Safari ya mafanikio ya Mwanamuziki Lauryn Hill: Usipuuze na kudharau watu na Usikate Tamaa

Safari ya mafanikio ya Mwanamuziki Lauryn Hill: Usipuuze na kudharau watu na Usikate Tamaa

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
21,113
Reaction score
65,124
dt.common.streams.StreamServer.jpg

Lauryn Hill
Leo hii ukizungumzia orodha ya wasanii wakubwa wa kike nchini Marekani na duniani kote, basi huwezi kumkosa Lauryn Hill.

Huyu ni moja kati ya binadamu wenye vipaji vikubwa sana vya utunzi wa mashairi na sauti ya kipekee kabisa. Anaweza kuimba muziki wa aina mbalimbali, kuanzia Soul, Blues, Jazz, Reggae, RnB na Hip-Hip.

Lakini kuna video inaonyesha akiwa mtoto wa miaka 13 akiimba wimbo wa Who's Lovin You wa The Jackson 5 akiwa anatetemeka na watu kumzomea (It's Heart Breaking), inashangaza kuona watu wakimbeza mtoto ambaye miaka michache baadaye alikuja kuwa mwanamuziki mkubwa sana duniani.




Somo: Usipuuze mtu, Usimchukulie mtu powa na Usikate Tamaa, Like Al Pacino said "Every dog has it's day"
 
Harmonize ni mfano mzuri.
Mazee acha kabisa, kuna siku nilikuwa namsikiliza Elon Musk alisema miaka ya 90's mwishoni alienda Urusi akitaka kununua ICBM ili aweze kufanya tafiti za kutengeneza roketi lakini Warusi walitema mate chini na kumtukana vibaya mno.

Leo hii anafanya tafiti ambazo zinaweza kuwatoa Warusi kwenye ramani ya ulimwengu wa anga za juu.
 
Mazee acha kabisa, kuna siku nilikuwa namsikiliza Elon Musk alisema miaka ya 90's mwishoni alienda Urusi akitaka kununua ICBM ili aweze kufanya tafiti za kutengeneza roketi lakini Warusi walitema mate chini na kumtukana vibaya mno. Leo hii anafanya tafiti ambazo zinaweza kuwatoa Warusi kwenye ramani ya ulimwengu wa anga za juu......

Comrade

Salama

Nasubiria Nondo zako juu ya hii Operasheni ya Urusi ndani ya YUkreini.

Hizi mambo za Sankisheni na mapigo ya Urusi.

Chonde Chonde Mkuu!
 
Mazee acha kabisa, kuna siku nilikuwa namsikiliza Elon Musk alisema miaka ya 90's mwishoni alienda Urusi akitaka kununua ICBM ili aweze kufanya tafiti za kutengeneza roketi lakini Warusi walitema mate chini na kumtukana vibaya mno. Leo hii anafanya tafiti ambazo zinaweza kuwatoa Warusi kwenye ramani ya ulimwengu wa anga za juu......
Ni kawaida kwa watu kukudharau kwasababu hawajui Wala hawajui uwezo wako.

Na ndio maana watu wajanja, wakishaonesha uwezo wao na ikaonekana unawahitaji zaidi huwa kama Ni malipo wanajipandisha thamani.
 
Hivi watu huwa wanadharau mtu au wanadharau kazi at that instant ?

Of course sio vema kudharau na kukatisha tamaa ila it does not mean hata mtu akifanya kitu mediocre tuseme / waseme ni kizuri sababu tu kesho au keshokutwa atakuwa mtu maarufu...., huenda hizo kebehi na kicheko ndio kinamfanya mtu aongeze bidiii

Sometimes what you dream
Can be deceiving
Na huwezi kuvuna usichokipanda
Thanks God for giving

Ghetto sikuwa na umeme wala cable
Hizi moja T-Shirt na yebo
Ati leo namiliki lebo
Lebo, Konde Gang lebo

Siku zote kisicho kuua
Kitakufanya uwe ngangari
Ata mwanga huwezi kumjua
So ishi nao kwa tahadhari

One love kwa wanangu wa kitaa
Nyie ndo mnanunua CD
Two love kwa wanafiki wa Insta
Mnafanya niongeze bidii
Three love kwa master na rita
Mlinifanya hasira zizidii
Four love njia ngumu nilizopita
Mkanipa na jina mkasema niitwe​
 
Watoto wa siku hizi hawamjui huyo musian genius
Lauryn Hill mara ya kwanza kumkariri ilikuwa kwenye movie ya sister act part 2. Nilikuwa namuona mzuriii 😅, sikujua hata kama alikuwa musician, I guess miaka anavuma sikuwa najielewa fresh au kufuatilia muziki wa nje kwa ukaribu japo crew members wake kama wyclef nawapata
 
Kila mtu Mungu kampa akili na kipaji, ila hivi vitu viwili haviwezi kufanya kazi vizuri bila kujituma.

