Sakata la DP World: Kamati ya Bunge Yaahirisha Kupokea Maoni ya Marekebisho ya Sheria za Maliasili ikitaka Ufafanuzi wa Serikali

Sakata la DP World: Kamati ya Bunge Yaahirisha Kupokea Maoni ya Marekebisho ya Sheria za Maliasili ikitaka Ufafanuzi wa Serikali

Umeaongea points sn, ubovu unaanza hapa kwanza
Angalia hawa wastaafu kupitia TISS watu wanaotuwekea kuongoza, hivi mtu km Bashungwa, Ndumbaro, Kijaji, Pinda mdogo, hata spika, MaDC wengi tu hawana uwezo na sifa hata kuwa VEO... kwa kutizama tu..unaona sifa yoyote ya kiuongozi kwenye sura za watu hao??? mtu mwenye sifa ya kuwa kiongozi hata kwa sura yake tu utaona kipo kitu anacho cha kiuongozi, TISS wanataka watu wa aina hii ili wao ndio wafanye maamuzi, huyo waliyemuweka ni km picha tu..hawataki watu wako na sharp mind na wenye independent brain wapewe nafasi kwenye uongozi sababu si rahisi kumdrive mtu wa aina hiyo..! wao ndio wametufikisha hapa..watanzania tudeal na chanzo cha tatizo..mambo ya DPW ni matokeo ya tatizo kubwa tunaliruka hata kulitaja! tunakalia kubishana na faiza foxy au mwashamba..
 
Angalia hawa wastaafu kupitia TISS watu wanaotuwekea kuongoza, hivi mtu km Bashungwa, Ndumbaro, Kijaji, Pinda mdogo, hata spika, MaDC wengi tu hawana uwezo na sifa hata kuwa VEO... kwa kutizama tu..unaona sifa yoyote ya kiuongozi kwenye sura za watu hao??? mtu mwenye sifa ya kuwa kiongozi hata kwa sura yake tu utaona kipo kitu anacho cha kiuongozi, TISS wanataka watu wa aina hii ili wao ndio wafanye maamuzi, huyo waliyemuweka ni km picha tu..hawataki watu wako na sharp mind na wenye independent brain wapewe nafasi kwenye uongozi sababu si rahisi kumdrive mtu wa aina hiyo..! wao ndio wametufikisha hapa..watanzania tudeal na chanzo cha tatizo..mambo ya DPW ni matokeo ya tatizo kubwa tunaliruka hata kulitaja! tunakalia kubishana na faiza foxy au mwashamba..
Hakuna vetting yoyote inayofanyika zaidi ya maigizo
 
Aisee, hivi inakuwaje muwekezaji mmoja tuu anafanya mpaka tubadili sheria za nchi ambazo zilitungwa kwa umakini mkubwa? Hii sheria ya maliasili ni mpya kabisa ya mwaka 2017 tuu hapo, ni kwa nini tubadili sheria inayolinda maliasili kwa ajili muwekezaji mmoja tuu?

Ina maana akija muwekezaji mwingine ambaye sheria itakuwa inambana kwenye masharti anayoyataka pia tutairudisha tena bungeni kuvichomoa hivyo vipengele?

Huyu muwekezaji ana nini hasa cha zaidi mpaka anafanya sheria za nchi zinanyumbulishwa ili tu yeye a-fit in?

Kwa nini yeye kama muwekezaji asi-blend in na sheria za nchi yetu?

Kimsingi yeye ndiyo anapaswa ajinyumbue ili kuendana na sheria halali za nchi zilizowekwa.

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Kamati ya Bunge ya Katiba na Masuala ya Kisheria imeahirisha kusikiliza maoni ya wadau kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Nchi Kuhusiana na Umiliki wa Maliasili ya mwaka 2017 na Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu Masharti Hasi Katika Maliasili ya nchi ya mwaka 2017.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joseph Mhagama, ameiambia The Chanzo Alhamisi hii kwamba wameomba ufafanuzi zaidi kutoka kwa Serikali kuhusu mabadiliko hayo ambayo yameibua mjadala mkubwa miongoni mwa wafuatiliaji wa mambo nchini.

Sheria hizo ni miongoni mwa sheria zilizojumuishwa katika Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 wa Mwaka 2023, uliokusudia kurekebisha, pamoja na sheria nyingine, sheria hizo mbili ili zisitumike katika uendeshaji wa miradi ya uendeshaji, uendelezaji na bandari.

