Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

KWA PAMOJA TUTASHINDA

Edward G. Hosea
Mkurugenzi Mkuu-TAKURU


Nadhani message hii imeeleza yote.. Ushirikiano kati ya Nyani na Ngedele -ushindi ni dhahiri.....
 
Mzee ES, Mkjj na wengineo, nimeiona na kuisoma hiyo report ya PCB (sikuimaliza kwa kukosa muda mwafaka). Sikuruhusiwa kutengeneza nakala kama nilivyotaka. Kitu kimoja kilichoni-strike ni kuwa apart from the Gires, Mohammed (m-Pakistan) wa Houston na PM mwenyewe, wahusika wengine wa kutoka wizara na taasisi zingine zote hawakutajwa majina hata kidogo. Siyo tu ndani ya report hata kwenye references za report.

Jamaa aliyenionyesha report alisema kuwa hiyo itakuwa imefanywa kwa makusudi kwani aidha wahusika hao hawakuhojiwa na TAKURU au maelezo yao yanaweza kugongana na yale yaliyotolewa na TAKURU.

Kwa hiyo jiulize, ikiwa TAKURU inaona ugumu kutaja kuwa fulani na fulani toka Tanesco, fulani na fulani toka Nishati, ...nk, how credible is the findings and the report itself?

Sitashangaa kama ni jamaa mmoja au wawili tu wa TAKURU walipewa kazi ya kutayarisha report na wakajifungia ndani na magazeti na kutoa report. Tuliokuwa serikalini tunajua haya yanafanyika kila leo.
Ukiambiwa lete report, suala la kwanza unauliza 'ya kurasa ngapi, mzee'. Mengine yote ni mapishi tu.

Kaaaazi kweli kweli ..... ndiyo maana JK aliomba wataalam toka Norway ili wamsaidie ...
 
Computer ikiingiliwa na "virusi" unatumia ant-virus kujaribu kuviondoa; ikishindikana unajaribu kufuta baadhi ya programs na files ambazo zinaonekana ziko infected ...... Loh! wakati mwingine unagundua bado haujatatua tatizo ... liko pale pale. Hauna jinsi ispokuwakupoteza kila kitu kwa kufanya re-installation!!

Hiyo (computer) ndiyo Tanzania. System nzima na kizazi chote hiki kilichopo ni CORRUPT ... Kuanzia level ya chini katika jamii hadi juu, serikalini, taasisi za dini, taasisi zisizo za kiserikali, vyama vya siasa, etc.

SOLUTION: Re-Installation. By whom? ..... ... The Creator.
 
Ilongo,
Maneno yako naanza kuona hekima za JK!... yawezekana kabisa kuna kila haja ya kufanya hivyo... Utamwamini nani ikiwa wasomi wetu ndio hawaaa!
 
RDC ilibadilisha jina kuw Dowans Holding, halafu tena ikabadilisha jina na kuwa Dowans Tanzania Limited. Upuuzi kweli jamani.

Matatizo ya Dowans yaelezwa

Mwandishi Wetu

HabariLeo; Wednesday,May 30, 2007 @00:03

KUCHELEWAkupata leseni ya kuiuzia Tanesco umeme wa megawati 100 kunatokana
na kampuni Richmond kubadilisha majina yake mara kwa mara, imefahamika.

Habari kutoka ndani ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), zinasema
kuwa kubadilisha majina kutoka Richmond, Dowans Holdings na sasa Dowans Tanzania ltd, kuliifanya mamlaka hiyo ikawie kutoa leseni.

Mkurugenzi wa Umeme wa Ewura, Anastas Mbawala aliiambia HabariLeo juzi kuwa kampuni ya
Richmond iliomba leseni ya biashara mwaka jana lakini baada ya mabadiliko hayo mamlaka ikabidi isubiri.

Mbawala alisema wao hawakuwa na taarifa kama kampuni hiyo ya Dowans Holdings pia
ilibadilika hadi ilipopeleka maombi ya leseni ofisini kwake na ndipo wao wakaenda kuthibitisha Brela kama Dowans Tanzania imesajiliwa kwa halali.

