Sakata la Baraka Shamte: Hatari ya kusema yasiyotakiwa kusemwa

Ujamaa...
Huna ujuzi wa somo hili.

Nina hakika hivyo vitabu vingi unavyosema umesoma si vitabu vinavyohusu historia ya uhuru wa Tanganyika ikiwa kweli umesoma vitabu vingi.

Nasema hivi kwa kukusoma hapa.
Sioni kama ni mtu uliyesoma vitabu vingi.

Nasema hivi tena kuwa wewe si msomaji kwa kuwa hapa unazungumza na mimi msomaji na pia mwandishi.

Katika historia ya uhuru wa Tanganyika nimeandika wazalendo wengi waliofutwa katika historia ya uhuru wa Tanganyika na chanzo changu ni Nyaraka za Sykes.

Hawa ndiyo waliounda African Association 1929 na wakaasisi TANU 1954.

Hakuna mtu muhimu aliyekuwa katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika ambae humkuti katika nyaraka hizo.

Ungesoma kitabu cha Abdul Sykes hili lingekudhihirikia.

Wewe unataka kujadili somo ambalo huna ujuzi nalo.

Wala sikuandika kwa mtazamo wangu nimeandika yale ambayo walifanya.

Mathalan nimeeleza uamuzi wa kumtia Nyerere katika uongozi wa TAA 1953 baada ya kikao cha watu watatu, Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Mwapachu.

Nimeeleza mkutano wa Abdul Sykes na Jomo Kenyatta Nairobi mwaka wa 1950 ikiwa ni juhudi za kuunganisha TAA na KAU katika kuzikomboa Tanganyika na Kenya.

Ushahidi wa haya yote upo katika Tanganyika Intelligence Summary (Special Branch).

Hii si historia ya Wapagani kwani hawakuwako si ndani ya TAA wala TANU.
Wala halikuwa suala la Ujamaa Vijijini.

Mwalimu alibakia kimya kwa hofu.
Siku ile haikuwa mara ya kwanza tatizo lile kalisikia likisemwa.

Suala lile lilikuwa suala nyeti sana.
Nimeeleza historia ya haya yote katika kitabu cha Abdul Sykes.
 

Umeeleza mambo mengi sana kwangu nayo nayaita ni “mtizamo”. Maelezo yangu hujayaelewa au umekwepa kuleta majibu stahiki toka mjadala uanze bali umeanza kuleta mjadala wa historia ya kupigania uhuru toka TAA (1929) mpaka TANU (1954) na majina ya wapigania uhuru walio wachache. Pia maelezo yako ya kua sina ujuzi wa somo hili na huoni kama mtu niliesoma vitabu au vitabu nilivyosoma uzani kama ni vya kupigania uhuru wa tanganyika haya nayaweka pembeni sitaki tukabiliane kwa udhibitisho, umeshajitapa kua ni wewe ni mwandishi na msomi wa vitabu inatosha.

Rudi usome na ulejee kuyaelewa maelezo yangu kwa ufasaha ili somo lieleweke juu ya maelezo ya shekhe mwilima dhidi ya hayati Julius na sio historia ya kupigania uhuru kwani toka 2010 humu jamvini mabishano hayajapata kuisha bado unakabiliwa na maoni ya wadau wengi na wewe unawakabili vilivyo na bado hapajapata kua na muafaka juu ya historia yako.

Maelezo yangu ni juu ya hali ya umaskini wa kutisha wa wananchi wa nchi hii toka uhuru mpaka leo hii, hali za waislamu na wakristu bado vipato vyao ni vya kusua sua na umaskini ni wa kiwango kikubwa sana huko mikoani na vijiji vyake. Jaribu ufunge safari uanze kutembelea mikoa na vijiji vya nchi hii then utayapata majibu ya nacho kisema usibakie tu magomeni, kariakoo na huko ulaya anza kufanya tafiti ya hali ya vipato na maisha halisi huko mikoani na vijiji vyake, hapa dar mamia kama sio maelfu ya waislamu na wakristu hawana makazi na wanalala nje.

Wadau wa huo mkutano waliamua kumpuuza shekhe mwilima kwani waliona huenda ni mjinga aliepotea kimawazo na kimtizano kwani hali ya jamii yote kwa kipindi hicho ilikua hoe hae na wachache ndo walikua kwene fursa chache sana za serikali, je mwalimu angejibu nini. Leo hii ni 2022 hali za kimaisha zikoje kwa waislamu na wakristu au mnajiziba pamba machoni hamuoni kua bado sote tulio wengi tena mamilioni twataabika kwa ukapuku.
 