Huku wadau wengi wakihusisha sheria hii na mkataba unaotegemea kuipa kampuni ya DP World ya Dubai, kazi ya kuendesha, kuboresha na kuendeleza bandari Tanzania.

Muswada huo uliosomwa bungeni kwa mara ya kwanza Juni 28, 2023, na Kamati ya Bunge ya Katiba na Masuala ya Kisheria ilialika maoni ya wadau kuhusu marekebisho yaliyotazamiwa kabla ya muswada huo kurejeshwa bungeni baadaye Agosti. Kamati ilisikiliza maoni ya wadau hao mnamo Agosti 16, 2023.

Sehemu ya IV na V ya muswada wa marekebisho zinapendekeza marekebisho ya sheria tajwa ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sheria hizo hauathiri uwekezaji utakaokuja kufanywa katika uendelezaji na uendeshaji wa bandari.

Serikali inasema marekebisho hayo yanalenga kuwezesha bandari za Tanzania “kufanya kazi katika viwango vya kimataifa na kuvutia meli nyingi za mizigo mikubwa kuhudumiwa na bandari” za Tanzania.

Sheria hizi mbili ambazo zilipitishwa mwaka 2017 ziliwekwa kwa madhumuni ya kuhakikisha Tanzania inanufaika na maliasili zake, lakini pia inatoa nafasi ya kurekebisha mikataba mibovu.

Dk Mhagama ameiambia The Chanzo kwamba kamati yake ilipokea maoni kuhusu sehemu nne za sheria ambazo Serikali inataka kuzifanyia marekebisho, na kuacha sehemu mbili zilizoundwa ili kuipa Tanzania mamlaka juu ya maliasili zake.

“Muswada huo una sehemu sita, kamati iliona ifanyie kazi vipengele vinne tu, na kuviacha vingine viwili ili kutengeneza njia ya mashauriano na Serikali kwa lengo la kupata ufafanuzi wa maudhui ya sheria hizo mbili,” Mhagama, ambaye ni mbunge wa Madaba (Chama cha Mapinduzi – CCM), anasema.

Anasema kuwa wadau wataalikwa kuwasilisha maoni yao mara baada ya kupata ufafanuzi na Serikali pindi ikiamua kuendelea na marekebisho yaliyopendekezwa na kuongeza kuwa kamati hiyo inatakiwa “kujiridhisha” na yaliyomo kwenye muswada huo kabla ya kuamua kuendelea nao.

Dk Mhagama ameiambia The Chanzo kwamba kamati yake iliomba maelezo kutoka kwa Serikali kuhusu marekebisho ya sheria hizo mbili, huku akishindwa kueleza ni lini hasa anatarajia mamlaka kujibu hoja zilizoibuliwa.

“Serikali itakuwa hapa milele; wakati wowote watakapoona inafaa kujibu hoja tulizoibua watakuja kwenye kamati na mapendekezo yao,” Dk Mhagama anafafanua. “Si lazima iwe leo, kesho au mwakani.”

Mapendekezo ya marekebisho ya sheria hizo yanakuja wakati mjadala mkubwa wa kitaifa ukiendelea kuhusu makubaliano baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai ili kuiruhusu DP World kuiendesha bandari ya Dar es Salaam.

Mnamo Juni 10, 2023, wabunge waliridhia kwa kauli moja mkataba huo tata ambao unaendelea kuleta mgawanyiko wa taifa, huku mgawanyiko wa maoni kati ya wafuasi wake na wakosoaji ukionekana wazi kila siku.

Serikali na chama tawala wanauelezea mkataba huo kuwa “mkataba bora zaidi kuwahi kutokea,” huku wanaharakati na vyama vya upinzani wakiuelezea kuwa “mkataba mbaya zaidi.”

Miongoni mwa waliokataa mpango huo ni Maaskofu wa Kanisa Katoliki, ambao kwenye taarifa yao ya pamoja ya Agosti 18, 2023, waliitaka Serikali kusikiliza matakwa ya wananachi ya kufuta mpango huo, wakisema, “Sauti ya watu ni sauti ya Mungu.”

“Ni lazima miradi kama hii [ya maendeleo ya bandari] iendeshwe na kusimamiwa na Watanzania wenyewe, huku wakikaribisha ushirikiano ambao wao wenyewe wataudhibiti,” Maaskofu hao 37 walisema katika taarifa yao hiyo ya pamoja.

