Safari yangu ya kisiwa cha Mafia na fununu za rupia ya Kijerumani

Safari yangu ya kisiwa cha Mafia na fununu za rupia ya Kijerumani

cmoney

JF-Expert Member
Joined
Oct 14, 2011
Posts
3,570
Reaction score
5,508
20180708_134721.jpg
20180708_085015.jpg
20180708_085644.jpg
20180708_085015.jpg
20180708_085644.jpg
20180708_115818.jpg
20180708_134715-1.jpg
Za jioni waungwana. Katika maisha nmejiwekea kila baada ya miezi mitatu huwa najitahidi kutembelea sehemu mbalimbali za nchi yetu ya Tanzania na kujionea vivutio tulivyonavyo.

Basi safari yangu ikanituma kwenda kisiwa cha Mafia ambapo nashukuru Jamiiforums ndo moja ya sehemu nilipopata maelekezo zaidi jinsi ya kufika huko kwa kupitia bandari ndogo ya nyamisati ambapo kuna majahazi yanayokupeleka hadi kisiwani.

Safari ilianzia mbagala mida ya saa 11 jioni ambapo kwa nauli ya 5500 iliweza nifikisha hadi bandari ya nyamisati ambapo tulifika saa 3 na kwa bahati mbaya tiketi za majahazi zilizokua zinakatwa kwa tsh 16000 zikawa zimeisha ila wenyeji wakaniambia itakapofika alfajiri tutaongea na Mabaharia na safari itakua sawa.hili ni swala la kuangaliwa kwa ukaribu kwani ilipofika saa 9 alfajiri waliona tiketi walifanikiwa panda ila bado tusiokuwa na tiketi tulikua zaidi nusu ya wasafiri na wote tulipanda ingawa kutokana na kutokua na uangalizi wa mamlaka zinazohusika jahazi lilionekana kabisa limepandisha kupita kiasi bila kua na vifaa vyovyote vya uokoaji kama vile maboya au vitu kama hivyo na jahazi likiwa limepandisha wanaume wanawake na watoto wakiwa wengi.

Tunashukuru Mungu safari ilifika salama bandari ya kilindoni na kutokana na tishio la ugaidi hata usalama ulikua juu ambapo kila abiria aliyekua anaingia alitakiwa kuonesha kitambulisho ili kujua wanaoingia kisiwani hapo.

Nilifikia nyumba ya wageni iliopo eneo la kilindoni na baada ya kuulizia wageni wakanielekeza eneo la utende ambapo kuna hotel za kitalii na fukwe za kuvutia.Nilipokua fukwe za bahari za utende zilizojaa hotel mbalimbali za kitalii hupendelea kukaa na wenyeji na kubadilishana nao mawaidha ili niweze ujua zaidi mji au eneo nnalolitembelea.

Ndipo nilipopata bahati ya kukutana na vijana wanaokaa fukwe za bahari kwa jina beach boys ambapo mmoja wapo akaja na katika kuonge naye akanambia anarupia ya kijerumania ambayo kama naweza mtafutia mteja.

Kusema kweli nilivutiwa kujua zaidi kuhusu hiyo sarafu kwani tumesikia historia mbalimbali kuhusu fedha hiyo.Kama alivyoahidi kijana alienda sehem na kurudi nayo na katika kuiangalia ilikua ni robo rupia ya mjerumani iliyotengenezwa kipindi cha utawala wao nchini Tanganyika.Kwa msaada wa google niliweza pata thamani yake kua kama paund 33 za kiingereza.Nilichojifunza hizi pesa kweli zinathamani hata kwenye masoko ya wenzetu wazungu na kama unapata bahati ya kuzipata nyingi let say 100 au 1000 unaweza jipatia kiasi kizuri...basi wadau wenzangu ambao mpo tayari kusaka utajiri*'TREASURE HUNTS. Bado hamjachelewa.

Nawasilisha
 
Hizo hela wanafanyia kitu gani mpaka ziwe na thamani?
 
Hebu fanya kwenda kule bweni ama chole ama tumbuju unaweza kuzipata nyingi tu huko hizo pesa
Waafrika hawana historia ya kuweka kumbukumbu ndo maana nawatengenezea treasure Map wanaotaka piga ela.
 
Mkuu... Asante kwa picha. Ila maelezo yako yana ndimu mno.
Mwisho wa siku hata Mungu mwenyewe hawezi lazimisha maamuzi ya binadamu mkuu ndo maana tumepewa utashi...kama huamini unaweza nipinga kwa reserch sehem unayohisi ni uongo
 
Kwanini Wanasafiri Usiku
Bado wanatumia majahazi kufika..so alfajiri ndo upepo unayasukuma kuelekea mafia...nasikia fununu bakhresa atawawekea boti...nadhan itasaidia sana kukifungua kisiwa kiutalii na kibiashara
 
Ukitaka kupotea ingia kwenye hizo biashara zimejaa utapeli na figisu nyingi na mwisho ya yote research kubwa ni je nani aliewahi kufanikiwa na hiyo biashara?jibu ni hakuna bali ni aina flani ya biashara iliojaa uwongo na utapeli
 
mkuu ela yenyewe ni hiyo hapo ebay ukitaka nikuconect upige mapesa nicheki tu ntakupeleka kwa wadau ah ah Data: 1907-MONETA D'ARGENTO-AFRICA ORIENTALE TEDESCA - 1/4 sicuramente migliori-Wilhelm II | eBay
Hahahahahaha kijana hebu acha kunichekesha hizo mambo tangu miaka ya 1981 nikiwa kijana na akili timamu nilikuwa nikiona watu wanahangaika nayo tu wanaingizwa chaka bila lolote hebu nikuulize huyo anayenunua hiyo sarafu kwa mamilioni ya pesa yeye anaenda kuifanyia nini?
 
ukitaka kupotea ingia kwenye hizo biashara zimejaa utapeli na figisu nyingi na mwisho ya yote research kubwa ni je nani aliewahi kufanikiwa na hiyo biashara?jibu ni hakuna bali ni aina flani ya biashara iliojaa uwongo na utapeli
Tatizo mkuu hawa vijana wanaamini sana drama na mambo mepesi tu mpaka nazeeka sijawahi ona mtu kafanikiwa kwa biashara ya rupia mara pasi ya mjerumani mara stove ya mjerumani zaidi tu ya watu kutapeliwa
 
Back
Top Bottom