Safari ya Lissu kuelekea Nairobi ilikuwa ni mateso na vilio, Spika Ndugai usitoneshe vidonda

Safari ya Lissu kuelekea Nairobi ilikuwa ni mateso na vilio, Spika Ndugai usitoneshe vidonda

Wanatukamata mkuu tukifanya hivyo.

Jana wamekamata watu Hospitali ya Temeke waliokuwa wanachangia damu
Tunakwenda bila kuonesha tunaandamana wa kama kundi ila baada ya damu kupatikana watatoa taarifa ya kiasi cha damu na ndipo kampeni yetu itakuwa imefanikiwa......
 
Ndungai nakumbuka alivyomchapa bakora mwana ccm mwenzake kwenye kura za maoni niliangalia huyu MTU ana elimu gani ? Nikaona ni bwana mifugo/agromechanics na kuoña na ule mhimili mwingiñe umeshikwa na mtaalamu wa bansen burner nikajuwa tumekwisha kama nchi
 
Halafu Ndugai ni very bright toka high school nilishasikia simuliz zake kutoka kwa masela. Naskia darasan zilikuwa zinacharge balaa. Nikati ya wakufunzi wachache tunao bongo. Tatizo sasa tunasoma tupite mitihani siyo kuelimika.

Mbaff!
ADUI wa NCH hii ni CCM Sema watu hawataki kuelewa
 
Kuna watu humu nimeona nao wanachangia kwa upotoshaji,akiwemo mtu anaitwa Tume ya Katiba juu ya namna Lissu alivyotoka Tanzania kwenda Nairobi.

Kwanza naomba ku-declare kuwa nilishiriki "indirectly" kuona namna gani usafiri wa kwenda Nairobi unapatikana,japo nilikuwa mbali na nyumbani,lakini niliwasiliana na wadau ili kuona huyu mtu anapata usafiri kufika eneo la matibabu baada ya kusikia uhitaji mkubwa ni kufika Nairobi usiku uleule.

Suala la kwanza lilioafikiwa na Bunge ilikuwa ni kumleta Dsm-Muhimbili,ndege iliyokodiwa ilikuwa ni ya kampuni ya Safari Air Link na si ya NHIF kama anavyosema huyo Ndugai,ambayo ni MEDEVAC,ilikuwa ni Caravan usajili wa 5H-EWA,mali ya Peter Fox(mmiliki wa kampuni ya Safari Air Link),bahati mbaya ikatokea mabadiliko ya kwenda Nairobi,na ile ndege ikawa na rubani mmoja na haiwezi kwenda Nairobi usiku ikiwa na rubani mmoja ambaye hakuwa na masaa ya kuruka usiku.TCAA walikuwa tayari kutoa kibali cha ndege kuruka usiku hata kama ina injini moja kwa sharti la kuwa na marubani wawili,Ukawa ni mtihani mwingine wa kuanza kutafuta ndege nyingine usiku uleule.

Ndege nyingine ya Safari Air Link aina ya Citation(Jet Engines) siku hiyo ilikuwa imeenda Pemba ya Mozambique kama si Zambia,Fox akawa hana option,sbb pia hiyo ndege isingeweza kubeba abiria wengi ambao CHADEMA walikusudia wasafiri na Lissu.

Ndege kubwa ya kuwatosha mgojwa,daktari pamoja na wasindikizaji akiwemo mkewe, ikawa ni hiyo Citation ya Flight Link,5H-ETG.Ambayo ilipaswa kutoka Dsm kuja Dodoma usiku uleule,ili inyanyuke kwenda Nairobi.

Jambo hili likawezekana,lakini ilipaswa pesa iwe juu ya meza kwa mlipo ya dola,Dodoma hakukuwa na Mbunge wala waziri mwenye dhamana ya dola,Turky wa Mpendae akachukua dhamana hiyo ya mali kauli,sababu mmiliki wa kampuni ya Flight-Link(Mhindi) wana ushirika naye.Ndege ilinyanyuka Dsm-Dodoma na baadae Nairobi

Siri ya safari ile wakiwa angani,naamini ipo siku Mbowe na Msigwa wataiandikia kitabu(A Day to Remember in a Dark Political Arena),Ilikuwa ni safari ngumu iliyojaa machozi na uchungu mkubwa,walisafiri kwa shida sana,kitanda kilikuwa kinacheza na pia dripu ilibidi Dokta asafiri akiwa ameishika mkononi kaining'iniza juu sababu ya "height" ya ndege,ilikuwa ni safari ya mateso na experience mbaya sana kwa kina Msigwa na Mbowe pamoja na mke wa Lissu.Mungu aliyemponya Danieli katikati ya Simba wenye njaa,alitenda miujiza.

