Safari ya miaka 9 tangu kuacha kazi. Hamasa kwa vijana wenye maono makubwa

Hongera mkuu na pole kwa changamoto ulizopitia.
 
You have a long way to go man , angalau unge stick na biashara zinakua kuliko ualimu, ualimu unaofanya kwasasa ungefika hata bila kuacha kazi. Ila wewe umeamua kuchukua njia ndefu tu. Unge stick kwenye biashara kwa miaka hio 9 ungekuwa mbali mno usingekuwa bado unawaza kupata 10k per day sawa na bumu tu ulipokuwa chuo.
Aisee nimekuonea huruma maana umepoteza muda mwingi sana
 
 
Thanks mkuu. Unajua nn mkuu sio kwamba ualimu ndio nguzo kuu hapana biashara nimezifanya/ nazifanya sana sema nimekuwa nikifeli sana. Lengo ilikuwa ni kupata biashara ya kupata faida ya 10K per day tofauti na shule na ndio imenichukua hiyo miaka 9 kuipata.

Bro biashara ni ngumu sana sio rahisi unavyodhani but namshukuru Mungu kuwa nimepata ufunguo so huko mbele ni kwepesi kuliko nilipotoka. Asante sana.
 
mwalim mzazi umejitahidi kuandika chapisho zuri sana na kuwatia wengine moyo wa kujiajiri naamini kupitia wewe wengi watapata funzo la kutochezea ajira na wengine watapokea funzo la kujiajiri pamoja na changamoto zake then kivipi wanaweza kusimama.

ila ushauri wangu tu,focus kwenye point moja hiyo elfu kumi ya mwezi wa tano ni ndogo sana,hujaweza kufikia lengo,uchumi huu wa kibepari mtu analala tajiri anaamka muokota makopo.

fanya hivi,tafuta mradi wa mda mrefu mfano kilimo na mradi wa mda mfupi ambao ni tuisheni yako hapo utaweza kujimudu..

kama unafanya biashara fanya ila biashara hubadilika wakati wowote.
 
Mkuu MUCOS, hongera sana kwa maamuzi uliyo chukua na hatua ulizofikia ni kweli Jamiiforums ni chimbo la mambo yote ni uamuzi wa mtu kuchimba na kuchukua kipi. Umekuwa ni moja ya Watanzania wenye dhamira ya dhati katika fikra mpya na mitizamo chanya kuyafikia yale maisha yaliyobeba ndoto za kila binadamu. Binafsi nakupongeza sana kwa huo moyo wa Kishujaa.
 
Njoo hapa brother Ivan Stepanov utoe neno

Mimi naona jamaa atafute shortcuts za NGO's. Kwa sababu kama ni mwalimu professionally, experience ya tution centre anayo, uwezo mkubwa wa kuandika lakini pia life experience kubwa

Nadhani angeanza kujichanganya kwenye NGO's kama volunteer kwa zile shule zenye mahitaji ili ajifunze wengine wanatengenezaje pesa kupitia foundations.

Lakini pia anaweza kujifunza kutengeneza propasals, machapisho ya kuombea grants and funds ambayo yanaweza mtengenezea stability kuliko hiyo pesa anayoingiza kwa sasa

Ukiachana na misoto ya mahusiano na kusomesha ndugu ambapo hataa Mimi nilikuwa na majukumu ya upande wangu lakini pia mimi sikuwa failure kwenye ajira za private sector maana nimeacha kazi zaidi ya mara tatu..

All I can say is, binadamu tunapambana kila siku lakini siku ya kufanikiwa ni moja hivyo, wengine wanachukua miezi na wengine wanachukua miaka lakini jambo la muhimu pia

Ni kuangalia angle zingine za kutafutia pesa kutokana na kipaji kama hicho cha kuandika au ualimu. Na hii huwezi kupata kama utakosa exposure au connections za kukufanya uingie kwenye milango flani ambayo 350k unayoitafuta kwa mwezi ni hela ya kupozea siku ya mtu..

So, story aliyoiandika imenikumbusha mengi sana na namuelewa anachopitia na pengine najua ana maumivu makubwa kuliko niliyopitia,

Lakini itakuwa vyema kama mkuu akijipatia healing na ayaache yaliyopita then aanze kuingia kwenye rooms za waliofanikiwa kama hizo nilizopendekeza ili aweze kufika anapotaka.
 
Miaka ya nyuma kabla ya shule za kata walimu wengi waliacha kazi serikalini wakaenda private. Mda si mrefu ufaulu ukaongezeka, shule za private zikaanza kukosa soko wale waalimu nao wakaanza kupunguziwa mishahara hadi wakaona bora wangebaki walikotoka. Serikali sasa imeanzisha mtindo kutotaja shule ya kwanza kitaifa hii imepunguza promo kwa shule binafsi. Hatua inayofuata Serikali inabidi iweke shule za serikali tatu za mtaala wa kingereza kwa elimu ya msingi kila wilaya ili wananchi wachini nao watoto wao wasome shule nzuri, maoni ya wananchi wanadai wapo tayar kulipa ada hata laki 3 kwa mwaka. Ikija hii mjue vishule uchwara mtaani vinaanza kufa. Serikali japo inachelewa ila haitazidi miaka mitano hii project itaanza.
 
Huu uzi hata kama mtu anataka kuacha kazi lazima aogope akiusoma. Imagine msoto wa miaka yote hyo🤣🤣. Kwanini usingekopa hata Million 10 ndo uache kazi ukiwa na Mtaji wa kueleweka?
Ni uthubutu tu , jamaa alijilipua .. hopefully hajasoma kile kitabu rich dad poor dad
 
Huu uzi hata kama mtu anataka kuacha kazi lazima aogope akiusoma. Imagine msoto wa miaka yote hyo🤣🤣. Kwanini usingekopa hata Million 10 ndo uache kazi ukiwa na Mtaji wa kueleweka?
Dhamana ya mkopo ingekuwa ni nini bro? Kumbuka kasema hakuwa na nyumba wala kishika uchumba chochote. Kikubwa unapopambana ni kujizira kabisa. Pambania ndoto yako kwenye njia sahihi, bila kujali dunia inasemaje kuhusu wewe!
 
Dhamana ya mkopo ingekuwa ni nini bro? Kumbuka kasema hakuwa na nyumba wala kishika uchumba chochote. Kikubwa unapopambana ni kujizira kabisa. Pambania ndoto yako kwenye njia sahihi, bila kujali dunia inasemaje kuhusu wewe!
Brother A. Upo kaka kitambo sana?
Mara ya mwisho tulionana PPF Towers mwaka 2010. Uko salama Mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…