Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

Sakata la uchaguzi: Pesa kwenye damu

SIMULIZI HAPA ITAENDELEA na tutakuja kuimaliza mpaka mwisho kabisa ila kwa wale wenzangu na mimi ambao huwa hatuna uvumilivu sana.

WhatsApp nakupa kwa 2500 tu tuumalize mwezi vizuri nikupe kitabu chake kwa softcopy au ukihitaji vipande vyote 94.

0745982347

0621567672 (WhatsApp)

Zote FEBIANI BABUYA.

Unaweza ukalipia ukaisoma yote kwa wakati mmoja au ukasubiri hapa hapa mdogo mdogo.


Good morning.

Tchao.
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MOJA
“Una maanisha nani na kwa sababu ipi?” swali lake liliashiria kwamba alikuwa anaulizia mtu ambaye alitakiwa kuishi kwenye sura yake na kwa sababu ipi mpaka awe huyo mtu.

“Mr Oscar” baada ya jina hilo kutajwa raisi alihema na kutikisa kichwa akiwa anasikitika, mzee huyo alikuwa mbele ya muda kwenye suala zima la kufikiria, alijiona mwamba sana kuwa na mtu mwenye akili kama huyo kwenye mkono wake hivyo alitaka kuelewa sababu ya msingi hasa ilikuwa ni ipi?

“Haujanipa sababu”

“Kosa ambalo Mr Oscar amelifanya kwa miaka yake ya uongozi na hata sasa ni kuamini kwamba yeye ni mtu mwenye nguvu kubwa sana na anaweza kufanya lolote ndiyo maana hata siku ile ulisema kwamba anaanza kukutishia kwa sababu aliamini kwamba anaweza kukuendesha hata wewe bila kukujua kiundani. Lakini ni kwamba vijana wake wengi ni vijana wetu hivyo ni suala la muda tu tukihitaji kumdondosha chini pale uingie wewe”

“Hiyo inahusiana vipi na mimi kuachia madaraka”

“Nadhani unakumbuka kwamba Mafupa siku kadhaa nyuma alikutana na mr Oscar na kuomba msaada wa kusaidiwa kwenye uchaguzi?”

“Hilo nalijua ndiyo”

“Sasa kwenye hayo makubaliano alimpa sharti Mafupa kwamba akiingia madarakani anatakiwa kufanya kazi chini yake hivyo yule atakuwa kama raisi kivuli tu ila nchi itakuwa inaendeshwa na mr Oscar. Sasa vipi kama wewe ukiwa mr Oscar ukawa unamuendesha mtu ambaye yupo madarakani kama unavyotaka mwenyewe na akafanya yale ambayo wewe unayahitaji kwa muda ambao unautaka wewe?”

“Hahahaahah hahaha” raisi alicheka sana huku akiwa anapiga makofi kwa furaha, ni michezo ya akili ambayo ilikuwa inatakiwa hapo. Maana raisi huyo kwa mambo ambayo alikuwa ameyafanya kwenye uongozi wake, viongozi wengi hususani wa vyombo vya usalama hawakuwa wakimkubali sana na huenda siku moja wangekuja kumuanika mabaya yake hivyo huo ushauri ulikuwa unamuweka nje ya mchezo mazima na angeendelea kula mema ya nchi kwa utulivu pasipo kuumiza kichwa huku misala yote akimuuzia mwenzake ambaye alitakiwa kuingia madarakani wakati huo.

“Itakuwa hivyo mheshimiwa, halafu kwenye hiyo frash kuna mazungumzo yao yote juu ya waliyo kubaliana lakini pia kuna historia nzima ya maisha ya mr Oscar na Mafupa mwenyewe”
“Maana yake mr Oscar anatakiwa kufa haraka sio?”

“Ndiyo mheshimiwa”

“Hahahahahaha hahahha nabaki na yule mwanamke wake pamoja na binti yake ambaye kamficha kwa muda mrefu sana”
“Kitu cha kusikitisha ni kwamba yule sio binti yake”

“Whaaaat?”

“Yule ni binti wa mwanamke ambaye yeye aliwahi kumpenda sana lakini baada ya kujichimbia kwenye siasa alikuja kupotea muda fulani alipo enda kwenye majukumu ya nje ya nchi wakati anarudi alimkuta mwanamke yule amezaa na mtu mwingine na wakati ule mtoto alikuwa ni mchanga na kwa bahati mbaya sana tangu mwanamke yule aweze kujifungua alisumbuliwa na magonjwa ambayo yaliuchukua uhai wake hivyo kwa sababu alikuwa na mapenzi mazito sana na mwanamke yule aliamua kumlea yule mtoto kama wake na anampenda kuliko kitu chochote kile huenda ni kwa sababu hana uwezo wa kuzaa”

“Kuna mwingine anaye lijua hili jambo?”

“Hapana mheshimiwa”

“Fanya kama hakuna kilichowahi kutokea na lisije likatoka kwa mtu yeyote yule. Nitakapokuwa tayari nitakupa taarifa hivyo jiandae maana wewe unatakiwa kubaki Ikulu hapa kwa namna yoyote ile ili yule mpuuzi kama akiingia hapa afanye kile ambacho nataka mimi” mheshimiwa alionekana moja kwa moja kuridhia ushuri huo wa mshauri wake kwani aliona ni ushauri mzuri sana na unao faa, angekaa sehemu akiwa anayafaidi mema ya nchi huku akimuuzia misala mwenzake ambaye yeye alikuwa anafikiria pesa tu huku wenzake wakiwa wanafikiria pesa kwa kuitawala akili ya mtu ambaye anaweza kuziwezesha hizo pesa kwanza.