Ndio maana huwaga si shangai kumwona mtu aliyekuwa chini baadae akawa mtu mwenye mafanikio katika nyanja fulani,kwani kujituma ndio kila kitu Mungu kishamaliza kazi yake tokea siku ya kwanza aliyo kuumba.

Kwa Afrika ni ngumu kugundua kipaji chako sababu ya hatuna miundombinu na watu wenye visions kama wenzetu mbele, mtoto anaanza kujitambua mapema na ndio maana dogo ana miaka 17 kishatoboa.

Wapo ambao wamebahatika kuvijua vipaji vyao mfano Ajibu, ila hatoboi sababu hajitumi.

So ukujituma ndio kitu kitakufanya uelekee njia ya mafanikio yako.
 
I need you, baby,
if it’s quite alright
I need you you, baby
to warm the the lonely nights
I love you, baby
trust in me when I say ok
Oh pretty baby, don’t let me down, I pray
Oh pretty baby, now that I’ve found you stay, and let me love you, oh baby …
 
Hivi watu huwa wanadharau mtu au wanadharau kazi at that instant ?

Of course sio vema kudharau na kukatisha tamaa ila it does not mean hata mtu akifanya kitu mediocre tuseme / waseme ni kizuri sababu tu kesho au keshokutwa atakuwa mtu maarufu...., huenda hizo kebehi na kicheko ndio kinamfanya mtu aongeze bidiii

Sometimes what you dream
Can be deceiving
Na huwezi kuvuna usichokipanda
Thanks God for giving

Ghetto sikuwa na umeme wala cable
Hizi moja T-Shirt na yebo
Ati leo namiliki lebo
Lebo, Konde Gang lebo

Siku zote kisicho kuua
Kitakufanya uwe ngangari
Ata mwanga huwezi kumjua
So ishi nao kwa tahadhari

One love kwa wanangu wa kitaa
Nyie ndo mnanunua CD
Two love kwa wanafiki wa Insta
Mnafanya niongeze bidii
Three love kwa master na rita
Mlinifanya hasira zizidii
Four love njia ngumu nilizopita
Mkanipa na jina mkasema niitwe​
Siyo sahihi kwa watu wazima kumzomea mtoto wa miaka 13, sambamba na hilo siyo sahihi kwa mwanadamu kumdharau mwanadamu mwingine anayejifunza.
 
Lauryn Hill mara ya kwanza kumkariri ilikuwa kwenye movie ya sister act part 2. Nilikuwa namuona mzuriii 😅, sikujua hata kama alikuwa musician, I guess miaka anavuma sikuwa najielewa fresh au kufuatilia muziki wa nje kwa ukaribu japo crew members wake kama wyclef nawapata
Bwahaha, mwana ulimtamani hadi Lauryn Hill,.....
 
Siyo sahihi kwa watu wazima kumzomea mtoto wa miaka 13, sambamba na hilo siyo sahihi kwa mwanadamu kumdharau mwanadamu mwingine anayejifunza.
Unaposimama kwenye stage wewe sio mtoto tena bali ni performer..., Game ni gumu sio lelemama, kiuhalisia ukitaka kusifiwa na kupewa kudos watakupa ndugu zako na jamaa zako ila waangaliaji / watazamaji (ambao wengine wametoa their hard earned cash, tegemea vitu kama hivyo); Hata ukiwa mzuri kuna watu wenye wivu ambao always will try to pull you down..., Kwahio ni vema mtu ukajua kabisa kabla ya hii safari (the going is rough and you have to get tough)

Pia kumbuka Lauryn ni talented wala hakuwa anajifunza hapo, bali huenda the audience was just not friendly na hizo zipo na zinaweza zikatokea anytime (huenda sio kwamba haujui bali unachoimba kwao haki-connect nao); Kwahio acha tu kuzomewa kwenye game unaweza mpaka kupondwa mawe... (its part and parcel of this hard job) Kutoboa its not only about talent bali ability to cope....

Ila kumbuka as a performer una-contract na watazamaji ambao wana haki kuonyesha their dissatisfaction na kazi yako.... (Cha kufanya ni ku-word harder ili kuwa-convert)....

 
Bwahaha, mwana ulimtamani hadi Lauryn Hill,.....
😆😆😆 ahh ni kusifia Tu God's creation, ana ile perfect black doll look, rich dark skin tone, rasta kwa kichwa, full dark lips and nice eyes. Sauti flani deep sio ya kislay queen, who won't adore such a beauty brother kaka, 😆
 
😆😆😆 ahh ni kusifia Tu God's creation, ana ile perfect black doll look, rich dark skin tone, rasta kwa kichwa, full dark lips and nice eyes. Sauti flani deep sio ya kislay queen, who won't adore such a beauty brother kaka, 😆
Teh, nakuelewa braza, nakuelewa!
 
Back
Top Bottom