Sababu za CCM kutoanguka tangu Uhuru hadi sasa

Sababu za CCM kutoanguka tangu Uhuru hadi sasa

CCM ni chama cha ukombozi, na vyama vingi vilivyopigania Uhuru wa nchi zao havipo tena madarakani lakini CCM bado ipo tu.
Yafuatayo ni baadhi ya michango iliyosababisha CCM iendelee kubaki madarakani:

1. Haina ubaguzi mkubwa wa wananchi wake: Baada ya uchaguzi kwisha Hakuna tofauti kimaisha kati ya walioichagua CCM na wasioipenda CCM, wote wanakufa njaa au wote wanashiba. Hakuna maduka, usafiri, mbolea wala masoko ya wanaCCM na wapinzani.

2. Kuruhusu uholela kwa wananchi: CCM na serikali wake inaruhusu watu wajifanyie mambo yao bila bughuza hata bila kufuata utaratibu, kanuni na sheria. Imeruhusu watu kulima, kufuga, kuvua, kuchimba, kuwinda, kujenga, kuua, kununua, kulipa, kuuza na kununua na kuendesha magari kiholela. Waliiweka serikali na sheria mbali na shughuli za wananchi wake, hivyo watu hawaipati harufu ya uwepo wa serikali na sheria kwenye maisha yao, hivyo hawaoni ubaya wa CCM na uzuri wa vyama vya upinzani. Siku CCM itakapoanza kuwaambia watu wafuate utaratibu na sheria kwenye mambo yao yote itaondoka madarakani siku hiyohiyo.

3. Kushirikisha wanajeshi kwenye serikali na Chama: Huu ni mtaji mwingine wa CCM kuwafanya wanajeshi wawe sehemu ya maamuzi ya serikali kwao.

4. Udhaifu wa vyama vya upinzani: Viongozi wa vyama vya upinzani ni waganga njaa, hivyo uongozi ni sehemu ya ajira yao. Ndiyo maana unawaona viongozi na wabunge wa upinzani wana majumba, mashamba, makampuni, mahoteli, wanasomesha watoto wao shule bora kabisa badala ya kutumia nguvu za kiuchumi zao kujenga vyama vyao. Hii ndio inayowafanya wasione tabu hata kuhamia vyama vingine wakati wowote kufuata maslahi makubwa zaidi. Wanawatumia wananchi wanaowapigia na kulinda kura zao kama mitaji yao tu.

5. Umasini wa wananchi: Maskini hana uchaguzi, akipewa uholela wa kuiba na kuuza hata vyuma vya madaraja, kofia na fulana inawatosha kabisa (Present is known!!!).

6. TUme ya uchaguzi: Tume ya uchaguzi inayoundwa na mwanaCCM mwenyewe ni vigumu kuidondosha.

Hivyo mtaji mkubwa wa CCM ni kuruhusu uholela kwa wananchi, kutobagua watanzania, kushirikisha wanajeshi, udhaifu wa vyama vya upinzani, umaskini wa kipato, chakula na elimu wa watu na tume isiyo huru

Siku CCM ikiachana na mitaji hii 6 inaweza kuondoka chaliii
Kianguke Mara ngapi ndio ujue?Chama ambacho kinakimbia uchaguzi na kuwategemea akina Kingai Mahita na Goodluck ndio Chama hai?
 
CCM ni chama cha ukombozi, na vyama vingi vilivyopigania Uhuru wa nchi zao havipo tena madarakani lakini CCM bado ipo tu.
Yafuatayo ni baadhi ya michango iliyosababisha CCM iendelee kubaki madarakani:

1. Haina ubaguzi mkubwa wa wananchi wake: Baada ya uchaguzi kwisha Hakuna tofauti kimaisha kati ya walioichagua CCM na wasioipenda CCM, wote wanakufa njaa au wote wanashiba. Hakuna maduka, usafiri, mbolea wala masoko ya wanaCCM na wapinzani.

2. Kuruhusu uholela kwa wananchi: CCM na serikali wake inaruhusu watu wajifanyie mambo yao bila bughuza hata bila kufuata utaratibu, kanuni na sheria. Imeruhusu watu kulima, kufuga, kuvua, kuchimba, kuwinda, kujenga, kuua, kununua, kulipa, kuuza na kununua na kuendesha magari kiholela. Waliiweka serikali na sheria mbali na shughuli za wananchi wake, hivyo watu hawaipati harufu ya uwepo wa serikali na sheria kwenye maisha yao, hivyo hawaoni ubaya wa CCM na uzuri wa vyama vya upinzani. Siku CCM itakapoanza kuwaambia watu wafuate utaratibu na sheria kwenye mambo yao yote itaondoka madarakani siku hiyohiyo.

3. Kushirikisha wanajeshi kwenye serikali na Chama: Huu ni mtaji mwingine wa CCM kuwafanya wanajeshi wawe sehemu ya maamuzi ya serikali kwao.

4. Udhaifu wa vyama vya upinzani: Viongozi wa vyama vya upinzani ni waganga njaa, hivyo uongozi ni sehemu ya ajira yao. Ndiyo maana unawaona viongozi na wabunge wa upinzani wana majumba, mashamba, makampuni, mahoteli, wanasomesha watoto wao shule bora kabisa badala ya kutumia nguvu za kiuchumi zao kujenga vyama vyao. Hii ndio inayowafanya wasione tabu hata kuhamia vyama vingine wakati wowote kufuata maslahi makubwa zaidi. Wanawatumia wananchi wanaowapigia na kulinda kura zao kama mitaji yao tu.

5. Umasini wa wananchi: Maskini hana uchaguzi, akipewa uholela wa kuiba na kuuza hata vyuma vya madaraja, kofia na fulana inawatosha kabisa (Present is known!!!).

6. TUme ya uchaguzi: Tume ya uchaguzi inayoundwa na mwanaCCM mwenyewe ni vigumu kuidondosha.

Hivyo mtaji mkubwa wa CCM ni kuruhusu uholela kwa wananchi, kutobagua watanzania, kushirikisha wanajeshi, udhaifu wa vyama vya upinzani, umaskini wa kipato, chakula na elimu wa watu na tume isiyo huru

Siku CCM ikiachana na mitaji hii 6 inaweza kuondoka chaliii
Kianguke Mara ngapi ndio ujue?Chama ambacho kinakimbia uchaguzi na kuwategemea akina Kingai Mahita na Goodluck ndio Chama hai?
 
Kwasababu ina mizizi ilio jichimbia kwa chini sanaaaaa
 
Heading yako ilitosha usubiri ujibiwe. Na jibu ni ili wizi wa kura, unyang'anyi wa ushindi, tume ambayo si huru, na unfear!
 
Nijuavyo technolojia itawaondoa tu, hata kama ni miaka 50 ijayo, itafika mahala tutapiga kura kwa kutumia simu zetu na kila kura inapododoka unaona idadi ya kura zilivyopigwa, kuiba kutakuwa hakuna nafasi, pili wajinga bado ni wengi na maisha bado ni rahisi mno nafikiri unaona walioko mjini ndio uleta kashikashi ila walioko vijijin wengi wanajua Nyerere bado yupo ikulu
 
Mtaji wa CCM ni wananchi masikini na wajinga, ndiyo sababu wanazalishwa kila siku…. usiku utapokwisha.!
 
5. Umasini wa wananchi: Masikini hana uchaguzi, akipewa uholela wa kuiba na kuuza hata vyuma vya madaraja, kofia na fulana inawatosha kabisa (Present is known!!!).

6. TUme ya uchaguzi: Tume ya uchaguzi inayoundwa na mwanaCCM mwenyewe ni vigumu kuidondosha.
Umaskini wa watanzania wengi ni mtaji mzuri sana kwa CCM hasa nyakati za uchaguzi
 
Imewekeza UJINGA na UPUMBAVU kwa raia wake, kwa namna hiyo hakuna raia atakayeenda kinyume na matakwa ya CCM. Leo 2022 bado tunatumia katiba ya 1977, miaka 45 iliyopita, katiba ya chama kimoja inatumika na vyama vingi na sisi wananchi tumekaa tu.

CCM ni walafi na waroho wa madaraka hivyo wataendelea kupanda mbegu ya UJINGA na UPUMBAVU miongoni mwa wananchi ili waendelee kuitafuna nchi.
 