“Sawa mkuu hilo nitalifanyia kazi mapema sana”

“Unaweza kwenda” Raisi alimruhusu mzee huyo aweze kutoweka ndani ya hilo eneo.

Tommy baada ya kutoka ndani ya kituo kikubwa cha polisi aliweze kurudi tena hospitali kuweza kujua hali ya baba yake kwani mara ya mwisho baada ya kumfikisha tu mzee huyo haspitali alikamatwa na kupelekwa kituoni ambako aliishia kuua polisi wawili ambao walikuwa wakimtesa tena mbele ya IGP. Kurudi kwake ndani ya hospitali ni kwa sababu alikuwa anahitaji kuweza kupata majibu ya ile oparesheni ambayo baba yake aliweza kufanyiwa.

Alikuta madaktari hao wamemaliza kazi na huenda walikuwa wanamsubiri ni yeye tu, majibu ambayo walimpatia yalimkatisha tamaa sana. Baba yake alikuwa ametolewa risasi kwenye mwili wake na kuondolewa kwenye hali ya hatari ambayo huenda ingeyachukua maisha yake ila kitu cha kusikitisha ni kwamba mzee Apson alikuwa amepata koma na angekaa kitandani huenda kwa miaka yake yote ambayo angekuwa hai labda kama ungetokea muujiza wa Mungu ndipo angeweza kupona na kurudi kwenye hali yake ya kawaida tena.

Tommy aliingia ndani ya hiyo wodi kumuangalia baba yake, mzee huyo alikuwa amelazwa kwenye kitanda huku akiwa anapumulia mipira, alisikitika kwa sababu kulikuwa na uwezekano baba yake kuyatumia maisha yake yaliyokuwa yamebakia akiwa juu ya hicho kitanda. Alikuwa anakumbuka mbali sana namna baba yake alivyokuwa mtu bora na baba bora sana kwa familia yake, alikuwa anaukumbuka ule ucheshi na utani wa baba yake, alikaa kwenye kiti akiwa anamwangalia kwa uchungu sana mwanaume.

Alikuwa anawaza mambo mengi sana kwenye kichwa chake lakini baadhi ya mambo ambayo yalikuwa yanamuwazisha kichwa ni kwamba mpaka wakati huo hakuwa amempata dada yake je angeanza vipi kutoa taarifa zingine hizo za baba yake kuwa kwenye hiyo hali kwa mama yake mzazi? Kilikuwa ni kitu ambacho kisingewezekana kabisa hivyo alitakiwa kwanza kumtafuta dada yake na kama angefanikiwa kumpata basi ndipo angetakiwa kumtaarifu mama yake kuhusu suala la baba yake huku akiwa amemrudisha Patrina nyumbani.

Hilo ndilo lilimkumbusha kwamba hakuwa na muda wa kulala wala kupoteza kwani usiku huo huo alitakiwa kumtafuta dada yake haraka sana hivyo akaitoa simu yake na kuwapigia walinzi ambao walikuwa wanashughulika na hiyo kesi ya dada yake tangu mchana wa siku hiyo. Baada ya kupewa maelekezo yote kuhusu mtu ambaye walimhisi lakini na hatua zote ambazo walikuwa wamezichukua, mwanaume aliamua kwanza kwenda kwenye kampuni ya urembo ya dada yake ambapo alikagua kila kitu mpaka zile cctv kamera za mle ndani kisha akatoka na kuelekea Upanga nyumbani kwa akina Noelia mwanamke ambaye alikuwa ndie rafiki mkubwa wa Linda au Patrina.

Baada ya kufika ndani ya hilo eneo mwanaume alishuka na kugonga geti ambapo ilichukua muda sana mpaka mlinzi kuweza kufungua geti hilo, baada ya kujitambulisha alikaribishwa mpaka ndani ambapo alikutana na bibi pamoja na mjukuu wake wote wakiwa sebuleni na mambo yao ila iliwalazimu kuweza kumsikiliza. Kwa Noelia ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza kabisa kuweza kumuona mwanaume huyo kwenye maskio yake ambaye sifa zake nyingi alikuwa akizisikia tu kwa dada yake, na alikuwa akivutiwa sana na mwanaume huyo kwa sababu alikuwa na mwonekano mzuri sana isivyokuwa kawaida.

“Shikamoo bibi” alimsalimia bibi huyo huku akiwa anampa mkono Noelia na binti alibakia ameushikilia tu huo mkono kana kwamba hakuwa akihitaji kuuachia kabisa.

“Marahaba mjukuu wangu karibu sana”

“Nadhani utakuwa haunifahamu ila mimi ni mtoto wa Apson Limo” alijitambulisha mbele ya mwanamke huyo mzee ambaye aliishia kutabasamu.

