anashiriki.
Zingatia hoja na maudhui ya uzi
 
Back
Top Bottom