Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Jamani Wanabodi,
haya maswala ya Umeme nchini yanashangaza sana.
Nimepitia home page ya hii site nimekuta kitu hiki! Sioni kabisa jina la JK wala bunge letu!

MRADI MKUBWA WA UMEME WAYEYUKA! Thursday, 21 December 2006
Mchoro wa bwawa la Mto Rufiji

WAKATI Rais Jakaya Kikwete akitimiza mwaka mmoja akiwa madarakani huku nchi ikilemewa na tatizo kubwa la ukosefu wa umeme, imebainika kwamba, maamuzi ya kitatanishi ya mamlaka moja ya umma yamelikosesha taifa mradi ambao ungezalisha nishati hiyo kwa kiwango cha mara tatu ya kile kinachopatikana hapa nchini.

Taarifa ambazo Tanzania Daima inazo zinaonyesha kwamba uamuzi wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) kuvunja mkataba na taasisi moja ya Kitanzania iliyokuwa ikifadhiliwa na wawekezaji wa nchini umeliweka taifa katika hatari ya kuchelewa kuanza kupata megawati 2,100 za umeme ambazo zingeanza kuzalishwa wakati wowote.

Hivi sasa Gridi ya Taifa ina uwezo wa kuzalisha megawati zisizodi 600 na ambazo kupungua kwake kumekuwa kukiisababishia nchi mgawo wa umeme.

Mamlaka hiyo inalaumiwa kuvuruga mpango wa mradi mkubwa wa umeme, uliokuwa ukifanywa na Kampuni ya wazawa ya CP Limited & Associates, kupitia mradi uliojulikana kama Stiegler's Gorge Hydropower Plant.

Taarifa zinaonyesha kwamba wakati mamlaka hiyo ya umma ikitangaza kuuvunja mkataba, CP ilikuwa imeshapata kiasi cha dola za Marekani bilioni 10, kwa ajili ya kuendesha mradi huo ambao ungekamilika baada ya miaka sita kuanzia sasa na ungemaliza kabisa tatizo la umeme nchini.

Habari za ndani ambazo Tanzania Daima imezipata, zinaeleza kuwa, RUBADA, iliingia mkataba wa kuendesha mradi huo na Trade CP Limited & Associates Machi 30 mwaka huu.

Chini ya mkataba huo ambao Tanzania Daima imeiona nakala yake, Trade CP Limited & Associates ilitakiwa kusaka fedha kwa ajili ya mradi huo muhimu nchini.

Mkataba huo, ulisainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa RUBADA, Barnabas Kabuzya na Mkurugenzi Mtendaji wa Trade CP, George Fuko.

Baada ya kusainiwa mkataba huo, Trade C.P Limited ilianza kusaka fedha na Juni 5, 2006 mwaka huu iliandika barua kwa RUBADA kujulisha maendeleo ya utafutaji wa fedha hizo kwa ajili ya mradi wa Stieglers's Gorge ambao ndani yake una miradi mingine mikubwa 23 ambayo inakadiriwa ingetoa ajira kwa watu 4,500.

Barua hiyo iliwajulisha RUBADA kuwa, hadi wakati huo, tayari Trade CP ilishafanya mawasiliano na wadau mbalimbali wa kutoka Norway na China.

Wakati Trade CP ikihaha kupata fedha za kuendesha mradi huo mkubwa, RUBADA iliiandikia barua kampuni hiyo Oktoba 12, ikielezea nia yake ya kutaka kuvunja mkataba kwa madai kuwa kampuni hiyo imeshindwa kutafuta fedha za kuendesha mradi huo kwa zaidi ya miezi mitano.

Hata hivyo Trade CP Septemba mwaka huu, ilifanikiwa kupata dola za Marekani 10,000,000, sawa na sh bilioni 10 kutoka Saudi Arabia ambazo zingetumika kwa ajili ya mradi huo.

Vyanzo vya habari vimeieleza Tanzania Daima kwamba, hata baada ya kupata fedha hizo, Trade CP Company, iliijulisha serikali juu ya ujio wa fedha hizo kwa vile ni nyingi.