“Hili ndilo ambalo wananchi wamekuwa wakililia ili tuweze kuboresha uwezo wetu wa kusimamia uwekezaji muhimu,” waliendelea kueleza. “Kwa sababu tayari tumeshachambua mapungufu ya jinsi tunavyoendesha bandari zetu, tunaweza kuyafanyia kazi huku njia za uchumi zikisalia mikononi mwetu.”

Source: The Chanzo
Vipi serikali ya UAE / Emirati ya Dubai inaweza kubadilisha sheria ili Tanzania, tuwekeze UAE/ Dubai?
 
Angalia hawa wastaafu kupitia TISS watu wanaotuwekea kuongoza, hivi mtu km Bashungwa, Ndumbaro, Kijaji, Pinda mdogo, hata spika, MaDC wengi tu hawana uwezo na sifa hata kuwa VEO... kwa kutizama tu..unaona sifa yoyote ya kiuongozi kwenye sura za watu hao??? mtu mwenye sifa ya kuwa kiongozi hata kwa sura yake tu utaona kipo kitu anacho cha kiuongozi, TISS wanataka watu wa aina hii ili wao ndio wafanye maamuzi, huyo waliyemuweka ni km picha tu..hawataki watu wako na sharp mind na wenye independent brain wapewe nafasi kwenye uongozi sababu si rahisi kumdrive mtu wa aina hiyo..! wao ndio wametufikisha hapa..watanzania tudeal na chanzo cha tatizo..mambo ya DPW ni matokeo ya tatizo kubwa tunaliruka hata kulitaja! tunakalia kubishana na faiza foxy au mwashamba..
Mkuu tatizo ni nini? Lipi? Tunalitatuaje?
 
Maelezo mengi ya nini badisheni uo mkataba au la muachane nao
Hata kusingekuwepo hayo makubaliano ya DPW, hizo sheria ilibidi zibadilishwe haziendani na stabilisation clauses za mikataba ya kimataifa. Clauses ambazo hakuna mwekezaji ataingia mkataba wa muda mrefu bila ya kuziweka.

Shida ni hizo sheria zenyewe katika ulinzi wa asset na rights za mwekezaji, lakini si IGA.
 
Yaani huyu Mwarabu amekuja kutubadilishia sheria zetu kwa faida yake.
Kwa faida ya Tanzania, mtegemee mabadiliko makubwa kila sehemu, msiishi kimazowea, ieleweni kwanza falsafa yake ya RRRR.

mkiielewa Hamtopata shida na kustuka kwa sheria zitazokuja kubadilishwa, ni nyingi sana, mpaka Katiba itabadilishwa:

 
Hata kusingekuwepo hayo makubaliano ya DPW, hizo sheria ilibidi zibadilishwe haziendani na stabilisation clauses za mikataba ya kimataifa. Clauses ambazo hakuna mwekezaji ataingia mkataba wa muda mrefu bila ya kuziweka.

Shida ni hizo sheria zenyewe katika ulinzi wa asset na rights za mwekezaji, lakini si IGA.

Shida serikali zetu haziko makini kwenye mikataba.

Ndio maana Magufuli akiweka hiyo sheria kulinda rasilimali za Taifa.

Hatujawahi kushinda kesi yoyote muhimu, IPTL, Escrow, Gesi, Madini, mengine zote.

Tulitumia ubabe tu kuishinda Acacia., Barrick Gold. Ndio maana Magu akaona aachane na huo ujinga na upumbavu wa kupigwa mabilioni kwa kuweka sheria na kulinda rasilimali zetu. Ukitaka mkataba fuata sheria zetu za ndani.
 
Hamna kitu hapo, zitapitishwa tu. Hapo labda wamerudisha tu huenda kuna mahali kuna nukta ama kama imekosekana...
 