“Kwa mtu ambaye yupo makini na macho yake basi hauna haja ya kujitambulisha mbele yake kwani unafanana sana na baba yako, jisikie upo nyumbani”

“Samahani sana bibi kwa kuwasumbua na usiku wote huu ila sina namna kwani jambo hili ni mhimu sana kwa upande wangu na familia, mimi kidogo sikuwepo nchini na baada ya kurudi ndo nakutana na hali kama hii ambayo inaendelea, imenifanya nisiwe na namna zaidi ya kufanya hivi”

“Usijali mjukuu wangu naelewa nini maana ya maumivu ya familia hivyo unacho kifanya upo sahihi kabisa” bibi huyo baada ya kumjibu hivyo ni kama alikuwa nampa ruhusa ya kumhoji mtu wake na hicho ndicho ambacho alikifanya

“Nina imani utakuwa na taarifa zozote kuhusu kupotea kwa dada yangu. Nimesikia mchana umefanikiwa kuwaeleza walinzi baadhi ya taarifa ambazo kwa namna moja ama nyingine zimesaidia sana lakini una uhakika kwamba hakuna kitu hata kimoja ambacho ulikisahau?” sauti hiyo ni kama ilimshtua Noelia maana muda wote alikuwa akimkadiria sana mwanaume huyo.

“Hapana mimi nina muda mrefu sana sijawasiliana naye kwa sababu nilitakiwa kusafiri hivyo sijakutana naye wala kuwasiliana naye kwa muda na kile ambacho nimewaeleza ndicho ambacho nilikuwa nakifahamu tu”

“Ushawahi kumuona labda anagombana na mtu au kujibishana na mtu vibaya?”

“Hapana hajawahi kuwa mtu wa hivyo hata siku moja”

“Wewe ni kipi ambacho unakijua kuhusu kupotea kwake?”

“Hakuna ninacho kijua”

“Unaweza ukaniazima simu yako?” swali la Tommy lilimfanya mwanamke huyo kuonyesha mashtuko wa wazi kwani hata Tommy aliuona kwenye macho yake, alifanya hivyo makusudi kwa sababu aliambiwa kwamba mwanamke huyo ilionekana kabisa kwamba kuna mambo alikuwa anayaficha na huenda anajua ukweli au kuna taarifa anazo ambazo hakuhitaji watu hao waweze kuzipata”

“Simu yangu nilikuwa nachezea imeisha chaji kwa sasa labda mpaka niichaji” jibu lake ndilo ambalo lilionyesha moja kwa moja kwamba ni kweli kuna mambo ambayo alikuwa anayajua mwanamke huyo. Tommy hakuongea kitu zaidi ya kubaki amemkazia macho tu kwa muda kisha akayarudisha tena kwa bibi na kuweza kumuaga.

“Bibi asante sana kwa kunikaribisha nyumbani, nina imani ipo siku nyingine tutaonana tena, nawatakieni usiku mwema” mwanaume aliaga ghafla sana kitu ambacho hata bibi huyo na Noelia mwenyewe kiliwashtua maana walihisi huenda anaweza kuendelea kuuliza maswali mengine hata bibi huyo alianza kuhisi kwamba labda huenda mjukuu wake anajua kitu maana alikuwa anatoa majibu ambayo ni wazi yalionyesha hakutaka kabisa kutoa ushirikiano wakati huyo alikuwa ni rafiki yake kabisa wa karibu.

Mwanaume baada ya kuaga alitoka mpaka nje ya geti kisha mlinzi akafunga geti hilo, Tommy aliiangalia saa yake, ulikuwa unasoma mshale was aa nane ya usiku, alitikisa kichwa chake kama kukubali jambo. Alisimama nje ya hilo geti kwa dakika tano kisha akaanza kuondoka huku akiwa ameiacha gari yake hilo eneo na haikujulikana kama ilikuwa ni kwa bahati mbaya au kwa makusudi. Alikuwa anatembea taratibu sana kama mtu mwenye mawazo ila ni kama vile kuna mtu ambaye alikuwa akimsubiri hilo eneo huenda ndiyo sababu aliamua kuiacha gari yake ambayo alikuja nayo. Mwendo wake ulikuwa unazidi kumsogeza mpaka alipofika mita kama miatatu kutoka nyumbani kwa akina Noelia ndipo aliposimama baada ya umeme kukatika ghafla.

Ishirini na moja naweka nukta hapa.

Wasalaamu,

Febiani Babuya.
 
Yaani namaanisha aligombana vipi na utawala wa Jf kama ulivyo sema?
Stori ndefu ila alipata umaarufu mkubwa kuliko JF yenyewe na hivyo aliweza kufungua magroup ambaye wana JF ndiyo walikuwa members wake, na pia aliweza kuiyumbisha JF
 
Stori ndefu ila alipata umaarufu mkubwa kuliko JF yenyewe na hivyo aliweza kufungua magroup ambaye wana JF ndiyo walikuwa members wake, na pia aliweza kuiyumbisha JF
Duuuuu mbona hiyo hatari sana mkuu.


Kwahiyo mwisho wake ukawaje sasa?


Na unanishauri nini?
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA MBILI
Hilo jambo ni kama alilitarajia kwani hakuonyesha mshtuko wowote ule kwenye uso wake bali alisimama na kujibanza sehemu ambayo ilikuwa ni kama uchochoro huku kwa pembeni yake kukiwa na kibanda cha chuma. Ndani ya muda mfupi zilianza kusikika hatua za mabuti zikiwa zinasogea hilo eneo na hatimaye walionekana wanaume sita ambao walikuwa kwenye buti nzito sana na miili iliyo shiba.

Wanaume hao walikuwa wakiangaza huku na huko mithili ya kushangazwa na kitu ambacho walikuwa wanakitafuta, aliwaangalia kwa mbali ni kama hawakuwa na silaha za moto mkononi zaidi ya mwanaume mmoja ambaye alikuwa anakizungusha kisu kwenye mkono wake. Alijitokeza na kukohoa kidogo ili waweze kujua kwamba walikuwa na mgeni mwingine hapo kama sio mtu ambaye bila shaka walikuwa wakimhitaji ndani ya hilo eneo. Kutokea kwake kuliwashtua kiasi kwani walitarajia kwamba mtu huyo atakuja hilo eneo ila sio kwa staili hiyo.

