Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,771
- 41,027
Hao wanasheria waliochambua hiyo mikataba yawezekana ndio mashujaa wasioonekana!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
"Kwa mujibu wa tangazo la zabuni la TANESCO, muda wa kukodi jenereta hizo
ulikuwa ni miezi kumi na mbili tu na ungeweza kuongezwa kutegemeana na hali
ya uzalishaji umeme nchini. Kamati ya Serikali ya Majadiliano iliongeza muda wa
kukodi mitambo hiyo kutoka miezi kumi na mbili mpaka ishirini na nne ambayo
itaanza kutumika rasmi baada ya uzinduzi wa mitambo (full capacity).
Kwa kuwa madhumuni ya Mkataba huu ilikuwa ni kuzalisha umeme wa dharura,
(Emergency Power Supply Agreement) Serikali ilipaswa kutilia maanani hali ya
uzalishaji umeme wa baadae ikiwa upatikanaji wa maji ungerejea katika hali yake
ya kawaida. Muda huo unafanya udharura wa mkataba huu utiliwe mashaka"
"Hata hivyo, utafiti wetu umebaini kuwa, Kampuni ya Richmond Development
Company LLC, ilitoa taarifa za uongo ( misreprestantion of its corporate status )
kuhusu uhalali wake kisheria wakati wa kuingia mkataba na TANESCO . [Tazama
Kifungu cha 5 cha Waraka wa Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO (Memorandum
for the TANESCO Board of Directors Concerning the Contract with Richmond
Development Company LLC)]
Kitendo hicho ni cha ukiukaji wa Mkataba kwa mujibu wa masharti ya Kifungu
12.1(g) cha Mkataba huo (i.e Event of Default) yanayotamka kwamba, Richmond
Development Company LLCitakuwa imekiuka Mkataba iwapo itatoa maelezo au
taarifa ambazo zitathibitika kuwa ni za uongo wakati zilipotolewa na ambazo
zinaathiri uwezo wa Kampuni hiyo kutekeleza majukumu yake yaliyoainishwa
katika Mkataba."
Aidha, kwa mujibu wa masharti ya Kifungu cha 12.3(c), Shirika la TANESCO
linayo haki ya kuvunja Mkataba huo kutokana na kitendo hicho cha Richmond
Development Companuy LLC cha kukiuka Mkataba.
Kwa ufasaha na uwazi zaidi, vifungu hivyo husika vya Mkataba vinatamka kama
ifuatavyo:-
12.1 Each of the following events shall become a supplier event of Default:-
(g) any statement, representation or warranty by the supplier in this Agreement
proving to have been incorrect, in any material respect, when made or when
deemed to have been made and such incorrect statement, representation or
warranty materially and adversely affects the suppliers ability to perform it
obligations under this Agreement.
12.3(c) TANESCO shall have the option, upon not less than 30 days prior written
notice, to terminate this Agreement on default and the supplier shall be entitled to
legal remedies as prescribed by the applicable laws.
Pamoja na TANESCO kuwa na haki ya kuvunja pia haki ya kulipwa fidia kwa
mujibu wa Kifungu cha 4.4 cha Mkataba, uchambuzi wetu umebaini kuwa
TANESCO haikuzitumia kabisa haki hizo.
Kamati Teule imepata bei za
mitambo kutoka kwa baadhi ya watengenezaji wa mitambo ya uzalishaji wa
umeme huko huko Houston Marekani kwa Kampuni iitwayo Kawasaki Gas Turbines
Americas. Mtambo mpya aina ya GPB180 wenye uwezo wa kuzalisha MWs
17.5 ni dola za kimarekani 7.5 milioni.
2. Iwapo TANESCO au Serikali iliweza kufungua Barua ya Dhamana ya Benki ya
thamani ya dola za kimarekani 30,696,598, je, fedha hizo zisingeweza kutosheleza
kununua mitambo mipya ya uzalishaji umeme, na mitambo hiyo
kubakia mali ya TANESCO, badala ya kuingia katika Mikataba ya ukodishaji
umeme?
Aidha, taarifa za watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini kwamba wakati wa
kipindi cha mchakato wa Zabuni ya umeme wa dharura kulikuwa na ugumu wa
kupatikana mitambo ya umeme wa dharura zimeonekana sio za kweli.
Ni ukweli kwamba kulikuwa na ukame, lakini ukame huo haukuwa wa majenereta
kwani majenereta hutengenezwa muda wote na sio kwa kutegemea mvua.
Aidha, utafiti wetu umebaini kuwa katika kipindi hicho cha matatizo ya umeme
nchini Kampuni hiyo ya Kawasaki ilikuwa na mitambo 8 ya kisasa tena ile yenye
kutumia gesi na dizeli (dual fuel plant). Mitambo hii pia ina uwezo wa kusukuma
maji na hapo hapo kuzalisha umeme. Na hii bei ya dola 7.5 miliono kwa mtambo
mmoja ni bei ya kuanzia tu kwani mteja anaweza kupunguziwa. Ushahidi wa hili
ni kwamba Serikali ya Nigeria mwaka huo 2006 iliuziwa mitambo hiyo kwa dola
6.7 milioni kwa mtambo mmoja.
Nijulisheni basi kama huu mziki umewakolea ili wengi zaidi washaurike kuusikiliza.........
Kumbuka kuwa hawa jamaa watatu waliweza kupitia mikataba hiyo sita ndani ya siku saba na kuichambua kama vile mtu anavyochambua mchele na chuya!