Sawa kabisa Rufiji dam..TISS ndio chanzo cha matatizo yote haya! na sababu kubwa ni mfumo uliopo wa namna wanavyopatikana na kazi wanazofanya haufai, viongozi wastaafu wa ccm wametumia ubovu wa mfumo huu kujaza watu wao kwenye hii taasisi kiasi kwamba Rais aliyepo madarakani anatumikia maslahi ya wastaafu kadri wanavyotaka..watanzania tusipoteze nguvu nyingi kulaumu Rais, tuungane tushughulike na hii taasisi, kwa kuanzia ni kuivunja yote na kuwaondoa wote waliopo sasa ili kupata wengine wapya kabisa..hii ni kazi kama kazi zingine, mtu yeyote mwenye utimamu wa akili na mwili anaweza kufanya kazi ya usalama..tuanzie hapo, tuache malalamiko!
Hiyo siyo ",approach" sahihi kwa utawala.

Kiutawa ulio bora , ni lazima uwe Resilience, ielewe R hiyo ya falsafa ya mama Samia utanielewa namaanisha nini.
 
Shida serikali zetu haziko makini kwenye mikataba.

Ndio maana Magufuli akiweka hiyo sheria kulinda rasilimali za Taifa.

Hatujawahi kushinda kesi yoyote muhimu, IPTL, Escrow, Gesi, Madini, mengine zote.

Tulitumia ubabe tu kuishinda Acacia., Barrick Gold. Ndio maana Magu akaona aachane na huo ujinga na upumbavu wa kupigwa mabilioni kwa kuweka sheria na kulinda rasilimali zetu. Ukitaka mkataba fuata sheria zetu za ndani.
Hakuna anaekataa nia njema ya hizo sheria, lakini haziendani na clauses za mwekezaji na yeye kwenye kulinda uwekezaji wake wa miaka mingi.

Njia pekee ya kupambana ni kutengeneza wanasheria wetu na negotiators wetu watusaidie kufunga hiyo mikataba na wenye uwezo wa kuitetea hiyo mikataba panapo migogoro.

Lakini tupeleweke wenyewe wanasheria kwenye tribunals. Wanapokuwa huko kwenye ‘cross examination’ waseme hawakulala vizuri jana yake, au unabeba sister duh ndani ya safari hata kama uwezo wake mdogo kwa sababu unazozijua mwenyewe team leader. Unapeleka mtaalamu wa sijui wa maswala gani ya sheria kujadili commercial contracts.

Halafu ukitoka hapo ulaumu mkataba mmbovu baadae na ukivunja kiholela baada kuona unapunjwa ukienda mahakamani ukashindwa kesi useme umeonewa mahakamani.

Unaweza kuona najiona mjuaji ila ukweli ni hivi kama wanasheria wengi wameshindwa kuilewa hiyo IGA ambayo ni framework tu, basi Tanzania ina nafasi ndogo sana ya kushinda kesi za uwekezaji nje ya nchi ambazo ni fully ‘commercial contracts’ huo ndio ukweli wenyewe.
 
Hakuna anaekataa nia njema ya hizo sheria, lakini haziendani na clauses za mwekezaji na yeye kwenye kulinda uwekezaji wake wa miaka mingi.

Njia pekee ya kupambana ni kutengeneza wanasheria wetu na negotiators wetu watusaidie kufunga hiyo mikataba na wenye uwezo wa kuitetea hiyo mikataba panapo migogoro.

Lakini tupeleweke wenyewe wanasheria wanaoenda kwenye tribunals wanapokuwa ‘cross examined’ waseme hawakulala vizuri jana yake, au unabeba sister duh ndani ya safari hata kama uwezo wa mdogo kwa sababu unazozijua mwenyewe team leader. Halafu ukitoka hapo ulaumu umeonewa mahakamani.

Unaweza kuona najiona mjuaji ila ukweli ni hivi kama wanasheria wengi wameshindwa kuilewa hiyo IGA ambayo ni framework tu, basi Tanzania ina nafasi ndogo sana ya kushinda kesi za uwekezaji nje ya nchi ambazo ni full ‘commercial contracts’ huo ndio ukweli wenyewe.
Flamework ni msingi muhimu , ni flame, nguzo zinazoibeba nyumba, jengo, familia, Taifa, mikataba yote inayokuja.

Makubaliano ya msingi ndio hayo IGA. Kutatua matatizo, haki, wajibu migogoro, tofauti. Ingawa kwenye HGA kunakuwa na specifics.

Wanasheria wetu huwa wako upande wa wawekezaji huku wakifanya kazi serikalini. Wanapiga huku na Kule kwa kukosa uzalendo. Serikali yetu mara nyingi ipo upande kwa maslahi ya wageni tunahiwaji w wawekezaji sahihi. Mara nyingi ni wapigaji wakishirikiana na serikali yetu.

