Sadaka kumpa mzazi ni bora kuliko kuipeleka kwenye nyumba za ibada

Sadaka kumpa mzazi ni bora kuliko kuipeleka kwenye nyumba za ibada

Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo ?

Baba je ?

Ndugu wengine wa karibu ?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee,hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza,sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi.sina maana ya kukosoa sadaka,lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema,sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
Kama kweli una Imani kweli na Mungu wako, wewe toa kunako husika, kumpa mzazi wako ni jukumu lako pia, watakao kula hiyo hela watakutana na Mungu wao. Usiingie kwenye mtego wa ibilisi na malaika zake.
 
Hio 10%sio sadaka ni zaka hii ni lazma ila inategemea utaitoa kwa mtindo gani.
Sadaka sio lazma yote uiweke Kanisa(japo kanisa pia linahiitaji kwaajir ya kuboresha huduma) unaweza igawa mfano asilimia 20% ya sadaka yako utaitoa Kanisa na 80% ya sadaka yako utawepa watu wenye uhitaji.
 
Huna maarifa mtoa mada
Maarifa anayo sana tu

Anachosema ni hiki: Ni udwanzi wa kiwango cha SGR kupeleka pesa yote church kwa mchungaji/nabii/chief prophet/mtume wakati mama yako mzazi (au wewe mwenyewe) kula na lala yake ni kwa kudra za mwenyezi Mungu.

Unapaswa kubalance mambo haya. Charity must begin at home.
 
Hata hiyo ya kanisani itaenda kutumiwa hivyo nayo ni matumizi.

Sadaka ni neno tu lakini lengo ni moja kufanya matumizi.
Imeandikwa Je, mwanadamu atamwibia Mungu? Nanyi mwasema tumekuibia nini? Mmeniibia ZAKA NA DHABIHU.."LETENI ZAKA NA SADAKA GHALANI, KIWEMI CHAKULA NYUMBANI MWANGU ASEMA BWANA" (Malaki 3)

Maelekezo ya Mungu ni zaka na sadaka kupelekwa kanisani, sio kwingineko na kuhudumia wahitaji sio mbadala wa Sadaka na zaka.. ukifanya hivyo utadaiwa kwani Mungu anakuita MWIZI WA ZAKA NA SADAKA. Unatakiwa kuhudumia wahitaji lakini sio kwa zaka.

Kanisani mnajifunzaga ujinga?
 
  • Thanks
Reactions: J C
Ni tofauti
Katika mfumo wa matumizi ni kitu kimoja.

Katika mfumo wa vile inavyopatikana ni mambo tofauti.

Mfano kwa sie waislamu zaka inahesabu maalumu kwa kiasi mabacho uko nacho ukifikia ndo unatakiwa upigiwe hesabu hizo ili utoe zaka.

Lakini sadaka haina kiwango maalumu ni imani yako na moyo wa kutoa.
Na kumpa mzazi haina kiwango maalumu ni imani yako tu na moyo wa kutoa.

Ile unayompa mzazi na unayopeleka msikitini haina tofauti zote ni sadaka.

Zaka haumpi mzazi wako unapeleka sehemu maalumu baada ya mahesabu
 
Kama kweli una Imani kweli na Mungu wako, wewe toa kunako husika, kumpa mzazi wako ni jukumu lako pia, watakao kula hiyo hela watakutana na Mungu wao. Usiingie kwenye mtego wa ibilisi na malaika zake.kama una
Kama una laki moja mzazi anashida na nyumba ya ibada inataka bati ukimpa mzazi wako ndio solution bora zaidi.
 
Mleta mada una uelewa wa kutosha juu ya mada uliyopost? Naomba uelewe kuwa sadaka sio msaada Bali ni requirement ya kufanya ibada usiijumuishe na misaada.
 
Yesu alilisha watu zaidi ya 5000, ila Sasa ivi wanaojiita watumishi WA Mungu wao ndo wanalishwa na watu zaidi ya 5000
 
Kama una laki moja yako usiipeleke msikitini/kanisani kwanza fikiria mama yako hana shida binafsi ambazo anaweza kutatua kwa pesa hiyo?

Baba je?

Ndugu wengine wa karibu?

Kuna watu wazazi wao wanahangaika kutafuta ugali wa siku mtu ile package ya kula wiki hana lakini mtu huyu anachukua pesa anapeleka kwenye nyumba ya ibada.

Mungu anakuona aisee, hautaadhibiwa na Mungu kwa nini pesa yako ulimpa mzazi akatatue shida zake wakati nyumba ya ibada haijapigwa rangi n.k

Lakini Mungu anaweza kukutia adabu kwa nini mzazi wako alilala njaa wakati wewe ulipeleka pesa kwingine.

Lengo la sadaka ni kuwasaidia wasiojiweza, sasa kama mzazi wako naye hajiwezi msapoti.

