Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Kama ilivyodokezwa hapo juu, uwezo wa Kampuni ya Richmond LLC, ulitegemea ushirikiano wake na kampuni ya Pratt & Whitney. Mara baada ya makubaliano kati ya Pratt & Whitney na Richmond LLC, kuvunjika, Richmond ilikosa uwezo wa kutekeleza yale yaliyo kwenye mkataba. Hali hii ililazimisha Richmond LLC, kuuza shughuli zake kwa Dowans Holding SA.

Aidha hakuna ushahidi uliopatikana kuonyesha uhusiano wa aina yoyote wa umiliki kati ya kampuni hizi mbili.
Imethibitika kiushahidi kwamba wamiliki wa hisa katika ya Dowans Holding SA ni,

1. Suleiman Mohamed Yahya Al Adawi.
2. Puthan N.C Menon.
3. Abasi Ibrahim Al Yousef.

Hawa wote ni raia wa nchi za Falme Za Kiarabu (U.A.E.), na aidha kwa upande wa Dowans (T) Ltd, menejiment yake inaongozwa na Guy Picard, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji.

Je Serikali Imepata Hasara Baaada ya Richmond Kushindwa kuzalisha Umeme?

........Coming Up Next........
 
Hizi kamati zilizoundwa kwa nini hazikutafuta somethings like these:
1. richmond inc - proof of funds kutoka kwenye bankers wao - very simple
2. Letter of readness from p&w company to supply such equipments backed by an agreement or contract

Anything is possible in this country, am not surprised, na hao kamati members tunaweza kuwaita ndiyo among the thinktanks wetu
 
Ni kweli kwamba Richmond LLC, ilishindwa kuzalisha umeme katika kipindi kilichokubaliwa kimkataba kati yake na TANESCO. Hivyo basi kwa mujibu wa mkataba, kampuni ya Richmond LLC, ilipaswa kuilipa TANESCO fidia ya ucheleweshaji huo. Faini hiyo ni kiasi cha Dola $ 10,000 kwa siku kuanzia tarehe 20/02/2007.

Lakini kwa kuwa shughuli za Richmond LLC, zilikuwa zimeuzwa kwa kampuni ya Dowans Holding SA, adhabu hi ilitakiwa kuruthiwa na hao Dowans Holdign SA.

.....(Hapa hiii taaarifa ya uchunguzi haisemi wazi iwapo adhabu hiyo ilitekelezwa au vipi?....)

Kwa hiyo kwa maoni yangu utaamua mwenyewe ndugu mwananchi!

.........Coimng Up Next.........

Madai ya kuwepo kwa uzembe katika usimamiaji na utekelezaji wa mchakato mzima!
 
Mzee Es,
hivyo serikali haikuilipa kampuni hii kiasi chochote cha fedha hadi ilipouza kazi zake kwa kampuni ya Dowans Holding SA, ndiyo iliyostahili kulipwa malipo hayo ya usafirishaji wa mtambo wa kwanza, $ 4,865,000.00 , uliongia nchini tarehe 21/10/2006 kwa ndege na si Richmond LLC,

Wait a minute, mzee Es navyokumbuka mauzo ya Richomond kwa Dorawans tumejulishwa mwaka huu na hata waziri mkuu pamoja na Karamage walipotembelea hapa walitujulisha kuwa Richmond waliomba muda uongezwe hadi February 07, imekuwaje leo tunambiwa ni Dorwins ndio walioingiza hata mtambo wa kwanza hali nakumbuka vizuri kuwa mtambo wa kwanza ulipofika yule wa mhindi wa Richmond alihojiwa na waandishi na akaahidi kuwa mitambo mingine ilikuwa njiani. Hata nakumbuka Michuzi aliweza toa picha za wafanyakazi wa Richmond wakishughulika ufungaji wa mtambo. Na mwisho nakumbuka hata malalamishi ya Richmond wenyewe baada yakufunga generator ya kwanza kudai kuwa gas yetu ilikuwa chafu hivyo kusababisha mambo yao kutofanya kazi vizuri - Malalamishi hayo yakiongozwa na mhindi huyo huyo wa Richmond baada ya majaribio ya mtambo wao kushindwa!

Mzee Es, naanza kusikia harufu mbaya toka kwa hawa jamaa wachunguzi wetu...wanaanza ku twist ushidi wao wenyewe!..kumbukumbu tunazo hatujasahau hivyo!
 
Mzee Bob

LETE USHAHIDI MAANA KWENYE HII MADATUNAMKOMA NYANI HASWA HAKUNA BLAH! BLAH! NINAKUAMINIA KUWA UNAO MAANA KULE NYUMA ULIWAHI KUUTOA KULE NYUMA AU KAMA UNAZO HOTUBA ZA HAWA JAMAA MAANA NINAYOYATOA SASA HIVI NI MWANZO TU BADO NINALETA MENGINE ON THIS ISHU!

WANANCHI TUNAFIKA MAHALI TUMECHOKA NA LIWALO LIWE ENOUGH!
 
Mzee Es,
Ziara ya Lowassa hapa mjini ilikuwa November 29, 2006 mwezi mzima baada ya uuzaji unaodaiwa leo1 na mkutano kwa Watanzania ulifanyika siku ya pili hotel Royal York, watanzania kibao walihudhulia mkutano huo bahati mbaya sina record ya maelezo ya viongozi hasa Karamage na Maghembe. Nitatafuta zaidi data na picha toka kwa Michuzi!
Ushahidi unaofunga kazi kabisa ni huu hapa toka gazeti la mwananchi ikiwa imenukuliwa na gazeti letu...(wakati huo kabla kijana wetu Mushi haja pewa kibano). Scroll hadi chini kwenye kichwa cha habari:- Waziri wa Nishati aitetea Richmond

http://jambotanzania.net/v2/content/view/902/2/
 
Naomba kurukia Basi kwa mbele,maana sijui lilipotoka Mzee ES.
Nani walikuwa mawakiri wakati Richmond inaingia mkataba na serikali????
Muhimu sana!
 
Kama ilivyokwishaelezwa hapo juu, ushaidi umethibitisha kuwa mchakato mzima ulifanywa kwa uwazi na umakini ukijumuisha wataalam kutoka TANESCO. Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Wataalamu kutoka TANESCO na Wizara ya Nishati walikuwa na jukumu la kuangalia masuala ya kiufundi, Hazina walikuwa wakiangalai masuala ya kifedha. Aidha ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilikuwa na jukumu la kupitia mkataba na kuona endapo kuna mapungufu kwa masilahi ya taifa.



.......itaendelea.........!
 
Tulipokuwa watoto wadogo wakubwa zetu walikuwa wakitumia mbinu mbalimbali kutuhadaa. Kitu ambacho hatukujua ni kuwa tulikuwa tunadhulumiwa kitu fulani kwa kutumia ulaghai wa maneno matamu, na vichekesho visivyo na kichwa wala miguu. Mojawapo ya janja ya wakubwa hao ni ile ya kupukuchua mahindi.

Katika ulaghai huu kaka mkubwa au dada mkubwa alikuwa anachukua hindi lililochomwa ambalo mdogo wake ameshikilia na anamuahidi "kumtengenezea njia". Basi, katika kufanya hivyo atapuchukua mistari michache na kutengeneza njia ya kwenda "Dodoma" na hata ya kwenda "Iringa".

Zile punje za mahindi walizopukuchua hata hivyo walizibugia mdomoni kwa mbwembwe zote. Sisi wadogo zao tulifurahia kukabidhiwa mahindi yaliyotengenezwa njia kadhaa!

Ndugu zangu, kile ambacho Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa nchini Bw. Edward Hosea alikifanya wiki iliyopita kina fanana kabisa na hadaa ya kupukuchua mahindi. Na alichofanya kamanda huyo kinazidi mazingaombwe ya Profesa Ndumba Nangae! Niwakumbushe kidogo kuhusu mazingaombwe. Katika mazingaombwe yoyote mwanamazingaombwe mahiri ni yule anayeweza kutumia "vipoteza lengo" ili kuficha vitu kwenye vidole au viganja vyake na hatimaye kufanya viini macho.

Bw. Hosea na wenzake wametumia suala la Waheshimiwa Zitto na Amina kutuletea taarifa muhimu na nyeti wakijua kwa hakika watanzania hawana muda wa kufuatilia na kuulizia kwa makini kwani wamenogewa na utamu wa kachumbari ya masuala ya mapenzi Bungeni!