Mkabata wa Gesi, IPTL, Sakata la Escrow, Issue za Loliondo, Ngorongoro zinalisaidiaje hili Taifa?
 
Flamework ni msingi muhimu , ni flame, nguzo zinazoibeba nyumba, jengo, familia, Taifa, mikataba yote inayokuja.

Makubaliano ya msingi ndio hayo IGA. Kutatua matatizo, haki, wajibu migogoro, tofauti. Ingawa kwenye HGA kunakuwa na specifics.

Wanasheria wetu huwa wako upande wa wawekezaji huku wakifanya kazi serikalini. Wanapiga huku na Kule kwa kukosa uzalendo. Serikali yetu mara nyingi ipo upande kwa maslahi ya wageni tunaowahita wawekezaji. Mara nyingi ni wapigaji wakishirikiana na serikali yetu.

Mkabata wa Gesi, IPTL, Sakata la Escrow, Issue za Loliondo, Ngorongoro zinalisaidiaje hili Taifa?
Upo sahihi 100% frameworks ndio nguzo ya msingi na baadhi ya clauses hapo kwenye IGA ni sehemu ya aspects za mikataba ya mbele.

Lakini hakuna kilichopo hapo ambapo hutakikuta katika BIT ya nchi nyingine yoyote; hizo ni standard clauses katika mikataba ya biashara za kimataifa kwenye kulinda investments.

Bila ya hayo mambo mwekezaji anakuwa anachukuwa risk kubwa sana katika usalama wa uwekezaji wake na hawa wenzetu wana experience tosha ya kugeukwa mbeleni ndio maana wanataka hayo mambo yawepo katika mkataba au sheria ya nchi kwanza.

Solution ni moja tu kama tunataka kufanya biashara na dunia, ni kuwajengea uwezo watanzania wa kuweza kujadiliana consideration ya hiyo mikataba (na hayo mambo huwa ni siri hatuoni n’go) vinginevyo tutaendelea kuibiwa tu na kushindwa kesi kwa sababu atujifunzi hayo majadiliano ni tenchical.

Tutalaumu miaka nenda miaka rudi wakati mchawi wetu sisi wenyewe.
 
Hiyo siyo ",approach" sahihi kwa utawala.

Kiutawa ulio bora , ni lazima uwe Resilience, ielewe R hiyo ya falsafa ya mama Samia utanielewa namaanisha nini.
Yeye aliyeianzisha aielewe na kuiweka kwenye vitendo..resilience anatakiwa kuwa nayo yeye na watu wake sio sisi, wanaharibu na kutufanyia maigizo kisa wana excuse ya sijui rrrr..we believe in action fullstop, muda wa kupindua pindua misemo mara kkk mara rrr ulishapita kitambo..we need ACTION, wakiharibu sisi hatuna muda wa kuchambua nani ndio nani, ni kuwamwaga wote, wakaulizane huko watakakokuwa wenyewe kwa wenyewe.
 
Upo sahihi 100% frameworks ndio nguzo ya msingi na baadhi ya clauses hapo kwenye IGA ni sehemu ya aspects za mikataba ya mbele.

Lakini hakuna kilichopo hapo ambapo hutakikuta katika BIT ya nchi nyingine yoyote; hizo ni standard clauses katika mikataba ya biashara za kimataifa kwenye kulinda investments.

Bila ya hayo mambo mwekezaji anakuwa anachukuwa risk kubwa sana katika usalama wa uwekezaji wake na hawa wenzetu wana experience tosha ya kugeukwa mbeleni ndio maana wanataka hayo mambo yawepo katika mkataba au sheria ya nchi kwanza.

Solution ni moja tu kama tunataka kufanya biashara na dunia, ni kuwajengea uwezo watanzania wa kuweza kujadiliana consideration ya hiyo mikataba (na hayo mambo huwa ni siri hatuoni n’go) vinginevyo tutaendelea kuibiwa tu na kushindwa kesi kwa sababu atujifunzi hayo majadiliano ni tenchical.

Tutalaumu miaka nenda miaka rudi wakati mchawi wetu sisi wenyewe.
Uzalendo unatokana Sana na uongozi, kiongozi, utamaduni, uwazi, uwajibikaji na kuwajibishwa, katiba nzuri.

Wataalmu wote, wanasheria, wachumi hawatafanikiwa wakiwa na Viongozi wabovu.
 