Kuna kitabu nilikichungulia kinasema toa walau 10% ya kipato chako ukatoe sadaka.

Niliamua tu sadaka yangu hiyo 10% nawapa wazazi. Sina maana ya kukosoa sadaka lakini nakumbusha tu wazee wetu wana dhiki nyingi, tusijifanye wema sana kwenye nyumba za ibada wakati wazee wetu hilo salio lingewasaidia.

Wema, sadaka huanzia nyumbani kwa watu wako wa karibu.

NB ; Kama wazazi wako wanajiweza hii mada haikugusi
Kumpa mzazi hela hiyo sio sadaka bali ni wajibu wako hivyo ni kama matumizi yako

Sadaka zinazotolewa kanisani ni kwa mujibu wa maamrisho ya Mungu mwenyewe hapewi mzazi bali wanapewa makuhani mzazi sio kuhani zipo
1) Sadaka za Mguso hizi ni za hiari wanaweka chombo mbele unaenda kutoa mwenyewe kwa hiari
2) ZAKA hizi unatoa sehemu ya 10 kwa mwaka unapeleka kwa makuhani anapewa kuhani si mzazi wako
3) MAVUNO kumtolea Mungu shukrani kama ilivyokuwa inafanyika nyakati za agano la kale anapewa kuhani si mzazi wako
4) MALIMBUKO hutoa sehemu ya kwanza ya tunda la kwanza anapewa kuhani si mzazi wako
5) MICHANGO KWA MAHITAJI MAALUMU hii huwezi kukwepa ujenzi, n.k
 
Kama watoto wameshafariki, then huyo mzazi atasaidiwa na nani? Maana kila mtoto atakuwa 'preoccupied' na mzazi wake tu. Hivyo, kuna umuhimu wa kujua kwamba kutoa sadaka kanisani (bila kulalamika) maana yake ni kumsaidia kila mtu mwenye shida even if huyo mtu hawezi kusaidiwa na ndugu zake. We have to learn to give as it is only through giving that we can receive abundantly. As for me, nimesoma kwa kusaidiwa na watu nje ya familia yangu (na kutokana na kusaidiwa niliwezeshwa kufika nchi zifuatazo nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Zambia, Malawi, Uingereza, Ireland, France, Poland, Kenya, Msumbiji, South Africa - so much so that kama nisingesaidiwa hata nisingeweza kutoka nje ya wilaya yangu) na mimi nimejifunza umuhimu wa kuguswa na shida za wengine, hasa wale wanaohitaji kusaidiwa na mtu anayeweza kufanya hivyo kwa muda huo. God rewards our generosity and kindness in ways that may be unfamiliar to us. So, usidanganyike!
Sijui kama umeelewa baba Mchungaji,issue ni hivi, kama mama yako,baba,kaka,mjomba,jirani nk ana uhitaji wa msingi halafu wewe ukaachana nao na kuamua kupeleka amana yako kwa prophet bilionea au bilionea gwajima siku Mungu akikutia kwapani utakula makwenzi ya kutosha baba mtumishi,lakini we endelea tu kupiga mluzi ili mbwa wajilete wamezwe!
 
Mimi.mwenyewe na waambiaga sana watu omba omba anaomba una mnyima afu unakuwa na kiele ele kutoa miela kanisani wakati kanisa lenyewe watu madon tatizo wabongo na unafiki.tunao
 
Hela ya matumizi kwa nin azazi unaiita sadaka? Ni kukosa maarifa

Sadaka sio lazma utolee kanisan, Kuna wahitaji wengi ambao unawajua kutokana na mazingira unayoishi waweza kuwatolea Kama sadaka

Wazazi ni wajibu wako kuwapa hiyo sio sadaka
 
Kumpa mzazi hela hiyo sio sadaka bali ni wajibu wako hivyo ni kama matumizi yako

Sadaka zinazotolewa kanisani ni kwa mujibu wa maamrisho ya Mungu mwenyewe hapewi mzazi bali wanapewa makuhani mzazi sio kuhani zipo
1) Sadaka za Mguso hizi ni za hiari wanaweka chombo mbele unaenda kutoa mwenyewe kwa hiari
2) ZAKA hizi unatoa sehemu ya 10 kwa mwaka unapeleka kwa makuhani anapewa kuhani si mzazi wako
3) MAVUNO kumtolea Mungu shukrani kama ilivyokuwa inafanyika nyakati za agano la kale anapewa kuhani si mzazi wako
4) MALIMBUKO hutoa sehemu ya kwanza ya tunda la kwanza anapewa kuhani si mzazi wako
5) MICHANGO KWA MAHITAJI MAALUMU hii huwezi kukwepa ujenzi, n.k
Kuyajua haya mpaka uanze kufundishwa ukiwa mdogo, kamawazazi wenyewe ndiyo hao sijui watoto wao watakuwaje!

Sent from my HUAWEI KII-L22 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom