Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Sakata la Kashfa ya Richmond: The Facts

Ni Watanzania pekee ndiyowenye jukumu lakuikomboa Tanzania kutoka kwenye makucha ya wakoloni weusi wachache wanaoendelea kusimika mirija yao kila siku.

Kulia lia kwenye vyombo vya kimataifa kama IMF, Wrld Bank nk ni ujinga usio weza pimika. Vyombo hivi viliundwa na Mabepari wakubwa wa dunia kugandamiza wanyonge wote duniani. Vipi leo wanyonge wanadhani vyombo hivi viko upande wao?

Uzito wa matatizoyetu ndo unatufanya tuone sela za WB na IMF kuwa nzuri kuliko sera muflisi za Serikali ya SISIEMU. Kuvililia vyombo vya kimataifa ni kuonyesha wazi kwamba tunakubali sera zao pia tuna kiri kwamba sisi ni watu duni kamwe hatuwezikujikomboa bila mkombozi kutoka nchi za magharibi.

Mapambano ya kuwaondoa wale wote wanaochzea Uhuru wetu ni yetu wenyewe Watanzania.
Mapambano ya kuwang'oa Mafisadi na kuangamiza kabisa mazalia yao ni yetu Watanzania.
Mapmbano ya kubadiri fikra za watanzania na kujenga utaifa kwa kuhimiza elimu ya uraia, ili kuamsha uzalendo na utaifa wa kila mtanzania ni yetu Watanzania wenyewe.
Mapambano ya kurejesha njia kuu zote za uchumi mikononi mwa watanzania kwa kubadiri sheria za umiriki wa ardhi na makapuni ya kibiashara yako juu ya mabega yetu na ndani ya akili zetu.

Mapambano ya kuiondoa Tanzania katika kundi la nchi masikini zaidi duniani kwa kuanzisha na kukuza uwezo wa kuzarisha bidhaa za viwandani, chakula mashambani,uvuvi badharini na kupandisha hali za maisha ya watanzania ni majukumu yetu watanzania wenyewe.

Wakoloni weupe walishindwa kutuletea maendeleo ya kweli walipo tutawala moja kwa moja. Leo hii wakoloni wale wale wanatutawala kwa kutumia makampuniyao ya kimataifa kupitia maajenti wao weusi ambao ni viongozi wanao ongoza taifa letu, wana hila zile zile za kuchelewesha au kukwamisha kabisa maendeleo yetu.

Watanzania hatuwezi kuendelea kukaa kimya na kuiacha Tanzania yetu ikigawanywa vipande vipande na kuuzwa sokoni na viongozi wetu ambao ni wakala wa ukoloni mambo leo.
Tukisubiri wagawane na kuuza hadi washibe tutasubiri hadi siku ya kiama, viongozi makupe hawa hawatashiba kamwe.

Gharama ya kuiachia Tanzania iendelee kuongozwa na kundi la watu wenye njozi za kuuza hata mama zao wazazi ni kubwa isiyo weza bebwa na mtanzania yeyote wakiwemo viongozi wenyewe.
Kwa kuzingatia ukubwa wa gharama ya kuiacha Tanzania iendelee kudharirishwa na makampuni ya kimataifa na yale kutoka nchi masikini kama yetu (IPTL ya Malaysia), Watanzania ni lazima tujiandae kupambana katika pambano la Ama zao Ama zetu.

Mapmbano ya kuikomboa Tanzania ni mapambano ya kufa na kupona.
Tukiacha kupambana na Ufisadi tutakufa kwa kihoro na utapiamlo, tukipambana naufiusadi kuna wengine kati yetu tutakufa kwa kisasi cha fisadi.

Ni bora kufa ukipambana kutetea haki yako kuliko kufa ukisononeka kwa kufanywa mtumwa katika nchi yako.

SAA YA UKOMBOZI NI SASA NA WAKOMBOZI NI MIMI NA WEWE
 
Sikia Muziki ndani ya Loho(sic), tunacheza, tunakula muziki tukunyema Wa wa!

For a minute I got depressed when I failed to see Dar Es Salaam, Kada, Shy and all those who are Pro-Ufisadi, come to find out Thumuni made an attempt to silence the truth... sad Tanzania inaliwa na wananchi wenyewe....
 
Jumapili Mar 16, 2008 16.03.2008 1429 EAT

*Sasa wanasheria waanza kumbana Lowassa
*Wahoji usahihi wa kauli zake nje ya Bunge


Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete alidanganywa na wasaidizi wake kuhusu mambo mbalimbali katika mchakato wa kusainiwa kwa mkataba wa Richmond kiasi cha yeye kujikuta akilitangazia Taifa habari zisizo sahihi kutoka kwa wasaidizi wake, Majira Jumapili imethibitisha.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa kina kuanzia katika mwenendo wa jinsi kampuni hiyo ilivyopewa tenda hadi ilivyosababisha vigogo kadhaa kung'oka serikalini, sasa ni dhahiri kuwa katika hatua mbalimbali za watu kuonekana walikuwa tayari kuibeba kampuni hiyo kwa gharama zozote, Rais Kikwete naye alijikuta mara kadhaa akipewa taarifa zilizokosa usahihi na kuzitumia majukwaani kufafanua mambo kwa Taifa.

Majira Jumapili sasa imethibitisha kuwa maelezo ya Rais Kikwete wakati wa mahojiano yake na kituo cha Televisheni ya Taifa (TvT) mwaka jana kuwa kampuni hiyo ya Richmond ilipewa tenda kwa kigezo cha kuwa na bei ya chini kuliko zote, sasa imebainika kuwa Rais alidanganywa na waliompa takwimu na yeye kuzitumia.

Kasoro hiyo ilibainika kufuatia aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa TANESCO, Bw. Yohanes Hans, kuiambia Kamati ya Bunge iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake, Dkt. Harrison Mwakyembe, kuwa suala hilo halikuwa sahihi na ilienezwa makusudi kuifanya Richmond ikubalike pamoja na kutokuwa na uwezo.

Katika madai hayo ambayo hata ripoti ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) nayo iliyashabikia kuwa ndicho kigezo cha msingi cha kuikubali kampuni hiyo, Richmond ilikubali kuuza umeme wake kwa senti 4.99 zilizojengewa uzushi kuwa ni za chini zaidi.

Rais Kikwete naye akitumia kigezo hicho hicho bila kufahamu ajenda pana ya wanamtandao wa Richmond waliohakikisha takwimu hiyo inamfikia na anazitumia, naye alilisisitizia Taifa kuwa TANESCO na hata wizara walikuwa wakitafuta kampuni yenye bei ndogo na hivyo kuipa tenda Richmond.

Lakini tofauti na takwimu alizopewa Rais, Mkurugenzi wa zamani wa TANESCO aliwaumbua walioeneza madai hayo ya Richmond kuwa na bei ndogo kwa kuiambia Kamati ya Mwakyembe kuwa kampuni iliyopeleka bei ndogo kuliko zote wakati wa zabuni, haikuwa Richmond bali Songas iliyokuwa tayari imekubali kuuza umeme wake kwa senti 3.84 za dola kwa uniti tena bila capacity charges (Richmond inalipwa sh. milioni 152 kwa siku za capacity charges).

Sehemu ya maswali kati ya Kamati Teule ya Bunge na Bw. Hans yalikuwa kama ifuatavyo;

Dkt. Harrison Mwakyembe: Tumeambiwa kwamba TANESCO ilijaribu kuwa na makubaliano na kampuni ya Songas wakati huo, lakini vipengele vya makubaliano havikukubaliwa na Wizara ya Serikali kwa kuwa Kampuni ya Songas ilipendekeza bei ya juu. Sijui kama hilo ni kweli au ni maelezo tu yaliyotolewa?

Bw. Yohanes Hans: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unatakiwa kujibu hilo, makubaliano yaliyosainiwa yanafanana na tuliyokuwa tumeafikiana na Songas, kwa hiyo swali hilo ni gumu kulijibu. Kuhusu bei kwa uniti tulijadiliana na Songas bei iwe senti 3.84, nafikiri ya Richmond ilikuwa senti tano.

Mwakyembe: 4.99?
Hans: Senti 4.99. Hiyo ni hoja ya kwanza, hoja ya pili ni kwamba jenereta za Songas zinafanana kabisa na jenereta zilizopo Ubungo ambazo DOWANS (Kampuni iliyonunua mkataba wa Richmond) imenunua. Kwa hiyo hayo uliyoelezwa yalikuwa na sababu zake, kwani tungeweza kununua umeme wa bei rahisi na mashine zilizopo ndizo ambazo Songas walikuwa wazilete. Nadhani hilo ni jibu zuri kwa swali lako.

Sasa wanasheria kadhaa waandamizi wameibuka na kusisitiza kuwa kauli ya hivi karibuni ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, kuwa alipata ushauri wa kisheria asivunje mkataba na Richmond ni mambo yanayoacha maswali magumu bila majibu.

Wanasheria hao wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kutoka kampuni kadhaa za uwakili binafsi jijini Dar es Salaam, waliiambia Majira Jumapili kuwa ni vyema Bw. Lowassa akawataja mawakili anaosema walimpa ushauri huo na hilo likaenda hadi kwa Rais, kwa sababu suala hilo linaweza kuidhalilisha taaluma ya sheria.

"Ukiutazama mkataba wa Richmond, jinsi walivyoshindwa kuutekeleza na kisha inakuja kauli ya Lowassa kuwa alitaka kuuvunja mkataba huo lakini wanasheria wakubwa tu, wakamshauri asifanye hivyo, ni suala linaloibua maswali mengi," alisema mhadhiri wa sheria kutoka Kitivo cha Sheria cha chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

"Mtazamo wangu ni kwamba kama kweli wapo waliomshauri hivyo basi tunapaswa kuwajua ili tuupime uadilifu wao kitaaluma na kwa Serikali, kwa sababu ukitazama mambo haya, kisheria kuna maeneo yalikuwa wazi kuwa Richmond ilidanganya," alisema mhadhiri huyo.

"Kusema uongo juu ya uwezo wake ni sababu tosha kwa mujibu wa sheria za mikataba, kuuvunja mkataba," alisema mhadhiri ambaye pia ni wakili wa Mahakama Kuu.

"Sisi tunawafundisha vijana wetu hapa kwa miaka mingi tu tena ni katika darasa la awali kabisa la sheria za mikataba kuwa udanganyifu kama ilivyofanya Richmond iliyojieleza kuwa ni kampuni yenye uwezo kumbe hata haipo kisheria, unatosha kuvunja mkataba.

"Ni vyema Lowassa akalisaidia Taifa kuwajua hao waliomwambia tofauti, tunataka kujua kama ni wanafunzi wetu au wametoka wapi, tuupime utaalamu wao?," alihoji mhadhiri huyo na kuomba asiwekwe bayana gazetini kwa sababu ya utumishi wake.

Katika fungu la (ii) B la mkataba kati ya TANESCO na Richmond (nakala tunayo), kampuni hiyo iliyojieleza kutoka Marekani, ilijifunga kimkataba ikijinasibu kuwa na uwezo. Fungu hilo linasema "Mleta mitambo (Richmond), ana vifaa na uwezo wa kifedha na kiufundi wa kujenga, kufunga na kuuendesha mtambo huo (wa megawati 100) kama inavyotakiwa na TANESCO."

Pamoja na ahadi hiyo ya kimkataba, Richmond walishindwa katika maeneo yote waliyoyaahidi kwenye kipengele hicho na bado Lowassa akasema alishauriwa asivunje mkataba huo.

