Sadaka kumpa mzazi ni bora kuliko kuipeleka kwenye nyumba za ibada

Sadaka kumpa mzazi ni bora kuliko kuipeleka kwenye nyumba za ibada

safuher

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2019
Posts
11,837
Reaction score
17,412
Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo?

Baba je?

Ndugu wengine wa karibu?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee, hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini Mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza, sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi. Sina maana ya kukosoa sadaka lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi, tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema, sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; Kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
 
Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo ?

Baba je ?

Ndugu wengine wa karibu ?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee,hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza,sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi.sina maana ya kukosoa sadaka,lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema,sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
Ungeongeza sauti kidogo ili wakuje!!!
 
Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo ?

Baba je ?

Ndugu wengine wa karibu ?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee,hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza,sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi.sina maana ya kukosoa sadaka,lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema,sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
Nami huwa nafanya hivi.

Zaka/Sadaka ni tafsiri tu. Sio lazima uweke yote kwenye chombo cha sadaka kanisani au msikitini. Japo ni muhimu kuchangia huduma na ustawi sehemu tunazoabudu.

Wahitaji/wasiojiweza ikiwemo wazazi na ndugu hakikisha wanapata msaada utokanao na kipato chako bila kutarajia manufaa fulani kutoka kwao
 
Nyumbani kwa wazazi hupeleki Sadaka. Unapeleka Matumizi.

Sadaka ipelekwe Kanisani.

Pia saidia Maskini na wajane.

Fedha unayoipeleka Nyumbani/ kwa wazazi si alternative ya Sadaka.
Hata hiyo ya kanisani itaenda kutumiwa hivyo nayo ni matumizi.

Sadaka ni neno tu lakini lengo ni moja kufanya matumizi.
 
Kuna watu “wameweka heshima” church kwenye kujenga majengo wakati Mama zao wanaishi kwenye vibanda vya mbwa huko vijijini.

Hii laana haiwezi kumuacha mtu salama!
Kosa la aliyemuoa
 
Dini zinafukarisha watu zaidi kuliko kuwaisaidia.

Hapana ni kutokujua tu na kuisoma, unaambiwa sadaka nzuri inaanzia kwako kwanza. Kama ndani kwako wana shida anza kuwasaidia wao halafu ndiyo uende nje. Unataka umsaidie labda jirani wakati kwenye familia yako kuna ndugu yako ana tatizo kama hilo anza na yeye kwanza.

Ukilitatua unaenda kusaidia nje, tatizo siyo dini. Tatizo waliozileta walizileta kwa malengo yao watupige, Dini hazina tatizo wala nini mfano uislam ulikuja na waarabu enzi za biashara ya utumwa walikuwa wamekuja kufanya biashara wakaleta dini wawapige watu na ukristo pia waliuleta missionari ili watupige mali zetu. Utagundua wao ndiyo walitumia dini kama kichaka tu ila dini zenyewe hazielezi kabisa mambo wanayotufanyia.
 
Achana na kupeleka pesa kwenye nyumba za ibada. Pesa zako peleka kwenye watu wenye mahitaji maalum. Pesa unampelekea Gwaji boy na shekhe wa MKoa wa Dar. Kama sio wehu ni nini. Dini zinapumbaza sana watu
 
Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo ?

Baba je ?

Ndugu wengine wa karibu ?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee,hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza,sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi.sina maana ya kukosoa sadaka,lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema,sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
Kama watoto wameshafariki, then huyo mzazi atasaidiwa na nani? Maana kila mtoto atakuwa 'preoccupied' na mzazi wake tu. Hivyo, kuna umuhimu wa kujua kwamba kutoa sadaka kanisani (bila kulalamika) maana yake ni kumsaidia kila mtu mwenye shida even if huyo mtu hawezi kusaidiwa na ndugu zake. We have to learn to give as it is only through giving that we can receive abundantly. As for me, nimesoma kwa kusaidiwa na watu nje ya familia yangu (na kutokana na kusaidiwa niliwezeshwa kufika nchi zifuatazo nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Zambia, Malawi, Uingereza, Ireland, France, Poland, Kenya, Msumbiji, South Africa - so much so that kama nisingesaidiwa hata nisingeweza kutoka nje ya wilaya yangu) na mimi nimejifunza umuhimu wa kuguswa na shida za wengine, hasa wale wanaohitaji kusaidiwa na mtu anayeweza kufanya hivyo kwa muda huo. God rewards our generosity and kindness in ways that may be unfamiliar to us. So, usidanganyike!
 
Back
Top Bottom