“Mvunje mguu mmoja kisha tuondoke naye” ilikuwa kauli nyepesi sana ya mwanaume mmoja kati yao akitoa maagizo kisha yeye akaiwasha sigara yake ndani ya hicho kiza totoro huku kikipoozwa na nyota chache ambazo zlikuwa angani na kuufanya mwaga wa sigara hiyo uonekane mithili ya taa inayowaka na kuzimika. Mwanaume mmoja ambaye alikuwa ameujaza mwili wake alisogea hilo eneo na kurusha ngumi nzito ambayo ilikuwa inalenga kwenye mbavu za Tommy lakini alimkosa baada ya Tommy kujivuta nyuma kwa nguvu kubwa kiasi kwamba urushaji wa mkono wa mwanaume yule haukuendana na kasi ya mkwepaji ambayo ilikuwa ni kali sana isivyo kawaida na huenda hata mrushaji hakuweza kuamini hilo jambo.

Aligeuka na mtama baada ya kuukaza mguu wake lakini aliishia kuifagia barabara tu, alinyanyuka na sarakasi huku akiyarusha mabuti yote mawili, Tommy alijigeuza kwa kasi sana na kumzunguka mtu huyo ambapo alipita kwa nyuma yake hivyo mwanaume huyo akahitaji kugeuka haraka sana, alipigwa ngumi ya uso kali mno mpaka ikasikika mifupa ya kwenye paji la uso ikiwa kama inavunjika vibaya. Alirudi nyuma kusikilizia maumivu hayo ila kwa bahati mbaya sana alipigwa kiatu cha goti wakati anashuka ili kushikilia goti hilo ngumi nyingine ilipenya kwnye shingo yake kisha shingo ikazungushwa kwa nguvu ilivyokuja kuachiwa mwanaume huyo alikuwa ni marehemu tayari.

Wale wote walishtushwa na hilo jambo kwani maelezo ambayo walipewa ni kwamba mtu huyo alikuwa ni mlaini laini sana hivyo walitakiwa kuifanya kazi yao kwa haraka na kuondoka eneo la tukio na ndiyo ilikuwa sababu kubwa sana ya wao kuweza kuukata umeme wa eneo hilo kwani waliamini ndani ya muda mfupi wangeimaliza kazi yao na kuondoka. Yule ambaye bila shaka alikuwa ndiye kiongozi wao hata ile nguvu ya kuendelea kuvuta sigara hakuwa nayo tena ilimlazimu kuiachia huku akiwa anashangaa lakini kwa Tommy ilikuwa tofauti sana kwani wakati huo alikuwa anawasogelea wanaume hao watano ambao walikuwepo mbele yake akiwa ndani ya suti.

Walimsogelea kwa pamoja isipokuwa yule ambaye alikuwa anavuta sigara, walirusha mateke kila mtu mawili kwa spidi kali, Tommy alifanikiwa kuyakwepa mawili na mengine yakazama kwenye mwili wake na kumrusha mbali sana, kitu ambacho alikifanya hakutua kwa kutumia mgongo bali miguu yake ilidunda kwenye vile vyuma ambavyo vilikuwa kwenye kile kibanda ambacho alikuwa amejificha mwanzo na kusimama tena akiwa anawahesabia watu hao hatua ambazo walikuwa wanapiga.

Walihisi amekuwa wao hivyo walikuja kwa kasi ili wachukue pointi tatu, mwanaume aliyekuwa mbele alimkwepa kwa kusogea pembeni hivyo teke lake likawa limepitiliza ila ilikuwa ni safari yake ya mwisho kuwa na uwezo wa kusimama kwani kupitiliza kwake kulimfanya ashindiliwe na ngumi nzito sana ya mgongoni kitu kilichoufanya uti wake wa mgongo kuvunjika. Ni sauti ya kilio tu ambayo iklisikika kwa mbali wakati anashuka chini. Waliokuwa nyuma wa mwisho alisita baada ya hilo tukio hivyo wakawa wamekuja wawili kwa mkupuo, wa mbele alihisi kama amehisi ila ndio ulikuwa uhalisia alidakwa mguu wake ambao ulipigwa na kiganja kwenye mfupa na mguu huo ukawa umemsaliti moja kwa moja wakati anashuka chini alipigwa na kiatu cha kichwa, kichwa chake kikajigongesha kwenye lami ambapo kilipasuka vibaya sana. Mwenzake alikuwa anasogea kwa hasira kali ila ziliishia kuwa majuto kwake, urushaji wake wa ngumi kwa hasira ulifanya apokee ngumi mithili ya nyundo kwenye eneo la kifua chake ambacho kilimfanya aheme kwa nguvu sana na kukohoa mfululilo kitu ambacho kilimfanya asogee nyuma maana hewa ni kama haikuwa ikipita vizuri kwenye koo lake.