Naye wakili wa kujitegemea ambaye ni mmoja wa mawakili waandamizi nchini ambaye pia aliomba kutowekwa bayana jina lake kwa sababu za kimaslahi, aliunga mkono hoja ya kumtaka Bw. Lowassa kuwataja wanasheria waliomshauri asiuvunje mkataba wa Richmond kwani hata yeye amestaajabishwa na kauli hiyo.

"Nina wasiwasi na wataalamu hao. Kama ulivyoniuliza, jibu langu ni kweli vipo vipengele vya wazi kabisa vya kuuvunja mkataba huo. Kwanza, kuna udanganyifu ambao uliathiri utekelezaji wa mkataba. Pili, kama Serikali ikithibitisha kuna viongozi walikula rushwa, nayo ni sababu ya kuvunja mkataba na tatu uhalali wa kampuni ya Richmond yenyewe kisheria," alisema Wakili huyo.

"Tumesikia kuwa hata Marekani haikusajiliwa na iliyosajiliwa hapa si iliyosaini mkataba. Hapa hao wanasheria wa Lowassa wangefanya vyema utafiti wa kisheria, naamini wasingempa ushauri anaodai kupewa," alisema kama angeulizwa ushauri wake kwa Serikali, angesema mkataba huo uvunjwe, ingawa alionesha wasiwasi iwapo hilo kwa sasa linawezekana kwani mkataba huo umeshatekelezwa na Dowans baada ya Richmond kukimbia.

Hata hivyo, ilibainika pia kuwa kwa mujibu wa kipengele cha fungu la 21.1 la mkataba wa TANESCO na Richmond, linalozungumzia matukio yanayoweza kuvunja mkataba (events of default), Richmond ilijifunga kimkataba kuwa watakuwa wamesababisha kuvunjika kwa mkataba huo.
Iwapo;

"Kauli yoyote au uhakika wowote uliotolewa na mleta mtambo (Richmond) katika mkataba huu vitabainika kuwa si sahihi na itabainika au kuwa hakika kwamba ahadi hiyo ilitolewa na ikawa ni sehemu ya msingi wa mkataba na ahadi au kauli hiyo ikaonekana haikuwa sahihi na kuathiri uwezo wa mleta mitambo kutimiza majukumu yake kimkataba." Wanasheria walipooneshwa kifungu hiki na gazeti hili, walisema kilitosha kuifukuza Richmond iliposhindwa hata kuleta mitambo nchini.

Zaidi gazeti hili limebaini kuwa kwa kipengele cha rushwa kwa mfano, hata Baraza la Kimataifa la Kutatua Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) la London, Uingereza, lililosikiliza kesi ya TANESCO na IPTL, lilisema katika hukumu yake kuwa ushahidi wa IPTL kutumia rushwa katika kupata mkataba ungewasilishwa, TANESCO ingekuwa na nafasi kubwa ya kushinda kesi hiyo.

Nyaraka rasmi za Baraza hilo, zinaonesha kuwa wanasheria kutoka kampuni ya Mkono Advocates na ushauri wa kitaalamu uliotolewa na mmoja wa wasomi waliobobea katika taaluma ya sheria mbalimbali zikiwamo za kimataifa, Profesa Palamagamba Kabudi wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ulionesha kuwa rushwa kwa mujibu wa fungu la 19 la Sheria ya Mikataba ya Tanzania, ni kigezo tosha cha kuvunja mkataba.

Hata hivyo, ushahidi huo wa rushwa haukupelekwa London, ikielezwa ulibaki Dar es Salaam ambako aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa PCB (sasa Mkurugenzi Mtendaji wa TAKUKURU), Bw. Edward Hosea, alikuwa akijiandaa kuutumia katika shauri la jinai lililotarajiwa kufunguliwa ambalo hata hivyo mpaka sasa halijafunguliwa na hakuna sababu rasmi zilizotolewa.

Kwa kushindikana ushahidi huo kupelekwa London, hukumu ya Baraza hilo iliyoibwaga TANESCO na kuilazimu iwalipe IPTL mabilioni ya fedha zikiwemo za capacity charges huku hali ikiwa ni ile ile kama Richmond; IPTL nao, wazalishe, wasizalishe, walitakiwa kulipwa. Hukumu ya London ilitolewa Februari 2, 2001.

Wasomi waliozungumza na gazeti hili na wanaojua vyema mwenendo wa kanuni za uendeshaji mashauri katika Baraza hilo la London, wanaamini kama Serikali ingeamua, ingeuvunja mkataba na Richmond bila kuwajibika, lakini kama ilivyokuwa kwa IPTL ambako ushahidi uliachwa Dar es Salaam, woga ni kwamba hata katika hatua hiyo, huenda wanamtandao wa Richmond wangeweza kuihujumu hata kesi hiyo; tatizo ni uadilifu na kujitoa, si sheria.

Source: Majira Jumapili

Hii ni dalili toshwa kuwa viongozi wetu huwatupia lawama wataalam pale wanapochemsha. Lakini ninasubiri kwa hamu kweli hiyo miezi mitatu itakapoisha bila kutekelezwa kwa maagizo ya BUNGE.
 
Rais yeye ni kudanganywa tu kila kukicha mara kashauriwa vibaya maana kichwani mwake ni hamnazo, OK tutaona mengi.
 
Rais yeye ni kudanganywa tu kila kukicha mara kashauriwa vibaya maana kichwani mwake ni hamnazo, OK tutaona mengi.


Ni utamaduni mbaya wa siasa zetu kwamba mkubwa huwa hakosei. Tumeona wenzetu hata majina ya watu yakipotea kwenye computer anayebeba lawama ni kiongozi wa juu kabisa. Kwa utamaduni wetu huu, viongozi wetu hawafanyi bidii ya kujua mambo kabla ya kutia masaini yao maana wanajua kuwa siku ya siku kikiharibika hawatalaumiwa wao. Hapa JK hana njia ya kukwepa; yeye alitangaza kwa mbwembwe jinsi ambavyo Richmond wange-solve tatizo la umeme, iweje leo waandishi wa habari wanajaribu kumkwepesha.

