Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
 
Kichwa cha habari jibu lake ni hili hapa!

CCM bado inatumia zana ikifanya maendeleo yote watakosa pengine kupigwa kula kama unavojua waziri kaenda kuzindua vyoo.
mabadiliko ya katiba na keki ya taifa.
 
Kuna kitu kinaitwa " the paradox of plenty" - Nchi zile zenye rasilimali nyingi kubakia kuwa maskini tofauti na ilivyotegemewa kuwa rasilimali hizo zingeboresha maisha na hali zao.

Huu ndio ukweli, angalia nchi kama uswiswi, milima, vijiji, barafu, lakini uswiswi ina GDP per capita ya dola 73,000. Tanzania na hali nzuri ya hewa, rasilimali kibao tuna GDP per capita ya hardly 1200 USD
 
Kila mmoja machinga
Sababu ya elimu duni kwa kizazi cha zamani na hata Sasa bado Kuna asilimia kubwa isiyo na elimu nzuri ila tunakoelekea asilimia kubwa watakuwa na elimu nzuri nambo mazuri yatakuja na kazi zitapatikana nyingi tofauti na Sasa hizo za Kila mtu kuwa chinga tena eneo moja la mjini maana vijijini watu hawana elimu na kufanya uwekezaji usiwepo vijijini maana wao wanajua kuishi ni kula tu na maisha mengine yenye kusipport jamii na kuleta ajira wamewaachia watu wa mjini tu.
 
Huu Uzi ni makin Sana ila kwa sababu watz wanapenda kuponda Ukweli ndo huo na haya yote Adui wa taifa Hili mkuu ni Chama Cha kula kulingana na urefu wa Kama yake(CCM)
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:
 
Sababu ya elimu duni kwa kizazi cha zamani na hata Sasa bado Kuna asilimia kubwa isiyo na elimu nzuri ila tunakoelekea asilimia kubwa watakuwa na elimu nzuri nambo mazuri yatakuja na kazi zitapatikana nyingi tofauti na Sasa hizo za Kila mtu kuwa chinga tena eneo moja la mjini maana vijijini watu hawana elimu na kufanya uwekezaji usiwepo vijijini maana wao wanajua kuishi ni kula tu na maisha mengine yenye kusipport jamii na kuleta ajira wamewaachia watu wa mjini tu.
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba.

.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu
 
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba
.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu
Umepiga nyundo kali sana hapa mkuu, punguza kidogo[emoji1787][emoji1787]
 
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba
.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu
Umeongea kishabiki bila hoja yoyote ya maana, umeshindwa kuunganisha doti kuhusiana na utawala wa ccm na umaskini wa watanzania ambao wamefikia hatua ya kuona fahari kwa kuwaita "Wanyonge". Poor you.
 
Shida nyingine kubwa ni siasa kuingilia mipango mwisho wa siku tunakuwa brainwashed na politics.

Tukitaka tupate maendeleo lazima tuache huo utopolo wa siasa uchwara na turuhusu professionalism ifanye Kazi na wanasiasa wa mobilise funds na kuwamobilise watu waunge mkono ndio tutoke hapa..

Wachumi tuna muarobaini wa wapi pa kuanzia ila shida ni siasa uchwara.

Lazima tuvunje "poverty circle" kwanza.
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:
Lugha ya Kiingereza ni muhimu sana kila Mtanzania aimudu.

Vitabu vingi historia ya Afrika, Historia ya ukweli, vitu vingi vya Science and Technology vimeandikwa kwenye English Language.

Exposure kwa viongozi ni muhimu sana. Tembelea nchi zingine, Soma nchi ni vipi zilijikomboa vipi kutoka majanga ya umaskini, magonjwa hadi kuwa nchi za viwanda.

Kilimo ni kitu muhimu, kitachosaidia Watanzania Wengi, zaidi ya 70%. Ukiwekeza hapo kwenye Irrigation, mbolea, Trekta utakuwa umewasaidia Wengi.
 
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba
.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu
Unaonekana una stress pumua kidogo
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

Point yako ya kwanza, kushabikia siasa, chuki, ukabila, udini ni vikwazo sisi kuendelea.