Alisema kwa mujibu wa maelezo ya viongozi Dowans Holdings, Dowans Tanzania ltd ilianzishwa kutokana na mkataba kati ya Tanesco na Dowans Holdings kwamba kampuni
nyingine isajiliwe kwa ajili ya kuendesha kazi hiyo ya kuuza umeme.

Kutokana na kuchelewa huko kupata leseni kampuni hiyo mpya ya Dowans sasa imepeleka maombi mapya Ewura ikiomba ipewe leseni ya miaka miwili kufanya kazi ya kuuza umeme.

Hata hivyo kampuni hiyo inakabiliwa na wakati mgumu wa kupata leseni hiyo katika kipindi kifupi baada ya Ewura kutoa matangazo yanayowataka wananchi kutoa maoni yao kama kampuni hiyo ipewe au isipewe leseni.

Endapo wananchi watapinga kampuni hiyo isipewe leseni basi kunauwezekano mkubwa uamuzi wa kutoa au kutotoa leseni utachukua muda mrefu na hivyo umeme huo kuendelea kusubiri kwani kisheria hawaruhusiwi kuuza umeme bila leseni.

Mbawala alisema maoni ya wananchi yatachukuliwa na yatafanyiwa kazi na kama yatakuwa
na hoja za msingi basi bodi ya Ewura itatoa uamuzi.
 
Kichuguu,
Habari hii niliipata kijiweni nikiwa Bongo ndio maana nimeuliza kama hao TARUKU wamefanya uchunguzi wa kampuni hii ya Dowans!...
 
Kichuguu,
Habari hii niliipata kijiweni nikiwa Bongo ndio maana nimeuliza kama hao TARUKU wamefanya uchunguzi wa kampuni hii ya Dowans!...

Mimi naona kama huu ni utapeli tu. Ni kama scheme za money laundering kujaribu kufuta ushahidi kabisa. Leo hii ukiongea na jamaa wa Dowans Tanzania Limited wakuambia kuwa hawajui matatizo ya Richmond kwani wao ni kampuni tofauti inayojitegemea.
 
Hivi inakuwaje mtu unapata tenda halafu ndio unaanzisha kampuni ya kutekeleza tenda hiyo? Wakati RDC inapewa mkataba wa bomba la mafuta la Mwanza - Dar... iliwahi kufanya shughuli kama hiyo wapi hadi ikapewa mradi huo mkubwa? Inakuwaje kampuni kama hiyo inapewa mkataba mkubwa wa aina hiyo mwaka mmoja tu baada ya kuanzishwa kwa kampuni? Hata wewe ukitafuta fundi mtaani akuezekee kibanda chako utatafuta angalau aliyeezeka nyumba mbili tatu.. sasa unaenda kumpata fundi akuezekee ghorofa lako wakati hata kibanda cha nyasi hajawahi kuezeka...
 
Ilongo,
Maneno yako naanza kuona hekima za JK!... yawezekana kabisa kuna kila haja ya kufanya hivyo... Utamwamini nani ikiwa wasomi wetu ndio hawaaa!


Mkandara,

Utapata ugonjwa wa moyo pale utakapofanya uchunguzi na kugundua kwamba hata wale tunaowaona kama wakombozi, kumbe wametunyonya kwa njia moja ama nyingine na sasa wanakuja na kelele za "uzalendo" wa kututoa kwenye umaskini. Wanasahau kwamba ndiyo waliochangia katika hali hii tuliyo nayo.

Ni vigumu sana kumwamini mtu aliyepata "utajiri" wake kwa kutumia njia zisizo halali (au asizoweza kuzithibitisha), halafu leo hii anakuja na wazo la kumkomboa huyo mlalahoi .... hii ni dharau ya hali ya juu. Tena wapo wengi.

Kwa mfano: Nikiri kwamba, I was shocked, eti Elvis Musiba huu utajiri alio nao umetokana na wizi akiwa mfanyakazi wa serikali. Kwa watu wengi tusiolijua hili tumekuwa tukimuona ni "mjasiriamali" mzuri sana na pindi angejitokeza kugombea, mimi ni mmoja wa wale ambao tungemuunga mkono.