Kusogea kwake nyuma kulimpa nafasi mwenzake ambaye alikuwa amesita wakati ule wenzake wawili wanasogea mbele kumkabili Tommy na huyo ndiye ambaye alikuwa na kisu kwenye mkono wake. Alikirusha kisu kwa mkono wake wa kushoto akiwa hajakitoa mkononi huku mkono wa kulia akiwa amelenga tumboni kwa Tommy kwa ngumi kali, ngumi ilifika ila mkono wenye kisu ulidakwa na kupindishwa, kitu ambacho kilikuwa cha ghafla sana kwani asingeweza kutekeleza mambo hayo mawili kwa wakati mmoja hivyo ngumi iliachwa iingie lakini mkono wake kisu ulikunjwa vibaya kiasi kwamba alishindwa kuyahimili maumivu yake akawa amekiachia kisu hicho ambacho kilitua kwenye mkono wa Tommy ambaye alikirudisha kwa nguvu sana kwenye kifua cha mtu huyo na kukizamisha kwenye moyo, aliyatoa macho yake huku akiwa anaimana kwamaumivu makali lakini mwanaume hakuwa na muda naye alimsukumia pembeni huku akiwa anakichomoa kisu hicho ambacho alikirusha kwa kutumia nguvu kubwa sana kuelekea kwa yule ambaye alikuwa amesimama baada ya kifua chake kuachia na hewa kuanza kupita kwa wakati huo ila kwa bahati mbaya sana alikutana na kisu cha koromeo hivyo habari yake ikawa imeishia hapo akawa amebakia mwanaume mmoja tu yule ambaye alikuwa anavuta sigara.

“Ulijua kama tutakuja hapa?” aliuliza akiwa analitoa koti lake mwilini na kubaki na vest ambayo bila shaka ilikuwa nyeusi maana kama ingekuwa nyeupe kwa ule mwanga ambao kwa mbali sana ulikuwa ukipenya kutoka kwenye nyota angani ungeakisi ikaonekana.

“Yeah”

“Umejuaje wakati tumekuja hapa kwa siri?”

“Dunia ya uongo inahitaji watu wenye uwezo mkubwa sana hususani wanasaikolojia au watu ambao wamefundishwa vyema ndio ambao wanaweza kudanganya na wasijulikane. Binti yule nimemuuliza swali rahisi sana kuhusu simu yake akasema imezima chaji wakati kiuhalia navyo ingia pale ndani nimemuona nayo mkononi ila ghafla akairushia kwenye sofa na kuifunika na mto wake. Jibu ambalo amenipa kudai kwamba simu imezima nikajua kabisa kuna mambo anayajua ila hataki kuyaweka wazi ila nilikuwa nataka nithibitishe kupitia hili hapa” alitulia akiwa anamwangalia bwana huyo ambaye alikuwa ameukaza sana mwili wake kisha akaendelea

“Nilijia kama kweli kuna mambo anayajua basi lazima kuna watu ambao watakuwa wanamfuatilia kila anacho kifanya ili asije akavujisha na lazima walikuwa na mawasiliano naye ya karibu ili akionekana mtu anawafuatilia sana taarifa zao awape taarifa waweze kumuua haraka sana kabla mambo yao hayajaharibika. Ni kweli nimethibitisha hilo ndiyo maana nimeliacha gari palepale kwao hivyo niliamini kama ana mawasiliano na watu fulani lazima atawapa taarifa haraka na ndicho ambacho kimetokea” mwanaume huyo aliishia kucheka kwani mwenzake alipiga mahesabu ambayo kiuhalisia ndio ulikuwa ukweli wenyewe juu ya wao kuwepo hapo.

“Unahisi baada ya kujua hilo ndiyo utapona labda?”
“Sipo kwenye hii hali ya kuweza kuua tena leo ndiyo maana hata vijana wako nimewaua kwa hali ya uzembe sana kwa sababu mwili wangu hauniruhusu kabisa kufanya haya kwa sasa. Nipeleke alipo dada yangu kisha nitayaacha maisha yako na kukupa nafasi nyingine ya kuishi” kauli ambayo ilitoka kwenye kinywa ambacho kilikuwa kinamaanisha sana.

“Hilo jambo sahau kabisa, kwanza tumepewa taarifa kwamba wewe ni kijana mnyonge, dhaifu usiye na lolote kivipi unaweza kufanya haya mambo wakati unajulikana kwamba wewe unaweza kuishika kalamu ya wino tu pekee? Wewe ni nani labda?” mwanaume huyo alikuwa akiongea sana huku akiwa anaitoa bastola yake mfukoni na huenda ndiyo ambayo ilikuwa ikimpa sana kiburi. Lilifanyika tukio la ghafla sana ambalo lilifanywa na Tommy kwani aliugusa mfumo wake na kutoa kitu kigumu chenye pembe nne ambacho alikirusha kwa kasi sana, kilitua kwenye mdomo wa yule mwanaume na kuuchana chana vibaya sana mdomo wake hata bastola ilimponyoka kwenye mkono wake.

Wakati anaendelea kupiga kelele za maumivu, Tommy alikimbia kwa kasi sana kuelekea hilo eneo ambapo alijigeuza kwa viwiko vya mikono ambapo mwanaume huyo alikikwepa kimoja lakini kimoja kilitua kwenye taya na kumletea maumivu makali sana, alikimbilia nyuma maana aliona kasi ya mtu huyo ilikuwa sio ya kawaida kabisa angekufa akiwa anajiona huku mdomo wake ukiwa unavuja damu maana ulichanika. Alikuwa anaipigia hesabu ile bastola yake chini hivyo aliruka ili aidake alitulizwa na kiatu cha uso na kumfanya adondokee kwenye lami na kujiburuza vibaya sana uso ukiwa umekwanguka kiasi cha kutosha.

Akiwa anayapiga hayo makelele Tommy alichomoa kisu kwa yule mwanaume ambaye alikizamisha kwenye koromeo lake na kumsogelea mwanaume huyo ambaye alikuwa analia barabarani hapo kwa namna sura yake ilivyokuwa imesagika.