Katika hali ya kushangaza, hata baada ya kufanikiwa kupata fedha hizo, RUBADA imeamua kuvunja mkataba na kampuni ya Trade CP kwa madai kuwa kampuni hiyo imeingia makubaliano ya kupata fedha Saudi Arabia kupitia Kampuni ya M/s Al Muweisaat Establishment bila kutoa taarifa kwa RUBADA.

"Kutokana na sababu hiyo, tumeamua kuvunja mkataba tuliosaini na kampuni yako Machi mwaka huu," ilisema barua hiyo ya RUBADA ya Desemba 14 mwaka huu.

Hata hivyo habari zaidi ambazo Tanzania Daima imezipata, zinasema RUBADA imeamua kuingia mkataba wa mradi huo wa umeme na kampuni nyingine ya kutoka Afrika Kusini.

Tayari RUBADA na Kampuni hiyo ya IDF, yenye namba za usajili 99/09749/07 walitiliana saini mkataba huo Desemba 8 mwaka huu, na kuwaacha Trade CP wakishangaa wasijue la kufanya na fedha walizokwishapata.

Kutokana na hali hiyo, Trade CP inakusudia kulifikisha suala hilo mahakamani kupinga kuvunjiwa mkataba huo na pia kudai fidia kutokana na gharama, usumbufu na hata kuvunjiwa heshima kwa kampuni hiyo.

Mradi huo mbali ya kuzalisha umeme wa uhakika kwa nchi nzima, pia ungezalisha umeme wa bei nafuu kuliko gharama za sasa na pia ungeweza kutumika kuanzisha uchimbaji wa chuma Liganga na kiasi kingine cha umeme kingeuzwa katika nchi jirani.

Alipoulizwa na Tanzania Daima kuhusu suala hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa RUBADA, Barnabas Kabuzya, kwanza alikiri mamlaka yake kuingia mkataba na Trade CP, na akakiri kuingia mkataba na kampuni nyingine ya Afrika Kusini aliyoitaja kwa jina la UDF.

Hata hivyo alisema wameamua kuvunja mkataba na kampuni hiyo ya Trade CP baada ya kubaini kuwa haina uwezo wa kuendesha mradi huo, kwani hata ofisi hawana.

"Huo mradi kwa sasa unahitaji dola za Marekani bilioni mbili, Trade CP haina uwezo na ndiyo maana tumeamua kuingia mkataba na Kampuni ya IDF.

Halafu, kwa nini amekwenda mahakamani au kwenye vyombo vya habari? Kwani amesambaza taarifa zake kwa mawaziri, Rais, badala ya kuwasiliana na RUBADA, lakini kama kweli amepata fedha, bado ana nafasi, kwani nia ya serikali ni kuona mradi huo unaanza ili kuondoa tatizo la umeme," alisema.

Hata hivyo alisema hawezi kuzungumzia kwa undani suala hilo, kwa madai kuwa kwa sasa liko mahakamani.
 
Dua unajua nitachemsha usiku ni mwingi lakini huna mipango ya kuslow down

duh!


unafanya night shift?

naamini mchango wako ni mkubwa kwa jins unavyochangia threads mbali mbali humu
 
Wapi mzee sikukuu hadi tarehe 2/01/2007, kwa hiyo ni kula kuku tu.
 
Maadam Mkataba hatujauona, ni vigumu kusema kwa uhakika kuwa vipengele vimekiukwa.... which reduce our complains to mere speculations.

Richmond hawajalipwa hata senti so far, so says JK. Kwa hiyo pesa bado hazijaliwa... inabidi wajitahidi kutimiza wajibu ndio waweze 'kuzila'.

'Tukiuvunja huu mkataba sasa hivi, serikali itaingia hasara kwa kulazimika kuwalipa Richmond fidia.' Kwa hiyo option iliyopo ni kuweka pressure ili Richmond, 'which happened to be a small company', waweze kudeliver. Na wakishindwa within 'muda tuliokubaliana katika mkataba', basi wao ndio wailipe serikali fidia.
 
