Safari ya Sudani Kusini

Safari ya Sudani Kusini

Well done mkuu. Nimesoma nimeelewa pa kikubwa kuhusu Sudan Kusini. Nina rafiki wa kwenye mtandao Bint toka Juba.

Mengi uliandika alinisimulia na ni muoga sana kuhusu huko kwao.
 
Vipi fursa za biashara huko kama mahindi,Mchele ,Maharagwe ki ujumla nafaka hukuwahi kudadisi kidogo.Make nasikia Mo anapeleka sana Nafaka huko.
 
Shukrani mkuu.
Na utaratibu wa kuipata ukoje?
Nataka niende kuchukua bidhaa flani
Nenda Ofisi yoyote ya uhamiaji watakupa utaratibu wote, kwenda kwenye Nchi za East Africa unaweza pata hata ya muda unalipia kidogo
 
Safi sana. Sasa natamani kusikia ya Syria na Yemen bila kusahau kule tigray Ethiopia
 
Inaonekana wazi wazi kuwa hii ni safari yako ya mwanzo kutoka nchini Tanzania.Afadhali umekuwa mkweli katika uandishi na kuonesha sura yako
Inaonekana wazi wazi kuwa hii ni safari yako ya mwanzo kutoka nchini Tanzania.Afadhali umekuwa mkweli katika uandishi na kuonesha sura yako halisi. Pale ulipoambiwa watanzania kuingia kule hakuna shida ulitafsiri hakuna visa wala masuala yoyote.Hivyo ulipodaiwa dola 50 ukaanza ubishi.Una bahati sana wale watu walikupenda na kukuwachia uingie bure.

Ujuwe kila nchi mpakani ina masuala ya uhamiaja na aina ya visa ya kituo unachoingia bila kupata mwaliko ni aina moja ya viza rahisi lakini sio bure.

Umeanza kutoka nje ya nchi kwa kutumia mabasi uliyoyazoea kule Tabora.Ungesafiri kwa kutumia ndege za kimataifa na ikawa safari yako ni ya kubadilisha ndege kwenye miwanja mikubwa ya kimataifa na sio kama ule wa Dar es salaam au ule wa Juba basi nadhani ungeaachwa uwanjani na ndege ukajitafutia balaa jengine. Ungekuwa unashangaa shangaa na usipate hata wa kumuuliza kwani kule huwa wanatumia mifumo ya kielektronic tu hata spika hawazitumii tena isipokuwa kwa dharura kubwa itakapokuwa kuna mtu kapotea hajaingia kwenye ndege.

Halafu tangu mwanzo umeshaambiwa ile nchi haina usalama, wewe umeshikilia kupiga piga picha na kutembea na kamera kwapani.Hiyo kamera kuporwa ni adhabu ndogo.Ungepigwa kabisa sijui ungmlaumu nani.

Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu urudi tena huko na siku moja ufike angalau London.Ukiniona utanishtua nitakuwa pamoja nawe lakini mambo ya kuingia mabaa kupata kinywaji itakuwa ndio mwisho wa urafiki wetu.
Wewe ni kajinga. There is first time for everything.

BTW, wewe ni Limbukeni wa karne.
 
Ndugu kama hutojali naomba contact zako kuna vitu natamani nikuulize kuhusu Sudan
 
KICHWA CHA HABARI KWA 75% KIMEBEBA MAUDHUI KUHUSU WAMASAI. LAKINI HABARI YENYE KWA 75% UMESIMULIA ULIYOYASHUHUDIA SUDAN KUSINI. AHSANTE KWA SIMULIZI. KWANI SIMULIZI KAMA HIZI HUWA NAZISOMAGA KULE KATIKA JUKWAA LA 'ENTERTAINMENT'
 
Hapo kwny sura zakutisha ni kwel,umenikumbusha kuna jiran yetu dereva was magar makubwa anasema walikua wakipeleka mzigo wa tajir Sudan kusin ,mara nyingine unakuta watu wamesimama mbele ya gari wameshika silaha wana sura mbaya za kutisha km vinyago,ole wako ucheke wanakupiga mawe gar yako mpaka wapasue vioo na wanakunyang'anya Mali zako, hivyo walikua wakisimama yy alikua kimya katulia anaenda kuchekea mbele,anasema Sudan kusin na Congo watoto wadogo kushika silaha na kuzitumia ni Jambo la kawaida sana
 
Hongera sana! Lakin vp kuhusu uchumi? Vp kuhusu chakula? Vp kuhusu miundombinu? Vipi kuhusu mahusiano ya kijamii (makabila) wanavyoishi? vipi kuhusu mademu? Vipi kuhusu utamaduni (entertainment)? Maswali mengi hujajibu. Umeelezea safari tu. Next time jitahid uyajibu yote
 
Mkuu niliweka picha naona wana jukwaa wameziondoa kwani inaruhusiwa pia kuweka video??
Kwanini mods wanaziondoa picha sasa? Mbona wanaleta mambo ya kishamba ya kudhibitiana Kama Magu yupo hai anatupeleka kidikteta? Kwani picha Zina shida gani, na Tena sio za nchi hii?
 
Back
Top Bottom