Sakata la vitendanishi; Aliyerekodi ageukwa, Rose hana kosa

Sakata la vitendanishi; Aliyerekodi ageukwa, Rose hana kosa

Yule dume ana mambo ya ki snitch

Watu kama wale black america huwa wanapiga shaba nyingii mapemaa tu
 
Rose Mzalendo pori, James Mzalendo alopitwa na wakati, this is what defines Tanzania as a community
 
Me najua kabisa itakuwa ni ukweli jamaa alikuwa anapinga hiyo tabia mbovu ya hapo hospital ila hadi hapo kashageuziwa kibao, Scendal chafu kama hizo angetakiwa awe na ushahidi wa kutosha japo katika clip yake angeonesha hizo expiredate zake.
 
Hii nchi kumbe humu wengi maofisini wa hovyo tu kaahhh....mnamtetea rose kabisa?kosa la James ni lipi?
Tuwe wazalendo bwana

Unamchafua anaekulisha? Na huoni kosa?
 
My Take
Nilijua tu yule jamaa ni mzushi, dume zima unakaa kurekodi watu. Kama mwanaume si upeleke kwenye vikao?
Mkuu inshu ya James haikuwa ya udume zima kama ulivyomuelewa. Inshu yake ilikuwa ni afya za watz, alituonyesha in backyard ambako hatuna access nako pakoje. Yule Rose anawakilisha wahudum wengi sana ambao wanatuhudumia kwenye ofisi za umma, hawana utu wala ubinadam. Wamejaa visilani na hawajali afya zetu. Kwenye clip Rose alisisitiza wagonjwa wachomwe hivyo hivyo hatakama zimexpai. Utetezi wa FIFO na FEFO ni sawa na TRUB na TRAT.
Hivi huwa mnaamin ufafanuzi wa Msigwa? Kama huwa mnauamin kama hata huu muuamini.

Ila tz ninaiskitikia lile limfumo la hovyo lililoshamiri enzi za Mkwere likang'olewa na Jiwe. Tukawa tunapata huduma safi ofisi za umma, sasa limerudi kwa kasi ya ajabu.
 
Taratibu za kazi zao katika kutumia simu na kuwasilisha taarifa Kwa Umma zikoje?
Kama aliyerekodi kakiuka taratibu, hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yake .
Mbona mapema tu.
 
Ni kamera ya kifaa kipi iliyotumika kumrekodi?, kama ni sim ya mkononi si angeona kuwa jamaa anamrekodi. Wataalam mnisaidie
Swali hili hata Mimi nilijiuliza maana camera imemlenga dada sawia lakini dada haioni Wala hashtuki kuwa anarekodiwa.
 
James akiambiwa atoe ushahidi atabaki kubabaika kuwa niliona, niliona!
Angetakiwa awe mjanja, awe na Akili, Akili yake, iende mbali.
Kama aliamua kufanya kitu angefanya kweli.

Angerekodi kwanza hivyo vifaa vilivyo-expire kisha ndio akamrekodi huyo Bidada.
Lakini Kwa vile anaakili ndogo, akashindwa kuona kitakachomtokea.

Ingawaje hata angerekodi hivyo vifaa bado isingemsaidia kutopewa adhabu Kali.
Ila ingemsaidia kutufanya Sisi tusiopenda maneno matupu kuuelewa ukweli.
Vinginevyo ameifanya kesi yake kuwa na maswali mengi.
Wapo watakaoona anaugomvi na Yule Rose.
Wapo watakaomuona mkweli lakini ushahidi WA maneno yake kuthibitisha ukweli haupo.

Mwisho ameichafua serikali. Na ukiwa Mtumishi WA serikali ukiichafua serikali matokeo yake yanajulikana
Hili nilitabiri mwanzo kabisa mwa sakata baada ya mkuu wa hospitali kutoa maelezo kama alivyoeleza mtoa mada.

Nikasema huyu anaripua mabomu ya sumu akifurahia maangamizi kwa wenzake bila ya kujua athari za miripuko hiyo lazima zimpate na kumwangimiza na yeye mwenyewe taratibu.

Sakata hili sasa ni lake, atajua mwenyewe atakavyomalizana nalo, maana kila lenye mwanzo halikosi mwisho.
 
Back
Top Bottom