mngony
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 5,555
- 6,972
Jasusi ni mtu anayechukua au kukusanya taarifa za nchi nyingine zinazochukuliwa kuwa ni siri bila ya ruhusa. Kwa upande wa anakopeleka taarifa hizo huwa ni faida lakini kwa upande anakozichukua huwa ni hasara kulingana na taarifa ziilizochukuliwa.
Jasusi huyo anaweza kuwa wakigeni, yaani kutoka nje ya nchi au wanyumbani yaani wa nchi husika ambaye hugeuka kuwa Double agent na huyu ndio huwa hatari zaidi hasa anapokuwa katika nafasi ambazo zinamuwezesha kuzipata taarifa mbalimbali kwani anakuwa ameaminiwa na huwa vigumu kumgundua japo hupatikana kulingana na ubora wa counter-intelligence measures za nchi husika, lakini kama hakuna tips au viashiria vyovyote kumgundua mwingine anaweza hadi kufa au kustaafu na asijulikane.
Tabia ya majasusi kuiba siri za nchi nyingine ni sehemu ya maisha yenyewe ya ujasusi, jinsi gani upo smart kupata taarifa za mwenzako either adui, au jirani au mshindani ndio jinsi utakavyokuwa bora.
Hawa double agent wanapatikana kwa kuwa spotted na maadui kwa kuchunguzwa vizuri na kisha kufuatwa au wenyewe ku-offer service kwa kujipeleka kwa sababu mbalimbali. Sehemu nyingie ambazo hawa double agent hupatikana ni pale nchi zetu zinazoendelea zinavyopeleka watu wetu nje kupata mafunzo zaidi kama vile MAREKANI, UINGEREZA n.k kwa vile wao ndio wanaendesha mafunzo ni rahisi kuwa-spot wale ambao ni the best kisha kuwa-approach wakijua watakuja kupata nafasi nzuri na nyeti sana katika taasisi zetu.
Hawa wa nje wapo tu hawazuliki, wengine wafanyabiashara, wanafunzi, wanadiplomasia, kwenye mashirika ya kimataifa, NGO's n.k. hakuna jinsi ya kuwazuia wakija kwa njia hii suala huwa ni kulimit tu wasipate taarifa za ndani, hawa wanaweza kupata taarifa za kawaida kupitia vyanzo vya wazi kama kupitia mitandao, magazeti, midahalo, bunge, n.k mfano yanayoendelea sasa kuhusu mijadala ya muungano wetu n.k ni wazi yanajulikana tu.
Sasa hawa wa ndani, ambao huigeuka nchi yao na kuisaliti kwa kutoa siri ndio hatari zaidi kulingana na nafasi aliyopo, kiasi cha muda wa usaliti wake na uwezo wake wa kujificha asijulikane. Hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea jasusi kuisaliti nchi yake.
1.PESA
Hii ndio motivating factor kubwa kabisa ya jasusi kuisaliti nchi yake kwa nchi nyingine, ndio maana hawa jamaa hulipwa vizuri kadri inavyowezekana. Sasa ikitokea either haridhiki na anachokipata kwa sababu zake binafsi kama vile kutaka kuishi maisha ya gharama au tu anahisi mshahara haumtoshelezi hivyo wakitokea watu wakamuahidi kiasi kikubwa cha pesa anaona atoe siri apate hizo pesa. Mfano ni jamaa mmoja John Walker alikuwa mtaalamu wa mawasiliano mwenye cheo cha Warrant Officer katika jeshi la maji la Marekani ambaye alipatikana na hatia ya ku-spy kwa ajili ya Soviet( Russia ya zamani) kuanzia mwaka 1968-1985. Motive yake ilikuwa pesa kwani alikuwa na matatizo ya kiuchumi.