Hata hivyo, kwa mzee wenu hapa kijijini hakuna jambo ambalo linahusu Tanzania litakaloachwa kupita bila kuangaliwa kwa karibu kama kupekua kwa kurunzi chini ya uvungu. Tulilizungumzia suala la Richmond tangu mwanzo wake na tukaweka wazi kuwa hicho kikampuni hakikuwa na uwezo wala ubavu wa kuleta majenereta na kuzalisha umeme!

Tukazua maswali ambayo maelezo ya Bw. Hosea hayakujaribu hata kidogo kujibu. Ni makusudio yangu kuyazua tena maswali haya ili kila Mtanzania aweze kuelewa ni jinsi gani Bw. Hosea na wenzake wamejaribu kutufunga kamba mbichi mchana kweupe.

Lengo langu ni kuonesha kuwa TAKURU ni chombo ambacho hakina ubavu wa kupambana na rushwa kubwa, na hakina uhuru wa kukabiliana na vigogo (na familia zao) katika vita za kutokomeza uovu huu. Miaka nenda rudi Takuru imekuwa ikikamata na kuwakaanga dagaa, ikiwachemsha kambare, wakati papa na nyangumi wakiendelea kuogelea bila hofu ya kukamatwa na nyavu hizo za TAKURU.

Takuru imebakia kuwa ni kama simba wa kwenye picha ambaye ametoa kucha na anaonekana kuunguruma huku meno yake yaliyochongoka yamekenuliwa! Wote tunajua simba huyo wa karatasi haumi ila anaweza kuwatisha watoto wadogo tu na watu wasio na akili timamu.

Kwa vile TAKURU wamesema kuwa kwenye suala la mkataba wa Richmond hakukuwa na vitendo vyovyote vya rushwa, tunaomba basi Bw. Hosea na wenzake wawajibu Watanzania wenzao maswali haya yafuatayo ambayo yamejengengeka tangu mkataba huu kuingiwa.

Kama ushahidi wa majibu yake anao wauweke hadharani au iundwe tumu huru yenye uwezo wa kuita mashahidi na wale wote waliohusika waweze kuitwa hadharani na kuhojiwa kuhusu kuhusika kwao. Maswali haya yana lengo la kutaka serikali iwe wazi na kutoa hadharani vidhibiti vyote ambavyo vimewafanya wafikie mahali pa kusema katika "mchakato mzima, hakuna rushwa"! Bw. Hosea, ya kweli hayo?

Kwanza, ilikuwaje kampuni ya hiyo ya Richmond Richmond Development (RDC) ipewe tenda hii? Majibu aliyoyatoa Bw. Hosea ni majibu ya kitoto na ya shule ya msingi. Iweje kampuni ya kupiga chapa na kuchapisha vijitabu na vielelezo ipewe tenda ya nishati? Tangu mwanzo wa suala hili kampuni hii imejivika majina ya ajabu ajabu na kutangaza uwezo wake.

Kinachoshangaza ni kuwa hakuna mtu katika serikali yetu aliyethubutu kuangalia kama kampuni hii ya RDC ina rekodi yoyote ya kushughulika na masuala ya nishati ukiondoa maelezo ya kwenye tovuti yao. Je, watendaji wetu walipitia ushahidi gani wa kazi za RDC na kuridhishwa nayo hadi kuamua kuwapa tenda ya mabilioni ya shilingi? Katika kuwapatia tenda hiyo, sheria ya manunuzi ya serikali ilizingatiwa kwa kiasi gani?

Pili, Wakati Balozi Andrew Daraja alipokwenda kutembelea Houston na kukaribishwa na viongozi wa kampuni ya Richmond Printing alioneshwa kitu gani hadi kukubali kuwa kampuni hiyo ina uwezo wa kushughulikia masuala ya nishati? Je aliona orodha gani ya nchi zilizoridhishwa na utendaji kazi wa RDC hadi kuipigia debe serikalini? Kama siyo yeye ni nani basi aliyesema kampuni hiyo ina uwezo wa kutuletea majenereta?

