Safari fupi ya kuzimu. Sijutii maisha yangu

Safari fupi ya kuzimu. Sijutii maisha yangu

Sehemu ya tatu.
Baada ya kuondoka kule niliamua kuondoka na kuelekea magetoni. Kesho yake asubuhi niliungana na kundi la kwetu pakavu, ambalo shughuli zake ilikuwa ni uchimbaji wa mitaro na mashimo ya choo. Kiujumla hapo ndio nilikutana na Tegee ambaye alinipa mawazo na kunifumbua akili katika haya maisha.
Tegee alikuwa mjanja mjanja sana hivyo mishe zake nyingi zilikuwa za ujanja ujanja na ndio alikuwa akinipa madini ya kutoboa kwenye maisha. Kazi yangu ya kwanza kuifanya na Tegee ilikuwa mwezi wa 8 siku ya jumapili jioni, ambapo tulimsokota mama mmoja wa kirombo tumuuzie mitumba kwa bei rahisi. Yeye alikubali tukamuuzia na akakagua ila wakati wa kumpakizia mzigo kwenye gari, tukamwekea mwingine bila yeye kujua.
Hiyo ndio ikaanza kuwa michezo yangu kwa maana ilikuwa inaniletea hela za urahisi ambazo hutoki jasho. Nikazoea na kama ujuavyo mazoea yana tabu. Siku moja jioni mzee mmoja wa kipare alikuja mjini kununua vifaa vya ujenzi. Nilikuwa mwenyewe sikuwa na Tegee, nikamsoma vizuri yule mzee nikaona huyu anahela.
Nikajisogeza kwake kuanza kujiulizisha maswali ili nipate kumsoma kirahisi. Nlimuuliza vipi mzee ni wapi naeza pata magari ya kwenda dar street? Akanijibu hajui yeye ni mgeni, namimi nikaona kweli huyu mgeni. Nikaanza kujieleza sasa kuwa mzee unajua mimi ni fundi ila kazi zimekuwa ngumu sana mtaani. Nayeye akaniambia amekuja kununua material za ujenzi hivyo nimshauri. Sasa wakati namsokota mzee yule kipare, akatokea mama muuza samaki ambaye nakumbuka nilimtapeli ndoo mbili za samaki sato wale mwanza.
Yule mama akanisimamisha na kumuuliza yule mzee, unamjua huyu kijana? Mzee akasema hapana sahiyo hiyo yule mama akaniimbia wimbo wa taifa(kelele za mwizi), na watu wakaitika nikakimbizwa na kuna watu wana mbio balaa. Nilikamatwa aiseeh kuna watu wanajua kupiga hii dunia! Niliiva ila kilichoniokoa siku hiyo ni watu kunifahamu ambapo ndio walinitetea nisiuwawe.
Kile kitendo kiujumla kiliniuma sana tena sana maana mwaka niliumaliza vibaya sana nikiuguza majeraha yangu kitandani. Mwaka ulipoanza nikauanza kiutofauti kwa kutulia tuli na mishe zangu nyingi ikawa ni kuweka tarazo kwenye majumba. Baada ya mwezi kuisha mitaa kalimani, nilikutana na yule mama muuza samaki akipita ile barabara ya ya dampo. Kigiza kilikuwa kimeshaanza kuingia yeye hakuniona ila mimi nimeshamuona. Nikatembea huku naangalia chini na kichwani nilikuwa sikosi boshori. Tulipokaribiana kupishana nlichomoa beto, na kumchoma kama mara sita kwa hasira kali sana, nilihisi vitu vya moto, yaani damu zikinirukia mkononi na yowe la yule mama akiuguguma. Mimi nilikimbilia huko dampo na kukaa kwanza kwa muda nikisikilizia huo msala. Hofu kiujumla nilikuwa nayo ila moyo ulikuwa na amani kabisa.
Usikose sehemu ya nne.......
 
