mbu wa dengue
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 8,860
- 11,554
Sheikh Ilunga ni yule wa mombasa?Sheikh Ponda ni kama sheikh Ilunga(Mola amjaalie pumziko jema) wote wanapigania maslahi ya waislamu wenzao.
Hawa masheikh ubwabwa ni wapuuzi tu.
Huna loloteMimi kinachoniuma Sheikh Kipozeo yupo Bakwata!
Huwa napenda kuangalia clip zake japo mi mkatoliki
Sheikh Ponda anajielewa sana yule Baba.Mungu ampe maisha marefu.
WamekandamizwajeKama ni upande unaotoa haki hakuna shida ila kama sio haki Wakristo wote wanajua watampa LISSU mtetezi wa haki hao hawana cha kuambiwa. Tatizo ni waislamu wamekandamizwa miaka 10 sasa na bado wamelala tu.
We umesikia padre gani kawekwa mahabusu hata siku moja tu eti ni gaidi au kamsema vibaya serikali. Waislamu amkeni mmelemazwa Sana na BAKWATA. Sisi Wakatoliki Magufuli tukimuita tu anakuja fasta.
mapico naheshimu sana mawazo yako kaka ila kwa hili la zanzibar kuhusu kuwatesa wakiristo kipindi cha mfungo sio kweli,kuna maeneo maalum yamewekwa kwa ajili ya watu kupata chakula ,kula hadharani kwa watu waliofunga ambao asilimia 98% ni waislam hii ni kuwadhihaki na kutoiheshim imani yao."No one is right no one is wrong."
mdai na haki zenu basi kuhusu yale magaidi ya kibiti wengi walikuwa wa upande wa Dini yenu.
Zanzibar kipindi Cha mifungo mmewatesa Sana wakristo.
mtafikiri hii Dunia ni ya kwenu mtu asile kisa mmefunga yani mnapiga kelele basi tu ila nyie watu mnachokipiganiaga sijui haki
haki gani mnajikutaga wajuba kumbe nyie ndiyo makafiri no #1
Tiini mamlaka zilizopo Duniani maana Mungu amezikubali nyakati hizo kwa wakati wake .
najua kuna wakati mnatamani hata shekhe ponda ndiyo awe rais lakini hilo haliwezekani mifumo ya nchi inahitaji msawazo(balance) kwa watu wote na Mungu humpa amtakaye sio mnayemtaka nyinyi .
mnapiga kelele Bakwata je kipindi cha mrisho mbona hakuwapa hizo haki zenu kama mjumbe kutoka kwenu.?
Uislamu ni Unyenyekevu na Usafi
wizi ,Ugaidi, maandamano, na machafuko yasitajwe kwenu.
Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
Ona sasa,kwa mfano huyo Lipumba asingerekodiwa ina maana ungekataa kuwa Lipumba hakuwahi kumpigia kampeni Kikwete kwa sababu hakuna video kumuonesha Lipumba akifanya hivyo. Na hapo ndipo lilipo tatizo,kwa sababu mfano huku misikitini yanatokea mengi tu ila hayarekodiwi hata huyo Lipumba mara nyingi tuanafanya siasa msikitini ila hakuna video wala audio.Havihitaji ubishi kivipi?! Haiwezekani uongee jambo halafu uombwe ushahidi, badala ya kutoa ushahidi unaishia kudai "mbona unataka tubishane"!
Lipumba kwa mfano, mbona video ilipatikana akikiri kumsaidia JK kwenye uchaguzi wa 2010, tena huko huko misikitini? Kwanini ya Ponda isiwepo na badala yake unataka tukubaliane na madai yako yasiyo na ushahidi!!
Ile hoja yako uliyoing'ang'ania kama luba kiasi kwamba kila siku lazima uwe unaisema kwamba TL alisema ACT sio chama cha upinzani, mbona huwa unawekaga ushahidi?!
In short, hujui what happened in 2010! Kwa bahati mbaya, nami siwezi kusema kwa sababu nisingependa kufukua makaburi katika kipindi hiki ambacho watu wameshikana!!
Ukitaka kujua what happened in 2010, do your home work kutafuta Waraka wa Maaskofu wa RC ambao baadae waliukana, na pia Waraka wa Shura ya Maimamu (akina Ponda) ambao na wenyewe kama ilivyo sasa, BAKWATA wakaukana na kusema huo sio Waraka wa Waislamu!!!
Naona unajizungusha tu na hii ni kwa sababu siku hizi imekuwa tatizo sio ccm bali Magufuli.Kila kitabu kina kurasa zake.
Isitoshe kipindi hicho Ccm ilitumia ajenda ya udini dhidi ya mgombea wa Chadema Dr Slaa ili kuvuna kura za waislamu na ndio kina Ponda walitumika.
Kwa sasa mazingira ya kisiasa yamebadilika, ndio maana hata Gwajima aliyekuwa anaiunga mkono Chadema hadharani sasa ni mgombea wa Ccm.
Kama Ponda hakuwa sahihi kumuunga mkono JK 2010 basi hata Gwajima hayupo sahihi maana 2015 aliwaunga mkono Chadema.
