Inaonekana wazi wazi kuwa hii ni safari yako ya mwanzo kutoka nchini Tanzania.Afadhali umekuwa mkweli katika uandishi na kuonesha sura yako
Inaonekana wazi wazi kuwa hii ni safari yako ya mwanzo kutoka nchini Tanzania.Afadhali umekuwa mkweli katika uandishi na kuonesha sura yako halisi. Pale ulipoambiwa watanzania kuingia kule hakuna shida ulitafsiri hakuna visa wala masuala yoyote.Hivyo ulipodaiwa dola 50 ukaanza ubishi.Una bahati sana wale watu walikupenda na kukuwachia uingie bure.
Ujuwe kila nchi mpakani ina masuala ya uhamiaja na aina ya visa ya kituo unachoingia bila kupata mwaliko ni aina moja ya viza rahisi lakini sio bure.
Umeanza kutoka nje ya nchi kwa kutumia mabasi uliyoyazoea kule Tabora.Ungesafiri kwa kutumia ndege za kimataifa na ikawa safari yako ni ya kubadilisha ndege kwenye miwanja mikubwa ya kimataifa na sio kama ule wa Dar es salaam au ule wa Juba basi nadhani ungeaachwa uwanjani na ndege ukajitafutia balaa jengine. Ungekuwa unashangaa shangaa na usipate hata wa kumuuliza kwani kule huwa wanatumia mifumo ya kielektronic tu hata spika hawazitumii tena isipokuwa kwa dharura kubwa itakapokuwa kuna mtu kapotea hajaingia kwenye ndege.
Halafu tangu mwanzo umeshaambiwa ile nchi haina usalama, wewe umeshikilia kupiga piga picha na kutembea na kamera kwapani.Hiyo kamera kuporwa ni adhabu ndogo.Ungepigwa kabisa sijui ungmlaumu nani.
Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu urudi tena huko na siku moja ufike angalau London.Ukiniona utanishtua nitakuwa pamoja nawe lakini mambo ya kuingia mabaa kupata kinywaji itakuwa ndio mwisho wa urafiki wetu.