Sakata la Wasafi Festival Mbeya, ishu sio sakata la PDiddy ni CCM. Wana nafasi bado ya kujirekebisha

Sakata la Wasafi Festival Mbeya, ishu sio sakata la PDiddy ni CCM. Wana nafasi bado ya kujirekebisha

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412

View: https://x.com/lifeofmshaba/status/1840444113025400944?t=HQa05gIZAhN0Xht5BZzddQ&s=09
Tamasha la mziki la Wasafi Festival lililoandaliwa kwa gharama kubwa limeingia dosari mkoani Mbeya baada ya nsanii wake Zuchu kurushiwa chupa za maji stejini pale alipoanza tu kutumbuiza hali iliyomfanya asiendelee
Ni utamaduni wa kiafrika na mwafika kushirikiana kila jambo kwenye jamii

Kiafrika wanasema tulie wote tucheke wote.. Ukienda tofauti na hii kanuni.. Wanakubiri pa kukupata!

Taifa liko kwenye mtanziko mkubwa wa watu kudhulumiwa uhai wao
Watu kutekwa na kuteswa mateso mabaya kabisa
Watu kutekwa na kupotezwa

Ilitarajiwa hata litoke tamko la kinafiki kutoa pole na walau kulaani haya matukio lakini ndio kwanza wako wanasema mitano tena kwa mama!

Walipaswa kujua ya kwamba mashabiki wanaowategemea kuwachangia na kuhudhuria matamasha yao ni wa
Itikadi zote
Vyama vyote
Jinsia zote nknk
Na ndio hawa wanaotekwa kuteswa na kupotezwa kila siku.. Ndio hawa hawa ambao ndugu jamaa na Watanyika wenzao wamefanyiwa yote haya.. Unategemea nini kuwaendea watu kama hawa ambao tayari umeshaonesha upande wako?

Kamati ya Wasafi Festival ina nafasi bado ya kujirudi na kuweka mambo sawa.. Mashabiki ndio kila kitu.. Wakipuuzia hili mwaka huu tamasha linaweza kuvunja rekodi ya kufanya vibaya.. Jambo ambalo ni baya sana kwa brand kubwa kama Wasafi kibiashara na kijamii
Sakata la Diddy ni kichocheo tuu cha kulipua yaliyojaa vifuani mwa watu
 

View: https://x.com/lifeofmshaba/status/1840444113025400944?t=HQa05gIZAhN0Xht5BZzddQ&s=09
Tamasha la mziki la Wasafi Festival lililoandaliwa kwa gharama kubwa limeingia dosari mkoani Mbeya baada ya nsanii wake Zuchu kurushiwa chupa za maji stejini pale alipoanza tu kutumbuiza hali iliyomfanya asiendelee
Ni utamaduni wa kiafrika na mwafika kushirikiana kila jambo kwenye jamii

Kiafrika wanasema tulie wote tucheke wote.. Ukienda tofauti na hii kanuni.. Wanakubiri pa kukupata!

Taifa liko kwenye mtanziko mkubwa wa watu kudhulumiwa uhai wao
Watu kutekwa na kuteswa mateso mabaya kabisa
Watu kutekwa na kupotezwa

Ilitarajiwa hata litoke tamko la kinafiki kutoa pole na walau kulaani haya matukio lakini ndio kwanza wako wanasema mitano tena kwa mama!

Walipaswa kujua ya kwamba mashabiki wanaowategemea kuwachangia na kuhudhuria matamasha yao ni wa
Itikadi zote
Vyama vyote
Jinsia zote nknk
Na ndio hawa wanaotekwa kuteswa na kupotezwa kila siku.. Ndio hawa hawa ambao ndugu jamaa na Watanyika wenzao wamefanyiwa yote haya.. Unategemea nini kuwaendea watu kama hawa ambao tayari umeshaonesha upande wako?

Kamati ya Wasafi Festival ina nafasi bado ya kujirudi na kuweka mambo sawa.. Mashabiki ndio kila kitu.. Wakipuuzia hili mwaka huu tamasha linaweza kuvunja rekodi ya kufanya vibaya.. Jambo ambalo ni baya sana kwa brand kubwa kama Wasafi kibiashara na kijamii
Sakata la Diddy ni kichocheo tuu cha kulipua yaliyojaa vifuani mwa watu

Mungu ibariki Mbeya
 
Huu ni mwanzo wa mwisho wa Zuchu.

Watanzania tuna itikadi ya kuiga. Chances ni kubwa kwingine kokote akienda wataiga kumpopoa.

Ajishushe kidogo na kuacha kuhisi amemaliza kila kitu. Akumbuke umaarufu wake unategemea zaidi bwana ake kuliko yeye mwenyewe.
 
Kwenye hizo kelele zao sijasikia neno lolote linalohusu mambo ya siasa wala bango la kisiasa kuhusu yanayoendelea kwenye siasa, sasa iweje mhusishe na mambo ya kisiasa?

Siikubali ccm ila chadema em tumieni akili aisee ipo siku mtashindwa kubeba mimba za mume zenu na kuilalamikia ccm
 
Kwahiyo hako kamti mkavu kalitaka kuwadindia wanaume wa huko jijini mbeya, alidhani ni wale kaka zake wala urojo!!! Na mchupi wake
Tatizo anajikuta ni Rihanna kusahau kuwa relevance yake pekee ni kuwa demu wa Diamond tu.

Ameanzisha itikadi ya kuvimba sana siku hizi kujihisi kuwa keshamiliza kila kitu.

Anasahau kuwa kuna wengi wenye vipaji kuliko yeye walichokosa ni support ya ukuni wa mmiliki label.
 
Kwenye hizo kelele zao sijasikia neno lolote linalohusu mambo ya siasa wala bango la kisiasa kuhusu yanayoendelea kwenye siasa, sasa iweje mhusishe na mambo ya kisiasa?

Siikubali ccm ila chadema em tumieni akili aisee ipo siku mtashindwa kubeba mimba za mume zenu na kuilalamikia ccm
Inawezekana hicho kipengele hakijarekodiwa ila waliokuwepo eneo la tukio wanashuhudia kuwa hiyo kurusha chupa na matakataka ilianza baada ya kusema mitano tena kwa maza
 
Kilicho wakera hasa ni hii ishara ya dole la lati
 

Attachments

  • Screenshot_20240929-195222_1.jpg
    Screenshot_20240929-195222_1.jpg
    359.2 KB · Views: 5
Back
Top Bottom