SEHEMU YA 4

Baada ya kuona maisha ya pale moshi ni yakuishi kama digi digi, niliamua kutembea mbele kwa mbele na kuamua kwenda kuanzisha maisha mapya. Sikuwa na mkoa rasmi kwamba niende wapi, ila niliamua kwenda mkoa wa Iringa huko kidabaga njombe.
Baada ya kufika njombe ndio mara ya kwanza hapo sina ndugu wala ninayemfahamu, lakini kutokana na kuwa na ujuzi wa ufundi niliamini ntaishi. Maisha hayakuwa rahisi kama nilivyodhania bali yalikuwa ya msoto sana na kupata marafiki ilikuwa ni mtihani kidogo kutokana na mimi kuonekana siyo mzaliwa wa eneo hilo. Nilipiga vibarua haswa kwenye mashamba ya viazi na miti walau nipate rizki yakila siku.
Siku moja ya jumatatu majira ya jioni, hapo nikiwa sielewi nishasota mwezi mzima vibarua hamna na kula yenyewe ilikuwa ni yakulenga kwa manati. Ndipo nilipofatwa na kijana mmoja kwa jina la kadinde. Kadinde alikuwa mtu wa masihara mengi na mcheshi, aliniambia kuna kazi ya kwenda kuifanya huko makambako hivyo atanigharamia kila kitu na malipo yangu ni baada ya kazi.
Kwakuwa mi najua kadinde anajua mi nifundi, sikuwa na shaka yoyote. Tulienda mpaka makambako, ambako kweli kulikuwa na kazi na site ilikuwa kubwa ya mzee mmoja anaitwa Sanga. Ilikuwa ni kujenga godown la kuhifadhia nafaka za chakula. Yeye ndio mwenye kazi hivyo ndio alipatana na bosi kuhusu hiyo kazi. Basi bana kikawaida kabla hujaanza kazi lazima uvute kiadvance kidogo ili nawewe upaache huko nyumbani salama. Mi sikutaka advance ikanibidi nimwambie mwisho wa kazi anipe yote ili niweze fanyia la maana.
Tulipiga kazi balaa nakumbuka ilikuwa nyakati za baridi kweli. Msingi tuliujenga kwa mawe, na tofali zilikuwa ni nchi sita mpaka juu. Miezi mitatu nliitumia kwenye hiyo kazi. Niliiva haswa mpaka kazi inakamilika kadinde akaniambia nimpe hesabu yangu nadai shs ngapi, nikampa na yeye akasema ngoja aongee na bosi Sanga ili ampe hesabu kamili. Nikasubiri na kweli kibunda changu kikaja, baada ya hapo nikaona nitoke nikajipongeze kidogo huko mtaani. Nilitoka mida ya usiku na kwenda kilabuni, huko nlipata mwanamke mmoja alinivutia na kwakuwa kibunda kipo nikaona huyu huyu tukalewa nawe nabaadae akaniambia nikalale kwake maana kule camp watu kibao.
Kutokana na ile hali ya ulevi, sikuweza kabisa kuichakata mbususu vizuri kwa usiku ule kiujumla sikuitendea haki mpaka kunakucha. Nikamwachia hela kidogo yule dada na mimi nikaondoka kurudi camp. Kufika camp nikakaa na kuwazua nikaona hataa hailipi, nikabeba virago vyangu nikarudi kwa yule dada alikuwa anaitwa chaula ni mtu wa kabila la wawanji. Kufika kule akanipokea tena na kunitaka nipumzine huku yeye akifanya mpango wa msosi. Chakula kilikuja tukala na kushiba ndindi baada ya hapo akanisusia mbususu, ili niichakate sasa vizuri. Na kwakeli niliichakata haswa, ni mwendo wa vifuu na kukuna nazi. Utelezi unakuja wenyewe mpaka unakauka hatimaye jua likazama.
Je! Nini kitafata usikose sehemu ya 5
 
