Sabuni ya jamaa na Tanzania ya viwanda

Sabuni ya jamaa na Tanzania ya viwanda

Msisahau na chumvi, sehemu kubwa ya chumvi nzuri inayouzwa Tanzania inatoka Mombasa, afadhali kidogo sasa ivi nimeona chumvi nyeupe toka Kigoma ila cjui kama wana mpango wa kushindana na zile za Kenya! Tatizo kubwa la wazalishaji wa tz wanakosa ubunifu.
Ngoja tutengeneze jamaa feki
 
Mbuni was the best enzi za Mwalimu
Mbuni iliyotengenezwa Mwanza kama ingekuwa inasmbazwa Tanzania leo Jamaa soap isingetamba kabisa. Hata Foma detergent ya enzi za mwalimu ilikuwa inacompete vizuri na Omo enzi hizo.

Mfano bora Wa bidhaa ya Tanzania imebakia Whitedent tooth paste. Tatizo la mabepari uchwara Tanzania wakipewa viwanda wanapunguza baadhi ya ingredients na kuua ubora , lengo likiwa kupata faida kubwa sana . Hata mafuta ya Okay ya lake oil yalikuwa mazuri tu, ila sasa ufisadi ulishaua viwanda vyote vizuri au hata makodi makubwa yanachangia. Nawapongeza whitedent siwezi kutumia dawa tofauti na hiyo.

Whitedent anamiliki 80% ya soko Tanzania.Kizuri kinajiuza na kibaya kinajitembeza. Hatuwezi kuhubiriwa eti penda bidhaa ya Tanzania jenga nchi yako. Weka good quality products huhitaji kutoa povu kupromote .

Kuna mafuta fulani yaalizeti kiwanda cha mchina yanaitwa Rafiki oil yakija mdukani huwa stock ya mwaka mzima yanaisha kwa miezi 3 tu.

Lakini wengi watalaumu wananchi kumbe kosa ni lao kudhani kuwa tunahitaji substandard products mradi being ni chini. Kama sio upepo kubadiika ilikuwa imefikia tunaanza kupata middle class wanaoangalia ubora sio bei muda huu.
 
Labda na pato la mtanzania linachangia kutoa viwanda vya bidhaa duni. Kama leokuns bado kuna sabuni za magwanji zenye caustic soda ya kuchubua mikono na inauzwa vizuri tusiwalaumu sana .
 
So hizo bidhaa mnazotumi zinazalishwa wapi??

Naona unaanza ubishi tuu
Zipo zinazotoka hadi sauzi, zingine UK n.k angalia vzuri details kwenye kopo lako mkuu. Tatizo wabongo tumekariri tukiona NIDO tu tunajua imetoka Kenya.
 
Watanzania hatuko serious wala hatufanyi kazi kwa.weledi tunaongea siasa taka tuuu。mchana kutwa likiwanda lipo linazindua tena sasa akili za kuboresha tutatoa wapi?

Ni watu waongo waongo kuanzia juu chini.aah
 
Kaaa, kumbe hii sabuni inatoka Kenya, binafsi kwangu ndo hii inatamba. Tanzania bado tunasafari ndefu sana
 
Waulize ccm zile sabuni zetu zilizotengenezwa na kiwanda chetu zilipotelea wapi
 
Shida ni siasa....
Bongo Nyoso sana. Ukiwa na kiwanda wanataka wawe wanakutumia kisiasa kama ilivyo kwa Antonio Diallo.
Wanataka uwe mlezi wa WANA
Wanataka uwe mlezi wa ccm Mara kaja Kiongozi ukaonane nae mwisho wa siku watu wanakukata na mabiashaara yako

Tatizo ni siasa apa Tanzania
 
Hapa home, tunaitumia hiyo sabuni ya jamaa kufulia, kuogea na kuosha vyombo
 
Kweli kabisa Sabuni ya jamaa,mafuta ya nazi ya minara,colgate,omo,ariel,blue band yaani bidhaa za uniliver hazina mshindani tanzania.Kuna masabuni ya unga ya MO ukifulia mikono lazima itoke vipele
Mo jamaa mjanja mjanja sana yani product zake za ovyo sana.
hizo sabuni zake ukifulia lazima uchubuke mikono
 
