Numbisa
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 301,221
- 1,172,274
Mama Wema Sepetu amshushia kipigo kikali Diana Kimaro na kuapa kumvunja mguu ! Kwa mujibu wa GPL Wema Sepetu siku kadhaa zilizopita alienda Arusha lakini alipewa onyo na mama yake mzazi kuwa ni marufuku kuongozana Na watu ambao mama Wema anaowaona wana tabia chafu.
Katika Safari hiyo Mama Wema alimwambia Wema aongozane na Petitiman na mpiga picha wake anayeitwa Bestizzo ila katika kufuatilia mama Wema akagundua Wema kaongozana na Diana Kimaro na jamaa mwingine anayetajwa Kwa jina la Kenneth Sepetu ambaye Mama Wema anashangaa jamaa huyo kalipata wapi jina la Sepetu kwakuwa sio ndugu yao.
Mama Wema hataki kabisa kuwaona kuwa karibu Na binti yake huyo asiyekaukiwa matukio akiamini Diana anamfundisha Wema tabia mbaya Licha ya Diana Kimaro kuwahi kupewa onyo mapema na Mama Wema aache urafiki na mwanae lakini akapuuza, waliporudi Arusha wote watatu walitinga nyumbani Kwa kina Wema ndipo mama Wema hasira zikampanda na kumshushia kipigo Diana huku Wema akitazama tu bila kufanya kitu kwakuwa alishakanywa muda aache urafiki na Diana.
Mama Wema alipoulizwa na GPL kuhusu kumnyuka Diana alikiri Kwa kusema "Siyo kumpiga, nimempiga hasa na bado kuna siku nitamvunja mguu, nimeshamwambia sitaki ushoga na mwanangu" “Wakati anaondoka nilimwambia aambatane na Petitman na mpiga picha wake Bestizo.
Nilipokuwa nawapokea nikashangaa kuwaona(kina Diana) nikasema sijui niende nikavae suruali kwanza ndipo nije niwafumue, basi nilijikuta nampiga teke Diana,” alisema mama Wema.
“Mimi naomba kumwambia Diana siku ile nimempiga haikutosha, kuna siku nitamuumiza ndugu zake watamkuta Muhimbili, maana Wema hawezi kuongozana kila mahali na watu wasiojielewa,” alisema mama huyo kwa ukali. Kwa mujibu wa GPL Bestizzo amethibitisha kutokea Kwa sokomoko hilo.
Hata hivyo, wema Sepetu anayedaiwa kufunzwa tabia mbaya kiumri anatajwa kumpita Diana Kwa miaka sita
Katika Safari hiyo Mama Wema alimwambia Wema aongozane na Petitiman na mpiga picha wake anayeitwa Bestizzo ila katika kufuatilia mama Wema akagundua Wema kaongozana na Diana Kimaro na jamaa mwingine anayetajwa Kwa jina la Kenneth Sepetu ambaye Mama Wema anashangaa jamaa huyo kalipata wapi jina la Sepetu kwakuwa sio ndugu yao.
Mama Wema hataki kabisa kuwaona kuwa karibu Na binti yake huyo asiyekaukiwa matukio akiamini Diana anamfundisha Wema tabia mbaya Licha ya Diana Kimaro kuwahi kupewa onyo mapema na Mama Wema aache urafiki na mwanae lakini akapuuza, waliporudi Arusha wote watatu walitinga nyumbani Kwa kina Wema ndipo mama Wema hasira zikampanda na kumshushia kipigo Diana huku Wema akitazama tu bila kufanya kitu kwakuwa alishakanywa muda aache urafiki na Diana.
Mama Wema alipoulizwa na GPL kuhusu kumnyuka Diana alikiri Kwa kusema "Siyo kumpiga, nimempiga hasa na bado kuna siku nitamvunja mguu, nimeshamwambia sitaki ushoga na mwanangu" “Wakati anaondoka nilimwambia aambatane na Petitman na mpiga picha wake Bestizo.
Nilipokuwa nawapokea nikashangaa kuwaona(kina Diana) nikasema sijui niende nikavae suruali kwanza ndipo nije niwafumue, basi nilijikuta nampiga teke Diana,” alisema mama Wema.
“Mimi naomba kumwambia Diana siku ile nimempiga haikutosha, kuna siku nitamuumiza ndugu zake watamkuta Muhimbili, maana Wema hawezi kuongozana kila mahali na watu wasiojielewa,” alisema mama huyo kwa ukali. Kwa mujibu wa GPL Bestizzo amethibitisha kutokea Kwa sokomoko hilo.
Hata hivyo, wema Sepetu anayedaiwa kufunzwa tabia mbaya kiumri anatajwa kumpita Diana Kwa miaka sita