“Kwanini mtu laini kama wewe unaamua kuyaharibu maisha yako kwa kuleta maumivu kwenye familia za watu namna hii?” alimuuliza swali akiwa amemfikia pale ambapo alikuwa amedondokea lakini mwanaume huyo hakujibu kitu ambacho kilimfanya Tommy amkanyage kwenye goti lake, ilipelekea hilo goti kuharibiwa vibaya sana, ilimfanya kupiga makelele sana lakini makelele yake yalimponza kwani kisu kilizaishwa kwenye bega lake karibu na shingo yake kwa nguvu na kumletea maumivu ambayo yalimfanya alie kama mtoto mdogo.

“Sikubembelezi ili unijibu nacho kuuliza, nakupa sekunde kumi na tano nitakuuliza tena kama ukishindwa kufanya hivyo basi nakuua” mwanaume aliongea kwa msisitizo sana, kulikuwa kuna kiza lakini macho yake yalikuwa yanaonekana kabisa kuwa mekundu mno, ni mtu ambaye alikuwa ameharibiwa familia yake hivyo hakuona kama alikuwa na muda wa kukaa na kuanza kumbembeleza mtu kitu ambacho kilikuwa ni lazima kufanyika.

“Dada yangu yuko wapi?”

“Nakuomba unihakikishie ulinzi baada ya mimi kukwambia ukwe………” sauti ya mwanaume huyo ya kuanza kuhitaji makubaliano badala ya kujibu ilikolezwa na kisu kuzamishwa kwenye paja lake kwa nguvu kisha kisu hicho kikiwa ndani kilivutwa kwa lazima mpaka kwenye goti ungehisi kwamba mtu alikuwa anampasua ni kuku kwa ajili ya sherehe, mwanaume huyo alijikojolea hapo hapo huku akiwa anahema sana, alikuwa anaulizwa maswali yeye anaanza kuleta stori za akina Juma na Uledi.

“Yupo Mikocheni, yupo Mikocheni” alijibu kwa pupa sana
“Kwa nani?”
“Kwenye safe hause”

“Ya nani?” hilo swali lilimfanya asite site lakini lilikuwa ni kosa lingine kwani Tommy alitoa bastola yake mkononi kisha akafyatua risasi moja ambayo ilizama kwenye paja moja ambalo lilikuwa halijaguswa na kuiweka hali ya mwanaume huyo rehani ikabidi ataje tu

“Remsi ambaye ni mpenzi wake”
“Na huyu binti Noelia anahusikaje?”

“Huyo ndiye ambaye huwa anatumika kukusanya taarifa za mwenzake na kuzifikisha kwa bosi na ndiye ambaye alifanikisha hili jambo kwa asilimia nyingi sana”

Unahisi ni muda sahihi wa kumjua Noelia? Ishirini na mbili inafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.
 
SIMULIZI: ELECTION SAGA (MONEY IN BLOOD)
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
WHATSAPP: 0621567672
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
AGE: 18+

UKURASA WA ISHIRINI NA TATU
“Ana mahusiano gani na huyo bosi wako?”

“Ni wapenzi wa muda mrefu sana”

“Kwahiyo dada yangu aliingizwa kama chambo ya familia sio?”
“Ndiyo”

“Na Noelia alikuwa anayajua haya yote?”

“Ndiyo, ndiyo alikuwa anayajua”

“Kipi kilimfanya mpaka awe karibu na dada yangu na kukubali kufanya ushetani kama huu wakati yeye aliaminiwa kama rafiki?”

“Ukiacha hilo la kuwa wapenzi yule binti alilipwa pesa nyingi sana ambazo ndizo hasa zimemfanya aifanye ile kazi kwa moyo wote japo ilikuwa ya mpenzi wake”

“Bibi yake analijua hilo?”

“Yule sio bibi yake”

“Yule ni nani?”

“Ni mwanamke tu ambaye alilipwa ili kukamilisha hilo jambo tangu anakutana na dada yako ili aweze kuamini kwamba naye ana familia ila yule sio bibi yake bali ni mwanamke mmoja ambaye ni mjanja mjanja aliwahi kuchukuliwa kwenye kasino na huwa anatumika kwenye kazi nyingi sana. Ule uzee ambao unamuona nao ulitengenezwa tu ila yule ni Malaya anaye jiuza na hata hivi unavyo ongea huenda wamesha ondoka pale nyumbani”

“Shiiiiiit!” Tommy alichoka, maana watu hao walionekana kuwa na mipango mikali sana pale ambapo wanakuwa wanahitaji kutimiza jambo lao na hilo jambo lilionekana kupangwa kwa muda mrefu sana.

“Sababu kubwa ni ipi hasa mpaka watumie gharama sana namna hiyo kumuingiza dada yangu kwenye huo mtego?”
“Mimi sijui kiundani sana ila nilisikia bosi akiwa anahusisha jambo hilo na mambo ya uchaguzo hivyo sina taarifa kamili ila ukimpata yule binti ambaye wewe unamjua kama Noelia japo jina lake la kweli anaitwa Sasha ndipo unaweza kuzipata taarifa zote kamili ambazo unazitaka”

“Mikocheni amehifadhiwa kwenye nyumba gani?” Tommy aliuliza kwa ghadhabu sana lakini mwanaume huyo pumzi yake ilikuwa inazidi kupungua kwa spidi sana kiasi kwamba alimvuta Tommy na kumnong’oneza sikioni kwake sehemu ambayo anatakiwa kwenda kisha akamsukuma kwa nguvu kama kumpa taarifa kwamba anatakiwa kuondoka haraka sana hilo eneo kumuwahi dada yake. Tommy alisogea pembeni na kuokota kile chuma chake ambacho alimchana nacho mdomoni mwanaume huyo kisha akaondoka kwa kukimbia sana akiwa ndani ya hiyo suti yake ili kuwahi nyumbani kwa akina Noelia maana aliambiwa kwamba kama angechelewa basi asingempata tena mwanamke huyo kwa wakati huo.