Upo sahihi 100% frameworks ndio nguzo ya msingi na baadhi ya clauses hapo kwenye IGA ni sehemu ya aspects za mikataba ya mbele.

Lakini hakuna kilichopo hapo ambapo hutakikuta katika BIT ya nchi nyingine yoyote; hizo ni standard clauses katika mikataba ya biashara za kimataifa kwenye kulinda investments.

Bila ya hayo mambo mwekezaji anakuwa anachukuwa risk kubwa sana katika usalama wa uwekezaji wake na hawa wenzetu wana experience tosha ya kugeukwa mbeleni ndio maana wanataka hayo mambo yawepo katika mkataba au sheria ya nchi kwanza.

Solution ni moja tu kama tunataka kufanya biashara na dunia, ni kuwajengea uwezo watanzania wa kuweza kujadiliana consideration ya hiyo mikataba (na hayo mambo huwa ni siri hatuoni n’go) vinginevyo tutaendelea kuibiwa tu na kushindwa kesi kwa sababu atujifunzi hayo majadiliano ni tenchical.

Tutalaumu miaka nenda miaka rudi wakati mchawi wetu sisi wenyewe.
Kuna nchi kama Saudi, UAE, Singapore, Hong Kong, Malaysia, South Korea, Oman, Namibia, Botswana hata Magufuli asingekubali mikataba kama hii.

Wanafuata katiba zao, Sheria zao zinafuatwa na wananchi ni wazalendo. Sio kama Wana akili kuliko Watanzania ni systems, structures zinawafanya wawe hivyo.
 
So as to fulfil Malicious Agendas, and nothing else !!
 
Hawa wenzetu wakishika nchi wanakuwa bize kukwapua kuliko kuangalia wengine
 
Aisee, hivi inakuwaje muwekezaji mmoja tuu anafanya mpaka tubadili sheria za nchi ambazo zilitungwa kwa umakini mkubwa? Hii sheria ya maliasili ni mpya kabisa ya mwaka 2017 tuu hapo, ni kwa nini tubadili sheria inayolinda maliasili kwa ajili muwekezaji mmoja tuu?

Ina maana akija muwekezaji mwingine ambaye sheria itakuwa inambana kwenye masharti anayoyataka pia tutairudisha tena bungeni kuvichomoa hivyo vipengele?

Huyu muwekezaji ana nini hasa cha zaidi mpaka anafanya sheria za nchi zinanyumbulishwa ili tu yeye a-fit in?

Kwa nini yeye kama muwekezaji asi-blend in na sheria za nchi yetu?

Kimsingi yeye ndiyo anapaswa ajinyumbue ili kuendana na sheria halali za nchi zilizowekwa.

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

Kamati ya Bunge ya Katiba na Masuala ya Kisheria imeahirisha kusikiliza maoni ya wadau kuhusu mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Nchi Kuhusiana na Umiliki wa Maliasili ya mwaka 2017 na Sheria ya Mapitio na Majadiliano Kuhusu Masharti Hasi Katika Maliasili ya nchi ya mwaka 2017.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Joseph Mhagama, ameiambia The Chanzo Alhamisi hii kwamba wameomba ufafanuzi zaidi kutoka kwa Serikali kuhusu mabadiliko hayo ambayo yameibua mjadala mkubwa miongoni mwa wafuatiliaji wa mambo nchini.

Sheria hizo ni miongoni mwa sheria zilizojumuishwa katika Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Na. 2 wa Mwaka 2023, uliokusudia kurekebisha, pamoja na sheria nyingine, sheria hizo mbili ili zisitumike katika uendeshaji wa miradi ya uendeshaji, uendelezaji na bandari.

Huku wadau wengi wakihusisha sheria hii na mkataba unaotegemea kuipa kampuni ya DP World ya Dubai, kazi ya kuendesha, kuboresha na kuendeleza bandari Tanzania.

Muswada huo uliosomwa bungeni kwa mara ya kwanza Juni 28, 2023, na Kamati ya Bunge ya Katiba na Masuala ya Kisheria ilialika maoni ya wadau kuhusu marekebisho yaliyotazamiwa kabla ya muswada huo kurejeshwa bungeni baadaye Agosti. Kamati ilisikiliza maoni ya wadau hao mnamo Agosti 16, 2023.