Tatu, kabla ya kampuni ya RDC kupewa tenda ya Nishati, ilipewa tenda nyingine ya kujenga bomba la mafuta toka Mwanza hadi Dar, bomba ambalo mradi wake ulibuniwa na kampuni ya Africommerce. RDC ilipopewa tenda hiyo kiulaini, watu wa Africommerce walilalamika kupokonywa mradi huo lakini viongozi wetu hawakujali hilo wakawapa RDC.

Miezi kumi na nane baadaye RDC walishindwa kufanya lolote na badala yake mradi huo ukapewa kampuni nyingine toka Uarabuni. Ilikuwaje kwa kampuni iliyoshindwa kuanza kutekeleza mkataba wa bomba la mafuta kwa miezi 18 kupewa mradi wa kuleta majenereta ndani ya wiki 14?

Jambo moja ni dhahiri. Mtu yule yule aliyeipigia debe kampuni hii hadi ikapewa mradi wa bomba la mafuta ndiye yule yule aliyeipigia debe na ikapewa mradi wa majenereta. Bw. Hosea yuko tayari kuwaambia na kuwathibitishia Watanzaina wenzake kuwa watu wale wale waliohusika na bomba la mafuta siyo waliohusika na mradi wa majenereta?

Nne, Kutokana na rekodi zilizoko kwenye ofisi ya Tarafa ya Harris (Harris County) kwenye jimbo la Texas, kampuni ya RDC imeorodheshwa kuanzia mwaka 2003 ikiwa ni sehemu ya kampuni mama ya Richmond Printing. Cha kushangaza ni kuwa chini ya mwaka mmoja baadaye kampuni hiyo ikapewa tenda ya bomba la mafuta nililotaja kwenye swali la tatu, na hivyo kina Elisante Muro kunyang'anywa mradi wao.

Je, Bw. Hosea na wakubwa wa Wizara ya Nishati na Madini wanaweza kuwaeleza Watanzania ilikuwaje kampuni changa namna hiyo kupewa mradi mkubwa wa nishati wakati haina historia ya biashara ya sekta husika? Je tukiwaambia kuwa hiyo ndiyo sababu ya mabenki ya Marekani kuikatalia mkopo wa fedha za awali kampuni hiyo kwa vile hawana historia ya mikopo kama kampuni ya nishati kina Hosea watakataa?

Kama Wamarekani wameona kuwa kampuni hiyo haina uwezo wa kustahili mkopo mkubwa wa fedha kiasi hicho ilikuwaje wasomi wetu na maafisa waliotajwa na Bw. Hosea wakakubali kuipa tenda? Ni nani huyo aliyeipigia debe kampuni hiyo na mtu huyo ana maslahi gani?

Tano, wakati Rais Kikwete anazungumza na wananchi mapema mwaka huu alielezea kusita kwake kukubali kampuni hiyo kupewa malipo ya aina yoyote na akawahakikishia wananchi kuwa RDC haikulipwa kwani alikuwa na mashaka nayo.

Je, TAKURU walimhoji Rais Kikwete awaelewe kwanini alisita na ni nani aliyemshawishi hadi akaacha mkataba huo kuendelea? Tukiwaambia kuwa yule aliyeipigia debe kampuni hii kwa Rais Kikwete na yule aliyehakikisha kampuni changa namna hii ilipewa tenda kuwa aidha ni mtu mmoja au wana udugu wa damu, Bw. Hosea anaweza kutuonesha kinyume chake?

Sita, inawezekana ni kweli kuwa hakukuwa na rushwa iliyolipwa moja kwa moja na ikapewa jina "rushwa" kwenye mchakato wa mkataba wa RDC. Hata hivyo hatuna budi kumuuliza Bw. Hosea kama alianza kuangalia mchakato huu kabla ya mkataba kuingiwa na umbali gani wa historia ya nyuma alienda.

Sijui kama Bw. Hosea anafahamu uhusiano wa karibu wa Bw. Msabaha na familia ya kina Gire uliodumu kwa miaka kadhaa sasa (kabla ya mikataba hii). Inapotokea kuwa rafiki wa familia anapewa mikataba miwili inayohusu sekta moja ambayo rafiki yao ndiye Waziri wa wizara hiyo hatuna budi kuhoji na kuchunguza mikataba hiyo.

