Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Sababu za Tanzania kupitwa kimaendeleo na nchi nyingine

Mfano wako wa Rwanda. Umeharibu point zako nzuri!
Rwanda kilicholeta maendeleo ni matumizi Bora ya ardhi ya Congo DRC, full stop!

Wamejua kuitumia DRC!
Mkuu Bambushka,

Ujue ardhi ya DRC ilikuwepo siku zote. Kama ndiyo iliyowapaisha Rwanda, basi ujue ni alipopatikana kiongozi mzuri ndipo ilipotumika vizuri hiyo ardhi.
 
hili ndio watu wengi hatuliangalii, tunapenda kuwanyooshea vidole walioko madarakani ilihali nao wametoka miongoni mwetu, tabia zile zile walizonazo ndio tulizonazo huku uraiani....

Tabia za wizi, uzinzi, uongo, usaliti, umalaya, unafiki, uchawi nk hizi ni tabia ambazo wote tuko nazo huku uswahili na sisi ndio tunaweza kuwa viongozi tukaendekeza ujinga huohuo..

La msingi ni watu katika ngazi ya familia kulea familia katika misingi inayowaweka mbali na tabia za hovyo hovyo kama wizi, uzinzi, uchawi nk....wote tukiyasimamia haya basi tutakuwa na jamii imara..
Safi kabisa
 
Ajabu nyingine ni kwamba mahakama zetu, maagizo mengi ya serikali, hukumu muhimu, vitu muhimu vinaandikwa Kiingereza wakati wengi hawajuhi hata wamehukumiwa nini, document zinasema nini? Mawakili nao wana- struggle to intepret hukumu.
Sure!
 
Nchi zote za afrika ya weusi uchumi wa mtu mmoja unafanana.
Mazingira, mifumo ya maisha wote ufanana.

Wengi hawajatoka hata nje ya mikoa yao wanajua kulalamika tu.

Mtu anakuja kusifia Senegal bila aibu. Rwanda ukitoa Kigali kwingine kote ni vijijini tu, Kigali yenyewe haiingii hata kwa Arusha zaidi ya usafi.
 
miaka 40 tangu vita ya kagera hatuja rekabisha uchumi watu kweli, kipindi hicho nchi nyingi kama Zimbabwe SA nk zilikua hazijapata uhuru, zimepata uhuru na kutupita, kwanini Tz hatuende mbele kiuchimi?

I reckon you know nothing about SA na Zim. Hakuna siku ambayo tumewahi kuipita SA kwa uchumi/maendeleo, matter of fact, SA imepitwa GDP na Nigeria kwa mara ya kwanza a few yrs ago.

Afu unajua SA ilipata uhuru lini? Au unaongelea 1994 Mandela alipopewa urais hata hapo SA tayari ilikua mbali sana. Urais wake ulikua ceremonial tu.
 
Nini kifanyike? Jamii ndo iamuke itoke kwenye ujinga kama ni elimu watu wa zamani wengi hawakupata elimu na ndo tatizo lilianzia hapo walisoma wachache na haohao kupata ajira moja kwa moja na vizazi vyao wamewapa elimu nzuri na ajira ni zawao tu maana wale waliokosa elimu hawakuona uzuri na umuhimu wa kuwapa watoto wao elimu nzuri labda watoto waliolazimisha kusoma kwa lazima au kwa msaada ndo tunaona wanavyeo nao wanajipendelea tu, hivyo tukazanie elimu za vizazi vyetu Kwanza Ili wengi waelimike na kujitambua na mazingira ya kuwekeza yataleta faida imagine mpaka Sasa bado tunaishi kizamani kwa kupoteza muda tu kama mtu kulima kwa jembe la mkono mazao kidogo yasiyo na faida, kushinda mtu anazunguka na mifugo kama vile na yeye ni mfugo badala ya kutengeneza au kuzalisha chakula cha mifugo na kufuga kisasa tena kama kampuni inayojitosheleza na mahitaji ya mifugo yake Sasa watu wenye akili za kizamani kama hizi wataweza kuzungusha uchumi kiasi cha wenye madaraka kutetemeka na kufanya mambo makubwa? Maana watu wakifanya mambo kisasa yanaleta ajira nyingi sana mfano elimu ya English medium inaajili watu wengi kuliko hizi za kata na hata huduma zingine kama kilimo kikiwa kisasa kinaleta pesa nyingi na ajira nyingi.
Elimu si tatizo, tatizo ni aina gani ya elimu unawapa watu wako.
Elimu ya sasa ni takataka imepitwa na wakati si tija kwa kizazi cha sasa zaidi ya kuwafanya watz wawe masikini tu.
Mfumo wa elimu wa mkoloni ndio mfumo sahihi zikiwemo mitaala yake.
 
Uongozi ndio tatizo bado atujapata kiongozi anaejua watz wanataka nini tangu UHURU,bali ni aina ya viongozi wanaotulazimisha vile watakavyo
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Pia baadhi ya wananchi kupenda kulalamikia serekali pasipo kujituma na kusubiri kufanyiwa kila kitu
 
Sababu kubwa ni ufisadi uliojikita katika ngazi za juu👇🤡🤡🤡
 
Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.

Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:

1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,

Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.

Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.

Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!

Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Yaani kama ulikuwa kwenye kichwa changu. Uliyosema yote ni kweli kabisa. Nini kifanyike? Misingi imekosewa tayari.
 
Wewe ndo pumba kwa kuwa unadanganyika kuwa Chama ndo Shida ya maendeleo yetu. Utasubiri sana. Hata hivyo Tz tuko vizuri. Sijui unajifananisha na nani. You can not have it all my brother.

Viongozi Ni wachache sana kuliko hao mliopo maofisni na wakamilishaji miradi. Huko ndo wanaiba sana hela zetu na kujenga.

Wanaopindisha mambo wengi wako mkoani na wilayani. Hao Ni wanachama wa vyama vyote.

Wavivu Ni wanachama wa vyama vyote

Wengi tumesoma ulaya na Marekani. Vyuo Bora. Lakini tukirudi tunataka tuibe haraka au tunakutana na wale wa la saba la mwaka 1947, kila ukipendekeza mabadiliko Utaskia wenzako ulitukuta na utatuacha.

Akitoke kiongozi mkali wa kutaka actions. Mnaanza wenyewe siasa.

Watz mmejiroga. Na siku mtakayokubali kukaa chini kajitafakari na kuacha kunyoesheana vidole ndo siku ya ushindi.
Njia pekee ni kwa watawala kuwaogopa wananchi kwamba wanaweza kuwaondoa madarakani pale wanapoleta ujinga kama huu wanaofanya ccm, sasa kwa bahati mbaya sana Tanzania ccm hawana hiyo hofu kwa sababu wanafahamu fika kwamba wananchi hawana jeuri ya kuwaondoa kwa sababu nchi imefikia hatua ambapo sasa hata uchaguzi haupo tena ni uhuni tu unafanywa.
 
Yaani kama ulikuwa kwenye kichwa changu. Uliyosema yote ni kweli kabisa. Nini kifanyike? Misingi imekosewa tayari.
Nini kifanyike?
Hili ni swali kila mtu ana maoni yake. Kama vile ugonjwa wa kansa, kuna wengine watapendelea kuichoma na wengine watasema tuikate!
Binafsi nimeshaona kuwa kipaumbele cha kuirekebisha nchi hii kwa hivi sasa ni KATIBA kwanza. Katiba itakayowapa raia madaraka ya kugeuza uongozi. Ni dhahiri Katiba tuliyonayo haikidhi jambo hilo. Tukiwa na Katiba inayowapa raia nguvu, angalau (angalau) twaweza kuzungumzia kuirekebisha nchi hii. Katiba hiyo iruhusu mgombea huru na kura ya maoni kwa maamuzi makubwa. Nadhani tuanzie hapo. Wengine huenda wakaja na mapendekezo mengine ambayo pia yanaweza kufaa. Kansa haina matibabu ya aina moja!
 
Can u imagine nchi inapiga marufuku watumishi wake kusafiri nje ya nchi...unategema watatunga sera gan kama sio kuimba mapambio ya gwajiboy
 
Kingereza kisingeweza kuunganisha makabila zaidi ya 100 yaliyopo hapa Tanzania. Wengi wangerudia kuongea lugha za makabila yao maana kingereza ni kigumu na ni lugha ya kigeni. Na hicho kingeleta ukabila alioupiga vita Nyerere.
Kiswahili lugha ya nani?
 
Matatizo ya Taifa hili ni[emoji116]
-Ccm na viongoz wake.

-Aina ya uongozi(democracy), hii haiwez leta maendeleo ktk taifa hili bila kutumia udicteta, maana kuna wapuuzi wachache wanaohujumu hili taifa wanatakiwa kushughlikiwa bila kujali Haki za kibinadamu na mashirika ya magharibi yatazungumzaje.

-Mifumo mibovu na hovyo ya Elimu

-ukoloni mamboleo, hapa unajionea mwnyewe yaan saut za mataifa ya mbali yananguvu kulko saut ya viongoz wa ndani ya nchi,
yaan mpka sas bado wageni wanaitawala hii nchi kiuchumi, kitechnolojia, kisiasa na kijamii, em fikil kuhusu suala la maadili ya wananchi wa taifa hili yanapokengeukwa na waTz wanapojarbu kukemea kuna hayo mashirika yenye nguvu tokea izo nchi babe yanakuja kutetea uovu na kuupa kinga mfano Ushoga,usagaji, malez mabaya ya watoto,
Pia bado sauti za hawa mabeberu zinanguvu kuikandamiza hii nchi kupitia vibaraka wao wanaojiita wawekezaji wanaokomba resources za nchi na kubakisha umasikin.

-Dini na imani ngeni, hapa ndpo tulpo harbu kwa kuikataa Nguvu ya Uungu ya kwel na kukubali Miungu migeni itutawale na kukumbatia utandawazi, jambo lililopelekea kupoteza ukuu wetu na nguvu zetu za akili na uvumbuzi,
kwa hil linaweza kuwa ndio jambo la kwanza sababishi la unyonge wa nchi ya Tz na nchi zote za watu weusi, maana maendeleo yanahitaji akili na maarifa, sasa sie tutapata wapi maarifa kama ubongo/bongo zetu zimekuwa washed na kuwa outdated kwa kuzipa kipaumbele imani zisizo zetu.

Acha tuendelee kupigika mpka tutakapoijua kweli.
 
Back
Top Bottom