Kulikoni

Nakubaliana na wewe lakini huu mkataba ulikuwa wa kunusuru hali mabaya ya umeme tangu June or July na hawana aibu kwani hata wabuunge wamekatazwa kuuliza suali lolote kuhusu hili – huoni hapa kuna mtu anacheza na maisha ya watanzania?

Ni watu wangapi wamepoteza maisha kwa sababu ya kukosekana umeme?

Kwa nini rais aliahidi umeme huu ungekuwa pumped kwenye grid la taifa October?

Kama sio kweli kwa nini serikali haitoa jibu sahihi kila mara wanapokabiliwa na maswali?

Karamagi alisema hii ni contract ambayo third party hana ulazima wa kuuona –This is absolutely wrong? Wananchi through Parliament ni one of stake holders kwa nini ukweli hautolewi?

Richmonduli anaogopa nini kuwanyamazisha wabunge? There is something very wrong here and we want to know.

Ni lazima vipengele vya mkataba huu vimekiukwa na ni lazima walioshiriki wawajibishwe kwa hasara ambayo haikuwa lazima.
 
Kulikoni,
Rais hakuwa forthright. Downpayment walishapewa Richmond.
 
Dua,
Maneno mazito hayo, yaani, mpaka hapo mkataba tutakapouona, these are very valid speculations!

Kama nlimuelewa vizuri JK, ameadmit indirectly kuwa kulifanyika kosa kuwapatia Richmond hili dili, lakini kuuvunja mkataba itakuwa ni kosa jingine litakaloigharimu serikali bila service kupatikana.

Yes, swali linabaki kuwa waliokosea wamechukuliwa hatua gani. Inawezekana wamepewa 'onyo kali' kuwa wasirudie tena mchezo huu!
 
Kulikoni,
Rais hakuwa forthright. Downpayment walishapewa Richmond.

Duh! Sijakuwa aware na hilo. I took his word for granted.

Lakini una hakika mzee? How much advance was paid?
When was it paid? Why then was Richmond still busy shopping for a credit line?

Ntakuwa disappointed kiasi ikiwa JK katudanganya.. maana mimi ni katika wale ambao bado hawajaloose hope nae.
 
RDC ni brokers, ni hatari sana kuingia mikataba na brokers kwenye dili za serikali, kwa sababu behind these brokers ndio kuna vigogo, trust me wala rushwa, thats how they eat wananchi's money.

believe me endapo serikali inge-deal na manufacturer's moja kwa moja, sasa hivi kusingekuwepo na hizi kelele.............
 
Wajameni,

Fungeni topic, muda huu unaposoma huu ujumbe Richmond hai exist!!! wamenunuliwa na kampuni nyingine stay tuned nakuja na facts....
Na hiyo kampuni mpya tayari wameshaleta jenereta nyingine ipo bandarini dar es salaam.

Ahahahaaa wabongo mtaliwa saaaaaana kwenye utawala huu.

FD
 
duuuhh, jamaa wanazidi kupoteza ushahidi wa mahusiano na vigogo
 
Ogah,

Hii nchi ni kichwa cha mwenda wazimu, hapo kilichofanyika mpaka jenereta ipo bandarini ndipo wananunuliwa ni kiini macho ina maana hili suala lilikuwepo toka zamani, watoto wa vigogo wanajitoa ili msi trace na kuwapata!

I love staili ya ULAJI BONGO, wanakula kijinga sana!

FD
 
Nashukuru kwa majibu so far...

Nikiamini maneno ya FD (kuwa RDC is no more), na kabla uzi huu haujafungwa...

Baada ya kupitia majibu hayo niulize tena:

1. Kwa nini serikali haikutaka kununua toka kwa watengenezaji moja kwa moja?

2. Je, huo ndiyo utaratibu, labda, unaopendekezwa na kina World Bank etc katika manunuzi? Ni wakati gani serikali itumie mawakala (third party) na wakati gani inunue moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji?

3. Kuna tofauti gani katika ununuzi kati ya RDC na kina Aggreko? Tuseme, hao kina Aggreko wao ni watengenezaji wa hiyo mitambo au nao wamenunua kama RDC alivyonunua?