Sijaelewa huu upotoshaji wa huyu Ndugai ameutoa wapi,kwamba kuna ndege ilikodiwa toka Nairobi?Hiyo ndege ni ipi?kwamba aliomba itumie "airspace" ya Tanzania kinyume na sheria za nchi?Kwani sheria za nchi zinavunjwaje kwa ndege iliyoomba kibali kutua Tanzania na ikaruhusiwa?

Huu uwongo ni wa nini?hiyo ndege mliyokodi toka Kenya ni ipi?Maana kila mtu hata siyekuwa Dodoma aliona ndege iliyoondoka na Lissu ni 5H-ETG mali ya kampuni ya FlightLink.

Hii ni kampuni ya Tanzania,ndio maana usajili wa ndege umeanza na "5H",ndege zote zilizosajiliwa Tanzania huanza na "5H",zile za Kenya huanza na "5Y" na majirani Uganda ni "5X"...Wewe Ndugai hiyo ndege ya Kenya mliyoiombea kibali cha kutumia "airspace" yetu tena kinyume cha sheria ni ipi?Na sheria zipi mlizovunja?

Sasa unaona mtu anakuja humu anasema eti Lissu alitoka na ndege Dodoma hadi Dsm then ndio akaenda Nairobi.Huu uwongo mnauzalisha toka wapi??Wacheni upumbavu katika uhai na maisha ya watu sbb ya siasa!!Eboooo!!!!

Nimemsikiliza Ndugai hapa Jf kwenye video,ameongea kwa uchungu na huzuni,sababu maneno ya Lema yamemuingia sana,amefikia hatua ya kusema kama CHADEMA wanataka kumpeleka Lissu India,bunge lipo tayari endapo Waziri atakubali.Maneno ya Lema yamegusa mfupa,Job anajua aliondoka na hali gani hapa nyumbani kwenda India,amekaa miezi kibao akiugua.

Kila aliyekuwa anasimama bungeni,kabla ya kuchangia,alimuombea Spika afya njema na arudi mzima nyumbani.Watu walisali...Kuna siku Bulaya aliongoza sala ya kuomba afya ya spika katika Canteen ya Bunge.

Malumbano yanayoanzishwa na Spika ndani ya bunge juu ya afya ya Lissu si afya kwa ubinadamu na utu.Kuanzia lile la kutofautiana idadi ya risasi na Kubenea mpaka kamati ya maadili,na lile la kusema Turky ndio kachangia.Turky ni muislam safi,sadaka isiyo na mawaa na yenye thawabu haitangazwi.

Palipo na tendo jema,Mungu hufungua riziki...Kuitangaza sadaka ya Turky bungeni ni kumuondolea neema na thawabu kubwakubwa na ndogondogo mja wake aliyetoa sadaka.Mh.Spika,tumia busara kufunga malumbano ya afya ya Lissu Bungeni,wakati upo India,watu walijibiidisha kukuombea na si kujadili na kulumbana juu ya afya yako na matibabu yako.FUNGA MJADALA WA KUSIMANGANA BUNGENI KUHUSU AFYA NA HALI YA TUNDU LISSU...HUU SI UBINADAMU.

Kuna kijana sijui ni msemaji wa chama naye katoka kabisa na "Press Release" kupongeza hali ya Mbunge Turky,kutoa "mali kauli" ya safari ya ndege.Jamani mnaharibu sadaka za wenzenu.Turky mwenyewe amenukuliwa akisema;
" Mbowe akaniomba kwa kuwa nafahamiana nao (wenye ndege) niwadhamini wamuwahishe Lissu halafu wao watalipa. Na ndicho nilichofanya (kuwadhamini kwa mali kauli) na pesa hiyo imelipwa jana. Tunamshukuru Mungu nia njema hufungua milango yake” .Watu mnaharibu sadaka za watu bila kujua,nia njema ya Turky ipo katika hayo maneno yake ya mwisho yenye "bold".