Mwanaume akiwa kwenye suti yake ambayo kwa wakati huo ilikuwa na jasho la kutosha, alifika ile sehemu na kuiona gari yake ng’ambo mwa ile barabara ikiwa imezimwa vile vile kama ilivyokuwa imeachwa lakini geti la jumba hilo lilikuwa wazi kabisa hali ambayo ilimfanya aishike bastola yake mkononi na kuingia akiwa makini sana ila kitu cha ajabu ni kwamba hata mlango wa ndani ulikuwa wazi na hakukuwa na dalili za uwepo hata wa mtu mmoja.

Baada ya kufika ndani alishangazwa na kitu ambacho alikutana nacho kwani nyumba ilikuwa tupu haikuwa na mtu hata mmoja, alichoka. Hali hiyo ilimfanya atoke haraka sana na kupanda kwenye gari yake kisha akaiwasha na kuelekea kule ambako alikuwa amemuacha yule mwanaume ambaye alimtesa vya kutosha mpaka akampa siri zote ambazo alikuwa anazihitaji. Kufika pale alipatwa na mshangao mwingine tena kwani mtu huyo alikuwa amepigwa risasi ya kichwa na kupoteza maisha yake hapo hapo barabarani, kurudi kwake ni baada ya kuona kwamba mtu huyo anaweza kuwa na umuhimu kwake mbele ya safari lakini kitu cha ajabu ni kwamba naye alikuwa ameuawa na hapo mahesabu yalimwambia kwamba kama ni kumuua mtu huyo maana yake ni huyo Sasha na huyo mwenzake ndio wametekeleza shambulio hilo kwani ndio ambao walikuwa jirani na huenda alipishana nao wakati anaenda kuwatafuta kule wao walienda alipokuwa na kumuua mwanaume huyo kisha wakatoweka.

Aliishia kupiga usukani wa gari kwa hasira sana huku akiliondoa gari eneo hiyo kwa kasi kubwa sana kuweza kuwahi huko Mikocheni ambako alikuwa amepewa taarifa hiyo. Akiwa anaendelea kuendesha gari yake alikuwa anaendelea kubadilisha nguo maana aliona suti iliyokuwa mwilini mwake ilikuwa inamsumbua wakati alikuwa kwenye majukumu ya kazi na wakati huo ilikuwa ni saa tisa ya usiku. Kwenye moyo wake alitamani sana amkute dada yake salama huko kwani kesho yake asubuhi alikuwa anahitaji mama yake anavyo amka amuone mwanae huyo wa kwanza kwenye uso wake.

Lakini mbali kidogo na ile sehemu alionekana mwanaume mwingine ambaye alikuwa amejifunika kwa kitambaa cheusi usoni kwake na nguo nyeusi mwilini akiwa amekaa sehemu anaangalia kila ambacho kilikuwa kinaendelea, baada ya Tommy kuondoka naye alipanda kwenye pikipiki yake ambayo alikuwa ameificha kwenye kichochoro kimoja na kuelekea ile njia ambayo Tommy alinyoosha nayo.

Alitembea na gari kwa kasi ya ajabu sana kiasi kwamba kama kingetokea kitu mbele yake basi ingetokea ajali mbaya sana ila hakuwa na namna licha ya kufika nchini siku hiyo hiyo hakuwa na budi kuingia kazini huku familia yake ikiwa haijui jambo lolote lile kuhusu yeye kwani walimjua kama msomi tu na kijana mwenye akili kubwa isivyo kawaida lakini huo upande wa hayo mambo yake ya gizani hakuna ambaye alikuwa anaujua.

Aliisimamisha gari kibabe sana huku ikiwa inaendelea kutoa muungurumo mkali, aliisimamisha na kuruka akiwa ndani ya vest nyeusi na jeans pamoja na buti la kazi ambavyo alivibadilisha akiwa barabarani. Nyumba ambayo alikuwo ameelekezwa ndiyo hiyo ambayo alikuwa amesimama mbele yake huku usoni kwake akiwa amejifunika na kitambaa cheusi ambacho kilikuwa sawa na vest yake pamoja na buti ambalo alikuwa amelivaa.

Mwanaume huyo aliparamia ukuta mithili ya paka, baada ya kufika juu sehemu ambayo ilikuwa na nyaya za umeme, aligusa ukutani kwa buti lake kisha akajigeuza na kurukia upande wa ndani ambapo alifikia goti moja chini akuwa ameinama. Baada ya kuinua macho yake mbele aliona kuna mlinzi akiwa anatembea tembea, alikifumua kichwa chake vibaya sana kwa kutumia bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Ule mdondoko wa yule mlinzi ndio ambao ulimshutua mwenzake ambaye alikuwa karibu na lile eneo hivyo akasogea kuona mwenzake huyo alikutwa na nini lakini wakati anayainua macho yake alipigwa ngumi mbaya sana ya koromeo kisha shingo ikazungushwa kama kuku habari yake ikawa imeshia hapo.