Hao nao wanaojiita wanasheria ambao wanaogopa hata kutaja majina yao kwa maoni wanayotoa mimi nawaita ni wachovu na hawaamini wanachokisema. Kuna kitu gani alichosema hapo ambacho kinahatarisha ajira yake kama sio unafiki na woga. Halafu hawa wana tabia ya kumsakama mtu akishaondoka madarakani; hawa hawa siku zote walikuwa kimya au wakimsifa Lowasa, lakini leo ametoka madarakani anaonekana mbaya kwa kila mtu. Haya huyo Mkapa, wanasheria wetu walikuwa wapi kumkosoa alipokuwa madarakani; walimwacha akafanya madudu yake tena kwa msaada wao wa kisheria, leo anapumzika zake huko Lushoto ndio wanajifanya kumbebea bango. Watanzania woga na unafiki unatutafuna, tena ni hatari kuliko hata ufisadi wenyewe.
 
Jamani mpaka lini? when will this end? So Lowassa quits and claims chuki za cheo, Mwanyika na Hosea bado wanapeta na wanakataa kuwajibika, na kila siku kuna habari mpya kudhihirisha kuwa Richmond ilikuwa ni bomu kubwa na machozi ya Raisi kumtetea Lowassa yanaanza kuonekana kuwa yalikuwa ya kenge kutughairi Watanzania.

Hosea kadiriki kukalia ushahidi muhimu ambao ungeliokoa Taifa kuingia gharama za kijinga za IPTL eti anafungua kesi ambayo mpaka leo ni yeye pekee anaijua.

Mwanasheria Mkuu anadai hausiki na uhujumu, je si jukumu la ofisi ya Mwanasheria Mkuu kupitia mikataba yote ya serikali na kuiidhinisha?

Tunaposema Kikwete aamke, wengine humu ndani mnasema tunamuonea hatumpi nafasi na eti mbona Nyerere, Mwinyi na Mkapa walifanya mengine mabovu!

It is absurd to anyone that we continue to have leadership in our country that is not being respected by people who are appointed to provide techinical support, advice and help Rais to execute his mission.

The question will now become, what is President Kikwete's mission and vision to lead our country?

Is his mission to lead us as a nation to prosperity, defeating ujinga, umasikini na maradhi and build strong national unity where people of Tanzania are proud of their country, their leadership and they can enjoy fruits of their labor and natural resources?

Or his mission is to cater and provide a plartform and perfect opportunity to a few groups of operatives whose objective is to rip our wealth for self interest and interest of those who are there to milk us down to the last drop with no hope or a chance of survival and enjoyment of our freedom, natural resources and sweat of our labor?

Kwa nini tuaendelea kuwa na viongozi na watendaji wabovu ambao kuna ushahidi tusha kuwa wamefanya uzembe wa hali ya juu ambao unatishia usalama wa Taifa letu kwa kuruhusu uhujumu wa uchumi na mali zetu?

http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=5999

16.03.2008 1429 EAT

Kikwete alidanganywa kuhusu Richmond

*Sasa wanasheria waanza kumbana Lowassa
*Wahoji usahihi wa kauli zake nje ya Bunge

Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete alidanganywa na wasaidizi wake kuhusu mambo mbalimbali katika mchakato wa kusainiwa kwa mkataba wa Richmond kiasi cha yeye kujikuta akilitangazia Taifa habari zisizo sahihi kutoka kwa wasaidizi wake, Majira Jumapili imethibitisha.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa kina kuanzia katika mwenendo wa jinsi kampuni hiyo ilivyopewa tenda hadi ilivyosababisha vigogo kadhaa kung'oka serikalini, sasa ni dhahiri kuwa katika hatua mbalimbali za watu kuonekana walikuwa tayari kuibeba kampuni hiyo kwa gharama zozote, Rais Kikwete naye alijikuta mara kadhaa akipewa taarifa zilizokosa usahihi na kuzitumia majukwaani kufafanua mambo kwa Taifa.

Majira Jumapili sasa imethibitisha kuwa maelezo ya Rais Kikwete wakati wa mahojiano yake na kituo cha Televisheni ya Taifa (TvT) mwaka jana kuwa kampuni hiyo ya Richmond ilipewa tenda kwa kigezo cha kuwa na bei ya chini kuliko zote, sasa imebainika kuwa Rais alidanganywa na waliompa takwimu na yeye kuzitumia.

Kasoro hiyo ilibainika kufuatia aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa TANESCO, Bw. Yohanes Hans, kuiambia Kamati ya Bunge iliyokuwa chini ya Mwenyekiti wake, Dkt. Harrison Mwakyembe, kuwa suala hilo halikuwa sahihi na ilienezwa makusudi kuifanya Richmond ikubalike pamoja na kutokuwa na uwezo.

Katika madai hayo ambayo hata ripoti ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) nayo iliyashabikia kuwa ndicho kigezo cha msingi cha kuikubali kampuni hiyo, Richmond ilikubali kuuza umeme wake kwa senti 4.99 zilizojengewa uzushi kuwa ni za chini zaidi.

Rais Kikwete naye akitumia kigezo hicho hicho bila kufahamu ajenda pana ya wanamtandao wa Richmond waliohakikisha takwimu hiyo inamfikia na anazitumia, naye alilisisitizia Taifa kuwa TANESCO na hata wizara walikuwa wakitafuta kampuni yenye bei ndogo na hivyo kuipa tenda Richmond.