Msaidieni Lissu kama nyie mlivyosaidiwa kwa kofia za ubunge na uspika wenu,wacheni masimango,tendeni kama vile mlivyotendewa,wengine mlikwenda India miguu haingii hata katika viatu,mlivaa suti na sandozi.Mungu amewaponya...Lipeni wema juu ya wema!!Mnaleta "urasimu" wa taratibu za matibabu nje ya nchi kwa mwili wa binadamu uliopigwa na kulowa risasi zaidi ya 10?Ebooo!!HIZO PESA ZA MAMA ZENU?

barafu wa JF

We Live Once,but Legacy Lives forever!!
View attachment 588456
Juu ni ndege ya kampuni ya FlightLink(Tanzania) iliyompeleka Lissu Nairobi

View attachment 588458
Hii ni ndege ya Safari Air Link iliyokusudiwa kumleta Dsm ikashindikana
Nasubiria kumwona Mh. Supika akimjibu [HASHTAG]#barafu[/HASHTAG] leo
 
Ndugu Barafu katika uzi huu umeandika kwa hisia sana, pole na wewe pia kwa uchungu ulionao juu ya haya mambo. Tuendelee kumuombea TL.
Mkuu,hata kama wengine sisi sio wanasiasa na kuna wakati hatukubaliani na Tundu Lissu,lakini ubinadamu kitu cha muhimu sana...Kabla ya vyeo na mali,tulianza kwanza kuwa binadamu!!Ubinadamu uanze,mengine yawe kwa ziada
 
Umeshindwa kujenga hoja unaanza matusi, ulitaka mtoa mada asijibiwe au wote tukubaliane na mawazo yake wakati tunaona anapotosha?, wajinga ni wale wanaoacha kutumia bima ya afya walioichangia kwa pesa yao wenyewe wanabaki kuomba omba misaada kwa watu wengine tena nje ya nchi, sasa hiyo milioni 10 kwa siku wanawalepa wakenya badala ya kuja kulipia pale Agakhan au Muhimbili ikazidi kuimarisha Hospital zetu ili ziendee kutuhudumia watanzania wengine vizuri zaidi, utaita huo ninini?
Kumbuka LISU hakuwa anaumwa MARALIA.....kwa muono wako Zuri lipi taratibu za Bima ya AFYA zafuatwe LISU afe au zisifuatwe kama ilivyofanyika Aishi Kama ilivyosasa Msifanye Utani na Maisha ya watu.....! Sisi tutachanga na atatibiwa atapona kabisa.. aturudi mjini kuendelea na Harakati zake mtaaibika sana...
 
Sasa kwanini Lema aanze kutupa lawama kwamba hajahudumiwa na Bunge wakati Mbowe mwenyewe aliomba kwamba wanaomba mgonjwa asipitie njia zinazoruhusiwa na bunge na akasema wapi tayari kubeba gharama?, hivi kama mtoto wako amefaulu kwenda sekondari ya serikali lakini ukaona kwamba kwasababu shule za private ni bora zaidi ukaamua kumpeleka huko, bado utaomba serikali ukamlipie huko private?

Inaonekana wanaolaumu bunge hawafanyi kazi za kuajiriwa kwa maana ya kulipwa mshaara, au hawana bima ya afya, kawaida waajiri walio wengi huwakatia bima za afya wafanyakazi wao, wanapoumwa sio mwajiri tena anayehusika kumlipia mfanya kazi wake, wala hiyo pesa haipo tena kwa sababu ilishapelekwa kulipia bima, sasa ukitaka bunge litoe hiyo pesa kwa bajeti ipi wakati pesa ya matibabu ya Lisu ilishapelekwa NHIF, ila kwa mapenzi ya familia yake na Uongozi wa chama chake wameamua wasiitumie?, sasa kwanini waanze kuomba katika balozi mbalimbali wakati hata hizo nchi hutumia utaratibu huu huu wa bima ya afya wakijua kwamba matibabu ni ghali sana duniani kote?, sio rahisi kwa hizo nchi kuchangia lolote kwa sababu wanajua Lisu ana bima ya afya ila ni kutaka kuendeleza kiburi kisichokua na maana yoyote
Huu nao ni ujinga ugonjwa unaulinganisha na shule...
 