.... Kuna haja ya kuwajua vizuri (historia zao) hawa watu wanaojitokeza kuwania uongozi ama wanaopewa nafasi nyeti za kuongoza taifa letu .... na hasa kuanzia sekondari ambapo ninaamini kila mtu anakuwa na akili timamu kabisa. Kuanzia kipindi hicho iwapo katika historia yake aliwahi kuonyesha kuvunja ama kushabikia uvunjaji wa maadili ... ATUPISHE ... we need clean people. Siyo watu wanaojifanya "clean" kumbe nia yao ni kupata nafasi ya kupanda ngazi na wakishafika huko juu wanatoa makucha yao (mfano ni Hosea wa TAKURU).

Na ndiyo maana hapo awali nikasema, iwapo itabainika kwamba sote katika Tanzania tayari tuko corrupt, kuanzia ngazi ya chini (family level) hadi ngazi ya juu katika taaasisi mbalimbali, basi hakuna jinsi isipokuwa "Re-Installation of the Operating Sytem in your hard disk". The "creator of Tanzania" can help us do it.

A corrupt parent will obvioulsly bring up a corrupt child.
 
Ilongo,
A corrupt parent will obvioulsly bring up a corrupt child.

Come to think of it?..... heee hapa mjomba umejibu hoja ile inayohoji watoto wa vigogo!... Mnnnnnh! mtoto wa nyoka ni NYOKA,
Can they prove otherwise?
 
Kuepuka utata kama huu kwenye hali kama hizo ndipo dhana nzima ya mgawanyo wa madaraka (Separation Of Power) na mamlaka ya mihimili mitatu ya dola kuchunguzana ilibuniwa. Kimsingi hili eneo la kuichunguza Richmond, lilikuwa ni la Bunge na sio TAUKURU, ambao ni part ya the executive branch.

Na kama shida ya serikali ilikuwa ni kutaka kuwasafisha watu wake wasiosafishika, ambao kila mmoja wetu anawajua, basi angalau ingesimama na kujieleza yenyewe, kuliko kuwatumia TAKURU. Maana nani ataiamini TAKURU, chombo ambacho si wananchi, wala huru kama Bunge kutokana na mujibu wa sheria zetu?


Hapa ni kitu gani kinafichwa? Hivi inaignia akilini kweli kwenye ndoa ushindwe kumuamini mwanandoa mwenzio badala yake umuamini mtoto wenu, halafu na mwenzio akuamini wakati wewe humuamini? Basi atakuwa bwege au kichaa! Wazungu husema " I may be foolish but not crazy. It is better to be either but not both."

.............Itaendelea.........
 
Tender gani mnazozisema? Kampuni kubwa za Genereta zinajulikana na sidhani kama GE itapandisha bei kwa sababu ya serikali je ni kwa nini wasinunue kiwandani? tender ni uizi mkubwa tu
 
Kamundu,
hapo ndipo naposhindwa kabisa kuelewa!.. Tanesco ina mafundi wa kuweza kuendesha mitambo, uwezo wa kufuatilia bill na kadhalika. Walichohitaji tu ilikuwa generators, sasa ilikuwaje hizi generator sizinunuliwe toka GE moja kwa moja na kuwakabidhi Tanesco?
Kwa nini kuwepo na mtu katikati ambaye sio wakala wa GE kwa nchi za Afrika maanake ndio sababu peke yake ambayo ningeweza kuikubali!..
Kuna sababu gani hasa iliyokuwa muhimu kwa kuweka tender ktk shughuli ambayo kampuni husika sii mzalishaji Umeme, msambazaji umeme ama mwenye ujuzi wa mitambo ya Umeme!.
Kitu gani hasa kilichosukuma tender hii?
 
.....Inaendelea.......!

Hata hivyo pamoja na ripoti hiyo kukiri kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ndiyo iliyoamua kubatilisha uamuzi wa kutafuta kampuni kwa njia ya kutangaza Zabuni kimataifa, bado imeshindwa kutoa tathmini iwapo uamuzi huo ulikuwa wa manufaaa kwa taifa au la! Na ilipata mamlaka hayo toka kifungu gani cha sheria za Jamhuri yetu!


