Saikolojia: Mtoto wa chini ya miaka 6 anayeshuhudia matukio ya Ukatili ana uwezekano wa kuyafanya akiwa mkubwa

Saikolojia: Mtoto wa chini ya miaka 6 anayeshuhudia matukio ya Ukatili ana uwezekano wa kuyafanya akiwa mkubwa

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Leo kuna jambo nimelisikia kutoka kwa Mtaalamu mmoja wa Saikolojia aliyehojiwa na Clouds FM akisema matukio ya Ukatili yamekuwa yakiendelea kutokea kwasababu Watoto wanaoishi katika mazingira hayo wanaharibiwa kisaikolojia na hali hiyo inawafanya kuja kutenda Ukatili pale wanapokuwa wakubwa.

Mtaalam huyo amesema ndio maana Watoto wengi wanaoishia Mazingira yanayowaonesha Vitendo vya Ngono katika umri mdogo wanakuja kuwa tabia chafu zikiwemo kupenda ngono kupita kiasi au kupenda ngono na Watoto wadogo au Watu waliowazidi umri.

Pia, Mtoto mwenye umri huo akishuhudia wazazi, ndugu au jamaa wa karibu wakitamka maneno makali, vipigo ubakaji wengi wao wanakuja kuwa watendaji wa mambo hayo.

Sasa ndugu yangu, mwanao anakuwa katika mazingira gani? Anaona na kusikia vitu gani kila wakati?

Tafakari
 
Leo kuna jambo nimelisikia kutoka kwa Mtaalamu mmoja wa Saikolojia aliyehojiwa na Clouds FM akisema matukio ya Ukatili yamekuwa yakiendelea kutokea kwasababu Watoto wanaoishi katika mazingira hayo wanaharibiwa kisaikolojia na hali hiyo inawafanya kuja kutenda Ukatili pale wanapokuwa wakubwa.

Mtaalam huyo amesema ndio maana Watoto wengi wanaoishia Mazingira yanayowaonesha Vitendo vya Ngono katika umri mdogo wanakuja kuwa tabia chafu zikiwemo kupenda ngono kupita kiasi au kupenda ngono na Watoto wadogo au Watu waliowazidi umri.

Pia, Mtoto mwenye umri huo akishuhudia wazazi, ndugu au jamaa wa karibu wakitamka maneno makali, vipigo ubakaji wengi wao wanakuja kuwa watendaji wa mambo hayo.

Sasa ndugu yangu, mwanao anakuwa katika mazingira gani? Anaona na kusikia vitu gani kila wakati?

Tafakari
Sio lazima ajifunze na kukitenda anaweza akachukia pia hicho kitendo na asije kukitenda maishani mwake.
 
Watoto hushape akili na matendo yao ya ukubwani kwa kucopy waliyoyashuhudia ukubwani.

Mfano: Mabinti wengi ambao wamekuwa masingle mother ukiwafutalia historia zao unakuta alilelewa na Baba ambaye si mzazi wake wa kumzaa. Sasa akikutana hata na mwanaume mzuri mwenye malengo mazuri atafanya kila namna ili aweze ku sabotage hayo mahusiano mazuri wagombane halafu mtoto wake au watoto wake wakalelewe na baba wa kambo. Kimachompa msukumo wa kufanya hivyo ni kuamini kuwa mtoto wake anatakiwa kulelewa na baba wa kambo ndio namna sahihi kama yeye alivyolelewa na baba wa kambo.

Au mtoto wa kiume au wa kike ambaye utotoni mwake lugha ya kuelekezwa na wazazi wake ilikuwa ni kipigo na kufokewa then na yeye akiwa mzazi atatumia the same parenting style ya kufokea na kupiga watoto wake akiwaelekeza jambo dogo tu.

Mtoto wa kiume ambaye akiwa mdogo alifanyiwa ufedhuli wa kingono kama kuingiliwa kinyume na maumbile yake, au kulala na mwanamke aliyemzidi umri ubongo wake utaregister kwamba kwenye ngono hakunaga mipaka so unaweza lala hata na watoto ili hali wewe ni mtu mzima.

Ndio unaona baba mtu mzima wa miaka 40 anavutiwa kingono na katoto ka miaka 13 hadi 16 umri ambao yeye pengine alifanyiwa ufedhuli.

Matokeo yake ndio unasikia mtu mzima kufanya ngono na mtoto mdogo bila aibu yoyote wala kujali madhara. And the cycle continues.
 
Niliona mtoto wa jirani ana matusi makubwa ya nguoni mpaka nilishtuka lakini nikaja kugundua kuwa wazazi wake huwa wanatukanana mbele yake ... kwahiyo dogo kaadapt aiseh

Baba yake ameshafariki kwa UKIMWI kwa sasa dogo anaishi na mama yake ni mtoto wa kike ..now kama miaka 8 hivi unadhani atakuja kuwa katika maadili mema???.....nope malezi uchangia sana kwenye uhalibifu wa mtoto
 
Back
Top Bottom