Je, Bw. Hosea ameweza kumhoji Bw. Msabaha chini ya kiapo na kuhakikishiwa hakupokea yeye (au ndugu zake) kitu chochote ambacho kinakatazwa katika sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004 na sheria nyingine?

Ni kwa kiasi gani urafiki wa Msabaha na kina Mohammed Gire,Naeem Gire, Zahor Gire, Abdul Gire, Imaduddin Gire, Mumtaz Gire, Adam Gire, Sharrifa Gire na ndugu zao walioko Ulaya na waliopo nyumbani ulichangia kwa wao kupewa tenda hizo?

Saba, katika maelezo yake kwa wananchi Bw. Hosea alisema wazi kuwa kutokana na dharura iliyotokea ya nishati Waziri Mkuu aliingilia kati na kuunda kamati ya watu watatu kuharakisha utatuzi wa tatizo la nishati. Swali langu kwa Bw. Hosea, je ni sheria gani inayompa madaraka Waziri Mkuu kusimamisha sheria ya ununuzi wa serikali ya 2004 na kuweza kuingilia utaratibu wa utoaji tenda?

Waziri Mkuu alipoingilia utaratibu uliowekwa wa kutoa tenda alifanya hivyo kwa mamlaka gani? Kusema kuwa ulikuwa ni "wakati wa dharura" ndio mwanzo wa kuleta maamuzi ya kiimla.

Kwa vile mtanzania mwenzetu ni Waziri Mkuu isiwe ni kisingizio cha mti huyo kupinda/kuvunja sheria kwani, ni wakati wa dharura ndipo tunataka kuona viongozi wetu wazisimamie sheria kwa umakini zaidi.

Kama kamati aliyounda Waziri Mkuu haina mamlaka ya kisheria, maamuzi yake basi pia ni batili hata kama yamefanywa kwa nia nzuri! Kwa maneno mengine, mkataba wa RDC uliingiwa kinyume na sheria na hivyo hauna nguvu ya kisheria, isipokuwa pale Bw. Hosea na wenzake watakapotuonesha utaratibu uliotumika kutoa tenda hiyo usiopingana na sheria ya Manunuzi ya Serikali ya mwaka 2004.

Nane, Bw. Mohammed Gire Afisa Mkuu Mtendaji wa RDC amekuwa akitoa michango wakati wa kampeni na bila ya shaka ndugu zake nao hufanya hivyo. Inafahamika kuwa kina Gire waliichangia CCM na kampeni yake ya uchaguzi ya mwaka 2005 (mwaka mmoja baada ya kampuni kuundwa).

Je, Bw. Hosea anaweza kuwaambia Watanzania ni kiasi gani kilipokewa toka kwa kina Gire kusaidia kampeni ya Rais Kikwete, ya Lowassa, na ya Msabaha? Tukimwambia kuwa kina Gire walichangia ya kutosha kampeni hizo wakiwa na matarajio ya kupewa mkataba wa Bomba la mafuta na kupewa mkataba mwingine wa nishati atatukatilia?

Je, michango ya namna hiyo haiwezi kuonekana kama ni rushwa? Kama CCM watapinga kuwa hawakupokea michango toka kina Gire, wako tayari kutoa orodha ya wachangiaji wao wakubwa wa ndani na nje ya nchi? Bw. Hosea anaweza kutaka orodha hiyo akapewa?

Tisa, katika suala hili zima, jina moja limekuwa likihusishwa na kupatikana kwa mkataba huu na kupewa tenda kwa RDC. Jina hilo ni la Waziri Mkuu Mhe. Edward Lowassa (Monduli - CCM). Wakati huo huo kumekuwa na tuhuma kuwa mmojawapo wa watu waliohusika katika kuipigia debe kampuni hii ni kijana mmoja mwenye mahusiano ya damu na Waziri Mkuu.

Ni kweli kuwa kijana huyo hayupo sasa kwenye orodha ya viongozi wa kampuni hiyo (kama alivyodai mmoja wa viongozi).

Swali kwa Bw. Hosea, je wakati wowote katika mchakato wa tenda hii kuna ndugu wa kiongozi aliyekuwa na nafasi ya uongozi na baadaye akajiondoa/kuondolewa kwa sababu ya kuonekana mgongano wa maslahi? Mtu huyo ni nani na nafasi yake ni ipi? Je serikali ilipata nafasi ya kumhoji?