Sehemu ya 5

Maisha yangu yalikuwa ni pale makambako kwa bibie chaula yaani ni pika pakua. Na kiujumla baada ya kuwa na yule mwanamke niseme tu mambo yalianza kuwa mazuri sana na yalininyookea haswa! Kuna wanawake ukiwa nao kwenye maisha ni kama bahati tena ile nzuri na kuna wengine ni mikosi tupu. Kwahuyu bibie chaula yeye alikuja na bahati sana kwangu. Ni mweusi kidogo, urefu wake kama nchi 5' na ana hips na kalio la kuzugia.
Hela zilikuwa zinanitembelea sana na mishe mishe zilianza kuwa nyingi kwa upande wangu. Nilifungua duka la vitu muhimu hivi vya majumbani mitaa ya lyamkena. Kwahyo mara moja moja nlikuwa nauza mimi ila muda mwingi alikuwa anauza yeye mwenyewe bibie chaula. Mimi nlikuwa naendelea na mishe mishe huko mtaani nikipata hela naongeza mtaji hapo dukani.
Majira ya masika ndio huyu bibie alijifungua mtoto wa kiume, kwangu mimi alikuwa ndio wa kwanza ila kwa upande wake yeye alikuwa wa pili. Hivyo familia iliongezeka na kuwa ya watoto wawili. Kwangu haikuwa shida maana hela ilikuwa hainipigi chenga. Kutokana na makambako kuwa highway magari yanapita mengi, huwa vitu vilikuwa vikiibiwa kwenye magari mara nyingi mimi ndio nlikuwa mnunuzi mkubwa, kwasababu jirani yetu kabisa kulikuwa na kilabu cha pombe hivyo vitu vya mishe vilikuwa vikipita mara kwa mara.
Nilianza kuwa mzoefu na sasa kazi yangu kubwa ilikuwa ni kununua vitu vya mishe na mtaji ulikuwa. Mpaka usiku mmoja naamshwa naambiwa oyaa! Mark. Kuna mzigo hapa wa maana, nilitoka nje nikiwa na lenge la usingizi. Nikaonyeshwa kopa ila nlikuwa sina uzoefu na kopa hivyo sikuwa nashawishika kununua haswa kulingana na bei pia niliona kubwa. Nikawaambia rudini asubuhi saivi sina hela. Asubuhi kulivokucha nikaununua ule mzigo wa kopa. Nilikaa nao mpaka nyakati nimeenda dar ndio niliuza huko ambako nlipata faida ila sio sana. Kule dar nilijifunza mambo mengi sana na ushauri wa kibiashara uliokuwa unataka moyo na ujasiri.
Niliporudi makambako niliamua sasa na mimi nitafte vijana wa kazi. Mpango wangu ulikuwa ni wakuteka mali kwenye malori makubwa, kama mahindi, petroli, kopa n.k. Wazo langu likawa niongea na Sanga kama atanikubalia tushirikiane pale Godown yake kuweka mizigo. Nilimfata na kweli akanikubalia na kunitajia gharama zake ntazokuwa nampa. Yeye hakujua kama zitakuwa ni mali za uwizi. Alichojua yeye ni kuwa saivi hela imenitembelea sishikiki. Ndani ya mwezi niliweza kupokea mizigo mingi haswa mahindi na maharage. Mafuta kwa uchache na vinginevyo. Na kutokana na uwizi kuwa ulishamiri kwenye highway na makachero walikuwa patrol mara kwa mara. Ila hawakuthubutu kunigusa maana nlikuwa nawashika mkono kidogo. Sikuwa na mkono wa birika.
Muda ulizidi kusonga na mimi kushamiri zaidi, ambapo sasa niliona kuna haja ya kutanua mbawa zangu na kuanza kuingia kwenye biashara ya mbao. Hilo halikuwa gumu haswa ukiwa na watu na mtaji yaani hela. Nilianza biashara ya mbao, haswa magogo ambayo nilikuwa nikiyaleta karakana na kuyachana. Kuna hela nilimkopesha mzee mmoja wa kibena akiwa anaumwa, na kumuandikisha sawmill yake na vimashine vingine vidogo. Yule mzee alipokuwa anakaribia kuvuta moto mimi nilifoji mkataba wa awali na kuwa sio mkopeshano tena bali ameniuzia mazima. Kwahyo hata watoto wa yule mzee baada ya msiba kuja kudai haki yao na umiliki wa sawmill na mashine nyingine mi niligoma na kutoa mkataba unaonyesha niliuziwa na baba yao. Nilitumia na nguvu ya ziada kidogo kuwatisha na kuichukua ile mali kimabavu. Hapo watu walianza sasa kuniogopa na kuona mimi ni katili.
Je! Nini kitafuata usikose sehemu ya 6
 