Unapigana na anaye kupa silaha ,anakulisha anakupa fedha,Utamuweza kweli?

Ova
 
Unataka ianguke Vipi chama kina mbunge moja Tanzania mzima wewe kwako ni ushindi akili za Bavicha bana.
baada ya kuwaengua wagombea wote wa upinzani, au...?
 
CCM ilishajenga msingi imara uliojengwa na Muasisi wake Nyerere na hivi vyama vya upinzani ni mapandikizi ya CCM kila chama kinachozaliwa CCM inapeleka mtu wake pale tena inahakikisha anafika katika ngazi za juu za uongozi katika hicho chama mwisho wa siku anakiharibu na kuanza upya ona NCCR Mageuzi (Mrema), CUF (Lipumba), CDM (Zitto) na ACT (Marehemu Anna). Kwahiyo tutasubiri sana CCM kuanguka
Mtei mwenyewe yuko kwenye system. Huwezi kuwa Gavana wa bank kuu bila kuwa mtu wa serikali kwelikweli.
 
Waache kutumia Polisi waache kutumia DED na watengeneze mfumo rafiki wa uchaguzi uone tukio.
 
Kwa jinsi watanzania wenyewe walivyo na hivyo vyama mbadala vilivyo ni bora ccm iendelee kutawala.
 
WaTanganyika wengi hawajui siasa, na pili hawana sababu ya kuiondoa CCM madarakani.
Kila Mtanganyika wa kawaida utakapomuuliza kuhusu kuiondoa CCM jibu atakwambia Maisha ni Haya haya hata wakija wapinzani hakuna jipya.
 
Imewekeza UJINGA na UPUMBAVU kwa raia wake, kwa namna hiyo hakuna raia atakayeenda kinyume na matakwa ya CCM. Leo 2022 bado tunatumia katiba ya 1977, miaka 45 iliyopita, katiba ya chama kimoja inatumika na vyama vingi na sisi wananchi tumekaa tu.

CCM ni walafi na waroho wa madaraka hivyo wataendelea kupanda mbegu ya UJINGA na UPUMBAVU miongoni mwa wananchi ili waendelee kuitafuna nchi.
kama wananchi ni wajinga kiasi hicho, wewe utafanye kuwaelimisha, au ni ule msemo wa ukiwashindwa ungana nao?
 
Siku ukifanikiwa kufika nchi zilizoendelea utajua umuhimu wa elimu.

Mfumo wa elimu wa kitanzania unakumbatiwa na CCM miaka kenda unamjenga mtu kuwa tegemezi wa serikali na asiyejua haki zake za msingi.

Mfano uliwahi kuona wananchi wa Marekani wanamsubiri kiongozi aje kuzindua kisima cha maji?

Kwa Tanzania wengi hawajui haki zao na hisani pia hawajui kipi ni chao kipi si chao,rais ametengenezewa mazingira ya kuonekana mungu mtu.

Polisi na wenzao wote wako chini ya CCM.

Kwa namna gani hapo CCM itatokaje madarakani.
 
WaTanganyika wengi hawajui siasa, na pili hawana sababu ya kuiondoa CCM madarakani.
Kila Mtanganyika wa kawaida utakapomuuliza kuhusu kuiondoa CCM jibu atakwambia Maisha ni Haya haya hata wakija wapinzani hakuna jipya.
Hayo ni matokeo ya kuachiwa kufanyakazi zao kiholela biba buguza na uwepo wa ardhi kubwa ya wazi. Siku ardhi ya wazi ikiisha na serikali kuwataka watu (machinga, wakulima, wafugaji, wavuvi, bodaboda na wachimba madini) wafuate taratibu zote zilizopo na za kisheria utaona timbwilitimbwili lake.
 
CCM ni chama cha ukombozi, na vyama vingi vilivyopigania Uhuru wa nchi zao havipo tena madarakani lakini CCM bado ipo tu.
Yafuatayo ni baadhi ya michango iliyosababisha CCM iendelee kubaki madarakani:

1. Haina ubaguzi mkubwa wa wananchi wake: Baada ya uchaguzi kwisha Hakuna tofauti kimaisha kati ya walioichagua CCM na wasioipenda CCM, wote wanakufa njaa au wote wanashiba. Hakuna maduka, usafiri, mbolea wala masoko ya wanaCCM na wapinzani.

