Augustine Moshi
JF-Expert Member
- Apr 22, 2006
- 2,556
- 1,385
Mkuu Bambushka,Mfano wako wa Rwanda. Umeharibu point zako nzuri!
Rwanda kilicholeta maendeleo ni matumizi Bora ya ardhi ya Congo DRC, full stop!
Wamejua kuitumia DRC!
Safi kabisahili ndio watu wengi hatuliangalii, tunapenda kuwanyooshea vidole walioko madarakani ilihali nao wametoka miongoni mwetu, tabia zile zile walizonazo ndio tulizonazo huku uraiani....
Tabia za wizi, uzinzi, uongo, usaliti, umalaya, unafiki, uchawi nk hizi ni tabia ambazo wote tuko nazo huku uswahili na sisi ndio tunaweza kuwa viongozi tukaendekeza ujinga huohuo..
La msingi ni watu katika ngazi ya familia kulea familia katika misingi inayowaweka mbali na tabia za hovyo hovyo kama wizi, uzinzi, uchawi nk....wote tukiyasimamia haya basi tutakuwa na jamii imara..
Sure!Ajabu nyingine ni kwamba mahakama zetu, maagizo mengi ya serikali, hukumu muhimu, vitu muhimu vinaandikwa Kiingereza wakati wengi hawajuhi hata wamehukumiwa nini, document zinasema nini? Mawakili nao wana- struggle to intepret hukumu.
Nchi zote za afrika ya weusi uchumi wa mtu mmoja unafanana.
Mazingira, mifumo ya maisha wote ufanana.
miaka 40 tangu vita ya kagera hatuja rekabisha uchumi watu kweli, kipindi hicho nchi nyingi kama Zimbabwe SA nk zilikua hazijapata uhuru, zimepata uhuru na kutupita, kwanini Tz hatuende mbele kiuchimi?
Elimu si tatizo, tatizo ni aina gani ya elimu unawapa watu wako.Nini kifanyike? Jamii ndo iamuke itoke kwenye ujinga kama ni elimu watu wa zamani wengi hawakupata elimu na ndo tatizo lilianzia hapo walisoma wachache na haohao kupata ajira moja kwa moja na vizazi vyao wamewapa elimu nzuri na ajira ni zawao tu maana wale waliokosa elimu hawakuona uzuri na umuhimu wa kuwapa watoto wao elimu nzuri labda watoto waliolazimisha kusoma kwa lazima au kwa msaada ndo tunaona wanavyeo nao wanajipendelea tu, hivyo tukazanie elimu za vizazi vyetu Kwanza Ili wengi waelimike na kujitambua na mazingira ya kuwekeza yataleta faida imagine mpaka Sasa bado tunaishi kizamani kwa kupoteza muda tu kama mtu kulima kwa jembe la mkono mazao kidogo yasiyo na faida, kushinda mtu anazunguka na mifugo kama vile na yeye ni mfugo badala ya kutengeneza au kuzalisha chakula cha mifugo na kufuga kisasa tena kama kampuni inayojitosheleza na mahitaji ya mifugo yake Sasa watu wenye akili za kizamani kama hizi wataweza kuzungusha uchumi kiasi cha wenye madaraka kutetemeka na kufanya mambo makubwa? Maana watu wakifanya mambo kisasa yanaleta ajira nyingi sana mfano elimu ya English medium inaajili watu wengi kuliko hizi za kata na hata huduma zingine kama kilimo kikiwa kisasa kinaleta pesa nyingi na ajira nyingi.
Pia baadhi ya wananchi kupenda kulalamikia serekali pasipo kujituma na kusubiri kufanyiwa kila kituTanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.
Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:
1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,
Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.
Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.
Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!
Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Yaani kama ulikuwa kwenye kichwa changu. Uliyosema yote ni kweli kabisa. Nini kifanyike? Misingi imekosewa tayari.Tanzania, kwa historia yake, rasilimali zake (watu na mali) na amani yake ingekuwa moja ya nchi tano Afrika zinazoongoza. Lakini kiuhalisia, inashindwa mbali na vinchi kama Senegal, Cote d'Ivoire, Botswana, Ghana. Ingawaje tuna GDP kubwa kuliko nchi hizo.