2. MTIZAMO, UZALENDO,IMANI NA UTAMADUNI
Kutofautiana kimtazamo na either jinsi nchi inavyoongozwa au sera zinazoongoza nchi mfano Kim Philby alikuwa agent wa shirika la kijasusi la uingereza MI6 aliamua ku-spy kwa ajili Soviet union kwa kuwa alikuwa akiamini katika ukomunist, mwingine ni Fritz Kolbe alikuwa mwanadiplomasia katika wizara ya mambo ya nje ya ujerumani, aliamua ku-spy kwa ajili ya wamarekani katika vita ya pili ya dunia kwa kuwa hakukubalina na sera za u-nazi.
Jonathan Pollard mmarekani mwenye asili ya uyahudi aliamua kuiba siri kuhusu jeshi la marekani kuzipeleka Israel akiwa katika kitengo cha intelijensia ya jeshi mwaka 1987, alipewa kifungo cha maisha ila anatarajiwa kutolewa mwakani.
Pia hii ya uzalendo, imani na utamaduni ndio silaha kubwa iliyotumiwa na Isreal kupata majasusi wengi katika nchi nyingi maadui zake hasa nchi za kiarabu ambao walikuwa wakipeleka taarifa na ikawa moja ya sababu ya kushinda kwa urahisi kabisa vita vile vya siku sita, kwani wahusika walijihisi wayahudi zaidi kuliko utaifa wa mataifa waliyozaliwa na ndio sababu pia Israel ilikuwa ikiwachunguza sana waisrael waarabu kiasi cha kutengeneza kikosi maalum kilichopelekwa kujipenyeza katika jamii hizo za kiarabu, japo ni raia waisreal lakini walihofiwa kutumiwa na mataifa ya kiarabu kutokana na uarabu wao.
Nadhani ndio maana kipindi fulani tulikuwa na uhusiano wa kusuasua na nchi moja jirani watu walianza kuhoji wale wenye asili ya huko walio sehemu nyeti kama ikulu, ni kwa sababu kama hii.
3.KULAZIMISHWA KWA KUTISHWA
Kutishiwa maisha ya familia yake au uhai wake, akaambiwa alete taarifa au siri juu jambo fulani ili yeye au familia iwe salama. Au una siri fulani ambayo hutaki Mwajiri wako(Shirika lako la kijasusi) aijue na inawezekana wakiijua ajira imekwisha, unaamwa tuoe tasrifa kuhusu kitu fulani, ukishapeleka tu wanaweza kusema uendelee kuwaletea usipofanya hivyo watatoa siri kuwa ulifanya uhaini kwa kuwaletea siri pale mwanzo inakuwa ndo tayari maisha yako u double agent. mfano Mathilde Carre alikuwa member wa french resistance waliokuwa wakipambana ufaransa dhidi ya uvamizi wa wa-nazi wakati wa vita ya pili ya dunia alikamatwa na nazi wamtishia maisha na akatakiwa akachukue taarifa awaletee wao. Akakubalia akawa anawaletea taarifa kwa ajili ya kuhofia vitisho vyao
4.KUTOKUTHAMINIWA
Inaweza kujitokeza pale mtu anajihisi anafanya kazi nzuri na kubwa akihitaji kuthaminiwa lakini hawi appreciated akionekana mtu mdogo tu wa kawaida, huku yeye akijiona bora kuliko wanaomzunguka na amekuwa akifanya makubwa. Anaweza kuamua kwenda kwa mshindani ku-offer his service. mfano ni Robert Hanssen, alikuwa agent wa FBI akaamua ku-spy kwa ajili ya Warusi kuanzia mwaka 1979-2001 alijion hapewi thamani a kuchukuliwa umuhimu kwa kazi aliyokuwa akifanya(aliona anafaya makubwa lakii anaonekana mdogo). Alikuwa Arrogant sana na ni katika doube agent aliyeiumiza sana marekani kwa kuiba siri nyingi na kupeleka Urusi, mfano kipindi hicho Warusi walijua siri nyingi za kijeshi kiasi kama wangeingia vitani basi ilikuwa shughuli nzito sana kwa marekani, warusi walijua kila submarine ya marekani ilipo.