2. Kuruhusu uholela kwa wananchi: CCM na serikali wake inaruhusu watu wajifanyie mambo yao bila bughuza hata bila kufuata utaratibu, kanuni na sheria. Imeruhusu watu kulima, kufuga, kuvua, kuchimba, kuwinda, kujenga, kuua, kununua, kulipa, kuuza na kununua na kuendesha magari kiholela. Waliiweka serikali na sheria mbali na shughuli za wananchi wake, hivyo watu hawaipati harufu ya uwepo wa serikali na sheria kwenye maisha yao, hivyo hawaoni ubaya wa CCM na uzuri wa vyama vya upinzani. Siku CCM itakapoanza kuwaambia watu wafuate utaratibu na sheria kwenye mambo yao yote itaondoka madarakani siku hiyohiyo.

3. Kushirikisha wanajeshi kwenye serikali na Chama: Huu ni mtaji mwingine wa CCM kuwafanya wanajeshi wawe sehemu ya maamuzi ya serikali kwao.

4. Udhaifu wa vyama vya upinzani: Viongozi wa vyama vya upinzani ni waganga njaa, hivyo uongozi ni sehemu ya ajira yao. Ndiyo maana unawaona viongozi na wabunge wa upinzani wana majumba, mashamba, makampuni, mahoteli, wanasomesha watoto wao shule bora kabisa badala ya kutumia nguvu za kiuchumi zao kujenga vyama vyao. Hii ndio inayowafanya wasione tabu hata kuhamia vyama vingine wakati wowote kufuata maslahi makubwa zaidi. Wanawatumia wananchi wanaowapigia na kulinda kura zao kama mitaji yao tu.

5. Umasini wa wananchi: Maskini hana uchaguzi, akipewa uholela wa kuiba na kuuza hata vyuma vya madaraja, kofia na fulana inawatosha kabisa (Present is known!!!).

6. TUme ya uchaguzi: Tume ya uchaguzi inayoundwa na mwanaCCM mwenyewe ni vigumu kuidondosha.

Hivyo mtaji mkubwa wa CCM ni kuruhusu uholela kwa wananchi, kutobagua watanzania, kushirikisha wanajeshi, udhaifu wa vyama vya upinzani, umaskini wa kipato, chakula na elimu wa watu na tume isiyo huru

Siku CCM ikiachana na mitaji hii 6 inaweza kuondoka chaliii
Sababu kubwa ni chama dola. Coercive instruments ndio wasindikizaji katika safari yao ya utawala. Si tembo wala simba watakatisha na kuzuia huo msafara... Iko mizinga ya kubomoa miamba, maburdoza ya kuchonga njia, a.k 47 za kusafisha njia, vipaaza sauti vya kutoa onyo yaani full masnondo.
But people's power kitakuwa kisambaratisho na kimechomoza na kinakua...
 
Sababu kubwa ni chama dola. Coercive instruments ndio wasindikizaji katika safari yao ya utawala. Si tembo wala simba watakatisha na kuzuia huo msafara... Iko mizinga ya kubomoa miamba, maburdoza ya kuchonga njia, a.k 47 za kusafisha njia, vipaaza sauti vya kutoa onyo yaani full masnondo.
But people's power kitakuwa kisambaratisho na kimechomoza na kinakua...
Shida ya vyama vya upinzani ni moja tu, viongozi na wananchi wamejitenga kama maji na mafuta. Hii ni kutokana na viongozi wao kuonekana kama wanaweza kurudi CCM wakati wowote kama vile Lowassa, Slaa, Sumaye, na wengine weeengi walioenda kuunga juhudi viongozi wa ccm. Viongozi na wabunge wa upinzani wanajilimbikizia mali wao wenyewe. Hii ndio maana hata viongozi wakikamatwa na kuwekwa ndani hakuna mwananchi wa kawaida anaejali, maana hawagusi maisha yao ya kila siku kwa lolote kwa chochote. Luzuku haijawahi kuchimba hata kisima kimoja cha maji cha mfano kwenye kijiji/mtaa mmoja, wanakula tu na kumtunzia Mtei na familia yake.
 
Back
Top Bottom