Safari za ATCL kwenda China ziwe neema kwa wafanyabiashara nchini

Safari za ATCL kwenda China ziwe neema kwa wafanyabiashara nchini

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Tanzania na China zimekuwa na mahusiano ya muda mrefu, toka enzi zile za kufuata misingi mikuu ya Ujamaa chini ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Baba wa Taifa la China Mao Ze Dong.

Kwa miaka 61 sasa nchi hizi zimeendelea kushirikiana katika mambo kadhaa lakini zaidi ni namna asilimia kubwa ya wafanyabishara wanavyotegemea kuagiza bidhaa kutoka China kwa ajili ya soko la ndani ya Tanzania na nchi za jirani.

Tangu janga la Korona lilivokuja kuitikisa dunia hadi sasa sehemu kubwa ya "Supply" ya mizigo kutoka China kuja hapa Tanzania imekuwa ni ya kusuasua na chanzo kikubwa ni gharama kubwa za usafirishaji kwani mashirika mengi bado yamesitisha safari za kwenda nchini China

Leo tarehe 17 Julai 2022, Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) limeanza rasmi safari za moja kwa moja (Direct flight) kutoka Dar es Salaam kwenda Guangzhou, China katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Baiyun, safari zitakazofanyika kila Jumapili, hii ni fursa hii ni neema kwa wafanyabiashara ikitumika vizuri

Pamoja na kwamba Uhusiano wa Tanzania na China utaimarika zaidi hii ni fursa kubwa ya kuimarisha biashara kati ya nchi hizi ambayo thamani yake hadi kufikia mwaka 2020 ilikuwa ni zaidi ya Shilingi Trilioni 10.

ATCL iangalie namna ya kuweka gharama rafiki ili kuweza kulisha na kuhudumu uhitaji mkubwa uliopo wa kufikisha (Delivery) mizigo na huduma kutoka China. Wakati wengine wakiwa wamesitisha safari zao, huu ni wakati wa ATCL kusimika mizizi na kujiimarisha ili hali itakaporejea kawaida wao wawe tayari wametengeneza wateja wanaowaamini (Loyal Customers) kutokana na huduma watakazowapatia.

All in all ni mwanzo mzuri, tushikilie hapo.
ATCL.jpeg
 
Mpaka sasa hivi kwenye website yao hakuna hiyo trip hivyo mtu akitaka kununua tiketi hajui afanyaje! Na wale amabo hawajui kuna trip kama hii ndiyo kabisaa!

Halafu mnasema eti mbona shirika halifanyi vizuri kama mashirika mengine!" Ila watanzania kusema kweli tuna laana.

Hatuwezi kufanya kitu bila kutanguliza uzembe wa hali ya juu kabisa mbele. Sasa hizo tiketi wameuzia ndugu zao? Wameshindwa kuweka matangazo ya hii trip na booking yake kwenye website yao wakati kila kitu siku hizi ni internet?
 
Mpaka sasa hivi kwenye website yao hakuna hiyo trip hivyo mtu akitaka kununua tiketi hajui afanyaje! Na wale amabo hawajui kuna trip kama hii ndiyo kabisaa! Halafu mnasema eti mbona shirika halifanyi vizuri kama mashirika mengine!"

Ahaaa ahaaa, hilo shirika linaendeshwa kienyeji, usishangae ukakuta wanawazonga abiria na kuwaonyesha ndege yao kama wapiga debe hapo stand ya magufuli.
 
Mpaka sasa hivi kwenye website yao hakuna hiyo trip hivyo mtu akitaka kununua tiketi hajui afanyaje! Na wale amabo hawajui kuna trip kama hii ndiyo kabisaa! Halafu mnasema eti mbona shirika halifanyi vizuri kama mashirika mengine!" Ila watanzania kusema kweli tuna laana. Hatuwezi kufanya kitu bila kutanguliza uzembe wa hali ya juu kabisa mbele. Sasa hizo tiketi wameuzia ndugu zao? Wameshindwa kuweka matangazo ya hii trip na booking yake kwenye website yao wakati kila kitu siku hizi ni internet?
Hizi ndio changamoto zinazotukwamisha, mambo madogo kama haya yalipaswa kuwa yamemalizwa na tayari kuna matangazo ya kutosha kuwahimiza wafanyabiashara kutumia ATCL
 
Ahaaa ahaaa, hilo shirika linaendeshwa kienyeji, usishangae ukakuta wanawazonga abiria na kuwaonyesha ndege yao kama wapiga debe hapo stand ya magufuli.
Hapa sasa wewe umemua kuwa mkorofi tu, hhaahahhaha
 
Hapa sasa wewe umemua kuwa mkorofi tu, hhaahahhaha

Ndio tunakoelekea, iko siku utashangaa unaenda kupakia fly Emirates kisha unaporwa bag linaingizwa air Tanzania. Kama viongozi wote wa nchi na wa vyombo vya usalama walikuwa wanaacha shuguli zao wanaenda kupokea kila ndege ikija, kipi kinashindikana boss?
 
Ni mwanzo mzuri ila nilitazama zile bei nikanyoosha mikono, kwa sasa wasafiri kwanza wakishua
Lakini hata bei za Kampuni kama Qatar Airways zimechangamka, nadhani hiyo route bado ni ngumu kiasi
 
Ndio tunakoelekea, iko siku utashangaa unaenda kupakia fly Emirates kisha unaporwa bag linaingizwa air Tanzania. Kama viongozi wote wa nchi na wa vyombo vya usalama walikuwa wanaacha shuguli zao wanaenda kupokea kila ndege ikija, kipi kinashindikana boss?
Nadhani zama zimebadilika, Mama Samia naona amekuja na approach tofauti kwenye mambo mengi sana
 
Ndio tunakoelekea, iko siku utashangaa unaenda kupakia fly Emirates kisha unaporwa bag linaingizwa air Tanzania. Kama viongozi wote wa nchi na wa vyombo vya usalama walikuwa wanaacha shuguli zao wanaenda kupokea kila ndege ikija, kipi kinashindikana boss?
Hiyo route haifiki mwakani maana abiria ni wachache sn
 
Mpaka sasa hivi kwenye website yao hakuna hiyo trip hivyo mtu akitaka kununua tiketi hajui afanyaje! Na wale amabo hawajui kuna trip kama hii ndiyo kabisaa!

Halafu mnasema eti mbona shirika halifanyi vizuri kama mashirika mengine!" Ila watanzania kusema kweli tuna laana.

Hatuwezi kufanya kitu bila kutanguliza uzembe wa hali ya juu kabisa mbele. Sasa hizo tiketi wameuzia ndugu zao? Wameshindwa kuweka matangazo ya hii trip na booking yake kwenye website yao wakati kila kitu siku hizi ni internet?
Hivi walisharudishwa kwenye mfumo wa IATA?
 
Back
Top Bottom