Karibuni kwa michango
Jasusi huyo anaweza kuwa wakigeni, yaani kutoka nje ya nchi au wanyumbani yaani wa nchi husika ambaye hugeuka kuwa Double agent na huyu ndio huwa hatari zaidi hasa anapokuwa katika nafasi ambazo zinamuwezesha kuzipata taarifa mbalimbali kwani anakuwa ameaminiwa na huwa vigumu kumgundua japo hupatikana kulingana na ubora wa counter-intelligence measures za nchi husika, lakini kama hakuna tips au viashiria vyovyote kumgundua mwingine anaweza hadi kufa au kustaafu na asijulikane.
Tabia ya majasusi kuiba siri za nchi nyingine ni sehemu ya maisha yenyewe ya ujasusi, jinsi gani upo smart kupata taarifa za mwenzako either adui, au jirani au mshindani ndio jinsi utakavyokuwa bora.
Hawa double agent wanapatikana kwa kuwa spotted na maadui kwa kuchunguzwa vizuri na kisha kufuatwa au wenyewe ku-offer service kwa kujipeleka kwa sababu mbalimbali. Sehemu nyingie ambazo hawa double agent hupatikana ni pale nchi zetu zinazoendelea zinavyopeleka watu wetu nje kupata mafunzo zaidi kama vile MAREKANI, UINGEREZA n.k kwa vile wao ndio wanaendesha mafunzo ni rahisi kuwa-spot wale ambao ni the best kisha kuwa-approach wakijua watakuja kupata nafasi nzuri na nyeti sana katika taasisi zetu.
Hawa wa nje wapo tu hawazuliki, wengine wafanyabiashara, wanafunzi, wanadiplomasia, kwenye mashirika ya kimataifa, NGO's n.k. hakuna jinsi ya kuwazuia wakija kwa njia hii suala huwa ni kulimit tu wasipate taarifa za ndani, hawa wanaweza kupata taarifa za kawaida kupitia vyanzo vya wazi kama kupitia mitandao, magazeti, midahalo, bunge, n.k mfano yanayoendelea sasa kuhusu mijadala ya muungano wetu n.k ni wazi yanajulikana tu.
Sasa hawa wa ndani, ambao huigeuka nchi yao na kuisaliti kwa kutoa siri ndio hatari zaidi kulingana na nafasi aliyopo, kiasi cha muda wa usaliti wake na uwezo wake wa kujificha asijulikane. Hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea jasusi kuisaliti nchi yake.
1.PESA
Hii ndio motivating factor kubwa kabisa ya jasusi kuisaliti nchi yake kwa nchi nyingine, ndio maana hawa jamaa hulipwa vizuri kadri inavyowezekana. Sasa ikitokea either haridhiki na anachokipata kwa sababu zake binafsi kama vile kutaka kuishi maisha ya gharama au tu anahisi mshahara haumtoshelezi hivyo wakitokea watu wakamuahidi kiasi kikubwa cha pesa anaona atoe siri apate hizo pesa. Mfano ni jamaa mmoja John Walker alikuwa mtaalamu wa mawasiliano mwenye cheo cha Warrant Officer katika jeshi la maji la Marekani ambaye alipatikana na hatia ya ku-spy kwa ajili ya Soviet( Russia ya zamani) kuanzia mwaka 1968-1985. Motive yake ilikuwa pesa kwani alikuwa na matatizo ya kiuchumi.
