Salama Jabir, kwa hili jirekebishe!

Salama Jabir, kwa hili jirekebishe!

Kweli kabisa mkuu usemayo. Lugha za kutatanisha kama hivi inabidi wawe wanazikwepa ukizingatia hichi kupindi kinaangaliwa na watu wa rika mbali mbali.
Sasa sijui huwa hakuna editing kabla ya kipindi kurushwa? Maana ingeondoa au ku block lugha chafu kama hivi.



Ndallo kuchanganya lugha ya kiswahili na kingereza mimi sioni km ni ttz sn kwasbb kwa saiv ndio kipimo cha usomi wetu,mtu akiongea maneno mawili ya kiswahili akitupia na la kingereza anaonekana ndo msomi!nikirud kwenye mada inabidi dada yetu salama awe makini na baadhi ya maswali yake na kuangalia lugha ya kutumia kwa kipindi chake kinaheshimika sn na kinafatiliwa na watazmaji wengi ila km ataendelea na hiyo tabia atapunguza km c kupoteza kbs watazamaji zaid itaonekana kijiwe cha wahuni wanaokutana saloon kupiga soga km zilivyo saloon zngne za uswahilini!
 
Hilo la kuchanganya lugha sio kwamba ndo wanawalenga wana East Africa wote?
Mi ndo ninavyoelewa hivyo.

Ila hayo maneno mabaya kwakweli hayapendezi.
Nadhani atakuwa anatusoma, ajirekebishe.
Sometimes huwa wanayakata na kimlio flani hivi kama walivyokuwa wanafanya Bongo Star Search.
Inabidi awe makini.
 
Habari wana jamii wenzangu!nimatumaini yangu kuwa wengi wenu mmekuwa mkikitazama kipindi maarufu sana cha MKASI kinachorushwa na na kituo cha runinga cha East Africa TV(chanel5) kikiongozwa na mtangazaji mahiri wa kike nchini salama jabiri!kiukweli maudhui ya kipindi ni mazuri sana hususani kwa sisi vijana kwani tunapata fursa adhimu ya kujua maisha ya watu mbalimbali maarufu hapa nchini hususan ktk tasnia ya siasa,michezo,filamu,muziki nk.niwape hongera wote waliobuni kipindi hiki.Tatizo langu mimi ni kuhusu matumizi ya lugha inayotumika wakati wa mahojiano kati ya salama na wageni wake,sometime inakera.ntatoa mfano mmoja wa hivi karibuni wakati anafanya kipindi na jackline wollper wakati majadiliano ya kiendelea alisikika akimwambia john" umedinda"nfkr ni baada ya john kumtazama sn Wollper mwanzoni nikajua labda amepitiwa ila wakarudia tena safari hii na muba na john wakalitamka hilo neno!Ashakum si matusi kwa mtazamo wangu kuna baadhi ya neno hili c matusi lkn ifahamike kwamba kipindi hiki kinatazamwa na watu wa rika tofauti tofauti kuanzia wototo wadogo mpk wazee!hebu upo imagin upo na mtoto wako unaangalia kipindi halafu akuulize hivi baba "kundinda"maana yake nini?cjui utamjibu nini?wito wangu kwa dada salama najua unauwezo mkubwa sana wa kuuliza maswali mazuri lkn kwa hili naomba ajitazame na kujirekebisha!ni mtazamo tu lakini wadau!

Utaki unaacha!
 
Mkasi Mbona Iko Poaa Kwa Kizazi Hiki Cha Facebook Sidhani Kama Kuna Mtoto Asieelewa Neno Kudinda Kama Akikuuliza Malizana Nae
 
Back
Top Bottom