Ujamaa...
Naanza na hili la ''kujitapa.''
Kama nikitaka kujitapa sitaweka hayo kuwa mimi ni mwandishi.

Ningekueleza kama nataka kujitapa ni miradi mingapi ya wachapaji wakubwa wa vitabu nimeshirikishwa kuandika na vitabu nilivyoandika vimechapwa vipo sokoni na vinasomeshwa.

Kwani wewe uliposema umesoma vitabu vingi umetaka kujitapa?

Nataka kukufahamisha kuwa kati yetu na Nyerere au kati ya Nyerere na wengi aliowakuta katika kupigania uhuru wa Tanganyika ni suala la historia hii na mchango wa Waislam na nini kimepatikana kwao?

Mimi hapa hilo ndilo suala langu kubwa ninalosomesha hapa JF kiasi wamenipa ''Certificate of Appreciation.''

Naamini hili unalifahamu.
Mimi siko katika mjadala huo unaouleta hapa wa Vijiji vya Ujamaa nk.

Ikiwa unataka tujadili hayo mimi simo jadili na wengine.

Muafaka wa kitabu changu nimeupata miaka zaidi ya 20 iliyopita pale Prof. Haroub Othman alipomkabili Julius Nyerere na nakala ya kitabu changu na kumuomba na yeye aeleza historia yake kwani historia niliyoandika ya Abdulwahid Kleist Sykes imefuta mengi ambayo watu walikuwa wanayaamini kuhusu yeye.

Haya nimekupa kwa kifupi.

Nyerere akakubali kuwa kiandikwe kitabu cha maisha yake yeye wakati ule alikuwa mgonjwa anaumwa hawezi kuandika.

Nyerere na yeyote awaye yule hawawezi kumpuuza Abubakar Mwilima wala yeyote yule anaemfahamu yeye toka enzi za kudai uhuru.

Historia hii niliyoandika ipo katika Dictionary of African Biography (DAB) mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York.

Haya hayajapata kuwa mambo ya kupuuzwa.

Hapa kulikuwa na njama ya kufuta historia ya kizazi cha jamii yangu, historia ya zaidi ya miaka 100.

Pale walipokuwa wameamini kuwa wamefanikiwa kuifuta historia hiyo ndipo niipokuja na kitabu cha Abdul Sykes mwaka wa 1998.

 

Aloooo ustadhi nazani unachanganya mada. Itoshe tu kusema kua unaleta maelezo mengi sana yaliyo nje ya mada unaeleza vitu vingi sana ambavyo sinyo navyovihitaji kwani unavyovisomesha kwangu tayali umeshakabiliana na mamia ya mijadala hapa na suluhisho halipo.

Mjadala ulikua ni swali la shekhe mwilima kwa mwalimu basi ila sio hizo historia bali ni swali la shekhe mwilima ndo ulikua mjadala wangu. Maelezo yako yapo nje ya mjadala wako au kwa lugha nyingine mjadala uliouanzisha
Umekushinda. Kila la kheri mkuu.
 
Ujamaa...
Hapa JF ilinichukua muda mrefu sana kueleza kuwa mimi si "Ustadh," kama vile kuwa wao hawawezi kuwa "Padri," "Mchungaji," au "Shamasi."

Mwishowe nikaeleweka.
Naamini tumefahamiana.

Jitahidi katika R na L.
"Tayari" si "Tayali."

Maelezo yangu unayoyaona mengi ni kuwa mimi hapa nimechukua nafasi ya mwalimu nasomesha historia ya uhuru ambayo kwa miaka mingi ilipotea.

Katika hili siandiki wewe ukiwa mlengwa bali darasa zima lenye wanafunzi lukuki na wasomaji wangu wananufaika na elimu hii mpya.

Mimi sitafuti suluhisho mimi nataka wasomaji wangu waisome historia ya kweli na wawajue wazalendo kama Mwalimu Abubakar Mwilima.

Ikiwa wewe hupendezewi hiyo ni bahati mbaya kwako na dawa yake ni ndogo sana.

Usinisome.
Kuhusu kushindwa.

Nakuhakikishia hakuna anaeweza kunishinda mimi katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika na TANU.

Kitabu cha Abdul Sykes toka kichapwe mwaka wa 1998 hadi sasa kimechapwa matoleo manne.

Hii haijapata kutokea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…