2. MTIZAMO, UZALENDO,IMANI NA UTAMADUNI
Kutofautiana kimtazamo na either jinsi nchi inavyoongozwa au sera zinazoongoza nchi mfano Kim Philby alikuwa agent wa shirika la kijasusi la uingereza MI6 aliamua ku-spy kwa ajili Soviet union kwa kuwa alikuwa akiamini katika ukomunist, mwingine ni Fritz Kolbe alikuwa mwanadiplomasia katika wizara ya mambo ya nje ya ujerumani, aliamua ku-spy kwa ajili ya wamarekani katika vita ya pili ya dunia kwa kuwa hakukubalina na sera za u-nazi.
Jonathan Pollard mmarekani mwenye asili ya uyahudi aliamua kuiba siri kuhusu jeshi la marekani kuzipeleka Israel akiwa katika kitengo cha intelijensia ya jeshi mwaka 1987, alipewa kifungo cha maisha ila anatarajiwa kutolewa mwakani.
Pia hii ya uzalendo, imani na utamaduni ndio silaha kubwa iliyotumiwa na Isreal kupata majasusi wengi katika nchi nyingi maadui zake hasa nchi za kiarabu ambao walikuwa wakipeleka taarifa na ikawa moja ya sababu ya kushinda kwa urahisi kabisa vita vile vya siku sita, kwani wahusika walijihisi wayahudi zaidi kuliko utaifa wa mataifa waliyozaliwa na ndio sababu pia Israel ilikuwa ikiwachunguza sana waisrael waarabu kiasi cha kutengeneza kikosi maalum kilichopelekwa kujipenyeza katika jamii hizo za kiarabu, japo ni raia waisreal lakini walihofiwa kutumiwa na mataifa ya kiarabu kutokana na uarabu wao.
Nadhani ndio maana kipindi fulani tulikuwa na uhusiano wa kusuasua na nchi moja jirani watu walianza kuhoji wale wenye asili ya huko walio sehemu nyeti kama ikulu, ni kwa sababu kama hii.
3.KULAZIMISHWA KWA KUTISHWA
Kutishiwa maisha ya familia yake au uhai wake, akaambiwa alete taarifa au siri juu jambo fulani ili yeye au familia iwe salama. Au una siri fulani ambayo hutaki Mwajiri wako(Shirika lako la kijasusi) aijue na inawezekana wakiijua ajira imekwisha, unaamwa tuoe tasrifa kuhusu kitu fulani, ukishapeleka tu wanaweza kusema uendelee kuwaletea usipofanya hivyo watatoa siri kuwa ulifanya uhaini kwa kuwaletea siri pale mwanzo inakuwa ndo tayari maisha yako u double agent. mfano Mathilde Carre alikuwa member wa french resistance waliokuwa wakipambana ufaransa dhidi ya uvamizi wa wa-nazi wakati wa vita ya pili ya dunia alikamatwa na nazi wamtishia maisha na akatakiwa akachukue taarifa awaletee wao. Akakubalia akawa anawaletea taarifa kwa ajili ya kuhofia vitisho vyao
4.KUTOKUTHAMINIWA
Inaweza kujitokeza pale mtu anajihisi anafanya kazi nzuri na kubwa akihitaji kuthaminiwa lakini hawi appreciated akionekana mtu mdogo tu wa kawaida, huku yeye akijiona bora kuliko wanaomzunguka na amekuwa akifanya makubwa. Anaweza kuamua kwenda kwa mshindani ku-offer his service. mfano ni Robert Hanssen, alikuwa agent wa FBI akaamua ku-spy kwa ajili ya Warusi kuanzia mwaka 1979-2001 alijion hapewi thamani a kuchukuliwa umuhimu kwa kazi aliyokuwa akifanya(aliona anafaya makubwa lakii anaonekana mdogo). Alikuwa Arrogant sana na ni katika doube agent aliyeiumiza sana marekani kwa kuiba siri nyingi na kupeleka Urusi, mfano kipindi hicho Warusi walijua siri nyingi za kijeshi kiasi kama wangeingia vitani basi ilikuwa shughuli nzito sana kwa marekani, warusi walijua kila submarine ya marekani ilipo.
Karibuni kwa michango