9.3.6 Kwa kuzingatia kuwa Mikataba mibovu kati ya TANESCO na Makampuni mbalimbali
ambapo Makampuni hayo yanalipiwa kodi yote na TANESCO imekuwa ni chanzo cha
bei kubwa za umeme katika nchi yetu, na kwa kuzingatia kuwa Mikataba hiyo inasababisha
Sera muhimu za Taifa, kama vile, Sera ya Kupiga vita Umaskini, Sera ya Huduma
Bora kwa Jamii, Sera ya Taifa ya Nishati inayolenga kusambaza nishati ya bei nafuu vijijini
n.k. kutotekelezeka, tunashauri kuwa Mikataba hiyo ipitiwe upya ili irekebishwe,
kwa maslahi na manufaa ya Taifa letu.
9.3.7 Mwisho, kwa kuzingatia ukweli kwamba, Mikataba hiyo mibovu, kwa kiasi kikubwa inadidimiza
uchumi wa nchi yetu, tunapendekeza Serikali ichukuwe hatua muafaka zinazofaa
ili kuondoa hali hiyo ambayo inalipeleka Taifa letu shimoni.
tuwekeeni basi huo wa EPA, naona huo utavunja rekodi ya THRILLER kwa mauzo. ila huu wa sasa hadi nimechoka pumzi zote zimeniisha, mapigo yangu ya moyo yanaenda kwa kasi ya ajabu, kweli mimi kama kijana wa kitanzania nimeshindwa kupata maneno ya kueleza ni jinsi gani najisikia hivi sasa, machozi yananilenga lenga, i feel hopeless kuishi katika nchi hii, nasita kuanzisha familia kwenye ardhi hii iliyo jaa neema, nikihofia fate ya mambo haya, najionea huruma nawaonea huruma vizazi vinavyoendelea kukua na vinavyokuja, lakini kuna sauti ndani inaniambia dont lose faith, huu ni wakati wa mpito, jisikie faraja kuishi wakati mambo haya yanatokea kwani kuna wengi waliziota siku kama hizi lakini hawakupata kuziona, mmoja wapo alikuwa ni baba yangu (RIP)
Hivi mnaona fahari gani kuweka mambo ya siri hadharani namna hii? Hii ripoti ilikuwa ni kwa ajili ya kamati teule, nyinyi sijui mmefanya nini mkaipata. Kwa kweli hamuisadii serikali kwa kuweka mazungumzo nyeti kama haya hadharani. Nakubali inaonesha jinsi gani wanasheria wetu walivyo wadhaifu katika mambo ya mikataba, lakini hii peke yake si sababu tosha ya kuweka ripoti nzima kwenye mtandao.
Natoa ushauri, kuna mambo mengine msithubutu kufanya hivi mnakaribisha matatizo. Niliwaonya mapema kuhusu JF mkadhani ninawatania. Mnaweza kuwa nguvu ya mabadiliko lakini wakati mwingine ni hapa JF panapohitaji mabadiliko.
asante.
Hivi mnaona fahari gani kuweka mambo ya siri hadharani namna hii? Hii ripoti ilikuwa ni kwa ajili ya kamati teule, nyinyi sijui mmefanya nini mkaipata. Kwa kweli hamuisadii serikali kwa kuweka mazungumzo nyeti kama haya hadharani. Nakubali inaonesha jinsi gani wanasheria wetu walivyo wadhaifu katika mambo ya mikataba, lakini hii peke yake si sababu tosha ya kuweka ripoti nzima kwenye mtandao.
Natoa ushauri, kuna mambo mengine msithubutu kufanya hivi mnakaribisha matatizo. Niliwaonya mapema kuhusu JF mkadhani ninawatania. Mnaweza kuwa nguvu ya mabadiliko lakini wakati mwingine ni hapa JF panapohitaji mabadiliko.
asante.
Hivi mnaona fahari gani kuweka mambo ya siri hadharani namna hii? Hii ripoti ilikuwa ni kwa ajili ya kamati teule, nyinyi sijui mmefanya nini mkaipata. Kwa kweli hamuisadii serikali kwa kuweka mazungumzo nyeti kama haya hadharani. Nakubali inaonesha jinsi gani wanasheria wetu walivyo wadhaifu katika mambo ya mikataba, lakini hii peke yake si sababu tosha ya kuweka ripoti nzima kwenye mtandao.
Natoa ushauri, kuna mambo mengine msithubutu kufanya hivi mnakaribisha matatizo. Niliwaonya mapema kuhusu JF mkadhani ninawatania. Mnaweza kuwa nguvu ya mabadiliko lakini wakati mwingine ni hapa JF panapohitaji mabadiliko.
asante.
Hivi mnaona fahari gani kuweka mambo ya siri hadharani namna hii? Hii ripoti ilikuwa ni kwa ajili ya kamati teule, nyinyi sijui mmefanya nini mkaipata. Kwa kweli hamuisadii serikali kwa kuweka mazungumzo nyeti kama haya hadharani. Nakubali inaonesha jinsi gani wanasheria wetu walivyo wadhaifu katika mambo ya mikataba, lakini hii peke yake si sababu tosha ya kuweka ripoti nzima kwenye mtandao.
Natoa ushauri, kuna mambo mengine msithubutu kufanya hivi mnakaribisha matatizo. Niliwaonya mapema kuhusu JF mkadhani ninawatania. Mnaweza kuwa nguvu ya mabadiliko lakini wakati mwingine ni hapa JF panapohitaji mabadiliko.
asante.