Sabaya: Haki Imetendeka na kuonekana ikitendeka

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Tathmini ya msingi inaonesha watu wengi kufurahishwa na hukumu ile bila kujali nini kitamtokea sasa baada ya hapa.

Waliokuwa wapambe wake katika uovu, mitaani na mitandaoni wote wamesambaratika. Hivi Wamepotelea mashimoni kama mapanya wakichungulia kama vile hawakuwahi kuwapo wala kusema jambo 😁😁.



Sabaya angenusuriwa vipi, na nani katika hali kama hii:

Your browser is not able to display this video.


Hiyo mahakama ingeeleweka kweli hata kwa wapambe wake tu?

"U haki wa hukumu kwa mshitakiwa ni furushi lote lijumuishalo kuzingatiwa sheria na muonekano wa uwazi wenye kuonyesha bayana ushahidi na sheria zinazingatiwa."

Kwa hakika kwa wahanga wa nduli Sabaya Mungu awape nini?

Haki imetendeka.
 
Mambo mengine yanakuja Kama elimu ili kila mtu apate kujifunza...........Sabaya amewafunza watu wengi kuwa wakipata uongozi waishi vipi japo wapo waliokua wakipata malipo juu ya kutumia vyeo na mamlaka yao vinabaya lakini walikua wanachukulia labda ni fitna tu au wamelogwa na wapinzani wao ila hapa pa OLE pana mazingatio sana.
 

Sabaya na wenzake wengi bado wapo uraiani, walitufikisha hapa:

Your browser is not able to display this video.


Samia anayo nafasi bado ya kuchagua kunyoa au kusuka.

Asilaumiwe Mdude.

Cc: Jumbe Brown
 
Ni funzo....

Wanaotaka kutuharibia nchi hawa itapendeza kuwakabili kwa umoja wetu bila kujali vyeo vyao.

Kweli nani kwa dhati yake moyoni, anaweza kuwa na taabu na haki, usawa, uhuru na demokrasia?
 
Hope leo una imani na mahakama, ndio maana nakwambia haya mambo ni hatua, kama mahakama zipo na majaji/mahakimu wapo, muhimu waachiwe kazi yao wafanye, wakienda kinyume na matarajio ya wengi, haki ya kukata rufaa ipo.
 
Mwanasheria wa Sabaya anadai kuwa adhabu aliopewa Sabaya ni ndogo😁😁😁
Your browser is not able to display this video.
 
Hope leo una imani na mahakama, ndio maana nakwambia haya mambo ni hatua, kama mahakama zipo na majaji/mahakimu wapo, muhimu waachiwe kazi yao wafanye, wakienda kinyume na matarajio ya wengi, haki ya kukata rufaa ipo.

Mkuu nakusoma vyema na heshima kwako kwa kweli.

Tuko pamoja.

Uthibitisho kamili kuwa nia yetu ni timamu. Uhuru kamili wa mihimili si jambo la kufanyiwa ajizi.

Hatutaki kuishi kwa hofu nchini mwetu wenyewe.

Washindwe wote wasiozingatia PGO!
 
Matukio yake yalikuwa yanaacha alama za ushahidi nyuma yake na kwa maelezo aliyoyatoa mahakamani na kwa kuzingatia sheria ilikuwa ni vigumu kwa sasa kuchomoka.
 
Matukio yake yalikuwa yanaacha alama za ushahidi nyuma yake na kwa maelezo aliyoyatoa mahakamani na kwa kuzingatia sheria ilikuwa ni vigumu kwa sasa kuchomoka.

Angeshinda kesi pale ingekuwa sokomoko
 
Bado ana kesi kibao za kujibu mpaka anyooke.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…