Sehemu ya 5

Maisha yangu yalikuwa ni pale makambako kwa bibie chaula yaani ni pika pakua. Na kiujumla baada ya kuwa na yule mwanamke niseme tu mambo yalianza kuwa mazuri sana na yalininyookea haswa! Kuna wanawake ukiwa nao kwenye maisha ni kama bahati tena ile nzuri na kuna wengine ni mikosi tupu. Kwahuyu bibie chaula yeye alikuja na bahati sana kwangu. Ni mweusi kidogo, urefu wake kama nchi 5' na ana hips na kalio la kuzugia.
Hela zilikuwa zinanitembelea sana na mishe mishe zilianza kuwa nyingi kwa upande wangu. Nilifungua duka la vitu muhimu hivi vya majumbani mitaa ya lyamkena. Kwahyo mara moja moja nlikuwa nauza mimi ila muda mwingi alikuwa anauza yeye mwenyewe bibie chaula. Mimi nlikuwa naendelea na mishe mishe huko mtaani nikipata hela naongeza mtaji hapo dukani.
Majira ya masika ndio huyu bibie alijifungua mtoto wa kiume, kwangu mimi alikuwa ndio wa kwanza ila kwa upande wake yeye alikuwa wa pili. Hivyo familia iliongezeka na kuwa ya watoto wawili. Kwangu haikuwa shida maana hela ilikuwa hainipigi chenga. Kutokana na makambako kuwa highway magari yanapita mengi, huwa vitu vilikuwa vikiibiwa kwenye magari mara nyingi mimi ndio nlikuwa mnunuzi mkubwa, kwasababu jirani yetu kabisa kulikuwa na kilabu cha pombe hivyo vitu vya mishe vilikuwa vikipita mara kwa mara.
Nilianza kuwa mzoefu na sasa kazi yangu kubwa ilikuwa ni kununua vitu vya mishe na mtaji ulikuwa. Mpaka usiku mmoja naamshwa naambiwa oyaa! Mark. Kuna mzigo hapa wa maana, nilitoka nje nikiwa na lenge la usingizi. Nikaonyeshwa kopa ila nlikuwa sina uzoefu na kopa hivyo sikuwa nashawishika kununua haswa kulingana na bei pia niliona kubwa. Nikawaambia rudini asubuhi saivi sina hela. Asubuhi kulivokucha nikaununua ule mzigo wa kopa. Nilikaa nao mpaka nyakati nimeenda dar ndio niliuza huko ambako nlipata faida ila sio sana. Kule dar nilijifunza mambo mengi sana na ushauri wa kibiashara uliokuwa unataka moyo na ujasiri.
Niliporudi makambako niliamua sasa na mimi nitafte vijana wa kazi. Mpango wangu ulikuwa ni wakuteka mali kwenye malori makubwa, kama mahindi, petroli, kopa n.k. Wazo langu likawa niongea na Sanga kama atanikubalia tushirikiane pale Godown yake kuweka mizigo. Nilimfata na kweli akanikubalia na kunitajia gharama zake ntazokuwa nampa. Yeye hakujua kama zitakuwa ni mali za uwizi. Alichojua yeye ni kuwa saivi hela imenitembelea sishikiki. Ndani ya mwezi niliweza kupokea mizigo mingi haswa mahindi na maharage. Mafuta kwa uchache na vinginevyo. Na kutokana na uwizi kuwa ulishamiri kwenye highway na makachero walikuwa patrol mara kwa mara. Ila hawakuthubutu kunigusa maana nlikuwa nawashika mkono kidogo. Sikuwa na mkono wa birika.
Muda ulizidi kusonga na mimi kushamiri zaidi, ambapo sasa niliona kuna haja ya kutanua mbawa zangu na kuanza kuingia kwenye biashara ya mbao. Hilo halikuwa gumu haswa ukiwa na watu na mtaji yaani hela. Nilianza biashara ya mbao, haswa magogo ambayo nilikuwa nikiyaleta karakana na kuyachana. Kuna hela nilimkopesha mzee mmoja wa kibena akiwa anaumwa, na kumuandikisha sawmill yake na vimashine vingine vidogo. Yule mzee alipokuwa anakaribia kuvuta moto mimi nilifoji mkataba wa awali na kuwa sio mkopeshano tena bali ameniuzia mazima. Kwahyo hata watoto wa yule mzee baada ya msiba kuja kudai haki yao na umiliki wa sawmill na mashine nyingine mi niligoma na kutoa mkataba unaonyesha niliuziwa na baba yao. Nilitumia na nguvu ya ziada kidogo kuwatisha na kuichukua ile mali kimabavu. Hapo watu walianza sasa kuniogopa na kuona mimi ni katili.
Je! Nini kitafuata usikose sehemu ya 6
 
Sehemu ya 6
Siku zote unapokuwa na mafanikio au tunasema penye mafanikio na maadui hawakosekani pia. Hivyo kutokana na umaarufu ambao tayari nlishajizolea na pesa kuwa zinanitembelea nilianza kuandamwa kwenye maisha yangu na mambo mengi sana ili tu wanishushe chini. Mimi pia sikuwa tayari, hivyo niliamua kutafta wataalam ambao walinielekeza niende mpaka ludewa kwa mtaalam mmoja ambaye angeniwekea kinga kwenye biashara zangu na mimi mwenyewe binafsi.

