Ngoma fulani hivi ya wachawi/ wanga, wenyewe wanaimba
"Cheketu cheketu, mahepeee
Nyama ya mutu, mutamuuuuu
Kasoro kidole cha mwishooo"
Ukikaa kaa na wazee wazee wa Kizaramo wanaojua habari za Wazaramo ukiwauliza ngoma ya mahepe wanaweza kukutajia.
Sasa hata hapa naona kuna watu wanachekelea depression na suicide za watu wengine kama wanga na wachawi wanaocheza ngomaza mahepe.
Yani mtu kupata kuwa T.O halafu akapata maisha mabaya baadaye badala ya kuwa kitu cha kusikitika, watu wanafurahia na kuchekelea.
Ndiyo maana hatuendelei.