Lakini tofauti na takwimu alizopewa Rais, Mkurugenzi wa zamani wa TANESCO aliwaumbua walioeneza madai hayo ya Richmond kuwa na bei ndogo kwa kuiambia Kamati ya Mwakyembe kuwa kampuni iliyopeleka bei ndogo kuliko zote wakati wa zabuni, haikuwa Richmond bali Songas iliyokuwa tayari imekubali kuuza umeme wake kwa senti 3.84 za dola kwa uniti tena bila capacity charges (Richmond inalipwa sh. milioni 152 kwa siku za capacity charges).

Sehemu ya maswali kati ya Kamati Teule ya Bunge na Bw. Hans yalikuwa kama ifuatavyo;

Dkt. Harrison Mwakyembe: Tumeambiwa kwamba TANESCO ilijaribu kuwa na makubaliano na kampuni ya Songas wakati huo, lakini vipengele vya makubaliano havikukubaliwa na Wizara ya Serikali kwa kuwa Kampuni ya Songas ilipendekeza bei ya juu. Sijui kama hilo ni kweli au ni maelezo tu yaliyotolewa?

Bw. Yohanes Hans: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unatakiwa kujibu hilo, makubaliano yaliyosainiwa yanafanana na tuliyokuwa tumeafikiana na Songas, kwa hiyo swali hilo ni gumu kulijibu. Kuhusu bei kwa uniti tulijadiliana na Songas bei iwe senti 3.84, nafikiri ya Richmond ilikuwa senti tano.

Mwakyembe: 4.99?
Hans: Senti 4.99. Hiyo ni hoja ya kwanza, hoja ya pili ni kwamba jenereta za Songas zinafanana kabisa na jenereta zilizopo Ubungo ambazo DOWANS (Kampuni iliyonunua mkataba wa Richmond) imenunua. Kwa hiyo hayo uliyoelezwa yalikuwa na sababu zake, kwani tungeweza kununua umeme wa bei rahisi na mashine zilizopo ndizo ambazo Songas walikuwa wazilete. Nadhani hilo ni jibu zuri kwa swali lako.

Sasa wanasheria kadhaa waandamizi wameibuka na kusisitiza kuwa kauli ya hivi karibuni ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa, kuwa alipata ushauri wa kisheria asivunje mkataba na Richmond ni mambo yanayoacha maswali magumu bila majibu.

Wanasheria hao wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kutoka kampuni kadhaa za uwakili binafsi jijini Dar es Salaam, waliiambia Majira Jumapili kuwa ni vyema Bw. Lowassa akawataja mawakili anaosema walimpa ushauri huo na hilo likaenda hadi kwa Rais, kwa sababu suala hilo linaweza kuidhalilisha taaluma ya sheria.

"Ukiutazama mkataba wa Richmond, jinsi walivyoshindwa kuutekeleza na kisha inakuja kauli ya Lowassa kuwa alitaka kuuvunja mkataba huo lakini wanasheria wakubwa tu, wakamshauri asifanye hivyo, ni suala linaloibua maswali mengi," alisema mhadhiri wa sheria kutoka Kitivo cha Sheria cha chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

"Mtazamo wangu ni kwamba kama kweli wapo waliomshauri hivyo basi tunapaswa kuwajua ili tuupime uadilifu wao kitaaluma na kwa Serikali, kwa sababu ukitazama mambo haya, kisheria kuna maeneo yalikuwa wazi kuwa Richmond ilidanganya," alisema mhadhiri huyo.

"Kusema uongo juu ya uwezo wake ni sababu tosha kwa mujibu wa sheria za mikataba, kuuvunja mkataba," alisema mhadhiri ambaye pia ni wakili wa Mahakama Kuu.

"Sisi tunawafundisha vijana wetu hapa kwa miaka mingi tu tena ni katika darasa la awali kabisa la sheria za mikataba kuwa udanganyifu kama ilivyofanya Richmond iliyojieleza kuwa ni kampuni yenye uwezo kumbe hata haipo kisheria, unatosha kuvunja mkataba.

"Ni vyema Lowassa akalisaidia Taifa kuwajua hao waliomwambia tofauti, tunataka kujua kama ni wanafunzi wetu au wametoka wapi, tuupime utaalamu wao?," alihoji mhadhiri huyo na kuomba asiwekwe bayana gazetini kwa sababu ya utumishi wake.

Katika fungu la (ii) B la mkataba kati ya TANESCO na Richmond (nakala tunayo), kampuni hiyo iliyojieleza kutoka Marekani, ilijifunga kimkataba ikijinasibu kuwa na uwezo. Fungu hilo linasema "Mleta mitambo (Richmond), ana vifaa na uwezo wa kifedha na kiufundi wa kujenga, kufunga na kuuendesha mtambo huo (wa megawati 100) kama inavyotakiwa na TANESCO."

Pamoja na ahadi hiyo ya kimkataba, Richmond walishindwa katika maeneo yote waliyoyaahidi kwenye kipengele hicho na bado Lowassa akasema alishauriwa asivunje mkataba huo.

Naye wakili wa kujitegemea ambaye ni mmoja wa mawakili waandamizi nchini ambaye pia aliomba kutowekwa bayana jina lake kwa sababu za kimaslahi, aliunga mkono hoja ya kumtaka Bw. Lowassa kuwataja wanasheria waliomshauri asiuvunje mkataba wa Richmond kwani hata yeye amestaajabishwa na kauli hiyo.

"Nina wasiwasi na wataalamu hao. Kama ulivyoniuliza, jibu langu ni kweli vipo vipengele vya wazi kabisa vya kuuvunja mkataba huo. Kwanza, kuna udanganyifu ambao uliathiri utekelezaji wa mkataba. Pili, kama Serikali ikithibitisha kuna viongozi walikula rushwa, nayo ni sababu ya kuvunja mkataba na tatu uhalali wa kampuni ya Richmond yenyewe kisheria," alisema Wakili huyo.