Ndio maana nasisitiza '' kila kitabu kina kurasa zake"
Upo nchi gani ndugu, unajifanya huelewi kabisa kama vile umeweka pamba masikioni. Ngoja nikujibu hapa hapa.1) Mzee Said unataka kusema kwamba waislamu wakimchagua Lissu mgombea alienadiwa na Ponda ndio matatizo ya waislamu yataisha, au huyo mgombea atakuwa sababu ya waislamu kuingia peponi?
2) Kwa mwendo huu wa Ponda kuwaambia waislamu wamchague Lissu akitokea kiongozi anaekubalika na wakristo wengi nae akasema wakristo wamchague JPM, huoni kwamba tunaelekea kuligawa taifa kidini?
Natanguliza shukran zangu kwako Mzee wetu Said wa jukwaa la history.
Kafir ni neno la kiarabu lenye maana ya mpingaji. Katika muktadha wa dini ya kiislamu, kafir ni yule anayepambana kuupinga uislamu hususani kwa njia za hila na udhalimu. Uislamu hauna tatizo na uwepo wa dini zingine au uwepo wa ubagani, maana dini hizo zilikuwepo na zitaendelea kuwepo regardless ya uwepo wa uislamu.Mkuu Zanzibar-ASP , ungeweza kujenga hoja yako bila kutumia lugha ya maudhi ya kuwaita watu makafir!. Kwa mujibu wa Waislamu, Kafir ni mtu asiye na dini, sasa kwa vile serikali yetu haina dini, ni haina dini kwa maana ya a secular state na sio haina dini kwa maana ni kafir, tena jina kasir lina bado connotation meaning ukisema kafiri, Wakiristo tunakasirika kama unamaanisha ni ya Mwenyeenzi Mungu ni Islam tuu, nje ya hapo, wote ni ma makafiri!.
This is not a fair comment!,
P
Ni vizuri umetambua hilo.Naona unajizungusha tu na hii ni kwa sababu siku hizi imekuwa tatizo sio ccm bali Magufuli.
Wafanye tu ndiyo demokrasiaSasa Mzee wangu, ikitokea Wakatoliki au walutheri au wakristo wote kwa ujumla wakatangaza kura ni kwa flani(upande tofauti na aliochagua sheikh wako) kama alivyofanya Sheikh Ponda unadhani nini kitatokea baada ya matokeo!?
Mkuu nichangie kidogo. Bakwata wao watangaze hadharani na mufti wao eti mitano tena. Akija huyu akisema mitano kwanza ndio nongwa. Nahisi wanaogopa km Tundu Lissu akichukua nchi wao na familia zao watakua hawana vibarua wachumia tumbo hawa.SAKATA LA SHEIKH PONDA: MASIKINI "MASHEIKH RASMI" HAWAJUI KUWA HAWANA WAISLAM WANAOWAONGOZA, WAKO PEKE YAO
Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.
Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.
Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.
Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.
Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.
Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.
Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.
Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.
Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.
Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.
Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.
Hakuna.
Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.
Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.
Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.
Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.
Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.
Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.
Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."
Chunguza.
Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.
Nimekosoma vyema na kukuelewa vizuri. CCM ndio adui mkubwa wa nchi yetu, anapenda kutugawa ili aweze kututawala. Kwa sasa mpango ni mmoja tu, watanzania tunapaswa kuweka tofauti zetu za kidini, kiitikadi au kikabila pembeni, tuwe kitu kimoja ili tuitoe CCM madarakani. Baada ya hapo tufanye maridhiano, tujenge upya mifumo yetu.Serikali ya ccm haiwezi kukwepa lawama hii ya kuliingiza taifa kwenye mpasuko mkubwa sana.
Kuna vitu mmevilea na sasa vinataka kulivuruga taifa.
Naona mpambano wa "wakristo"(waprotestanti) wakiungana na waislamu dhidi ya mfumo wanaoamini ni "mfumo katoliki".
Nikitazama kauli za viongozi wengi wanoheshimika wa madhehebu ya kiprotestanti na uislamu,ndani ya miaka hii 5 wamekuwa very negative na uongozi uliopo.
Na mwenendo wa kampeni hivi sasa unadhihirisha mpasuko huu.
Sikuwaza kabisa kuwa huenda uchaguzi huu ukawa mgumu hivi!
Haya mazimwi mliyatengeneza na kuyatumia dhidi ya upinzani miaka ya nyuma,sasa yanataka kuwatafuneni wenyewe.Mungu atunusuru,yawatafune peke yenu na kutuachia taifa letu salama.
Ila namtahadharisha Lissu asiingie makosa ya wakina Mzee wetu (namheshimu sana) Nyerere.
Viongozi wengi wa taifa hili wamekuwa wakitumia makundi fulani yenye nguvu (kama ukristo au uislamu) kisiri kupata majority.Halafu baada ya kupata uongozi wanayaswaga makundi hayo na yanawaletea shida baadae.
Mfano mzuri ni Nyerere na waislamu waliomsaidia sana wakati wa kupigania uhuru wa nchi.