Kumi, tumeambiwa kuwa RDC hawakulipwa na serikali kwa sababu ya kushindwa kutimiza mkataba, hilo linawezekana kuwa ni kweli lakini ni kweli kuwa fedha za serikali hazikufikia mifuko ya kampuni hiyo? Ni nani aliuza mkataba wa RDC kwa Dowans?

Kama Richmond waliuza mkataba huo kwa kipengele walichoweka kwenye mkataba, na serikali ikailipa Dowans dola milioni zaidi ya mia moja, je RDC hawakulipwa na Dowans? Bw. Hosea anaweza kuuhakikishia umma wa Watanzania kuwa hilo la kuuza mkataba halikuwa "janja ya nyani" kwa RDC kulipwa bila ya kufanya kazi!

Naweza kuendelea kuuliza maswali mengi, lakini kwa leo wacha niishie hapa ili niwape muda wa TAKURU kutafuta majibu. Wakisha jibu hayo nitaangalia kama nina maswali mengine ya ziada (na uzee huu maswali yanajileta yenyewe tu). Nafahamu ugumu wa Bw. Hosea na waliohusika kujibu maswali haya kwa undani na kwa ukweli kwani wameshafikia uamuzi wa kusema "hakukuwa na rushwa".

Kilichotokea ndugu zangu ni kile ambacho kilishuhudiwa kwenye fainali ya kombe la dunia mwaka 1986 kule Mexico wakati timu ya Argentina ikiongozwa na mchawi wa soka Diego Armando Maradona ilipoweza kuifunga timu ngumu ya Uingereza kwa lile goli ambalo limebakia likijulikana kama "goli la mkono wa Mungu".

Maradona alifunga goli hilo kwa kunyanyua mkono wake juu ya kichwa chake na mwamuzi alidhania ameona goli la kichwa. Wakati wachezaji wa Uingereza wanalalamika mwamuzi alielekeza mkono katikati ya uwanja. Watanzania tumefungwa goli la Maradona, hakuna pa kulalamika isipokuwa kuendelea kuuliza maswali.

Hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa ili kuionesha RDC kwa ukweli wake na jinsi mkataba huu ulivyokuwa na maswali mengi. Mwamuzi (Bw. Hosea) keshahesabu goli, na kapiga kipenga mkono ukielekezwa kwenye mduara wa uwanja, mpira kati! Tushangilie au tulie?
 
Mkjj, very fundamental questions you have posed there. Let those who seek to take Tanzanians for a ride know that, even thou we may lack the means to bring them to account for their misdeeds, we are aware of their devious ways.

Somehow the truth will set us free someday.
 
Kalamu, suala hili la RDC nimelifuatilia tangu mwanzo hadi kuweza kufikia kule Houston.. nina info ambazo hakuna mtu anazo.. na inasikitisha kuwa kutokana na ukata au sababu mbalimbali ni vigumu vyombo vya habari vya nyumbani kufuatilia habari.
 
Aidha kamati ya mawaziri wa Fedha na Nishati, walishirikishwa juu ya maendeleo yaliyokuwa yakifikiwa na kamati maalum. Pia waziri mkuuu alikuwa akifahamishwa kila hatua ya mchakato huuu. Maendeleo ya mradi baada ya Dowans Holdings SA kuchukua shughuli za Richmond LLC.

Baada ya Dowans kuchukua shughuli za Richmond LLC, hali ya maendeleo ya kazi ni nzuri kwa vile hadi sasa jenereta tatu zinazofanana na ile iliyoletwa na Richmond LLC, 22.8 MW ziliingizwa nchini tarehe 27/12/2006. Ufungaji wa mitambo hii ulianza mapema January, 2007. Aidha mtambo mkubwa wenye uwezo wa kutoa 42MW umeingizwa chini mwezi March, 2007. Ufungaji wa jenereta hii ulianza April, 2007. Uzalishaji wa umeme kwa kutumia jenereta ya kwanza ulianza rasmi tarehe 26/01/2007 na umeme huuu iluiingizwa kwenye gridi ya taifa.

MAPUNGUFU!