"Tumesikia kuwa hata Marekani haikusajiliwa na iliyosajiliwa hapa si iliyosaini mkataba. Hapa hao wanasheria wa Lowassa wangefanya vyema utafiti wa kisheria, naamini wasingempa ushauri anaodai kupewa," alisema kama angeulizwa ushauri wake kwa Serikali, angesema mkataba huo uvunjwe, ingawa alionesha wasiwasi iwapo hilo kwa sasa linawezekana kwani mkataba huo umeshatekelezwa na Dowans baada ya Richmond kukimbia.

Hata hivyo, ilibainika pia kuwa kwa mujibu wa kipengele cha fungu la 21.1 la mkataba wa TANESCO na Richmond, linalozungumzia matukio yanayoweza kuvunja mkataba (events of default), Richmond ilijifunga kimkataba kuwa watakuwa wamesababisha kuvunjika kwa mkataba huo.
Iwapo;

"Kauli yoyote au uhakika wowote uliotolewa na mleta mtambo (Richmond) katika mkataba huu vitabainika kuwa si sahihi na itabainika au kuwa hakika kwamba ahadi hiyo ilitolewa na ikawa ni sehemu ya msingi wa mkataba na ahadi au kauli hiyo ikaonekana haikuwa sahihi na kuathiri uwezo wa mleta mitambo kutimiza majukumu yake kimkataba." Wanasheria walipooneshwa kifungu hiki na gazeti hili, walisema kilitosha kuifukuza Richmond iliposhindwa hata kuleta mitambo nchini.

Zaidi gazeti hili limebaini kuwa kwa kipengele cha rushwa kwa mfano, hata Baraza la Kimataifa la Kutatua Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) la London, Uingereza, lililosikiliza kesi ya TANESCO na IPTL, lilisema katika hukumu yake kuwa ushahidi wa IPTL kutumia rushwa katika kupata mkataba ungewasilishwa, TANESCO ingekuwa na nafasi kubwa ya kushinda kesi hiyo.

Nyaraka rasmi za Baraza hilo, zinaonesha kuwa wanasheria kutoka kampuni ya Mkono Advocates na ushauri wa kitaalamu uliotolewa na mmoja wa wasomi waliobobea katika taaluma ya sheria mbalimbali zikiwamo za kimataifa, Profesa Palamagamba Kabudi wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ulionesha kuwa rushwa kwa mujibu wa fungu la 19 la Sheria ya Mikataba ya Tanzania, ni kigezo tosha cha kuvunja mkataba.

Hata hivyo, ushahidi huo wa rushwa haukupelekwa London, ikielezwa ulibaki Dar es Salaam ambako aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa PCB (sasa Mkurugenzi Mtendaji wa TAKUKURU), Bw. Edward Hosea, alikuwa akijiandaa kuutumia katika shauri la jinai lililotarajiwa kufunguliwa ambalo hata hivyo mpaka sasa halijafunguliwa na hakuna sababu rasmi zilizotolewa.

Kwa kushindikana ushahidi huo kupelekwa London, hukumu ya Baraza hilo iliyoibwaga TANESCO na kuilazimu iwalipe IPTL mabilioni ya fedha zikiwemo za capacity charges huku hali ikiwa ni ile ile kama Richmond; IPTL nao, wazalishe, wasizalishe, walitakiwa kulipwa. Hukumu ya London ilitolewa Februari 2, 2001.

Wasomi waliozungumza na gazeti hili na wanaojua vyema mwenendo wa kanuni za uendeshaji mashauri katika Baraza hilo la London, wanaamini kama Serikali ingeamua, ingeuvunja mkataba na Richmond bila kuwajibika, lakini kama ilivyokuwa kwa IPTL ambako ushahidi uliachwa Dar es Salaam, woga ni kwamba hata katika hatua hiyo, huenda wanamtandao wa Richmond wangeweza kuihujumu hata kesi hiyo; tatizo ni uadilifu na kujitoa, si sheria.
 
Rais alidanganywa na wasaidizi wake? Au Alikubali aonekane kuwa anadanganywa?
Anazo 'resources' zote anazoweza kuzitumia kama angekuwa hataki kudanganywa!

Haya ya Richmond Kikwete aliyaelewa thika tokea mwazo wake, waandishi wa habari wasitafute njia za kusafisha uchafu unaoonekana wazi.

Kuna wanasheria gani tena zaidi ya hao wa Mwanyika ambao Lowasa atakuwa anawazungumzia. Mwanyika mwenyewe shasema wao walikuwepo tu katika vikao mbalimbali vya mkataba bila ya kufanya kazi ya kisheria.

Ni dhahiri kwamba baadhi ya yaliyotokea katika Richmond, yamekopwa toka IPTL. Wahusika walidhamiria kutumia 'model' ile ile ya IPTL. Ndio maana Lowasa anaonekana kutumia kesi ya IPTL kule London, ambako serikali ya Tanzania iliamua maksudi kubwagwa, na kuendelea kulipia mabilioni ya walalahoi kwa IPTL hata kama huduma haitolewi.

Hivi hawa viongozi bado kweli wanaamini Tanzania tutaendelea kuwa salama?
 
Ukiona Raisi anadanganywa hujue hamna kitu hapo, Jiulize hao wanaomdanganya wanapata wapi ujasiri wa kumdanganya, ni kwa sababu wanajua hayuko makini hivyo wanaweza kumrubuni


Mkuu BabaH,
Nakubaliana na wewe kabisa kuwa JK hayuko makini, kwa maana nyingine ni kuwa hatufai, ingawa ana kikosi kizima cha usalama wa taifa.
 
Kinachoudhi zaidi ni kujua kuwa kuna watu kwa makusudi kabisa waliamua kumlaghai Rais kuhusiana na hili.