Nani aliipa Mamlaka ofisi hiyo ya Waziri mkuu, kuingilia kati masuala ya tenda za serikali, bila ya kuwa na jambo la msingi kufanya hivyo iwapo kanuni za ununuzi na sheria yake (Government Procurement Act) ziko wazi? Ofisi hiyo iliogopa nini kutangaza iwapo sheria zote ziko wazi kuwa shughuli kama hiyo ni lazima itangazwe kwenye gazeti la (Government Gazette), inapotokea kukawa na udhuru?

TAKURU, hawalelezi vyanzo huru vya ushaidi wao, maana hata waliotoa ushaidi huo hawajulikani ni kina nani? Na waliochunguzwa ni kina nani? Zaidi tu ya kuisemea na kuihami serikali! Kusema kweli, hii ni danganya toto, ukweli bado kuwekwa hadharani. TAKURU, hawaelezi walifanya uchunguzi kutokana na shutuma toka kwa wananchi, serikali, au wabunge? Je ni nani aliyekuwa akituhumiwa? na wapi ikiwa ni kwa mambo gani? Ukweli ni kwamba hii kesi ni ya upande mmoja ambapo kinachoonekana ni hakimu kuwa mwendesha mashitaka, mshitakiwa, shahidi na baadaye mtoa hukumu! Kwa mtu anayejua jinsi watwala wetu wanavyosema tofauti na wanavyofanya au kufanya tofauti,

na inavyosemwa, hawezi kuamini ripoti ya TAKURU, hata chembe! Na inatukumbusha wakati wa mchakato wa ununuzi wa Radar, mtakumbuka rais mstaafu Mkapa, alivyotuhakikishia kuwa dili lote la Radar, halikuwa na harufu ya rushwa hata chembe, kuachilia mbali rushwa yenyewe!


Tunachoelewa sasa, ni kwamba rushwa zaidi ya shilingi billioni 16, zilitumika kwenye dili hilo la Radar, wanachi tulipotaka kumkaba shati Mkapa, atueleze kulikoni kutudanganya, Rais Kikwete, akamkingia kifua na kutuonya kuwa tusimbughudhi na tumuache apumzike kwa amani! Na ni hivi karibuni, ili kumsafisha Mkapa na dili hilo la Radar, utafanyika uchunguzi mwingine wa TAKURU, acheni kucheza ma masilahi ya wananchi jamani!

Ukienda kwenye uuuzaji wa NBC, tulikuwa tumeaminishwa kuwa hakukuwa na rushwa hata kidogo na kwamba Mkapa ni Mr. Clean! Lakini wenye akili walikataa na kuamua kuhoji anyway! Bahati nzuri wakati huo Mwalimu alikuwepo bado hai, na aliamua kuwatolea uvivu kina "Uza Uza" hadi kuzuia baadhi miradi muhimu kuuzwa kama Kiwanda Cha Nguo cha Urafiki, Mzee wetu Mwalimu alipiga kiguuuu mpaka U-China, na kumleta muwekezaji ambaye anaingia akilini, na mpaka leo hatujasikia mauza uza ya Richmond, huko Urafiki!





.............Itaendelea..........!
 
.....Inaendelea.......!

Hata hivyo pamoja na ripoti hiyo kukiri kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu ndiyo iliyoamua kubatilisha uamuzi wa kutafuta kampuni kwa njia ya kutangaza Zabuni kimataifa, bado imeshindwa kutoa tathmini iwapo uamuzi huo ulikuwa wa manufaaa kwa taifa au la! Na ilipata mamlaka hayo toka kifungu gani cha sheria za Jamhuri yetu!


Nani aliipa Mamlaka ofisi hiyo ya Waziri mkuu, kuingilia kati masuala ya tenda za serikali, bila ya kuwa na jambo la msingi kufanya hivyo iwapo kanuni za ununuzi na sheria yake (Government Procurement Act) ziko wazi? Ofisi hiyo iliogopa nini kutangaza iwapo sheria zote ziko wazi kuwa shughuli kama hiyo ni lazima itangazwe kwenye gazeti la (Government Gazette), inapotokea kukawa na udhuru?