Uchunguzi umeweza kubaini kwamba kulikuwa na mapungufu katika usimamizi na utekelezaji wa mchakato. Mapungufu haya ni ya kawaida ambayo hayajengi makosa ya jinai. Mapungufu haya yalitokana na ukweli kwamba mchakato mzima ulikumbwa na msukumo wa hali halisii ya dharura katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo sugu la umeme ambalo taifa lilikuwa likiathirika. Mapungufu hayo ni:-

Kamati malaum iliyoundwa haikupata muda wa kutosha wa kufanyia uchambuzi wa kina kampuni ya Richmond LLC, ili kufafanua uwezo wake kiufundi na kifedha na badala yake ilitegemea uwezo wa kampuni ya Pratt & Whitney, ambayo ina sifa ya umahiri katika eneo hilo duniani, kama kigezo cha kuipatia zabuni Richmond LLC, yaani Richmond LTD (T).

..........Coming Up Next!.......

4.0 HITIMISHO
 
Kalamu, suala hili la RDC nimelifuatilia tangu mwanzo hadi kuweza kufikia kule Houston.. nina info ambazo hakuna mtu anazo.. na inasikitisha kuwa kutokana na ukata au sababu mbalimbali ni vigumu vyombo vya habari vya nyumbani kufuatilia habari.

Nadhani sasa inabidi tuuite kuwa ni sehemu ya 'utamaduni' wa waTanzania. We're so laid back to the point of annoyance! Hakuna jambo linalotushtua, na hata likitushtua, ni wepesi wa kusahau au kutojali matokeo ya jambo.

Vyombo vya habari binafsi vinalinda maslahi; na sidhani kuwa unapozungumzia vyombo vya habari Tanzania unavihusisha pia vinavyomilikiwa na serikali. I am getting to respect 'Thisdays' efforts, but I am not sure for how long they are capable of sustaining their solo effort.

It has more to do with "Scratch my back, and I'll scrach yours"; than 'ukata'.
 
Mzee ES, Mkjj na wengineo, nimeiona na kuisoma hiyo report ya PCB (sikuimaliza kwa kukosa muda mwafaka). Sikuruhusiwa kutengeneza nakala kama nilivyotaka. Kitu kimoja kilichoni-strike ni kuwa apart from the Gires, Mohammed (m-Pakistan) wa Houston na PM mwenyewe, wahusika wengine wa kutoka wizara na taasisi zingine zote hawakutajwa majina hata kidogo. Siyo tu ndani ya report hata kwenye references za report.

Jamaa aliyenionyesha report alisema kuwa hiyo itakuwa imefanywa kwa makusudi kwani aidha wahusika hao hawakuhojiwa na TAKURU au maelezo yao yanaweza kugongana na yale yaliyotolewa na TAKURU.

Kwa hiyo jiulize, ikiwa TAKURU inaona ugumu kutaja kuwa fulani na fulani toka Tanesco, fulani na fulani toka Nishati, ...nk, how credible is the findings and the report itself?

Sitashangaa kama ni jamaa mmoja au wawili tu wa TAKURU walipewa kazi ya kutayarisha report na wakajifungia ndani na magazeti na kutoa report. Tuliokuwa serikalini tunajua haya yanafanyika kila leo.
Ukiambiwa lete report, suala la kwanza unauliza 'ya kurasa ngapi, mzee'. Mengine yote ni mapishi tu.
 
Ama kweli haya yanatokea Tanzania tuuuuu!...

Sasa ikiwa TARUKU wamefikia uamuzi kama huu sisi wananchi tutakuwa na uwezo gani kupinga maamuzi kama haya... kesi ya nyani kushughulikiwa na Ngedele!..kwanza hawa ni Jamii moja, kisha Ngedele siku zote ni chakula maalum (protein) cha Nyani.... sikutegemea tofauti ila kama swala hili lingechunguzwa kisha kuwakilishwa ktk kikao maalum cha bunge.
Haya watuambie kama wamefanya uchunguzi kuhusu hiyo uwezo wa hiyo kampuni ya DOWANS? nakumbuka hadi naondoka umeme ulikuwa ukitatika kila siku... Je, Dar inatumia umeme wa maji ya Mtera ama umeme wa generators za Dowans na inakuwaje bado tatizo la umeme lipo!
 