Hakuna mchawi, isipokuwa tumeanza vibaya baada ya kupata uhuru, na hadi sasa baadhi ya makosa yaleyale tunaendelea nayo. Makosa makubwa:
1 - Kushabikia mno siasa kuliko uchumi
2 - Kupuuza elimu na rasilimali watu
3 - Kupuuza kilimo ambacho ndiyo mategemeo ya wengi
4 - Kutokuwa na viongozi wengi wenye upeo wa fikra na exposure (matokeo yake kiongozi mmoja anadiriki kudai kujua kila kitu, mungu mtu)
5 - Kutokuwa na dira, stability ya sera za uongozi (kila kiongozi anaanza upya)
6 - Kupuuza Kiingereza (hii watu hawataifahamu, lakini ni kweli nchi za Afrika ambazo raia wake wengi wanafahamu Kiingereza,
Kifaransa, Kireno, Kijerumani, Kispaniola, Kiarabu, huwa akili zao, taste zao zimeendelea zaidi kwa vile wana nchi za kuiga zilizoendelea kuliko wao.
Hii ni kwa sababu raia hao ni rahisi ku 'incoporate' fikra mpya kama zile zilizoko kwenye nchi hizo zilizoendelea. Katika nchi za Afrika zilizoendelea sana katika kukumbatia fikra mpya: Social media, capital ventures, masoko ya hisa, Bitcoin na innovations za aina mbali mbali ni zile zenye uelewa mkubwa wa lugha hizo.
Nimetazama katika nchi 15 za Afrika zinazotabiriwa kuona mapinduzi makubwa ya 'start up tech ventures' Tanzania haimo! Hakuna shaka ni kwa sababu ya lugha. Ukitazama matumizi ya Twitter, WhatsApp, na social platforms nyingine katika nchi za Kenya na Uganda utaona namna gani Tanzania iko nyuma. Lugha!
Hii haina maana tusijivunie Kiswahili na tusifundishe kwa Kiswahili. Tatizo ni kwamba bado hatujakifanyia kazi Kiswahili kiasi ambacho kinastahiki kuwa lugha ya kufundishia. Huwezi kupata hata vitabu 10 vya rejea kwa katika fani yeyote!
Njia pekee ni kwa watawala kuwaogopa wananchi kwamba wanaweza kuwaondoa madarakani pale wanapoleta ujinga kama huu wanaofanya ccm, sasa kwa bahati mbaya sana Tanzania ccm hawana hiyo hofu kwa sababu wanafahamu fika kwamba wananchi hawana jeuri ya kuwaondoa kwa sababu nchi imefikia hatua ambapo sasa hata uchaguzi haupo tena ni uhuni tu unafanywa.Wewe ndo pumba kwa kuwa unadanganyika kuwa Chama ndo Shida ya maendeleo yetu. Utasubiri sana. Hata hivyo Tz tuko vizuri. Sijui unajifananisha na nani. You can not have it all my brother.
Viongozi Ni wachache sana kuliko hao mliopo maofisni na wakamilishaji miradi. Huko ndo wanaiba sana hela zetu na kujenga.
Wanaopindisha mambo wengi wako mkoani na wilayani. Hao Ni wanachama wa vyama vyote.
Wavivu Ni wanachama wa vyama vyote
Wengi tumesoma ulaya na Marekani. Vyuo Bora. Lakini tukirudi tunataka tuibe haraka au tunakutana na wale wa la saba la mwaka 1947, kila ukipendekeza mabadiliko Utaskia wenzako ulitukuta na utatuacha.
Akitoke kiongozi mkali wa kutaka actions. Mnaanza wenyewe siasa.
Watz mmejiroga. Na siku mtakayokubali kukaa chini kajitafakari na kuacha kunyoesheana vidole ndo siku ya ushindi.
Nini kifanyike?Yaani kama ulikuwa kwenye kichwa changu. Uliyosema yote ni kweli kabisa. Nini kifanyike? Misingi imekosewa tayari.
Kiswahili lugha ya nani?Kingereza kisingeweza kuunganisha makabila zaidi ya 100 yaliyopo hapa Tanzania. Wengi wangerudia kuongea lugha za makabila yao maana kingereza ni kigumu na ni lugha ya kigeni. Na hicho kingeleta ukabila alioupiga vita Nyerere.