Wewe ni mwongo tena mzandiki sana, clip ya video ya Turky inasambaa akihojiwa na waandishi wa habari anakubaliana na yote yaliyosemwa na Ndugai kwamba alitoa dhamana na CHADEMA wamelipa jana saa sita na nusu, acha mapenzi ya kitoto na lawama zisizokua na tija kwa mgonjwa, kama kweli mnampenda Lisu endeleeni kumchangia hadi apone, ama mrudisheni Muhimbili au Aga khan pale DSM ambapo NHIF itamlipia, na kama hofu ni usalama wake, kwanini vijana wa kikundi cha ulinzi wa viongozi wa Chadema tunaowaona wakati wa uchaguzi wasewekwe kumlinda masaa 24 hapo Hospitalini?, acheni kutumia hasira, kiburi na mihemuko isiyo kuwa na maana, haiwezi kumsaidia mgonjwa
Halafu kama wamelipa jana kwa nin invoice imeankwa tarehe 7/9/2017?
 
RESPECT! Heshima kwa mkuu Barafu! Kama ni nondo basi viwango vyake si vya sayari hii! Ni vya sayari nyingine kabisa! Ni nondo za kufunga vinywa na mjadala! Once again high RESPECT! Nondo zilizojaa utu!
 
Kumbuka LISU hakuwa anaumwa MARALIA.....kwa muono wako Zuri lipi taratibu za Bima ya AFYA zafuatwe LISU afe au zisifuatwe kama ilivyofanyika Aishi Kama ilivyosasa Msifanye Utani na Maisha ya watu.....! Sisi tutachanga na atatibiwa atapona kabisa.. aturudi mjini kuendelea na Harakati zake mtaaibika sana...
Acha kujifanya huelewi, na kama huelewi uombe ufahamishwe uache ubishi usio na msingi, Muhimbili au Agakhan kwa sasa ni Hospital bora kuliko zote katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kati, hat huko Nairobi walikompeleka kwa sasa tunapokea wagonjwa wengi kutoka kwenye nchi hizo kuja kuhudumiwa hapa Tanzania, nenda Jakaya Kikwete Cardiac Institute, au Ocean road cancer institue, au KCMC uone na uzungumze na wakenya walivyojazana kufuata huduma. Acha kuishi kizamani, kwa sasa Tanzania imepiga hatua kubwa sana katika fani ya tiba kuliko nchi zote za ukandaa huu, na kama ulimsikiliza vizuri Mbowe alisema hana wasiwasi wowote na ubora za huduma hapa nchini, kilichowafanya waende Kenya ni sababu za kiusalama, sasa kwanini wasitumie blue guards na walinzi wengine wa chadema kumlnda kipindi chote akiwepo hapo Hospitalini?, Mbona yule Generali wa jeshi aliyepigwa risasi anahudumiwa Lugalo na hali yake inaendelea vizuri?

Kwa taarifa yako, kama risasi hazijapiga kichwani, shingoni, kifuani au kuchanachana Ini, basi mgonjwa hayuko katika hatari sana hasahasa akiwaishwa Hospitalini na kuwekewa damu haraka kama ilivyofanyika kwa Lisu na yule jenerali mstaafu, wakati anapelekwa Nairobi tayari hali yake ilikuwa stable(all vital signs were stable), kwamba BP ilikua normal, oxygen concentration, breathing parten, kidogo renal functions zilikua altered kwa sababu ya less renal poerfussion because of bleeding, lakini baada ya kumuwekea damu na maji ikajirekebisha.

Nani amewakataza msimuhudumie, fanyeni mpendavyo ila msilalamikie mtu, mkitaka ahudumiwe na serikali ni lazima sheria na taratibu za nchi zifuatwe, sheria tumejiwekea lazima zifuatwe, kungeonekana kwamba maisha ya Lisu yapo hatarini wala asingepelekwa Kenya, angepelekwa India, kwa sababu hao wakenya wenyewe hawaendi hapo alipopelekwa Lisu, wao pia hukimbilia India viongozi wao wakihitaji matibabu, wanawashangaa walioamua kumpeleka Kenya
 
Huu nao ni ujinga ugonjwa unaulinganisha na shule...
Akili ndogo kamwe haziwezi kuelewa mithali za kiutu uzima, tukisema mpanda farasi wawili hupasuka msamba, ulishawahi kuona mtu anayepanda farasi wawili kwa wakati mmoja?, sasa kama ubongo wako umelala kiasi hicho cha kushindwa kutumia mifano na kuirudisha katika mada tukusaidieje?
 