Mkandara niliisoma hiyo report na kilichonishangaza siyo ilichosema, bali ilichoacha kusema (not what was reported, but what was omitted!". Jibu la suala hili haliko katika maandishi ambayo Mzee ES ametuwekea hapa bali katikati ya mistari ya kile kilichoandikwa. Kwa vile waandishi wetu (baadhi yao) ni vigumu kuunda masuali ya kufuatilia kwa vile hawajui the other side basi neno la serikali linakuwa la mwisho na ndio maana watu walitarajia baada ya serikali kutoa jibu kuhusu wanafunzi Ukraine basi jambo hilo litafikia mwisho... how wrong they were.... hata hili la RDC halitaishia hapa...
 
Kutokana na uchunguzi wa kina na makini uliofanyika, ushaidi umethibitisha yafuatayo:-

(1). Mchakato mzima wa kumtafuta mzabuni ulikuwa wa wazi na shindanishi.

(2). Hakuna ushaidi wowote uliopatikana kuthibitisha vitendo vya rushwa, uzembe wala upokeaji wa kamisheni kwa watendaji wa serikali.

(3). Hakuna ushaidi wowote uliopatikana kuthibitisha Afisa yoyote wa serikali kumiliki hisa au kuwa na madaraka katika kampuni ya Richmond LLC.


(4). Uchunguzi umethibitisha kwamba mapungufu yalikuwepo, hata hivyo mapungufu hayo yalikuwa ni ya kawaida katika utendaji na ambayo hayakuhusisha rushwa au manufaaa ya aina yoyote ile kwa upande wa watendaji na hakuna hasara iliyosababishwa na mapungufu hayo!


Mwisho kabisa TAKURU inatoa shukrani kwa wananchi wote walioshhiriki kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha uchunguzi huuu. TAKURU, inatoa mwito kwa jamiii kuendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha mapambano dhidi ya rushwa.

KWA PAMOJA TUTASHINDA

Edward G. Hosea
Mkurugenzi Mkuu-TAKURU
 
Kwa mtu yoyote makini ambaye ameisoma hiyo ripoti huko nyuma ya TAKURU, kuhusu Richmond, licha ya kutooona mantiki wala sababu ya TAKURU kuja na kazi nyingine ya U-PS, na haina mshiko kabisaaa!

(1). Kwanza kwa nini TAKURU ndiyop ichunguze na kueleza hali halisi ya mambo yalivyokuwa badala ya serikali ambayo kwanza ndiyo iliyoingia mkataba huo?

(2). Kwa nini serikali ilitoa tamko bungeni kupinga wabunge wasiichunguze Richmond na mikataba mingine kwa madai kuwa kufanya hivyo ni kuingilia mgawanyo wa madaraka?

Hapa nani anamdanganya nani? Kwanza TAKURU ni nani? Maana nijuavyo TAKURU ni chombo cha serikali na iko chini ya Ofisi ya Rais, sasa haki itapatikanaje iwapo serikali inachunguzwa na chomnbo kidogo ambacho ni toothless kuliko bunge la wananchi lenye wabunge toka vyama tofauti?


.........itaendelea..........
 
BTW, si Tanzania tu...

Mkurugenzi wa tume ya kudhibiti rushwa Kenya ashutumiwa

2007-06-03
Na EAR Habari

Chama cha Wanasheria nchini Kenya kimemshutumu Mkurugenzi wa tume ya Kudhibiti Rushwa nchini humo, kwa madai ya kushindwa kuchua hatua dhidi ya wanasiasa wanaojihusisha na vitendo vya rushwa.

Mwenyekiti wa Chama hicho Eric Omogeni amesema Mkurugenzi wa tume ya kudhibiti rushwa Bw. Aaron Ringera, ameshindwa wajibu wake kama mwanasheria mlinzi wa umma, dhidi ya watu wanaoiibia jamii.

Omongeni aikuwa alikiijibu madai yaliyotolewa na Bw. Ringera, kuwa hawezi kuyarejesha mabilioni ya shilingi yaliyoiwa katika kashfa ya Goldenberg, na kufichwa ndani na nje ya Kenya, kutokana na vikwazo vya kisheria.

Hivi huyu Ringera ndiye aliyechukua nafasi ya Githongo?
 
Back
Top Bottom