Wakati wengi tunashupalia kuwa tunapoteza pesa kuwalima Richmond na Dowans, kila siku, wengi wetu tumesahau ukweli ni kuwa Nchi ilipotoza nguvu za Uzalishaji mali kwa kipindo chote ambacho tulihitaji umeme wa dharura na kuchelewa kwa Richmond kuanza kazi.

Sasa nauliza, huyu alieamua kumlaghai Raisi, alikuwa na nia gani? Je mtu huyu ni nani? anafanyiwa nini na Rais kwa kumlaghai Rais na kuruhusu kuingia Mkataba mbovu uliotugharimu pesa za kulipia mkataba na kukosekana kwa mapato kwa Taifa kutokana na uhaba wa umeme?

Je mlaghai huyu alikuwa na kiburi na nguvu gani bila woga kufanya alichofanya? Je Rais alipobaini kalaghaiwa, amefanya nini kisheria kwa huyu aliyemlaghai na kuhatarisha usalama wa Taifa letu?

Je mlaghai huyu na wenzake inawezekana waliamua kufanya ulaghai huu kutokana na kukosa heshima kwa Rais Kikwete na kujua kuwa Kikwete hana ubavu wa kufanya kazi na kuwajibisha? Je walaghai hawa inawezekana walifanya walilofanya kwa kushirikiana na Rais Kikwete?

Maswali ni mengi sana na hakuna majibu ya maana mpaka sasa. Kujiuzulu kwa Lowassa, Karamagi na Msabaha si suluhisho au sahihisho la makosa, uzembe, uhujumu na wizi wa mchana kweupe uliotokea.

Tunahitaji Rais Kikwete afanye kweli na si danganya toto. Afikishe waliomdanganya kwenye mkondo wa sheria na kutoa karipio kali na kuwanyanganya mafao na nafasi za kuendelea kutumia pesa za walipa kodi na wavuja jasho au akubali hadharani kuwa miaka yake miwili ya kwanza alikuwa amelala kwa makusudi akifanya majaribio ya kuwa Raisi!
 
Rais alidanganywa na wasaidizi wake? Au Alikubali aonekane kuwa anadanganywa?
Anazo 'resources' zote anazoweza kuzitumia kama angekuwa hataki kudanganywa!

Haya ya Richmond Kikwete aliyaelewa thika tokea mwazo wake, waandishi wa habari wasitafute njia za kusafisha uchafu unaoonekana wazi.

Kuna wanasheria gani tena zaidi ya hao wa Mwanyika ambao Lowasa atakuwa anawazungumzia. Mwanyika mwenyewe shasema wao walikuwepo tu katika vikao mbalimbali vya mkataba bila ya kufanya kazi ya kisheria.

Ni dhahiri kwamba baadhi ya yaliyotokea katika Richmond, yamekopwa toka IPTL. Wahusika walidhamiria kutumia 'model' ile ile ya IPTL. Ndio maana Lowasa anaonekana kutumia kesi ya IPTL kule London, ambako serikali ya Tanzania iliamua maksudi kubwagwa, na kuendelea kulipia mabilioni ya walalahoi kwa IPTL hata kama huduma haitolewi.

Hivi hawa viongozi bado kweli wanaamini Tanzania tutaendelea kuwa salama?

.......Mkuu Kalamu nakubaliana na wewe kwa saana tu,

hivi kweli kuna watu wanafikiri kuwa eti JK alidanganywa???!!!........

katika issue ya RICHMOND et al......hakuna cha coincidence wala kuteleza........mipango yake hufanywa sawia kabisa na ya KIGAIDI.......the one you feel/think SIYE kumbe NDIYE and kinyume chake
 
Wakuu naomba kuuliza, maneno ya Rais kudanganywa kuhusu Richimonduli, ameyasema yeye mwenyewe kwa mdomo wake, au ni kama kawaida ya waandishi wetu waliochipukia toka Lowassa ajiuzulu?

Maana sikuyaona kwenye ripoti ya Mwakyembe, au?
 
Mkuu Babah,

Heshima mbele, vipi hayo maandishi kama yapo yakiwekwa hap JF ili tuyaangalie kwa undani na kutoa hukumu? Mimi sijawahi kuyaona au kuiona hiyo ishu ya TVT mkuu, lakini naaamini kuwa kuna mwenye nayo hapa ayaweke tuchambue, maana sikatai kuwa yapo!
 
Mkuu Babah,

Heshima mbele, vipi hayo maandishi kama yapo yakiwekwa hap JF ili tuyaangalie kwa undani na kutoa hukumu? Mimi sijawahi kuyaona au kuiona hiyo ishu ya TVT mkuu, lakini naaamini kuwa kuna mwenye nayo hapa ayaweke tuchambue, maana sikatai kuwa yapo!


Mkuu FMES,
Haya toa hukumu sasa.




http://www.ippmedia.com/ipp/guardian/2006/12/21/80790.html


President speaks on Richmond

2006-12-21 08:46:47
By Guardian reporter


President Jakaya Mrisho Kikwete has categorically rejected allegations that the country’s power crisis has been mismanaged.

The President was speaking during an exclusive interview with The Guardian at the State House in Dar es Salaam.

”During my first speech (as President), I discussed fears about the looming drought, that we were going to grapple with food scarcity, after which I discussed the condition of power generation.

I gave a precaution on January 31, this year,” President Kikwete said.

Asked to comment about public complaints that the power crisis had been mismanaged, and if any heads were going to roll, the President said:” There is power rationing. The hydro-electric power dams are short of water.

So who has mismanaged the crisis? The Pangani Falls have inadequate water. Kidatu has inadequate water.

It cannot be a factor of mismanagement by a person� Let us pray to God for sufficient rains to fall.”

However, he said that if somebody was committing sabotage, then he would be dealt with.

The President then discussed the Richmond saga, and how the company had won a tender to generate electricity.