Ukiangalia US, UK, wanajali zaidi point zako kuliko unaweza kuwa Mweusi, Asian ila ukiwa na maono, uwezo unachaguliwa kuwa Kiongozi.

Kwetu ni Rais anakupenda au hakupendi. Upuuzi mtupu.
Tatizo sio elimu duni dunia nzima nchi zote zilizoebdelea technolojia huguduliwa na watu binafsi sio serikali zao

Tanzania tumesomesha mijitu kibao nchi hizo zinazosifiwa kwa elimu kubwa kuanzia chekechea hadiI PhD lakini hawana LA maana walilogundua kubadilisha kuanzia maisha yao wenyewe wanadandia siasa tu wawe akina Tundu Lisu au mbatia ambao walisoma ulaya kwenye elimu bora ni waganga njaaa tu kama wasoma kayumba
.Hata ma diaspora yaliyobaki nje yakapata elimu bora huko yaliko yanajitwika mabox tu misiba ikitokea inakuja kutuchangisha Huku Tanzania haina hela milofa tu

Ni kiasi gani kinatumwa na Diaspora kila siku,mwezi mwaka. Hizi ni Dollar,pound,,Euro.

Zinasaidia nchi kupata foreign reserve. Wengi Diaspora wana uchungu sana na hii nchi kutaka ifanikiwe.

Wamegundua nyumbani ni nyumbani kwa kuishi nje.
 
Ukishaona mipango ya Nchi inaongozwa na sera za chama ambazo zinaandaliwa wakati wa uchaguzi, hapo kama Taifa msahau maendeleo....kazi iendelee...hapakazi tu....kilimo kwanza...na takataka nyingine. Miaka 5 ikipita wanabuni msemeo mwingine.
Kila kiongozi na hata ambao wasingetakiwa kushabikia siasa anatembea na ilani ya chama mfukoni. Hatuna mipango ya maendelo ya muda mrefu ambayo haitafungama na siasa. Nasasahivi ....."eat according the length of your rope"
 
Hatuna mipango ya maendelo ya muda mrefu ambayo haitafungama na siasa. Nasasahivi ....."eat according the length of your rope"
Rais amepata nafasi, dakika tano hazijapita, hajafanya lolote la maana, anaangalia 2025.

Wameambiwa waibe ila wajipime, wasivimbiwe, wale kwa ulefu wa kamba zao.

Rais Kilaza,tutegemee nini kwa Watendaji wake?
 
Lugha ya Kiingereza ni muhimu sana kila Mtanzania aimudu.

Vitabu vingi historia ya Afrika, Historia ya ukweli, vitu vingi vya Science and Technology vimeandikwa kwenye English Language.

Exposure kwa viongozi ni muhimu sana. Tembelea nchi zingine, Soma nchi ni vipi zilijikomboa vipi kutoka majanga ya umaskini, magonjwa hadi kuwa nchi za viwanda.

Kilimo ni kitu muhimu, kitachosaidia Watanzania Wengi, zaidi ya 70%. Ukiwekeza hapo kwenye Irrigation, mbolea, Trekta utakuwa umewasaidia Wengi.
Siyo hichi kilimo cha chakula tu sisi bado kukifanya kilimo kilipe, imagine mazao yenye faida za afya na kuleta pesa hata wanaolima hawali wanategemea watu wengine hasa mjini ndo wanunue, kingine viwanda vya kuongeza thamani mazao bado havipo na utaalamu mwingi wa kuyafanya mazao yatumike hata wakati wa kiangazi au nje ya msimu wa mavuno haupo kama mboga za kukausha na matunda ya kukausha kwa vile wengi wanapenda kuishi kama mababu zetu kula vyakula kwa msimu wake baada ya msimu au mavuno yakizidi yanaozea shambani bila kuleta faida na kuinua uchumi wowote.
 
Kingereza kisingeweza kuunganisha makabila zaidi ya 100 yaliyopo hapa Tanzania. Wengi wangerudia kuongea lugha za makabila yao maana kingereza ni kigumu na ni lugha ya kigeni. Na hicho kingeleta ukabila alioupiga vita Nyerere.
 
Back
Top Bottom