Tommy alisikia mchakacho upande wa nyuma hivyo akageuka haraka sana akiwa ameielekezea bastola eneo hilo ambalo huo mchakacho ulikuwa umetokea hakuona kitu zaidi ya kiza hivyo akaishusha bastola yake lakini ghafla sana akasikia sauti za mtu akiwa anapiga makofi na kuangua kicheko kikali sana upande huo huo kisha taa zikawaka hilo eneo wakaonekana wanaume wanne ambao walikuwa ndani ya nguo nyeusi.

“Tuna taarifa yako kwamba kuna mtu anakuja hapa muda huu hivyo tulikuwa tunakusubiri kwa hamu sana uweze kufika ili tuongee kiume. Acha uoga huo kama mtoto wa kike kuanza kutumia bastola wakati una mikono ambayo inaweza kutufanya tukazungumza kwa mapana” mwanaume huyo ambaye jeuri ilionekana kuwa sehemu yake alitamka huku akiwa anaendelea kutafuna bigji kwenye mdomo wake akiwa anasogea na wenzake. Ilikuwa ni dharau kubwa sana kwa Tommy ambaye aliishia kusikitika na kutoa risasi zote kwenye hiyo bastola kisha akaitupa pamoja na kuzitupa risasi hizo bila wasiwasi.

Lakini hakuwa amewatazama vyema sana wanaume hao kwani mwanaume wa mwisho alikuwa anaufuta futa upanga wake kwa mafuta ambao ulikuwa ungang’aa sana
“Una miaka mingapi bwana mdogo?” mwanaume huyo aliuliza swali baada ya kuona Tommy hamjibu chochote, Tommy naye akazisogeza hatua kadhaa mbele ambapo palikuwa na mwanga wa kutosha na mwili wake ulionekana vyema. Mwili ambao ulikuwa kwenye mpangilio wa pingili safi ambazo zilikuwa zimejigawa vyema sana ulikuwa unaonekana mbele ya wanaume hao huku mishipa ikiwa imejichora kwa wingi sana kwenye mikono yake.

Hata yule ambaye alikuwa anaongea wakati ule ilimlazimu kunyamaza kwanza nadhani hakutegemea kuweza kukutana na hali kama ile hususani kwa mtu ambaye hata hakuwa akimfahamu kabisa kwenye maisha yake. Mwili na macho ya binadamu huyo ambaye alikuwa mbele yao hayakuonyesha kwamba yalikuwa tayari kujibu kile ambacho alikuwa anakiuliza muda huo hivyo namna pekee ambayo ingewafanya waweze kuzungumza vizuri ni kupitia mikono yao.

Alisogea pembeni na kumuacha kijana wake mmoja aweze kupita kumnyoosha mtu huyo ambaye hakuwa akiongea mbele yao, alitaka kwenda mwanaume mmoja ambaye mwili wake ulikuwa umeshiba sana kwa mazoezi makali ambayo yalionekana kuukubali mwili huo lakini alisimamishwa na yule mwanaume ambaye alikuwa anaufuta upanga wake. Mwanaume huyo aliuangalia upanga huo na kuubusu kisha alimfuata Tommy kwa spidi kiasi kwamba aliambiwa kwamba akichelewa basi mtu huyo angeweza kukimbia hilo eneo.

Upanga ulikuwa umeelekezwa eneo la begani na kama ungefanikiwa kutua basi huenda ungelitenganisha vibaya sana lakini hakumpata mlengwa wake kwani alikutana na hewa baada ya Tommy kukwepea pembeni, mwanaume huyo alizunguka na upanga wake ambao ulipita sentimita chache sana kwenye paja la Tommy hivyo ukamkosa kwa mara nyingine ila kwa bahati mbaya sana kukwepa kwake huko kulimfanya akutane na buti la uso ambalo lilimfanya afumbe macho yake kwa sekunde moja tu pekee kisha akayafumbua tena.

Wakati anafumbua hayo macho yake upanga ulikuwa unaletwa maeneo ya tumboni ikionyesha wazi mrushaji alikuwa amedhamiria sana maana hakuwa akimpa mwenzake hata nafasi ya kusema apangue, Tommy alijifanya kama anaufuata upanga huo pia ila alivyo ukaribia sana alijiviringisha na kuipitia pembeni ambapo alirusha ngumi mbili ambazo ziliutengua mkono baada ya kutua karibu na bega na kumfanya mwanaume huyo apige kelele za maumivu kitu kilicho mpelekea kuweza kuuachia upanga huo kwani hakuwa na namna lakini upanga huo haukufika chini, ulidakwa na mkono wa Tommy kisha aliuzungusha kwa nguvu na kuuzamisha kwenye upande wa kulia wa sikio la mwanaume huyo.

Kilisikika kilio kikali sana baada ya upanga huo kuzama kwenye sikio la mtu huyo na kisha ukalazimishwa kuingia mpaka ndani sana kitu kilicho mfanya mtu huyo kuanza kuzunguka humo ndani kila sehemu kwa makelele ila wakati huo Tommy aliuchomoa upanga huo na habari ya mwanaume huyo ikawa imeishia hapo, wakawa wamebaki watatu wanaangaliana naye huku kwenye mkono wake akiwa na upanga ambao ulikuwa na makali ya kutosha.

Ukurasa wa ishirini na tatu unafika mwisho.

Wasalaam,

Febiani Babuya.
 
Back
Top Bottom