Hadi leo vilio vya waislamu hao bado vipo,mwandishi wa uzi huu ni mfano mzuri.Makala zake nyingi zinajieleza zenyewe.
Kama Lissu anasimamisha sheikh kumuombea kura za waislamu,aelewe kuwa atakapopata kiti cha urais,ana deni nao na anapaswa kudeal nalo bila kuathiri wale wengine.
Kwa ufupi atakumbwa na mtihani wa kuunganisha taifa kutoka katika makundi ambayo yeye pia amefaidika nayo.
Hili ni suala gumu,Lissu pamoja na Magufuli,yeyote atakayeshinda uchaguzi huu,anapaswa kuhakikisha kufikia 2022 makundi haya either yameungana au yanaheshimiana na kukubaliana kwa amani na pia kuanzia 2025 watanzania wahamasike kupiga kura kama watanzania,na sio kama waislamu,wakristo,wasukuma,wachaga,maskini,matajiri etc.
Ila kwa hili ccm mtuombe msamaha,mmetutia kwenye wakati mgumu kama taifa.Haikuwa lazima kutufikisha huku na muda wa kutosha mmekuwa nao madarakani.
Kwani hawajatangaza bado? Hivi Askofu kwenda kwenye kampeni za Magufuli na kutangaza huyu ndio anayefaa kuchaguliwa, si ndio Kama alivyofanya Ponda?Sasa Mzee wangu, ikitokea Wakatoliki au walutheri au wakristo wote kwa ujumla wakatangaza kura ni kwa flani(upande tofauti na aliochagua sheikh wako) kama alivyofanya Sheikh Ponda unadhani nini kitatokea baada ya matokeo!?
Umetoa mada nzuri sana. Labda kwa kuongezea, waislam wa Tanzania kwa muda mrefu wamekuwa wakiongozwa kama ng'ombe. Ng'ombe ukiwatia kwenye zizi moja ni rahisi kuwadhibiti.SAKATA LA SHEIKH PONDA: MASIKINI "MASHEIKH RASMI" HAWAJUI KUWA HAWANA WAISLAM WANAOWAONGOZA, WAKO PEKE YAO
Awali ya yote mimi sitajiingiza katika propaganda za uchaguzi bali nitajaribu kueleza hali ya Waislam ilivyo.
Kwanza ni kuwa Waislam toka ilipovunjwa EAMWS na serikali mwaka wa 1968 na Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir kukamatwa na kufukuzwa nchini na serikali kuwaundia Waislam BAKWATA, Waislam wameishi na kinyongo miaka yote sasa inafika nusu karne.
Ndiyo unasikia lugha za "sheikh wa BAKWATA," Waislam wakijiweka mbali na BAKWATA.
Na ukweli ni kuwa BAKWATA haijaweza kukubalika na sababu ni ndogo kuwa si taasisi iliyoundwa na Waislam wenyewe.
Matokeo yake ni kuwa katika hii jamii kubwa ya Kiislam Waislam wana viongozi wao wanaowakubali, kuwaamini, kuwapenda na kuwasikiliza wanachowaambia.
Sheikh Ponda ni mmoja wa masheikh hawa.
Sheikh Ponda amewaeleza Waislam nani adui ya Waislam wa Tanzania na akasimama kupambana na adui huyu huku akiungwa mkono na Waislam wengi sana.
Katika juhudi hizi Sheikh Ponda kakutwa na shida nyingi.
Kalipa kwa ajili ya Allah kwa machozi na damu.
Kwa damu yake na machozi ya nduguze Waislam.
Nimeweka hapa FB makala fupi ya maisha ya Sheikh Ponda katika kuwatumikia Waislam sasa mtafute sheikh yeyote wa BAKWATA ambae amepata kusimama na Waislam katika dhiki na shida zao.
Hakuna.
Katika hali kama hii ni tabu sana kujaribu kumchafua sheikh kwa propaganda hizi za uchaguzi kwa kuwa Waislam wanamjua Ponda ni nani.
Ponda anawakilisha sauti ya Waislam wengi, wengi, wengi sana.
Wako waliotambua hili na wamejua nini wafanye waweze kupata kura za Waislam.
Hawa ni watu wenye kufikiri na kukubali ukweli kuwa Waislam wanaishi na kinyongo dhidi ya utawala kwa miaka mingi.
Hawa wametumia fursa hii kwa kuhaidi kutoka haki na fursa sawa kwa wote.
Ndiyo maana hujasikia Waislam wamefanya maandamano kumpinga Sheikh Ponda.
Wanaompinga Sheikh Ponda si masheikh bali ni "masheikh wa BAKWATA."
Chunguza.
Picha: Kulia ni Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir (1880 - 1979) na kushoto ni Sheikh Issa Ponda.
Madaraja ni sehemu ya maisha na hayakuja kuondoka ili watu wote tulingane,Cha msingi pambania maisha yako achana na siasa uchwara.Hata hao unaowapigania waingie madarakani nao wanatembelea VX na wana maisha mazuri,Ila Shida yao ni wanafiki.Maisha yataacha kwenda kwako wakati unatembelea VX la serikali? Maisha yanakwamaje kwako kwa mfano?