Sehemu ya IV na V ya muswada wa marekebisho zinapendekeza marekebisho ya sheria tajwa ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa sheria hizo hauathiri uwekezaji utakaokuja kufanywa katika uendelezaji na uendeshaji wa bandari.

Serikali inasema marekebisho hayo yanalenga kuwezesha bandari za Tanzania “kufanya kazi katika viwango vya kimataifa na kuvutia meli nyingi za mizigo mikubwa kuhudumiwa na bandari” za Tanzania.

Sheria hizi mbili ambazo zilipitishwa mwaka 2017 ziliwekwa kwa madhumuni ya kuhakikisha Tanzania inanufaika na maliasili zake, lakini pia inatoa nafasi ya kurekebisha mikataba mibovu.

Dk Mhagama ameiambia The Chanzo kwamba kamati yake ilipokea maoni kuhusu sehemu nne za sheria ambazo Serikali inataka kuzifanyia marekebisho, na kuacha sehemu mbili zilizoundwa ili kuipa Tanzania mamlaka juu ya maliasili zake.

“Muswada huo una sehemu sita, kamati iliona ifanyie kazi vipengele vinne tu, na kuviacha vingine viwili ili kutengeneza njia ya mashauriano na Serikali kwa lengo la kupata ufafanuzi wa maudhui ya sheria hizo mbili,” Mhagama, ambaye ni mbunge wa Madaba (Chama cha Mapinduzi – CCM), anasema.

Anasema kuwa wadau wataalikwa kuwasilisha maoni yao mara baada ya kupata ufafanuzi na Serikali pindi ikiamua kuendelea na marekebisho yaliyopendekezwa na kuongeza kuwa kamati hiyo inatakiwa “kujiridhisha” na yaliyomo kwenye muswada huo kabla ya kuamua kuendelea nao.

Dk Mhagama ameiambia The Chanzo kwamba kamati yake iliomba maelezo kutoka kwa Serikali kuhusu marekebisho ya sheria hizo mbili, huku akishindwa kueleza ni lini hasa anatarajia mamlaka kujibu hoja zilizoibuliwa.

“Serikali itakuwa hapa milele; wakati wowote watakapoona inafaa kujibu hoja tulizoibua watakuja kwenye kamati na mapendekezo yao,” Dk Mhagama anafafanua. “Si lazima iwe leo, kesho au mwakani.”

Mapendekezo ya marekebisho ya sheria hizo yanakuja wakati mjadala mkubwa wa kitaifa ukiendelea kuhusu makubaliano baina ya Serikali ya Tanzania na Dubai ili kuiruhusu DP World kuiendesha bandari ya Dar es Salaam.

Mnamo Juni 10, 2023, wabunge waliridhia kwa kauli moja mkataba huo tata ambao unaendelea kuleta mgawanyiko wa taifa, huku mgawanyiko wa maoni kati ya wafuasi wake na wakosoaji ukionekana wazi kila siku.

Serikali na chama tawala wanauelezea mkataba huo kuwa “mkataba bora zaidi kuwahi kutokea,” huku wanaharakati na vyama vya upinzani wakiuelezea kuwa “mkataba mbaya zaidi.”

Miongoni mwa waliokataa mpango huo ni Maaskofu wa Kanisa Katoliki, ambao kwenye taarifa yao ya pamoja ya Agosti 18, 2023, waliitaka Serikali kusikiliza matakwa ya wananachi ya kufuta mpango huo, wakisema, “Sauti ya watu ni sauti ya Mungu.”

“Ni lazima miradi kama hii [ya maendeleo ya bandari] iendeshwe na kusimamiwa na Watanzania wenyewe, huku wakikaribisha ushirikiano ambao wao wenyewe wataudhibiti,” Maaskofu hao 37 walisema katika taarifa yao hiyo ya pamoja.

“Hili ndilo ambalo wananchi wamekuwa wakililia ili tuweze kuboresha uwezo wetu wa kusimamia uwekezaji muhimu,” waliendelea kueleza. “Kwa sababu tayari tumeshachambua mapungufu ya jinsi tunavyoendesha bandari zetu, tunaweza kuyafanyia kazi huku njia za uchumi zikisalia mikononi mwetu.”

Source: The Chanzo
Wabunge akili zimeanza kuwarudia.
Kupiga plaste ukuta uliobomoka kazi kwer kwer!
 
Back
Top Bottom