Kabisa Mkuu tizama walivyoisambaratisha Tanesco kwa kuingiza siasa ili walazimishe mikataba yao mbali mbali ya kifisadi. Mikataba ya IPTL, Escrow, Richmond, Umeme wa gas etc yote hii ilijaa ufisadi wa kutisha na haikuwa na maslahi yoyote kwa Watanzania bali kwa hili genge la wahuni ndani ya Serikali kuanzia fisadi Mkapa, Kikwete na huyu fisadi dhalimu. Matokeo yake Tanesco ambalo lilikuwa moja ya mashirika bora nchini sasa hivi limegubikwa na madeni makubwa mno na mikataba hiyo kusababisha Tanesco iendeshwe kwa hasara kubwa miaka nenda miaka rudi.
Acha siasa mkuu.
Kwani tatizo serikali au sisi wenyewe?
Kwani viwanda hazipo? Je wataalam wabunifu wapo?
Au vyuo vikuu vinazalisha wanasiasa zaidi kuliko wanasayansi?
 
We rais mwenyew anasema cherehani moja ni kiwanda, mawazo ya wazir wake ni vyerehani vinne. Sasa saa ngap utashindana na wenzetu wenye mawazo ya kurusha satellite yao.
 
nje ya mada kidogo hivi baada ya ile blue band ya kibongo kwa jina Tandbond kupotea kuna kiwanda cha blueband tena hapa bongo?
 
Mbuni iliyotengenezwa Mwanza kama ingekuwa inasmbazwa Tanzania leo Jamaa soap isingetamba kabisa. Hata Foma detergent ya enzi za mwalimu ilikuwa inacompete vizuri na Omo enzi hizo.Mfano bora Wa bidhaa ya Tanzania imebakia Whitedent tooth paste. Tatizo la mabepari uchwara Tanzania wakipewa viwanda wanapunguza baadhi ya ingredients na kuua ubora , lengo likiwa kupata faida kubwa sana . Hata mafuta ya Okay ya lake oil yalikuwa mazuri tu, ila sasa ufisadi ulishaua viwanda vyote vizuri au hata makodi makubwa yanachangia. Nawapongeza whitedent siwezi kutumia dawa tofauti na hiyo. Whitedent anamiliki 80% ya soko Tanzania.Kizuri kinajiuza na kibaya kinajitembeza. Hatuwezi kuhubiriwa eti penda bidhaa ya Tanzania jenga nchi yako. Weka good quality products huhitaji kutoa povu kupromote . Kuna mafuta fulani yaalizeti kiwanda cha mchina yanaitwa Rafiki oil yakija mdukani huwa stock ya mwaka mzima yanaisha kwa miezi 3 tu. Lakini wengi watalaumu wananchi kumbe kosa ni lao kudhani kuwa tunahitaji substandard products mradi being ni chini. Kama sio upepo kubadiika ilikuwa imefikia tunaanza kupata middle class wanaoangalia ubora sio bei muda huu.
Nani asambaze? Si mwenye kiwanda ndo anatakiwa asambaze au! tupo katika soko huria. Ukitoa product hafifu unatolewa kwenye soko.
 
Mo soap
Bakhresa soap
Mengi soap
Patel soap
Azania soap.

Sabuni nyingi tu zipo hapa nchini zenye ubora kabisa.
[emoji1] [emoji23] [emoji119] [emoji119] [emoji119]
 
Usifananishe jamaa na sabuni za ajabu
 
Shida ni siasa....

Hivi katika hali ya kawaida shida ni siasa au hawa jamaa wenye viwanda nchini kutokubadilika na kutumia teknolojia ya kisasa katika uzalishaji au kutojua waumudu vipi ushindani huu wa soko huria?

Mimi nafikiri si siasa tatizo ni wenye viwanda tulionao.

Kuna chumvi inaitwa kaysalt toka Kenya ina ubora wa hali ya juu kuanzia chumvi yenyewe hadi kifungashio. Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na viwanda kadhaa vya chumvi
ikiwepo malindi salt.

Kutokana na ubovu wa vifungashio(muonekano) na chumvi yenyewe, kaysalt ilipenya kwa urahisi sana soko la Tanzania na viwanda vya ndani kwa kutobadilika vikapotea mazima.
Huu ni mfano mdogo na ipo mingi sana.
 
Back
Top Bottom