Sakata la Bandari linaenda kuongeza mpasuko wa kidini. Tukosoe kwa tahadhari

Huu waraka ulitakiwa kutolewa kwenye neutral ground.Watu hawaoni madhara ya hiki
 
Hawajakosea kabisa.
Wao wanahubiri maisha ya watu na kuokoa watu.

Hata Yohana alichinjwa kwa kumkosoa mtawala katika mahubiri yake ndivyo wanavyofanya hawa. Kazi yao siyo kufufua misukule. Ni kukemea yasiyofaa, na kamwe hawawezi kuhubiri yasiyo kwa watu.

Zungumzieni mambo waliyosema na point zao siyo kuzungumzia habari za dini, kila mtu ana dini
 
Mkuu uo ndiyo utaratibu ulivyo kwa kanisa Katoliki! Kule juu likitoka tamko linashuka chini na huku chini linashuka kupitia nyumba za ibada maana limetolewa na maaskofu.

TEC haijaanza leo kutoa Waraka! Kila awamu iliyopita walitoa tamko kama waliona mahala pana shida, na wanatoa waraka mara baada ya kuwahoji wote ambao wahusika wakuu! Kama issue hii waliwaita mpaka Waziri Mbalawa Mwenyewe na team yake, wakiwa na ao wakina Hamza Johari ila ukweli ni kuwa Serikali walishindwa kuwashawishi Baraza la Maaskofu.

Issue ninayoiona mimi ni pale wajibu hoja wao wanahisi Rais anapingwa kwasababu ya Dini yake na kwakuwa hawa waliotoka leo ni wa dini nyingine.


Nakuekea gazeti la 2018 hapa TEC wakimpiga Magufuli na pia ulishuka kama leo hii ukasomwa.
 
Basi wasio wa TEC wakae kimya. Kama wamesoma kanisani basi wasio wa kanisa haiwahusu na wakae kimya. Wakitaka kusema waseme kuhusu mambo yaliyomo humo na si waliosema ni akina nani.

Wamesema yana maana?
 
Hizi waraka huwa zinatolewa kwa marais wa kiislam tu jaman...?mzee kikwete alipata tabu sana licha ya kujipendekeza na mama naye anapata tabu....
Qur an ina sema nn ...mm nanukuu tu...
"يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا بِطَانَةً مِّن دُونِكُمْ لَا يَأْلُونَكُمْ خَبَالًا وَدُّوا مَا عَنِتُّمْ قَدْ بَدَتِ الْبَغْضَاءُ مِنْ أَفْوَاهِهِمْ وَمَا تُخْفِي صُدُورُهُمْ أَكْبَرُ ۚ قَدْ بَيَّنَّا لَكُمُ الْآيَاتِ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ

[ AL I'MRAN - 118 ]
Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini..
 
Jamani msipotoshe,
1. Kila inapotokea kuna kitu kinalalamikiwa na watu (wala si wa dini moja) kitaifa hawa huwa wanatoa waraka. Mwaka 2018 walitoa kwa Magufuli.Alikuwa Muislam?
2. Waraka huu haujaenda kwa dini, unazungumzia mkataba, na wametaja vipengele vyenye shida, dini imetajwa wapi katika waraka kama siyo kupotosha.
3. Mkataba siyo wa rais, ni hasa wabunge waliopitisha kama hawajui kusoma chochote, wamepekeewa washauri wakasema wanayojua. Sasa dini inaanzia wapi?

Kama hatujaelewa tutafute nafasi kueleweshwa badala ya kuleta uchonganishi usiofaa.
 
Dini inashughulika na watu wanaokuja kulia kwenye nyumba za ibada kwa maamuzi mabovu ya wanasiasa ni waumini.
Amani ikitoweka chanzo ni wanasiasa watapanda ndege wanaondoka wanawaachia wanadini kazi ya kuhudumia wakimbizi
 
Pitieni vipengele vya mkataba mje n hoja za udhaifu wa waraka na Sio kujifichia kwenye dini kutafuta huruma kwa wafu
 
Kwanini majibizano yasiwe kati ya Kanisa KATOLIKI na Serikali. Sasa Mimi ninachoshangaa kwanini baadhi ya viongozi wa serikali na viongozi wastaafu wanaingilia kwenye suala Dini. Kwanini majibizano yasiwe kwenye Hoja za Mkataba ila wanalazimisha uhamie kwenye Dini.
 
Kama hawataki kuubatilisha mkataba wa kihuni basi watumishi wa Mungu watawapigania watanzania.Ni bora amani itoweke ili kuwalazimisha hawa viongozi kutii matakwa ya wananchi ya kurekebisha mkataba wa kihuni au wauvunje kabisa.kufanya hivyo tutakuwa tumetengeneza mazingira mazuri kwa wajukuu wetu.OKOA BANDARI ZETU
 
Wanalazimisha watu waseme vibaya. Mkataba umeoneshwa sehemu chache zenye mapungufu, dini hakuna ilipotajwa.
Ila wao wanahangaika kupindishia kwenye dini kwakuwa wanaona huko ndiyo kitisho kikubwa zaid. Waache hizo tabia.
 
Mkuu akikupa jibu la maana niite kobe nimekaa pale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…