Halafu kama wamelipa jana kwa nin invoice imeankwa tarehe 7/9/2017?
Tatizo lako wewe huna uelewa wa basic knowledge kabisa unaendekeza ubishi badala ya kutaka ueleweshwe, invoice is request for payment, while receipt is the proof for payment, mwambie huyo Msigwa aonyeshe risiti waliyolipia hiyo $9,200 tuone tarehee yake. Tatizo la watanzania wengi ni kutosumbua vichwa vyao katikw kufikiria kwa undani wanaendeshwa na ushabiki na kusikiliza maneno ya mitaani, tubadilikeni dunia inatuacha
 
Malumbano wanaoanzisha ni chadema wenyewe..wakijibiwa wanaona wanaonewa..ndugai alielezea taifa wingi wa risasi alizopigwa lisu kwenye gari..kubenea akasema ndugai muongo..wakati kitendo tu cha kutaja wingi kule wa risasi ilibidi mumpongeze..maana angeweza pia kukaa kimya..kamsema zito bungeni..zito akagusia lisu..wakati lisu hausiki..Lema nae anamshutumu kuhusu lissu..
Sasa vitu mnaanzisha wenyewe..mkijibiwa mnasema malumbano..basi kaeni kimya uguzeni mgonjwa wenu..ila msidhani shughuli zitasimama kwa sababu ya ugonjwa au kifo cha lisu..hata vikao vya Acacia na timu ya magufuli havijasimama
[emoji90]
 
Acha kujifanya huelewi, na kama huelewi uombe ufahamishwe uache ubishi usio na msingi, Muhimbili au Agakhan kwa sasa ni Hospital bora kuliko zote katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kati, hat huko Nairobi walikompeleka kwa sasa tunapokea wagonjwa wengi kutoka kwenye nchi hizo kuja kuhudumiwa hapa Tanzania, nenda Jakaya Kikwete Cardiac Institute, au Ocean road cancer institue, au KCMC uone na uzungumze na wakenya walivyojazana kufuata huduma. Acha kuishi kizamani, kwa sasa Tanzania imepiga hatua kubwa sana katika fani ya tiba kuliko nchi zote za ukandaa huu, na kama ulimsikiliza vizuri Mbowe alisema hana wasiwasi wowote na ubora za huduma hapa nchini, kilichowafanya waende Kenya ni sababu za kiusalama, sasa kwanini wasitumie blue guards na walinzi wengine wa chadema kumlnda kipindi chote akiwepo hapo Hospitalini?, Mbona yule Generali wa jeshi aliyepigwa risasi anahudumiwa Lugalo na hali yake inaendelea vizuri?

Kwa taarifa yako, kama risasi hazijapiga kichwani, shingoni, kifuani au kuchanachana Ini, basi mgonjwa hayuko katika hatari sana hasahasa akiwaishwa Hospitalini na kuwekewa damu haraka kama ilivyofanyika kwa Lisu na yule jenerali mstaafu, wakati anapelekwa Nairobi tayari hali yake ilikuwa stable(all vital signs were stable), kwamba BP ilikua normal, oxygen concentration, breathing parten, kidogo renal functions zilikua altered kwa sababu ya less renal poerfussion because of bleeding, lakini baada ya kumuwekea damu na maji ikajirekebisha.

Nani amewakataza msimuhudumie, fanyeni mpendavyo ila msilalamikie mtu, mkitaka ahudumiwe na serikali ni lazima sheria na taratibu za nchi zifuatwe, sheria tumejiwekea lazima zifuatwe, kungeonekana kwamba maisha ya Lisu yapo hatarini wala asingepelekwa Kenya, angepelekwa India, kwa sababu hao wakenya wenyewe hawaendi hapo alipopelekwa Lisu, wao pia hukimbilia India viongozi wao wakihitaji matibabu, wanawashangaa walioamua kumpeleka Kenya
Umeshaeleweka!!Punguza kumjadili sana na kusimanga hali ya ugonjwa wa mtu
 
Daah! inasikitisha sana hasa hapo ambapo kitanda cha mgonjwa kinachezacheza huku drip ikiwa imeshikiliwa na daktari.

Hii itakua iliwaweka katika hali ya wasiwasi sana akina Mbowe na wenzake juu ya hali ya mgonjwa.

Mungu amponye Lissu.
 
Back
Top Bottom