TAKURU, hawalelezi vyanzo huru vya ushaidi wao, maana hata waliotoa ushaidi huo hawajulikani ni kina nani? Na waliochunguzwa ni kina nani? Zaidi tu ya kuisemea na kuihami serikali! Kusema kweli, hii ni danganya toto, ukweli bado kuwekwa hadharani. TAKURU, hawaelezi walifanya uchunguzi kutokana na shutuma toka kwa wananchi, serikali, au wabunge? Je ni nani aliyekuwa akituhumiwa? na wapi ikiwa ni kwa mambo gani? Ukweli ni kwamba hii kesi ni ya upande mmoja ambapo kinachoonekana ni hakimu kuwa mwendesha mashitaka, mshitakiwa, shahidi na baadaye mtoa hukumu! Kwa mtu anayejua jinsi watwala wetu wanavyosema tofauti na wanavyofanya au kufanya tofauti,

na inavyosemwa, hawezi kuamini ripoti ya TAKURU, hata chembe! Na inatukumbusha wakati wa mchakato wa ununuzi wa Radar, mtakumbuka rais mstaafu Mkapa, alivyotuhakikishia kuwa dili lote la Radar, halikuwa na harufu ya rushwa hata chembe, kuachilia mbali rushwa yenyewe!


Tunachoelewa sasa, ni kwamba rushwa zaidi ya shilingi billioni 16, zilitumika kwenye dili hilo la Radar, wanachi tulipotaka kumkaba shati Mkapa, atueleze kulikoni kutudanganya, Rais Kikwete, akamkingia kifua na kutuonya kuwa tusimbughudhi na tumuache apumzike kwa amani! Na ni hivi karibuni, ili kumsafisha Mkapa na dili hilo la Radar, utafanyika uchunguzi mwingine wa TAKURU, acheni kucheza ma masilahi ya wananchi jamani!

Ukienda kwenye uuuzaji wa NBC, tulikuwa tumeaminishwa kuwa hakukuwa na rushwa hata kidogo na kwamba Mkapa ni Mr. Clean! Lakini wenye akili walikataa na kuamua kuhoji anyway! Bahati nzuri wakati huo Mwalimu alikuwepo bado hai, na aliamua kuwatolea uvivu kina "Uza Uza" hadi kuzuia baadhi miradi muhimu kuuzwa kama Kiwanda Cha Nguo cha Urafiki, Mzee wetu Mwalimu alipiga kiguuuu mpaka U-China, na kumleta muwekezaji ambaye anaingia akilini, na mpaka leo hatujasikia mauza uza ya Richmond, huko Urafiki!





.............Itaendelea..........!


This one is really good, it is in line with the kind of questions clinging in my mind since this saga started.
 
Mzee Es, ninajiuliza: Hivi TAKURU wanaposoma uchambuzi makini kama huo wako ulioutoa hapo juu, na kuulinganisha na matokeo ya uchunguzi wao wanajihisi vipi? How do they justify their pay?

It is good to show them that we are not as gullible as they take Tanzanians to be. We may not have the means to discipline them now, but hey, who knows what tomorrow will bring!
 
... Walichohitaji tu ilikuwa generators, sasa ilikuwaje hizi generator sizinunuliwe toka GE moja kwa moja na kuwakabidhi Tanesco?

Si rahisi kama unavyosema. Mbona majenereta ya SONGAS yalikuwa ya TANESCO? Wakaambiwa wayauze halafu wanunue umeme toka SANGOS + kulipa capacity charges. Upuuzi ambao hauelezeki. Kama nilivyosema zamani, ni kama kujenga nyumba yako, halafu unaiuza na kuwa mpangaji kwa hiyo hiyo nyumba, ukikamuliwa kodi isiyo mfano.
 
Kama ameweza kumfumbia macho kaka yake aliyemuachia kiti ,huoni kuwa na yeye anahusika? mumesahau kuwa yupo chini ya ccm? chukua chako mapema?
 
Back
Top Bottom