4. JK alivyodai kuwa "Msabaha, ukiwalipa hawa wakashindwa kuleta utachukua kamba ujinyonge", hakuwa serious?
 
Mwanagenzi,

Sina hata haja ya kukujibu ndugu yangu kwasababu unayofikiria ndiyo majibu. Wameona watafikiwa kwahiyo wameamua kuuza kampuni ambayo haikuwa ina exist ya RDC.... nadhani utakuwa umeelewa ndugu yangu.

FD
 
Richmonduli imekuwa replaced na kampuni inayoitwa Dowans(T) LTD.Hii kampuni ndio ita-run operations za RDC.Hii kampuni ni ya kutoka UAE,na ina wamiliki kutoka Singapore na UAE.Pia inasemekana kuwa Rostam Aziz naye ana-share kwenye hii kampuni.
 
Richmonduli imekuwa replaced na kampuni inayoitwa Dowans(T) LTD.Hii kampuni ndio ita-run operations za RDC.Hii kampuni ni ya kutoka UAE,na ina wamiliki kutoka Singapore na UAE.Pia inasemekana kuwa Rostam Aziz naye ana-share kwenye hii kampuni.


Mimi sijali nani anaimili au tenda ilipewa kampuni gani...NACHOTAKA MIMI UMEME UWEPO KWA BEI INAYOWEZEKANA kwa uchumi wa walio wengi. Sasa mbona wanashindwa kitu kidogo hivyo...imagine kama wangetakiwa kujenga mtambo wa kuzalisha umeme wa nuclia ingechukua karne ngapi. Yaani kununua genereta off the shelf na kulifikisha bongo wao wakiwa kama serikali wanashindwa...hivi jamani kuna haja ya kuwa na serikali.

Mhhhh sasa naona kuna umuhimu wa kuomba passport ya ngambo maana nyumbani haya mambo yanakatisha tamaa kabisa....taabu kweli kweli.
 
Mwanagenzi,

1. KICKBACKS
2.Kwa procurement procedures za WORLD BANK or ADB or EU , RDC wasinge kuwa pre-qualified trust me, angalia procurement documents zao mtandaoni
3. ni rahisi kujua ukitafiti history zao
4.Acrobatics(gymnastics), Mazingaombwe ndio Usanii wenyewe
 
Toka mwanzo nililia suala la mazingaombwe na watu wanadhania tunapita kelele ya bure. Jambo rahisi ni kwa JK kuamuru mkataba huu kuwekwa hadharani ili tujue unasema nini na hivyo kukatisha mzizi wa "kizabizabina". Je mkiambiwa kuwa wakati watu wanalalamika wakubwa walikaa chini tena na kuufanyia madaraka mkataba huu ili kukidhi mahitaji ya wakati huu na kuondoa utata mtakataa?

Kwanini tunauliza maswali?
Tunauliza maswali kwa sababu majibu hayatoshelezi! Watanzania tushalizwa mara nyingi kuhusu suala hili la Mikataba. Na hii ilikuwa ni mojawapo ya sababu za wananchi kumpigia kura Kikwete kwa sababu aliahidi kushughulikia mikataba hii. Kitu ambacho tunagundua sasa ni kuwa HAKUAHIDI kuwa serikali chini yake haitaingia kwenye mikataba mibovu!!!! Je huu ni mkataba mbovu?

Absolutely! Inakuwaje kampuni ya uchapishaji ipewe tenda ya kuzalisha umeme wa nchi? Inakuwaje kampuni ambayo haikuwepo (literally) iwepo kwa kusudio moja tu nalo ni kuuza umeme kwa serikali? Hivi kwanini hawakujiuliza kuwa kwanini mabenki ya Marekani yalikataa kuwapa a line of credit? Kuna sababu, na sababu ni kuwa RDC hawana Credit History ya kuaminika, au ratings za credit history yao ni mbaya!!

Je kama ni kweli kampuni hiyo imeuzwa kwa kampuni nyingine, Mkataba huo unasemaje?
 
Na imeuzwa kwa bei gani? Kilichouzwa ni nini? Jina la Richmond au nini? Kuna maswali mengi tu yanayohitaji kujibiwa.
 
Back
Top Bottom