Safari ya kwenda kule haikuwa nzito wala nyepesi. Nilifika na nilionana na mtaalam ambaye alinipika vizuri sana na mimi nikapewa masharti yakufuata ili mambo yazidi kuwa mazuri zaidi. Nilirudi makambako ambako sasa nilianza mipango ya chini chini kuhamia dar na kujikita huko na biashara zangu zaidi. Nilimshirikisha mke wangu bi chaula ambaye aliridhia hivyo mimi nilienda dar na kuzunguka maeneo tofauti tofauti kutafta location nzuri. Eneo ambalo niliona ni zuri kwa upande wangu ni buguruni. Hapo kwa dar ndipo nilipoanzia biashara ambako nilikuwa na ofisi ya timber. Na pia nilikuwa msambazaji pia wa mbao maeneo tofauti tofauti kwa dar.

Kutokana na mji kuzidi kushamiri siku hadi siku na mimi kuona mahitaji ya huduma yanaongezeka niliamua kuingia ubia na wahindi fulani, ili wawekeze kwangu zaidi na mimi nizidi kuongeza mtaji wangu wa mbao ambao ulikuwa umechanganya sana. Walikubali na tuliandikishiana vizuri baada ya kuwapeleka huko makambako kwenye viwanda vyangu vya kuchana mbao nakuona namna navyoendesha biashara zangu. Walitokea kunikubali sana ila kiujumla kwa upande wangu nilikuwa nawaza hela tu. Baada ya miezi kama mitatu kupita biashara zikiendelea wahindi walianza kunisumbua na marejesho yao na kudai faida juu. Kila ukikaa dakika 5 hao wako ofisini ni hela wanataka na sio kingine. Nikaona isiwe kesi nikaamua kuwashirikisha vijana wa kazi na kuwaeleza namna navyosumbuliwa na hao wahindi nao wakaahidi kulitatua hilo suala.

Nikiwa nimetokea maeneo ya tabata kuangalia viwanja, nilikutana na wale vijana wa kazi ambao walinitaka niwapatie milioni 5 kwaajili ya kutekeleza jambo kwa hao wahindi. Mimi sikuwa na hiyana tuliongozana nao hadi ofisini ambapo nliwapatia kiasi hicho cha fedha na wao kuniahidi ntapata majibu mazuri mno. Sikuwa na shaka nao wala sikuwafatilia sana ila baada ya mwezi nikiwa mafinga sasa katika utafutaji nlipata habari juu ya vifo vya wale wahindi. Walipata ajali ya gari wakiwa wanatokea dar kuja makambako kuniona wakijua ntakuwepo huko. Ilinibidi nirudi ili njiani gari tulilokuwa nalo lilipasuka tairi na kupoteza muelekeo na kupinduka. Hakuna aliye umia vibaya ila majeraha madogo tuu. Hivyo niliamua kughairisha safari ya makambako na kuelekea huko kasanga. Huko nlikaa wiki nzima ndio nikarudi makambako, ambapo nlipata taarifa za ile ajali kwa kina. Moyo ulitulia kidogo kwa amani kisha nikapanga safari ya kurudi dar ili nijue kifuatacho ni nini?

Nilifika dar salama na ndugu wa marehemu walipofika ofisini kudai haki yao, mimi nilisema kuna shamba la miti huko kasanga niliwauzia lote hivyo hakuna wanachonidai. Na hela nyingine nilishawalipa na mikataba ninayo. Kikawaida kabisa ulikuwa ukishaweka saini yako basi huwa sisi tunafoji ile saini yako tena na kuonesha tumeshakulipa ila kwa kutumia mabavu. Wale wahindi walikuwa wajanja ila hawakufua dafu maana mkono mtupu haulambwi. Niliwashinda na walipanga kupeleka kesi mahakamani, ilipofika na penyewe hola! Niliwashinda pia na lile shamba kule kasanga lilikuwa ni zuga sikuwahi kuwauzia chochote huko kasanga. Wahindi wengi wa pale mjini hawakunipenda na walianza kupeana taarifa kuwa mimi ni tapeli na sio mtu wa kufanya naye biashara.
Je? Nini kitaendelea usikose sehemu ya 7
 
Mpaka Sasa Jela ulishaenda? Kulipia uharifu uliotenda? Nategemea huko mbele nikute ulinyea debe. Twende kazi.
 
Back
Top Bottom