BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 525
- 1,257
KESI ya uhujumu uchumi na rushwa inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne, itatajwa kwa mara ya pili leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi.
Ole Sabaya na wenzake, ambao ni Sylvester Nyegu, John Aweyo, Nathan Msuya na Antoro Assey, wanakabiliwa na mashtaka mapya saba, ikiwamo kuongeza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha, vitendo vya kuomba na kupokea rushwa pamoja ukiukwaji wa maadili ya kiutumishi.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, kosa la kwanza katika kesi hiyo ambalo linawahusu washtakiwa wote ni la kuongoza na kushiriki genge la uhalifu katika Wilaya ya Hai, Februari 2, mwaka jana.
Shtaka la pili, linamkabili mshtakiwa wa kwanza, Lengai Ole Sabaya, ambalo anadaiwa kulifanya Februari 22, mwaka jana, kwa kuomba rushwa ya milioni 30 kutoka kwa Godbless Swai katika eneo la Bomangombe, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Katika shtaka la tatu, Ole Sabaya peke yake, anadaiwa kujipatia rushwa ya milioni 30 kutoka kwa Elibariki Swai, kwa nia ya kuzuia taarifa za uchunguzi zilizohusiana na ukwepaji wa kodi.
Wakati shtaka la nne na la tano, linawakabili mshtakiwa wa pili, tatu, nne na tano, ambalo ni kumsaidia mshtakiwa wa kwanza (Ole Sabaya), kushawishi na kujipatia manufaa asiyostahili ya Sh. milioni 30 kutoka kwa Alex Swai, huku akijua ni kinyume na sheria.
Shtaka la sita linamkabili mshtakiwa wa kwanza (Ole Sabaya), ambalo ni ukiukwaji wa maadili ya utumishi, akiwa ni mtumishi wa umma katika Wilaya ya Hai, na shtaka la saba ni utakatishaji wa fedha, ambalo linawakabili washtakiwa wote.
========================
KESI INAYOMKABILI SABAYA YAAHIRISHWA HADI JUNI 20, 2022
Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake 4 imeahirishwa mpaka Juni 20, 2022 kwa ajili ya kutajwa. Kesi hiyo imeahirishwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Moshi Salome Mshasha.
Mawakili upande wa utetezi wakiongozwa wameiomba Mahakama kuharakisha upande wa Jamhuri kukamilisha ushahidi wao ili mtuhumiwa namba moja Sabaya akatibiwe uvimbe uliopo kichwani baada ya kupata ajali pindi akiwa kazini kwa kuwa ni mgongwa.
#JamiiForums
Ole Sabaya na wenzake, ambao ni Sylvester Nyegu, John Aweyo, Nathan Msuya na Antoro Assey, wanakabiliwa na mashtaka mapya saba, ikiwamo kuongeza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha, vitendo vya kuomba na kupokea rushwa pamoja ukiukwaji wa maadili ya kiutumishi.
Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, kosa la kwanza katika kesi hiyo ambalo linawahusu washtakiwa wote ni la kuongoza na kushiriki genge la uhalifu katika Wilaya ya Hai, Februari 2, mwaka jana.
Shtaka la pili, linamkabili mshtakiwa wa kwanza, Lengai Ole Sabaya, ambalo anadaiwa kulifanya Februari 22, mwaka jana, kwa kuomba rushwa ya milioni 30 kutoka kwa Godbless Swai katika eneo la Bomangombe, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Katika shtaka la tatu, Ole Sabaya peke yake, anadaiwa kujipatia rushwa ya milioni 30 kutoka kwa Elibariki Swai, kwa nia ya kuzuia taarifa za uchunguzi zilizohusiana na ukwepaji wa kodi.
Wakati shtaka la nne na la tano, linawakabili mshtakiwa wa pili, tatu, nne na tano, ambalo ni kumsaidia mshtakiwa wa kwanza (Ole Sabaya), kushawishi na kujipatia manufaa asiyostahili ya Sh. milioni 30 kutoka kwa Alex Swai, huku akijua ni kinyume na sheria.
Shtaka la sita linamkabili mshtakiwa wa kwanza (Ole Sabaya), ambalo ni ukiukwaji wa maadili ya utumishi, akiwa ni mtumishi wa umma katika Wilaya ya Hai, na shtaka la saba ni utakatishaji wa fedha, ambalo linawakabili washtakiwa wote.
========================
KESI INAYOMKABILI SABAYA YAAHIRISHWA HADI JUNI 20, 2022
Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake 4 imeahirishwa mpaka Juni 20, 2022 kwa ajili ya kutajwa. Kesi hiyo imeahirishwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Moshi Salome Mshasha.
Mawakili upande wa utetezi wakiongozwa wameiomba Mahakama kuharakisha upande wa Jamhuri kukamilisha ushahidi wao ili mtuhumiwa namba moja Sabaya akatibiwe uvimbe uliopo kichwani baada ya kupata ajali pindi akiwa kazini kwa kuwa ni mgongwa.
#JamiiForums