He said that due to the acute power shortage, while long term solutions were still in the pipeline, the government negotiating team was keen to apply short-term measures to deal with the problem and a tender was duly floated.

He said the government negotiating team had been looking for cheap power generation at a reasonable price and considerable conditions. There is only one company which offered that, he said.

The President further explained: ”There was a company whose condition was that their generators should be leased for five years.

But then I queried, suppose our power problems fizzle out in two years, does it mean that we are going to pay them for the remaining three years without using the generators? They refused,” the President said.

He added that Richmond was the only company that accepted to sell power to Tanesco at 4.6 cents. The power committee was convinced by the terms.

”On the other hand, Richmond turned out to be a small company with little capacity, and their hopes were that once they got the contract they could secure loans from the banks, which refused to do so,” he said.

”Gossiping started� that some people have been bribed, that there were sons of big wigs involved (laughter),” Kikwete said.

”If there is anybody who was bribed, it is not from the money we gave to Richmond. I blocked the payment to the company because I thought what if we gave them a down payment and they disappear with the money?” he said.

The President said that he told (Dr Ibrahim) Msabaha; ”if these people (Richmond) are contracted, they might disappear with the money and you will take a rope and hang yourself.

Don’t give them a down payment. Tell them that once they have brought the generators, we are going to pay them.”

Kikwete said that when things became difficult on the Government’s part, he was advised to revoke the contract.

”We stood firmly to say that the government would not accept it because by allowing them to pull out, it would amount to giving them a financial advantage,” President Kikwete said.

He said what remained was to press Richmond so that they could deliver.

The President said that if Richmond’s contract was revoked, they might have taken advantage to take the matter to court and seek redress from the government.

”The government has guarded itself to ensure that this does not happen,” he said.

President Kikwete said that the hiring of generators was a short term goal.

”We will buy our own power generating equipment so that once the hired ones are taken back by the owners, we shall find ourselves well equipped,” he said.

He said that the government had purchased a 100MW generator from Wartsila of Finland, which would be installed in July next year.

”Another 46MW generator to be stationed at Tegeta is being built by a Netherlands company,” he said.

He was optimistic that the power supply would significantly improve by next year after the plants had been commissioned.


SOURCE: Guardian
 
Mkuu Babah,

Ni vyema ukaacha lugha mbovu za chooni na huko kwenye vilabu vya gongo, hoja sio lazima iwe na abusive tone maana wote tunaweza kuitumia sio wewe unayeweza, hapa hakuna vijibaraka vya mafisadi kama vile ambavyo siamini wote ni lazima tuwe vijibaraka kama wewe vya upinzani, one thing ni kwamba huwezi kulazimisha hoja kama haipo ndio maan unahitaji kutumia lugha za chooni lakini ninaamini you know better kama nilivyokuonya in the past huwa sina tatizo na subira, mkuu Jf imejengwa kwa hoja za pande mbili sio moja tu kama unavyotaka wote hapa tuwe, sasa heshimu hilo mkuu hapa sio kilabu cha pombe mkuu! Msema njia mkuu ni lazima awe amewahi kuipitia kwa hiyo haya ya ujibaraka naona unayafahamu sana, au?

Nimeisoma hii article sioni mahali popote ambapo Rais anasema alidanganywa, mkuu KJ computer yangu kwa sasa kama kawaida imerushiwa virus kwa hiyo kuna functions siwezi kuzifanya ili kujadili ishus ninavyotaka, lakini itarekebishwa karibuni, lakini mkuu samahani labda unieleweshe kidogo ni wapi rais ametamka kuwa alidanganywa? Nilichoona ni kukubali kuwa alikuwa anazo habari za kinachoendelea na Richimond, lakini sikuona akisema kudanganywa, au?
 
Mkuu ninasema hivi hapa hakuna vijibaraka, kuna watu wazima wenye uchungu na taifa letu, lakini haina maana kuwa sasa tutaanza kumakamata kila mtu uchawi bila sababu za msingi, wala ukweli,

binafsi ninaomba kusema kuwa sijaona mahali kwenye hii article ambapo rais anasema kuwa alidanganywa, lakini huenda wengine ndivyo manvyooona, sasa siwezi kuendelea kubishana tuu hapana nitawachieni muendelee, unless kuna something else convincing zaidi ya hii article.
 
Phew! That is a damning article!
Knowing what we know now on Richmond, and what was said then, it is only for a die hard sycomphant who cannot see the picture.

Nadhani lile shairi la Mkjj - Kuwadi na mafisadi linajieleza lenyewe. Wengine tutaendelea kuwa 'aspiring' mafisadi hadi hapo wakati utakapowadia. Bahati mbaya kabisa kwa nchi hii ya waTanzania.
 
Mimi nilishaboeka, swali la alilosema Kikwete mwaka mmoja uliopita tuliliuliza wakati ule, inashangaza magazeti yanarukia mwaka mmoja baadaye!!! It is pathetic!
 
Hakuna hoja ya kudanganywa rais hapa, kwani inaonekana he was quite on top of the issue kabisa.

Kikwete said that when things became difficult on the government's part, he was advised to revoke the contract. We stood firmly to say that the government would not accept it because by allowing them to pull out, it would amount to giving them a financial advantage,"

The President said that "if Richmond's contract was revoked, they might have taken advantage to take the matter to court and seek redress from the government. The government has guarded itself to ensure that this does not happen." he said.

Hao wanasheria wa chuo kikuu wanaombishia Lowasa, sasa na watueleze kama bado wana mashaka na ushauri hawa wakuu wanavyodai walipewa. Richmond was meant to be a clone of IPTL, only the experiment failed miserably, kwa hasara kubwa.
 
Huku ni kuhujumu uchumi kabisa! Hiyo miaka miwili iliyobaki ni hatari, miaka mingine mitano na taifa litabaki na nini? Huwezi kuosha na mikono michafu..
 
Back
Top Bottom