Sakata la Fei Toto na Yanga SC, hatimaye ukweli wajulikana

Sakata la Fei Toto na Yanga SC, hatimaye ukweli wajulikana

denooJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
18,509
Reaction score
68,228
Salaam..!!

Kama tujuavyo lile sakata la Fei na Yanga kuhusu suala la mkataba namna lilivyoendeshwa kwa magumashi na TFF kwa kushirikiana na wanasiasa, na jinsi maamuzi ya kesi ile yalivyokuwa ya ajabu, baada ya TFF kudai Fei ni mchezaji wa Yanga Sc bila kusema amekiuka vipengele gani kwenye mkataba wake.

Sasa taarifa zilizopo rasmi ni kwamba, Fei Toto amesaini mkataba mpya na utopolo wenye thamani ya milioni 350 za kitanzaniaa ili kurejea jangwani, mpaka kufikia hapa, inaonesha wazi, Fei ndie alikuwa na haki kwenye lile sakata.

Kwasababu, huwezi kwa akili ya kawaida ukamuongezea mkataba mpya muajiriwa wako aliyevunja mkataba wa awali kinyume cha sheria, kitendo cha uto kumuongezea Fei mkataba kinaonesha mchezaji ndie alikuwa na haki, na bado ni tegemeo kwao, ndio maana Nabi kila siku alikuwa akihangaika kupiga simu za kubembeleza kwa mchezaji.

Mwisho nitoe wito kwa wanasheria wetu wa makaratasi hapa JF, haya mambo ya kisheria siku zote sio ya kukariri kama hesabu za darasani, eti kilichopo kwenye mkataba wako, lazima kiwepo kwenye mkataba wa mwenzio, huko ni kujidanganya, kisheria kila mkataba unaamuliwa na vipengele vilivyopo kwenye mkataba husika, sio nje ya hapo.

Screenshot_20230216-054155_Gallery.jpg
 
Na wale wengine waliokuwa wakijidanganya Fei ameachwa peke yake hana support tena, habari hizo ziwafikie, sasa ni wazi, utopolo kama kawaida yenu hamjui kuingia mikataba itakayowalinda, matokeo yake kila siku nyie ni vurugu na wachezaji wenu, au wadhamini.

Viongozi wenu wamelazimika kumfuata Zanzibar na kumbembeleza, hatimaye wakakubali kufikia makubaliano na mchezaji kwa kumpa alichotaka, mshahara wa tsh. 15 milioni kwa mwezi, kwa miaka miwili, sio kelele za mitandaoni

Muhimu kwenu muende darasani kujifunza haya mambo, ubishi wa mitandaoni ni kujidanganya tu, na kuwaponza viongozi wenu wasio na kitu kichwani, kwani hata kama mkifichiwa aibu na TFF, lakini bado ukweli lazima iko siku utajulikana tu, kama ilivyotokea kwa Fei.
 
Gongo wazi kanda mbili

Kazi yao kuvunja vipengele katika mikataba, ngoja ipo siku tutawashitaki MIGA

Hawataki kuvaa nembo sahihi ya mdhamini
Walianza kwa vodacom na sasa nbc, pamoja na mikataba sheria na kanuni za TFF kuwa wazi

Nembo ya GSM ni red lakini wamebadil rangi

Mikataba ya wachezaji na makocha ni kisanga kuna muda mpaka CAS na Fifa wana ingilia kati
 
We waache wafuate yasiyowahusu hawa akina mama. Siku ya Raja watatueleza vzur
Makasiriko hatupendi, mkajifunze kuheshimu mikataba ya kimbumbumbu mnayoingia na wachezaji wenu.
 
Back
Top Bottom